Ashakhum si Matusi: Tuliozaliwa nje ya ndoa wote ni wana haramu

Ashakhum si Matusi: Tuliozaliwa nje ya ndoa wote ni wana haramu

Zanzibar wanafatilia sana sheria za ndoa yani mtoto akizaliwa nje ya ndoa anaishi bira furaha na anakosa upendo kutoka kwa kwenye familia ya Baba yake mzazi, yani utakuta kwenye familia anaweza kupendwa mtoto yatima kuliko mtoto wa nje ya ndoa, Kuna rafiki yangu aliniambia yeye ni mtoto wa nje ya ndoa kuna kipindi alienda kumsalimia Baba yake alipofika nyumbani kwa Baba yake huyo baba yake akamkataza kumuita Baba ila amuite mzee Juma kwasababu huyu Baba yake ana mke na ataki mke wake ajue kama alizaa nje ya ndoa, Kwakifupi Wazanzibari wana piga vita sana kuzaa nje ya ndoa na mtoto wa nje ya ndoa hana thamani kabisa kwenye familia ya Baba yani wakijua kijana wakiume kazaa nje ya ndoa huyo mtoto ataishi na kulelewa upande wa Mama tu.
Hivi wanalo andiko linalowakataza kuwahudumia watoto wa nje ya ndoa au wamejiundia style yao tu ya kukwepa majukumu?
 
Kwa waislam hawezi kuwa mrithi wa mali za babaye.
Kwa wakristo angalia nchi kama England ukizaliwa na bava mfalme we ni bastard sio prince,huwezi kurithi hata ufalme,ofcoz kama baba yako ni tajiri ikatokea akafa ndio utajua umuhimu wake ila kwa masikini hakuna shida
Kwaiyo kwa Uingereza mtoto wa nje ya ndoa amrithi Baba yake? ata kama Baba yake kamuandika kwenye urithi wake, Tunasikiaga Tajiri mali zake kamrithisha mbwa,paka
 
Kwa Imaan ya dini ya kiislam, kuna watoto wa aina nne
1) mtoto wa halali
2) mtoto wa haramu
3) mtoto wa zinaa
4) mtoto wa shubha
Kuna watoto wengi ambao wanatokana na ndoa lakini ni wa haramu kutokana na kila alichokichuma mzazi wake wa kiume pindo akapatikana
 
Kwaiyo kwa Uingereza mtoto wa nje ya ndoa amrithi Baba yake? ata kama Baba yake kamuandika kwenye urithi wake, Tunasikiaga Tajiri mali zake kamrithisha mbwa,paka
Mbwa, paka wanathaminiwa kuliko bastard,tena ukiwa ukoo wa kifalme huwezi kurithi ufalme wababa yako hata ukiwa first born
 
Hivi wanalo andiko linalowakataza kuwahudumia watoto wa nje ya ndoa au wamejiundia style yao tu ya kukwepa majukumu?
Huenda walijiongeza ,ila lipo andiko la kuwabagua wanaharamu kwenye vitabu vyote
 
Hivi wanalo andiko linalowakataza kuwahudumia watoto wa nje ya ndoa au wamejiundia style yao tu ya kukwepa majukumu?
Wao wanasema kumuhudumia siyo kosa inaruhusiwa kumpa huduma za kibinadamu, lakini wao wanamuona huyo mtoto tofauti na watoto wengine mfano uwezi kusikia mtoto wa nje ya ndoa kupewa kipaumbele kipindi cha sikukuu aende kula na kufurahi kwa Bibi na Babu wala huwezi kusikia akipewa zawadi kutoka kwa Bibi na Babu au Shangazi, Baba wadogo, kwa Zanzibar mwanaume ukizaa nje ya ndoa mtoto anakuwa siyo wako umuesabu kama una mtoto ata ukimuoa huyo mwanamke mtoto mliye mpata nje ya ndoa awezi kukurithi, kwenye mgawanyo wa urithi yeye apati ataachia wadogo zake Mali zote labda hao ndugu zake waingiwe na huruma wamgaiye nje ya urithi.
 
Wao wanasema kumuhudumia siyo kosa inaruhusiwa kumpa huduma za kibinadamu, lakini wao wanamuona huyo mtoto tofauti na watoto wengine mfano uwezi kusikia mtoto wa nje ya ndoa kupewa kipaumbele kipindi cha sikukuu aende kula na kufurahi kwa Bibi na Babu wala huwezi kusikia akipewa zawadi kutoka kwa Bibi na Babu au Shangazi, Baba wadogo, kwa Zanzibar mwanaume ukizaa nje ya ndoa mtoto anakuwa siyo wako umuesabu kama una mtoto ata ukimuoa huyo mwanamke mtoto mliye mpata nje ya ndoa awezi kukurithi, kwenye mgawanyo wa urithi yeye apati ataachia wadogo zake Mali zote labda hao ndugu zake waingiwe na huruma wamgaiye nje ya urithi.
Hawana maandiko yanayowaruhusu kuwabagua , ni swaga tu kaka , kama yapo wayalete hapa tujifunze maana elimu ni endless safari
 
Kwa maana hiyo tuliozaliwa nje ya ndoa ni wanaalam hivyo hutatakiwi kwenda makanisani na misikitini. Ole wake mtu aniombe msaada wakati mimi mtoto wa halaam patachimbika
 
Sisi tumefundishwa mitume walikuwa binadamu kama sisi, ninyi mmefundishwa mitume wenu walikuwa ni viumbe wa aina gani?
Mitume wote ni binadamu kma sisi tu ila wao wamekingwa na maasi yoote

Sasa nyinyi mnasema mitume wanazini,wanakunywa pombe yni full tafrani
 
Waliofunga ndoa ndio wanaongoza kufanya zinaa,hata wewe mtoa post ni mwanaharamu mamako hajakueleza?
 
Tusipunguze ukali wa maneno wala nini, mliozaliwa nje ya ndoa wote ni wana haramu.

Mlipatikana kwa njia ya uzinzi kinyume na mipango ya Mungu.

Na mnaozaa nje ya ndoa watoto wenu ni wana haramu.

Vijana fungeni ndoa mpunguze kizazi cha wana haramu

[emoji23][emoji23][emoji23] Mungu ni wa wote ndugu yangu
Haramu ni wewe umesema lakini Mungu amemwona anafaa akampatia pumzi
 
Ukipita uswahilini ndio utajua hujui,Kila mtoto ana mtoto Sasa Anza kuuliza majina Yao.!!!!!
 
Na mfano halisi ni Suleiman , alizaliwa kwa mama wa kuiba yaani mamake Suleiman aliachishwa kuwa mke wa Uria (ndoa ilivunjwa) kwa lazima ya mfalme Daud ila hiyo ndoa yenye uharamu ikamzaa mtu tajiri na mwenye hekima zaidi katika uzao wote wa dunia tangu ilipoumbwa
Kabisa mkuu.
 
Fafanua wamekingwa vipi?
First of All I am Muslim

Kwaio naamini mafundisho ya kiislamu
Mitume wote wamekingwa kua hawafanyi dhambi na mola wao yni hawawezi kumuasi Mungu wao ata iweje like hawawezi kuzini,kuiba na mengineyo ktka yle ambayo yanaplkea kumuasi Mungu
 
First of All I am Muslim

Kwaio naamini mafundisho ya kiislamu
Mitume wote wamekingwa kua hawafanyi dhambi na mola wao yni hawawezi kumuasi Mungu wao ata iweje like hawawezi kuzini,kuiba na mengineyo ktka yle ambayo yanaplkea kumuasi Mungu
Weka andiko ndugu yangu , nami nitakupa andiko kutoka ndani ya Quran kuwa hata Mtume Mohammad alikuwa na dhambi ukibisha nitakuongeza hata hadith sahih

Kila mtu anaweza kujikinga na dhambi mwenyewe sio Mungu kumkinga maana ukisema Mungu anamkinga mtu dhidi ya uovu maana yake ni kwamba Mungu anawabagua watu na kuwapendelea maana atakuwa anawatengeneza wazuri na wengine anawaacha tu mwisho aliowaacha anawatupa jehanamu jambo ambalo si la kweli.
 
Back
Top Bottom