Asili ya jina Tanzania na mwasisi wake: Mohammed Iqbal Dar

Asili ya jina Tanzania na mwasisi wake: Mohammed Iqbal Dar

evaluate its present value you'll find out!

vipi thamani yake kipindi kile? Mbona wavaa trauza kabla ya kufuli?
Kipindi kile ilikuwa na thamani kubwa.jaribu kuendana na wakati. Kama ingekuwa leo ni dhahir asingepewa hicho kiasi bali mamilioni.
 
Si Kiarabu tu, ni jina linalopatikana ndani ya Qur'an 10:25:

وَاللّهُ يَدْعُو إِلَى دَارِ السَّلاَمِ وَيَهْدِي مَن يَشَاء إِلَى صِرَاطٍ مُّسْتَقِيمٍ

WaAllahu yadAAoo ila dari alssalami wayahdee man yashao ila siratin mustaqeemin

But Allah doth call to the Home of Peace: He doth guide whom He pleaseth to a way that is straight.

Na Mwenyezi Mungu anaita kwendea Nyumba ya Amani, na anamwongoa amtakaye kwenye Njia Iliyo Nyooka.



wewe mbona subjective sana. Me historia naifahamu sana. Me sioni uhusiano kati ya koran na neno dar es salaa. Hili ni neno la kiarabu na kwa kuwa koran imeandikwa kwa kiarabu ni waz litakuwepo ndani. Jaribu kutofautisha imani na utamaduni. Mfano neno good hope au tumaini jema lipo ktk biblia. Je tunaweza kuihusianisha rasi ya tumaini jema nchin afrika kusini na biblia?
Hiv upo uhusiano gani kt ya jina lako na ww? Hakuna sema mazoea na utamaduni ndo umekuathir ndo mana kama waitwa hamis utakuta wapo hamis wengi. Au waweza kutueleza wana jf nini lengo lako kupost haya makamburu[machicha]?
 
Si Kiarabu tu, ni jina linalopatikana ndani ya Qur'an 10:25:

وَاللّهُ يَدْعُو إِلَى دَارِ السَّلاَمِ وَيَهْدِي مَن يَشَاء إِلَى صِرَاطٍ مُّسْتَقِيمٍ

WaAllahu yadAAoo ila dari alssalami wayahdee man yashao ila siratin mustaqeemin

But Allah doth call to the Home of Peace: He doth guide whom He pleaseth to a way that is straight.

Na Mwenyezi Mungu anaita kwendea Nyumba ya Amani, na anamwongoa amtakaye kwenye Njia Iliyo Nyooka.



wewe kuwa objective. Mpaka umo htmu najua wewe ni mwanataaluma flani na mising ya kila taaluma ni kuwa wa mrengo wa kati na kutazama mambo ktk mtazamo chanya. Mi ninajua hst kuwa jina dar ni la kiarabu. Swala la kuwa kwe koran ni rahs kuwa imeandikwa kwa kiarabu. Au unamaana gan kupost hii coment?
 
wewe kuwa objective. Mpaka umo htmu najua wewe ni mwanataaluma flani na mising ya kila taaluma ni kuwa wa mrengo wa kati na kutazama mambo ktk mtazamo chanya. Mi ninajua hst kuwa jina dar ni la kiarabu. Swala la kuwa kwe koran ni rahs kuwa imeandikwa kwa kiarabu. Au unamaana gan kupost hii coment?

Hiyo si comment hilo ni darsa kwa wale wasioelewa kuwa maana ya Dar Es Salaam si "Bandari salama" kama wengi wanavyotaka iwe. Maana halisi ni hiyo hapo na huo ni ushahidi wa hiyo maana?

Una swali jingine?
 
kama kawa waliomwambia mwl kuwa watagomea uhuru, asipokubali mashari yao bado wana propaganda kuwa waligombania uhuru na si mwalimu.uhuru wenyewe ulikuwepo mezani ni mwalimu tuu kuthibitisha kuwa alikuwa na uwezo wa kuongoza na umoja wa kitaifa ambao alithibitisha.
 
Mwandishi Alphonce Tonny Kapelah kutoka Mtwara Leo ameona vyema aufahamishe umma juu ya mwasisi wa jina la Tanzania.

Anasema...
Nimeona niwafahamishe hili huenda likatusaidia hasa kwa hivi sasa wakati tukisherekea miaka 50 ya Uhuru wa Tangayika, najua wengi wetu hatujui historia ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar maana tuliwakuta waasisi wetu wameishafanya zoezi hilo, tusilijadili sana kwa kuwa lengo lao lilikuwa zuri.

Lakini je unamjua huyu Bwana aliyetunga jina la Tanzania pata historia ya namnaalivyofanikiwa kupata jina la T A N Z A N I A.

Sherehe za Muungano kati ya Tanganyika na Zanzibar huwa tunasherekea kila Mwaka Tarehe 26/04/ lakini Tangu mimi binafsi nipate ufahamu na kuanza kushuhudia sherehe za Muungano nimekuwa nikisikia kuwa jina la Tanzania lilipendekezwa na Watanganyika, Wazanzibar na Raia wengine wa nje lakini sikuwahi kukutana na huyo ambae alibuni jina hili tamu la Tanzania.

Imekuwa kama Bahati nimekutana na Mtu huyu aliyebuni jina la Tanzania Mkoani Mtwara, sehemu ambayo tayari naiweka kwenye Historia yangu hata kesho nikiondokaMtwara nitaikumbuka Radio yangu Safari Radio.

Huyu bwana aliyebuni jina la Tanzania ni Muhindi na Dini yake ni AHMADIYA MUSLIM JAMAAT TANZANIA majina yake ni MOHAMMED IQBAL DAR.

Mohammed alizaliwa Mkoani Tanga miaka ya 1944, Baba mzazi wa Mohammed alikuwa Daktari huko mkoani Morogoro alikuwa anaitwa Dr. T A DAR alikuwa Tanganyika kuanzia mwaka 1930.

Mohammed Iqbal Dar alipata elimu yake ya Msingi Mkoani Morogoro shule ya Msingi H H D AGHAKHAN kwa sasa ni Shule ya Serikali na baada ya hapo alikuja baadae kujiunga na Chuo cha Mzumbe akasoma Kidato cha Kwanza mpaka cha Sita.

Aliingiaje kwenye shindano la kupendekeza jina la Muungano kati Tanganyika na Zanzibar?

Mohammed anasema alikuwa Maktaba akijisoma gazeti la Tanganyika Standard, siku hizi Daily News, akaona Tangazo linasema Muungano wa Tanganyika na Zanzibar unafahamika kama Republic of Tanganyika and Zanzibar jina likaonekana refu sana kwa hiyo Wananchi wote wakaombwa Washiriki kwenye shindano la Kupendekeza jina moja litakalo zitaja nchi zote mbili yaani Tanganyika na Zanzibar Mohammed Iqbal Dar anasema aliamua kuingia kwenye Shindano na hivi ndivyo alianza Safari ya Kubuni Jina la Muungano.

Kwanza anasema alichukua karatasi akaandika Bismillah Raahman Rahimu hii ni kutokana na Imani yake na baada ya hapo akaandika jina la Tanganyika baada ya hapo akaandika Zanzibar halafu akaandika jina lake Iqbal halafu akaandika jina la Jumuiya yake ya Ahmadiya baada ya Hapo akamrudia tena Mwenyezi Mungu akamwomba amsaidie ili apate jina zuri kutoka katika majina hayo aliyokuwa ameyaandika. Baada ya hapo Mohammed Iqbal Dar alichukua herufi tatu kutoka Tanganyika yaani TAN na kwa upande wa Zanzibar akachukua Herufi tatu za Mwanzo ZAN ukiunganisha unapataTANZAN alivyoona hivyo akachukua I herufi ya kwanza katika jina lake la Iqbal na akachukuaA kutoka jina la dini yake yaani Ahmadiyya kwa maana hiyo ukiongeza herufi hizi mbili I na Akwenye TANZAN unapata jina kamili TANZANIA akalisoma jina akaliona ni zuri lakini akajiridhisha pia kwamba akiongeza herufi hizo za I na A kwenye TANZAN italeta maana kwakuwa nchi nyingi za Afrika zinaishia na IA, mfano EthiopIA, ZambIA ,NigerIA, TunisIA, SomalIA, GambIA, NamibIA, LiberIA, MauritanIA alivyoona hivyo akaamua apendekeze kuwa jina TANZANIA ndio litumike kuwakilisha nnchi hizi mbili yaani Tanganyika na Zanzibar kwa maana hiyo jina TANZANIA limezaliwa kutoka majina manne majina hayo ni Tanganyika, Zanzibar, Iqbal na Ahmadiyya.

Mohammed Iqbal Dar baada ya kupata jina hilo akalituma jina hilo kwenye kamati ya kuratibu Shindano. Baada ya Muda mwingi kupita baba yake na Mohammed Iqbal Dar alipokea barua nzito kutoka Serikalini ikiwa inasomeka kama ifuatavyo…


REPRESENTED BY THE
MINISTRY OF INFORMATION AND TOURISM,TANZANIA
TO
MOHAMED IQBAL DAR
IN RECOGNATION OF THE ACHIEVEMENT OF CHOOSING THE NEW NAME FOR THE
UNITED REPUBLIC OF TANGANYIKA AND ZANZIBAR NAMELY
“REPUBLIC OF TANZANIA”
DURING THE NATIONAL COMPETITION DAY IN 19TH NOVEMBER 1964
I A WAKIL
MINISTER FOR INFORMATION AND TOURISM


Barua hiyo pia ilisema...

Utakumbuka kuwa miezi michache iliyopita ulituandikia kutupa ushauri kuhusu jina jipya la Muungano wa Tanganyika na Zanzibar na wewe pamoja na wananchi wenzio 16 ulishauri nnchi yetu iitwe Tanzania. Nafurahi kukuarifu kuwa mshirikiane ile Zawadi ya sh. 200 iliyoahidiwa na leo nakuletea check ya sh. 12/50 ikiwa ni hisa yako katika zile sh.200. Nashukuru sana kwa jitihada ya kufikiri jina la Jamuhuri yetu.

Barua ikasainiwa na Idrisa Abdul Wakil Waziri wa Habari na utalii kipindi hicho.

Sasa kwa nini Mohamedi Iqbal Dar anadai yeye kuwa mshindi pekee wakati barua ilikuwa inaonyesha kulikuwa na washindi wengine 15 ambao nao walishinda?

Jibu ni kuwa wakati wa kutolewa kwa Zawadi hizo hakuna aliyejitokeza zaidi ya Bwana Mohammed Iqbal Dar na Bwana Yusufal Pir Mohamed ambaye hata hivyo alikosa sifa baada ya kushindwa kutoa barua ya kumpongeza kuwa ameshinda kwa madai kuwa Barua ameipoteza, hivyo Wizara ya Habari na Utalii iliamua kumtangaza bwana Mohammed Iqbal Dar kuwa Mshindi na kumpatia zawadi yote ya sh.200/; pamoja na Ngao.

Bwana Mohammedi Iqbal Dar anasema anachosikitika ni kuwa mchango wake bado Watanzania hawathamini mchango wake lakini yeye anaipenda Tanzania na anajivunia kuwa Mtanzania japo anadhani dini yake ya Uislamu ndiyo tatizo hawataki kutambua mchango wake ila anaamini kuwa siku moja ukweli utajulikana.

Hayo ni maelezo ya Mohammed Iqbal Dar ambaye kwa sasa anaishi Uingereza kwa kuwa huko ndiko alipata kazi eneo la Birmigham b35 6ps UK, Dar– es-Salaam House, 18 TURNHOUSE ROAD, PHONE 44 121-747-9822

Nimeona niwatumie hii wadau wangu ili tuweze kuongeza ufahamu na kama ulikuwa unalijua hili basi nimekukumbusha pia mambo yalivyokuwa miaka ya 1964.

Tutumie picha yake na ya nyumba yake na watoto wake, separately, ili tuzihifadhi. Huenda mmoja wetu akapenda kuandika kitabu juu ya historia ya Tanzania tangu Uhuru! Waache hawa Mawaziri wa Habari wakae tu wale rushwa zao badala ya kujali mambo muhimu kwa vizazi vijavyo!
 
Kwanza mjina wenyewe alioubuni ni kama una laana hata yeye alijua katupeleka chaka kwa hilo jina ndiyo maana akakimbia na kubadili kabisa uraia.

Kama angekuwa yeye mwenyewe yupo proud asingekimbia bali angeuishi uvumbuzi alioufanya. Katutia nuksi na hilo jina halafu anatupigia kelele, alitaka apewe nini? Mgodi? Jimbo? Au....?

Acha mambo ya kihuni, si kila mtu hapa ni mvutaji. Umemeza dawa zako leo?
 
Tutumie picha yake na ya nyumba yake na watoto wake, separately, ili tuzihifadhi. Huenda mmoja wetu akapenda kuandika kitabu juu ya historia ya Tanzania tangu Uhuru! Waache hawa Mawaziri wa Habari wakae tu wale rushwa zao badala ya kujali mambo muhimu kwa vizazi vijavyo!

Huyu Iqbal ana bahati sana! Wajua wangejitokeza wote washindi 15 angeambulia Shs.13 na senti 30 tu? Kweli 'early bird catches the worm'!
 
Jina Tanzania limetokana na Takanyika na Nzanzibar. Majina yeto haya yametoka kwa Wasambaa na si mtu yeyote ambaye anataka kudanganya kupata credit.

Yalijiunda yenyewe?..uctumie pua kufikiria na sitaki utokwe na povu ukirudi rudi taratibu
 
Habari wanajf.
Baada ya kusoma habari hii nimeona ni vyema ku share nanyi pia kupata michango yenu juu ya habari hii.

Mwandishi wa habari hizi anaanza kwa kusema:

Historia ya Tanzania haiwezi kukamilika bila kutaja jina la mtu maarufu aliyebuni jina la Tanzania ambaye kwa bahati mbaya au makusudi hakumbukwi tena.
Wengi tunaambiwa kuwa jina la Tanzania lilipendekezwa na Watanganyika na Wazanzibari, na raia wengine wa nje lakini hawatajwi waziwazi na picha zao tukaziona.
Inaaminika kuwa mtu aliyebuni jina la Tanzania ni MOHAMED IQBAL DAR, raia wa India ambaye alikuwa miongoni mwa watu walioshindana katika shindano la kubuni jina la nchi mpya baada ya Tanganyika na Zanzibari kuungana.
Mohamed alizaliwa Mkoani Tanga miaka ya 1944; baba wa Mohamed alikuwa daktari huko mkoani Morogoro akiitwa Dk. T. A DAR aliyefika Tanganyika kuanzia mwaka 1930.

Mohamed Iqbal Dar alipata elimu yake ya msingi mkoani Morogoro katika shule ya H. H D Agakhan ambayo kwa sasa ni mali ya serikali. Alijiunga na Shule ya Sekondari Mzumbe alikosoma kidato cha kwanza na cha sita.

Aliingiaje kwenye shindano la kupendekeza jina la Muungano kati ya Tanganika na Zanzibar?

Mohamed anasema alikuwa maktaba akisoma gazeti la Tanganyika Standard (siku hizi Daily News) akaona tangazo lililowataka wananchi washiriki shindano la kupendekeza jina moja ambalo lingezitaja nchi zote mbili yaani Tanganyika na Zanzibar.
Mohamed anasema alichukua kipande cha karatasi akaanza kwa kuandika jina la Tanganyika ikafuatia Zanzibar, alafu aliandika jina lake Iqbal kisha akaandika jina la jumuia yake Ahmadiya.
Aqbal Dar alichukua helufi tatu kutoka Tanganyika yaani TAN na kwa upande wa Zanzibar akachukua herufi tatu za mwanzo ZAN na kuziunganisha akapata neno TANZAN. Anadai alianza kutafakari na kuona nchi nyingi za Afrika ziliishia na herufi za IA, kama vile Zambia, Tunisia, Namibia, Gambia, Nigeria n.k, hivyo akaamua kuchukua herufi ya kwanza ya jina lake Iqbal yaani I pia akachukua herufi ya kwanza kutoka jila l;a dhehebu lake Ahmadiya yaani A na kuziunganisha akapata jina kamili la TANZANIA, ikiwa limezakiwa kutoka majina ya Tanganyika, Zanzibar, Iqbal na Ahmadiya.

Mohamed Aqbal Dar alituma jina hilo kwenye kamati ya kuratibu shindano, ambapo baada ya muda alipokea barua nzito kutoka serikalini na kusainiwa na Idrisa Abdul Wakil ambaye alikuwa Waziri wa Habari na Utalii wa wakati huo akimjulisha kuwa alikuwa miongoni mwa washindi katika shindano hilo.
Jumla ya washindi 16 walipatikana, ambapo iltakiwa kila mmoja ilibidi apate kiasi cha shilingi 12.50 kwa maana ilikuwa imetengwa shilingi 200 kwa ajili yao.

Mohamed aliibuka kuwa mshindi kwa kuwa wenzake 14 hawakutokea ile siku ya kutolewa zawadi hizo ila alikuwepo mtu mwingine aliyejulikana kwa jina la Yusufal Pir Mohamed ambaye hata hivyo alikosa sifa baada ya kushindwa kutoa barua ya pongezi ya kushinda kwa madai kuwa amepoteza (barua hizo za pongezi walitumiwa kabla ya tukio lenyewe).
Hivyo Wizara ya Habari na Utalii ikaamua kumtangaza Aqbal Dar kuwa mshindi na kumpatia zawadi yote ya sh. 200 pamoja na ngao.

Aqbal Dar anayo masikitiko ya mchango wake kutotambuliwa ingawa anaipenda Tanzania na kujivunia kuwa Mtanzania japo ana asili ya India.

Mohamed Iqbal Dar kwa sasa anaishi Uingereza kwa kuwa huko ndiko alikopata kazi eneo la Birmigham b35 6ps UK, Dar -es-salaam House, 18 TURNHOUSE ROAD, PHONE 44 21-7479822.

Source: Tanzania Daima 16 Februari, 2013.
 
Habari wanajf.

Baada ya kusoma habari hii nimeona ni vyema ku share nanyi hasa wale wanaoujua ukweli huu waweze kunijuza kwa undani.

Mwandishi wa habari hizi anaanza kwa kusema:

Historia ya Tanzania haiwezi kukamilika bila kutaja jina la mtu maarufu aliyebuni jina la Tanzania ambaye kwa bahati mbaya au makusudi hakumbukwi tena.
Wengi tunaambiwa kuwa jina la Tanzania lilipendekezwa na Watanganyika na Wazanzibari, na raia wengine wa nje lakini hawatajwi waziwazi na picha zao tukaziona.
Inaaminika kuwa mtu aliyebuni jina la Tanzania ni MOHAMED IQBAL DAR, raia wa India ambaye alikuwa miongoni mwa watu walioshindana katika shindano la kubuni jina la nchi mpya baada ya Tanganyika na Zanzibari kuungana.
Mohamed alizaliwa Mkoani Tanga miaka ya 1944; baba wa Mohamed alikuwa daktari huko mkoani Morogoro akiitwa Dk. T. A DAR aliyefika Tanganyika kuanzia mwaka 1930.

Mohamed Iqbal Dar alipata elimu yake ya msingi mkoani Morogoro katika shule ya H. H D Agakhan ambayo kwa sasa ni mali ya serikali. Alijiunga na Shule ya Sekondari Mzumbe alikosoma kidato cha kwanza na cha sita.

Aliingiaje kwenye shindano la kupendekeza jina la Muungano kati ya Tanganika na Zanzibar?

Mohamed anasema alikuwa maktaba akisoma gazeti la Tanganyika Standard (siku hizi Daily News) akaona tangazo lililowataka wananchi washiriki shindano la kupendekeza jina moja ambalo lingezitaja nchi zote mbili yaani Tanganyika na Zanzibar.
Mohamed anasema alichukua kipande cha karatasi akaanza kwa kuandika jina la Tanganyika ikafuatia Zanzibar, alafu aliandika jina lake Iqbal kisha akaandika jina la jumuia yake Ahmadiya.
Aqbal Dar alichukua helufi tatu kutoka Tanganyika yaani TAN na kwa upande wa Zanzibar akachukua herufi tatu za mwanzo ZAN na kuziunganisha akapata neno TANZAN. Anadai alianza kutafakari na kuona nchi nyingi za Afrika ziliishia na herufi za IA, kama vile Zambia, Tunisia, Namibia, Gambia, Nigeria n.k, hivyo akaamua kuchukua herufi ya kwanza ya jina lake Iqbal yaani I pia akachukua herufi ya kwanza kutoka jila l;a dhehebu lake Ahmadiya yaani A na kuziunganisha akapata jina kamili la TANZANIA, ikiwa limezakiwa kutoka majina ya Tanganyika, Zanzibar, Iqbal na Ahmadiya.

Mohamed Aqbal Dar alituma jina hilo kwenye kamati ya kuratibu shindano, ambapo baada ya muda alipokea barua nzito kutoka serikalini na kusainiwa na Idrisa Abdul Wakil ambaye alikuwa Waziri wa Habari na Utalii wa wakati huo akimjulisha kuwa alikuwa miongoni mwa washindi katika shindano hilo.
Jumla ya washindi 16 walipatikana, ambapo iltakiwa kila mmoja ilibidi apate kiasi cha shilingi 12.50 kwa maana ilikuwa imetengwa shilingi 200 kwa ajili yao.

Mohamed aliibuka kuwa mshindi kwa kuwa wenzake 14 hawakutokea ile siku ya kutolewa zawadi hizo ila alikuwepo mtu mwingine aliyejulikana kwa jina la Yusufal Pir Mohamed ambaye hata hivyo alikosa sifa baada ya kushindwa kutoa barua ya pongezi ya kushinda kwa madai kuwa amepoteza (barua hizo za pongezi walitumiwa kabla ya tukio lenyewe).
Hivyo Wizara ya Habari na Utalii ikaamua kumtangaza Aqbal Dar kuwa mshindi na kumpatia zawadi yote ya sh. 200 pamoja na ngao.

Aqbal Dar anayo masikitiko ya mchango wake kutotambuliwa ingawa anaipenda Tanzania na kujivunia kuwa Mtanzania japo ana asili ya India.

Mohamed Iqbal Dar kwa sasa anaishi Uingereza kwa kuwa huko ndiko alikopata kazi eneo la Birmigham b35 6ps UK, Dar -es-salaam House, 18 TURNHOUSE ROAD, PHONE 44 21-7479822.

Source: Tanzania Daima 16 Februari, 2013.
 
hii habari ilishawahi kuelezewa hapahapa jf kipindi ha nyuma BTW nice remembrance..
 
Ni kweli ila inawezekana wengine hatukubahatika kuisoma, si unajua jf kila siku inapata watu wapya.
 
Kwa kumbukumbu zangu Mwl Nyerere aliwahi kusema hajui asili ya jina hilo Tanzania; sasa tumwamini nani, Nyerere au Aqbal? Hivyo, anayosema Aqbal ni kweli, au ni usanii. Achapishe hiyo barua ya pongezi iliyosainiwa na Abdulwakil. Na bado tuna MIULIZO, Abdulwakil alikuwa Waziri wa Muungano au wa Zanziba?
 
Mkuu Kyenju, mbona huu uzi upo humu jf! jamani wanajf wenzangu muwe mnatembelea majukwaa tofauti tofouti, nenda kwenye jukwaa la historia utaukuta uzi huu!!!
 
Mkuu Kyenju, mbona huu uzi upo humu jf! jamani wanajf wenzangu muwe mnatembelea majukwaa tofauti tofouti, nenda kwenye jukwaa la historia utaukuta uzi huu!!!

Nikweli mkuu pia nimegundua kitu kimoja, habari nyingine waandishi wanazichota kutoka jf hivyo ni vyema mtu kabla uleta habari yako kwenye jamvi ukatembelea majukwaa yote.
 
Mkuu Kyenju, mbona huu uzi upo humu jf! jamani wanajf wenzangu muwe mnatembelea majukwaa tofauti tofouti, nenda kwenye jukwaa la historia utaukuta uzi huu!!!
Kweli kabisa, mie nilimsikia mdosi huyu akihojiwa na BBC.
 
Wana Jamiiforums,,binafsi naamini jambo lolote kubwa lina sababu.Na kama lina sababu basi nyuma yake kuna mwazilishi wa wazo hilo.

Napenda kujua,,Baada ya Mwl Nyerere kutangaza nia ya kuunganisha visiwa vya Zanzibar na Tanganyika,,je nani alikuja na jina la "TANZANIA"? Je,ni Nyerere mwenyewe? Kama si yeye,ni nani? Aliishi mkoa gani? Kama ni wengi, Nani walikuwa kwenye kamati ya mchujo? JE, wako wapi hadi sasa?

Nikiwa mwananchi wa nchi hii nitafuraji kujua,mengi kuhusu Taifa langu kutoka kwa yeyote mwenye uelewa.
ASANTENI
 
Back
Top Bottom