Asili ya Waislamu wa Masama, Hai Kilimanjaro ni wapi?

Asili ya Waislamu wa Masama, Hai Kilimanjaro ni wapi?

Nenda oman mkuu, utakutana na waarab weusi tena wana kipilipili kama wewe, halafu vp kuhusu hawa machotara wa kiarabu na kiswahili waliopo uku? Tafakari usikurupuke
Mkuu hapo UMEDANGANYA HASWA
Toka lini Oman kukawa na Waswahili, hebu nitajie hata Sheia (Balozi ) aliyechaguliwa katika Nchi hiyo ya Oman
Tafuta tafsiri ya neno PUNDA HAPANDI MUSCAT


Ndipo uje na jibu la kutueleza eti hata huku kuna Machotara wa Kiarabu
Hawa Machotara wote unaowaona km wana asili ya Oman basi Mama ni muafrika Baba ndio MuOman au Saudi Arabi au UAE 9ni marufuku kwa Binti wa kiarabu kuzaa na nyani toka afrika)fuatilia kisa cha tajiri wa Home Shopping Center ndio utajua udhalimu wenu kwa ubaguzi.
ungeniambia WaYemen (WaKoja) au Wasomali kidogo
 
Asili ya Uislamu katika eneo la Masama hasa Mudio, ni Wazee (ambao walikuwa vijana miaka hiyo) kwenda kufanya kazi Mombasa. Waliporudi, walikuja na Imani hiyo mpya.
Pia walirudi na aina fulani ya mabati ya kuezeka nyumba yanayofanana na madebe. Nyumba nyiiingi uchaggani, hasa Wilaya ya Hai ziliezekwa kwa mabati hayo. Yalitoka Mombasa.
 
lazima mwarabu atakuwa alipita hapo, ngoja niingie maktaba nitarudi hapo maana nataka kujifunza na baadhi ya wahaya nao walipata wapi mapokeo ya uislamu.

Ukikuta Mhaya Muislam ujue hao walihamia kutokea Uganda.... Waislam ni watu wa pwani huko bara wanasingiziwa tu...
 
Wakuu, Kwa wale wanaoifahamu Jiografia ya Mkoa wa Kilimanjaro,
Kunasehemu moja inaitwa Masama iko wilaya ya Hai, hili eneo limekaliwa na Waislamu kadhaa tena wale wenye misimamo ya wastani. ni nini asili yao?
Hata kisiasa ni watu wapenda mabadiliko..
Ni chimbuko la kina Former I GP Said Mwema.
Yeah ni kweli mkuu, nimeishi masama few years ago kwa ndugu zangu ni waislam,
Ila wilaya ya Hai ndo inaongoza kuwa na waislam hata wachaga wamachame pia nao wengi ni muslim.
Tembosa uzi huu ni mpana zaidi lakini kwa asili ya Waislamu wa maeneo ya Masama na Sanya juu, ujio wao ni tofauti na ule wa maeneo ya Pwani wakaingia Bagamoyo na Kondoa hawa ni WamaHra na Wakoja kutoka Oman, Yemen na Falme za Kiarabu (na hata walivyo ni wababe na wakali kwa kila kitu)

Wale Waislamu wa maeneo ya kuanzia Masama na kuendelea chanzo chao ni Somalia baada ya Vita ya kwanza WW1 Nchi hiyo ilikuwa iitawaliwa na Italia hivyo Koloni hilo liliposambatatishwa Wapiganaji wake wakaletwa Kijiji cha Kware na Askari wengine wa Kisomali wakapelekwa Tabora
Kwa hiyo asili ya Waislamu wa Kware ambao walikuwa ni wanaume wakachanganyika na wakaoa na kuiendeleza Dini hiyo hata Sura na maumbo yao ni tofauti na Waislamu wa maeneo mengine
Labda swali lipo tofauti na ninavyojua Tembosa ulivyouliza nitaitafuta hii story ktk Wikipedia
 
Last edited by a moderator:
Mada imetaliwa na ushabiki wa kidini kiasi cha kuwafanya watu wapeleke akili zao likizo kiasi cha kushindwa kuchambua mambo kwa kina! Mathalani kuna wengi tu humu wanadai eti Waarabu hawakujenga shule Tanzania wakati Wazungu walifanya hivyo! Kwavile tumepeleka akili zetu likizo tunashindwa kufahamu kwamba malengo ya Mwarabu na Mzungu yalikuwa tofauti kabisa, hususani huku bara kwahiyo kusema Mwarabu hakujenga shule ni kuonesha kwamba wala hatuifahamu historia!!!

Tofauti na Wazungu ambao walikuja kama Watawala, Waarabu wao walikuja kama wasaka noti! Wazungu hawakujemga mashule kwa kutupenda bali kwa kuwa walikuwa ni watawala, walihitaji labor force inayofahamu ABC ya mfumo wao kule walikotoka! Wazungu hawa walihitaji kuwa na makarani, manyapara n.k kwahiyo suala la kujenga shule lilikuwa inevitable. In contrast, Mwarabu hakuwa na shida hiyo coz' yeye kaja kutafuta noti, BASI! Sasa mlitarajia ajenge mashule kisha hao wahitimu awapeleke wapi wakati hakuwa na serikali? Wakamsaidie kudaka watumwa, au?

Labda hapa tuseme Sultan wa Zanzibar ambae kabla ya ujaji wa wakoloni, yeye alikuwa mtawala kule! Lakini hata hivyo, si kwamba hakutoa elimu moja kwa moja bali alitoa elimu inayolingana na mazingira ya kule anakotoka! Asingeweza kufundisha kiingereza wakati alikotoka wanaongea Kiarabu! Asingeweza kufundisha elimu ya kizungu wakati alikotoka elimu yao ilikuwa ni ya Kiarabu! Kwa bahati mbaya sana, baada ya kuja Wakoloni wa Kijerumani na Kiingereza ambao sasa wakawa ndio watawala sio tu wa Tanganyika bali hata Zanzibar, elimu ile ya Sultan ikaonekana haina maana tena kwavile ni tofauti kwa kila nyanja na elimu ya watawala wapya! Kwahiyo hata wale ambao walikuwa wanafahamu kusoma na kuandika kwa lugha ya Kiarabu kwa ufasaha kabisa, wakaja kuambiwa hawajui kusoma wala kuandika coz' Kiarabu kikawa not applicable any more! Kwa mfano nakumbuka Babu yangu alikuwa hawezi kuandika hata mama lakini kwenye Kiarabu alikuwa anatiririka katika kusoma na kuandika kama ambavyo ninavyotiririka kwenye kusoma na kuandika Kiswahili leo hii! Hata hivyo, huyu babu yangu nae alikuwa kwenye kundi la wasiojua kusoma na kuandika ingawaje ukweli ni kwamba alikuwa hajui kusoma na kuandika Kiswahili na Kiingereza! Ni sawa sawa na leo hii ije Uturuki halafu ifute mfumo wa sasa wa elimu kisha wa-introduce wa kwao ambao utatumia Kituruki na mfumo wa sasa kuzikwa kabisa... hapa maana yake ni kwamba, karibu Watanzania wote tutageuka kuwa tusiojua kusoma na kuandika!!!!!

Kama nilivyosema, Mzungu alipokuja akalazimika kujenga mashule ili apate wafanyakazi wanaofahamu ABC! Lakini kwa bahati mbaya, Waarabu tayari walikuwa wameshaweka mizizi yao ya kufahamiana na Wenyeji... sina hakika, lakini bila shaka Waarabu hawa wakawa wanamwaga sumu kwa wenyeji wao kwamba elimu ya hao jamaa itawaingiza motoni, mkienda kule mtalishwa nguruwe! Ama sumu hizi walimwaga wenyewe au kwa kutumia vibaraka wao!

Sasa basi, ikiwa leo hii watu wameshaelimika bado unaweza kukuta Mkristo anashindwa kumpeleka mwanae shule ya Kiislamu kwavile tu ni shule ya Kiislamu na Muislamu hawezi kumpeleka mwanae shule ya Kikristo kwavile tu ni shule ya Kikristo; sasa unatarajia nini kwa wazee wa enzi ambayo dunia ilikuwa haijaelimika vya kutosha! Kwahiyo mtu kumdhihaki Babu yangu kwamba hakusoma ni kuonesha namna gani usivyoweza kuyachambua kimantiki mazingira yaliyokuzunguka!!

Kwa upande mwingine, Wazungu wengi walifikia mikoa ya bara kabisa! Na ingawaje humu jamvini kuna vilaza wanaopenda kukashifu watu wa pwani kwamba hawajasoma, lakini ukweli ni kwamba hata huko bara, walikosoma ni mikoa ile ile ambako Wazungu walifikia!!! Sasa basi, ikiwa hadi miaka ya tisini, mtu alikuwa anatumia mwezi mmoja kutoka Lindi hadi Dar es salaam, hivi kweli ulitarajia Babu yangu aliyeko kijijini huko Lindi angefahamu kwamba kuna shule inaitwa Umbwe, Uru, Mirambo n.k?! Did you expect that Great Thinkers wa JF? Ikiwa mtu alikuwa anaishi Chalinze na Dar es salaam haijui, ulitarajia mtu kama huyo afahamu kwamba kuna sehemu inaitwa Machame na huko kuna mashule?

Lakini yote kwa yote, tuache ujinga kidogo! Hivi kweli nchi kuna watu wanaweza wakajigamba kabisa kifua mbele kusema kwamba "kwetu matajiri... kwetu tumesoma!" Wanamaliza kidato cha nne wanafunzi laki 4, kati yao wanaopata division one hawafiki hata 5000 lakini wanaopata zero na four wana-constitute more than 75%!!! Hivi kweli wale ni Waislamu peke yao? Ina maana nchi hii ina-recruit wanafunzi wa Kiislamu zaidi ya 75% kuingia sekondari na Wakristo ni less than 75%? AMA KWELI, AKILI NI NYWELE!!!
 
Tembosa uzi huu ni mpana zaidi lakini kwa asili ya Waislamu wa maeneo ya Masama na Sanya juu, ujio wao ni tofauti na ule wa maeneo ya Pwani wakaingia Bagamoyo na Kondoa hawa ni WamaHra na Wakoja kutoka Oman, Yemen na Falme za Kiarabu (na hata walivyo ni wababe na wakali kwa kila kitu)

Wale Waislamu wa maeneo ya kuanzia Masama na kuendelea chanzo chao ni Somalia baada ya Vita ya kwanza WW1 Nchi hiyo ilikuwa iitawaliwa na Italia hivyo Koloni hilo liliposambatatishwa Wapiganaji wake wakaletwa Kijiji cha Kware na Askari wengine wa Kisomali wakapelekwa Tabora
Kwa hiyo asili ya Waislamu wa Kware ambao walikuwa ni wanaume wakachanganyika na wakaoa na kuiendeleza Dini hiyo hata Sura na maumbo yao ni tofauti na Waislamu wa maeneo mengine
Labda swali lipo tofauti na ninavyojua Tembosa ulivyouliza nitaitafuta hii story ktk Wikipedia

walipelekwa Kware sehemu gani Ndugu? Hatujaona masalia yao pale kwa maana ya sura zenye asili ya Somalia. Labda kina Masoud, Kadria na Shete
 
Last edited by a moderator:
Tembosa uzi huu ni mpana zaidi lakini kwa asili ya Waislamu wa maeneo ya Masama na Sanya juu, ujio wao ni tofauti na ule wa maeneo ya Pwani wakaingia Bagamoyo na Kondoa hawa ni WamaHra na Wakoja kutoka Oman, Yemen na Falme za Kiarabu (na hata walivyo ni wababe na wakali kwa kila kitu)

Wale Waislamu wa maeneo ya kuanzia Masama na kuendelea chanzo chao ni Somalia baada ya Vita ya kwanza WW1 Nchi hiyo ilikuwa iitawaliwa na Italia hivyo Koloni hilo liliposambatatishwa Wapiganaji wake wakaletwa Kijiji cha Kware na Askari wengine wa Kisomali wakapelekwa Tabora
Kwa hiyo asili ya Waislamu wa Kware ambao walikuwa ni wanaume wakachanganyika na wakaoa na kuiendeleza Dini hiyo hata Sura na maumbo yao ni tofauti na Waislamu wa maeneo mengine
Labda swali lipo tofauti na ninavyojua Tembosa ulivyouliza nitaitafuta hii story ktk Wikipedia

Mbona hakuna masalia yao kule mkuu tofauti na Tabora unakosema kule Wasomali ni wengi mpaka leo...
 
Last edited by a moderator:
Mkuu kwa mujibu ya maandiko ya uislam...umepasi kuwekwa katika kundi la Makafiri i.e Yaani mkuu waislamu kutokua na time na dini yao au kua misimamo ya wastani(kufata maadhi ya mambo na kuacha baadhi yake) kwako wewe ndo inakua safi sana?....Pole sana Moyo utazidi kukuuma...
 
walipelekwa Kware sehemu gani
Ndugu? Hatujaona masalia yao pale kwa maana ya sura zenye asili ya
Somalia. Labda kina Masoud, Kadria na Shete

watu wa kware wengi wana asili ya sudani kusini
 
watu wa kware wengi wana asili ya sudani kusini

Hilo naliamini lkn si la Somalia.
Kulikuwa na usemi miaka ile ya 80's kwamba hao wenye asili ya Sudan Kusini wanaudugu na Idd Amin. Na eti aliwahi kuja Kware kusalimia
 
saa nyingine hapa ndugu ndio huwa kidogo mnapitiwa, misikiti yakutosha maana yake ni nini?

pale moshi maeneo ya rau kuna msikiti mkubwa lakini wanaswali waislamu 6 tu miaka nenda rudi, ndio maana kule angola misikiti imebomolewa si kwa sababu za kidini bali haina kazi na watu wanahitaji maeneo wayafanyie kazi.
Ni kweli mkuu, kuna watu wana kampeni ya kujenga misikiti mingi along the main roads na highways nyingi ili kuwafurahisha wafadhili wao, lakini matokeo yake ni kwamba inahudhuriwa na watu sita !
 
Tembosa uzi huu ni mpana zaidi lakini kwa asili ya Waislamu wa maeneo ya Masama na Sanya juu, ujio wao ni tofauti na ule wa maeneo ya Pwani wakaingia Bagamoyo na Kondoa hawa ni WamaHra na Wakoja kutoka Oman, Yemen na Falme za Kiarabu (na hata walivyo ni wababe na wakali kwa kila kitu)

Wale Waislamu wa maeneo ya kuanzia Masama na kuendelea chanzo chao ni Somalia baada ya Vita ya kwanza WW1 Nchi hiyo ilikuwa iitawaliwa na Italia hivyo Koloni hilo liliposambatatishwa Wapiganaji wake wakaletwa Kijiji cha Kware na Askari wengine wa Kisomali wakapelekwa Tabora
Kwa hiyo asili ya Waislamu wa Kware ambao walikuwa ni wanaume wakachanganyika na wakaoa na kuiendeleza Dini hiyo hata Sura na maumbo yao ni tofauti na Waislamu wa maeneo mengine
Labda swali lipo tofauti na ninavyojua Tembosa ulivyouliza nitaitafuta hii story ktk Wikipedia

mkuu naona umeitaja Historia kwa Undani kidogo,
hapo Kware mbona sio Masama? Kware hakuna Uislam kama ilivyo Masama mudio au pale Kwasadala.

Pili kama asili yake ni Somalia, mbona wanamajina ya koo zao yanaendana na uchagga? mf. kina Kiriwe, huu ni ukoo wa wachaga wanaoamini katika Uislamu.
 
Last edited by a moderator:
Asili ya Uislamu katika eneo la Masama hasa Mudio, ni Wazee (ambao walikuwa vijana miaka hiyo) kwenda kufanya kazi Mombasa. Waliporudi, walikuja na Imani hiyo mpya.
Pia walirudi na aina fulani ya mabati ya kuezeka nyumba yanayofanana na madebe. Nyumba nyiiingi uchaggani, hasa Wilaya ya Hai ziliezekwa kwa mabati hayo. Yalitoka Mombasa.

this can possible wemba..
asante sana.
 
Wachaga kwa longo longo hawajambo! Mara Waislamu wa kilimanjaro ni vijana waliotoka mombasa, mara Wasomali! Tangu lini Msomali akaitwa Juma Massawe? Tangu lini Msomali aitwe Kimario? Nimeshawàambia, Chief wenu Mangi Meli alikuwa anapiga dili za kuuza watumwa na tajiri yake alikuwa mwarabu aliyeitwa Hassan! Ni haya madili ya Mangi ndyo yalipeleka Uislam Uparen coz' mshikaji aliingiza Wapare kibao sokoni! Najua mnaona noma kuckia Chief wenu alikuwa anapiga dili za watumwa but ndo ukweli wenyewe!
 
kama asili yake ni Somalia, mbona wanamajina ya koo zao yanaendana na uchagga? mf. kina Kiriwe, huu ni ukoo wa wachaga wanaoamini katika Uislamu.
umeuliza swali la msingi-kama ni wasomali why wawe na majina ya kichaga! mkùu, amin maneno yangu, as it was 4 other Chiefs, Mangi Meli nae alipiga sana dili za kùuza watumwa! Ni hizi deal za Mangi ndizo ziliingiza Uislam Uparen coz' Wapare wengi aliwaingiza sokon! so, hawa Wachaga nadhan ni wa kutoka koo hasimu na ukoo wa Mangi
 
umeuliza swali la msingi-kama ni wasomali why wawe na majina ya kichaga! mkùu, amin maneno yangu, as it was 4 other Chiefs, Mangi Meli nae alipiga sana dili za kùuza watumwa! Ni hizi deal za Mangi ndizo ziliingiza Uislam Uparen coz' Wapare wengi aliwaingiza sokon! so, hawa Wachaga nadhan ni wa kutoka koo hasimu na ukoo wa Mangi

huyo bwana Hasani ni wa muda wote? means Mangi na Hassan ndiyo walifanya hiyo biashara walipotoka ikawa akuna tena mwendelezo?
nimeuliza hivyo kwa sababu na wewe umespecify .
 
Kama wapo wakuhamia labda kama wale wa masama..

wapo wapi? kibosho sehemu gani yenye waislamu?
Kwa nini useme hao wa masama ni wa kuhamia?
Vipi na wale wengi waliopo pale Kwa Sadala?
nimekuuliza hivyo baada yakuona maelezo yako hapo juu.
ni kama unaijua Kilimanjaro.
 
Back
Top Bottom