Asilimia 60 ya maafa ya mafuriko Dar es Salaam yanatokana na uzembe wa serikali, Raisi Samia akubali ukweli huu

Asilimia 60 ya maafa ya mafuriko Dar es Salaam yanatokana na uzembe wa serikali, Raisi Samia akubali ukweli huu

Mleta mara mwehu Tena Unakuta msomi kabisa kajenga mabondeni bonde la msimbazi au kando ya mito kibao au eneo la mabonde na hati Hana Wala hakuna wa kumpa hati mafuriko yakitokea anaongea kingereza ITV utafikiri ITV ni TV ya BBC kingereza
Kama ungeelewa mambo, ungejua kuwa athari za mafuriko hazijawakumba walio mambondeni tu. Hii mada si kwa ajili ya watu walio mambondeni, ni kwa ajili ya mfumo wa mtititiko wa maji kwenda baharini bila kuharibu miundombinu.

Hayo madaraja yaliyobomolewa, ni kwa sababu serikali imeyajenga bondeni?
 
Sometimes hii nch tunalaumu mno serikali,
Watu wanajenga kwenye mikondo ya maji, wengine hadi wanatoa rushwa ili wajenge, then yakija mafuriko wanakimbilia kusema serikali, hahah
Dodoma, ukijenga ukuta wa fence, bila kibali, haipiti siku mbili,lazima maofisa wa jiji, watafika kubomoa,hulka ya binadamu, ni kuvunja sheria, ndio maana serikali ipo,kusimamia sheria,
Watu wapo wanakula mishahara kwanini hawafatilii wanaovunja sheria za, ujenzi, nchi imeoza.
Huku Afrika, ni aibu tupu
 
Serikali ni watu kama ulivyo wewe, hivyo si kila kitu lazima usubiri mwongozo wa binadamu mwenzio ili uchukue hatua.


Janga unaliona hilo linakuja, unasubiri nini kuchukua hatua kwa ajili ya usalama wako mwenyewe?

Tusipende kulaumu kila kitu, hakuna namna nyingine zaidi ya kuhama ili kuwa salama wewe na mali zako.

Watu wamegoma kuhama pamoja na kuhamasishwa wahame, sasa unataka nani aache kuhangaika na maisha ya familia yake aje ahangaikie familia za wengine?.


Miaka nenda rudi wimbo ni uleule ikifika msimu wa mvua, kwani nyie ni kenge kuwa hamsikii hadi damu iwatoke masikioni?.

Endeleeni kupambana na hiyo hali ya kujitakia.
Hivi hizi mvua zimeathiri walio mambondeni tu? Mie naongelea mpandilio wa drainage ya Dar baada ya hizi mvua kuathiri walio na wasio mabondeni. Ndio maana Bibi yule Faiza, anawauliza mlienda shule gani hata post hamuwezi kusoma mkaelewa kabla ya kujibu??
 
Mleta mara mwehu Tena Unakuta msomi kabisa kajenga mabondeni bonde la msimbazi au kando ya mito kibao au eneo la mabonde na hati Hana Wala hakuna wa kumpa hati mafuriko yakitokea anaongea kingereza ITV utafikiri ITV ni TV ya BBC kingereza
Soma uelewe, ulienda shule gani? Mada haiongelei kujenga mabondeni, bali drainage ya Dar es Salaam
 
Kupanga miji tu shida,
South Korea wamezindua Air tax, UAM, urban air mobility tex,
Hizi, ni ndege ndogo kama kama drones, zinabeba watu, Zita kuwa kama tex mjini,
Dunia ipo mbaaaali sana. Huku kwetu, mi ccm, ni kama imeoza, u bongo, kilimo shida, elimu hovyo, dunia inafanya vitu vikubwa, huku kwetu, unakuta watu wanakusnyika kumsikiliza, Makonda, anapigia mawaziri simu! Kama, vile ni kitu cha maaana, sana!
 
Nilikua na wazo kama hiyo point yako namba mbili.

Serikali iangalie namna ya kutendeka mifumo ya kukusanya maji na kuyapeleka baharini.
 
Hameni, acheni kuongea kwa sauti.


Suluhisho ni moja tu, KUHAMA au kubaki kusubiri maafa zaidi.
Siku zote mchuma janga hula na wakwao.
Daraja la kunduchi limebomoka. Kwa hiyo unasgai watu waishio Kunduchi wahame? Hivi mmesoma kweli nyie? Unaelewa thread inaongea juu ya nini? Au unamaanisha watu wote Dar wahame?

1705858906678.png
 
Pale jangwani mvua kidogo unakuta magred yanatoa tope kila mwaka wameridhika ...Ile barabara kutokea magomeni hata uendeshe gari unaona kabisa unashuka kama kweny shimo.


Wanashindwa vip pale kujaza enzi za kutengeneza kituo cha mwendo kasi pale level mpaka mapipa hapa
 
Tatizo ni wanasiasa maana wao ndo huonea watu huruma kisa Kura.

Ilitakiwa watu wote ambao wapo kando ya mito waondolewe kwa umbali wa 60m
 
Dar es salaam yote inatakiwa isombwe na maji ibaki nyeupe Kama jangwa la Sahara. Mji gani haujapangiliwa vizuri sio masaki wa obey Wala tandale kote nyumba zimerundikana Kama taka ndani ya dustbin.wacha isombwe tu tumewachoka watu wa dar kwa kulia lia
 
Mfano pale Tegeta waathirika wote wamefata mto wenyewe na serikali imeona bora imuache akae hapo tu mto utamuondoa
 
Sometimes hii nch tunalaumu mno serikali,
Watu wanajenga kwenye mikondo ya maji, wengine hadi wanatoa rushwa ili wajenge, then yakija mafuriko wanakimbilia kusema serikali, hahah
Mnatoaje kibali cha ujenzi kwenye bonde?
 
Ni kweli maafa ya mafuriko yanaitwa natural disasters, lakini sio lazima natural disasters zilete maafa kwa raia na mali zao.

Asilimia 60 ya maafa ya mafuriko Dar es Salaam yanatokana na uzembe, ubinafsi, kutojali, na uongozi mbovu kwa ujumla wa viongozi wa serikali. Si mara ya kwanza Dar es Salaam inapata mafuriko. Ni zaidi ya miaka 20 tunaishi kwa kudhani kwamba tatizo la mafuriko Dar dawa yake ni kumwomba Mungu atuepushe na vifo na upotevu wa mali, kutia ndani uharibifu wa miundombinu.

Mji wowote ulio pembezoni mwa bahari kuwa na tatizo la mafuriko yanayotokana na mvua kwa zaidi ya miaka 20 hakuna kingine zaidi ya uzembe. Serikali yetu imejisahau mno, hasa wakijua Watanzania sio rahisi kuiondoa serikali iliyopo madarakani kwa kuwa tu inafanya uzembe, ufisadi, ubinafsi nk. Kwa hiyo wanajisahau sana.

Tatizo la mafuriko linahitaji suluhisho ambalo gharama yake huenda hata isifikie gharama ya kununua ndege mbili za dreamliner, au pesa tunayolipa makampuni yanayotushitaki kukiuka mikataba.
  1. Wakusanye wataalamu wa physical geography watengeneze topographical na contour maps za Dar es Salaam na ukanda wa pwani, wakionyesha ilikupata elevation na terrain ya ukanda wote wa Dar na contour lines zinavyokwenda
  2. Kwa kutumia topographical map na contour lines, wakusanye civil engineers wachore line kupitisha maji kwa kutumia channel za ukubwa wa kiasi na kupeleka kwenye channel kubwa ambazo zitaelekeza maji baharini
Sasa, katika kufanya design ya channel za maji, factor of safety isiwe tena historical data, bali iwe projection iliyo informed na modeling za climate change impact scenarios katika masuala ya mvua, na ipigwe factor kubwa zaidi ya standard factors (najua mainjinia tu ndio wataelewa hii paragraph)

Ikibidi, baadhi ya majengo itabidi yaondoke, yabomolewe, hata kama ni mazuri kiasi gani.
View attachment 2878486
Ninatamani sana nimpigie Samia simu nimwambia nipe hii kazi nisimamie huu mkakati. Raisi Samia nakuhakikishia kwamba mji wowote uliopo kando ya bahari haupaswi kuwa na mafuriko kama tunayoona Dar. Au mwambie Prof. Tibaijuka asimamie hili.

Tatizo lililop kwako Samia ni kuteua watu ambao wanaona kipao mbele cha Dar ni kushughulika na changudoa na maandamano ya Chadema badala ya matatizo yanayoathiri wananchi na taifa kwa ujumla kwa kiwango cha juu sana. Unapewa sifa kila siku katika mambo ambayo ni routine sana, usiridhike au kudanganywa na hizo sifa. Kutoa hela za kujenga Zahanati na nini sijui sio sifa za kuwa raisi mzuri. Kwanza wengine tunaona hilo ni uongozi mbovu tu, kwa sababau pesa hizo zinapaswa kutolewa kupitia mipango ya maendeleo na bajeti za maeneo hayo. Kwa nini unakubali kuleweshwa na sifa za mambo yanayotakiwa kufanywa na wakuu wa mikoa na wakurgenzi wa miji na majiji? Fanya kazi za kitaifa tukusifie, sio mambo ya vijijini, wilayani na mikoani. Hiyo sio ligi yako.

Bado hatuoni unayofanya katika mambo makubwa ambayo yataacha legacy yako, pamoja na hili la mafuriko Dar. Japo tunaelewa ni suala la majiji haya matatu, Ilala, Kindondoni na Temeke, lakini lichukue sura ya kitaifa ili kuwe na coordination rahisi.
Wewe kajamaaa mtu wa lawama tu January 05.2024 London mji mzuri umapangwa ukapangika mito imepigwa hadi sakafu na kingo zinakuta ila tu nayo imeflood all river zimeoverflow ndio maana ya natural disaster panga upangavyo ila zikija ndio inakuwa hivyo.
 
Ni kweli maafa ya mafuriko yanaitwa natural disasters, lakini sio lazima natural disasters zilete maafa kwa raia na mali zao.

Asilimia 60 ya maafa ya mafuriko Dar es Salaam yanatokana na uzembe, ubinafsi, kutojali, na uongozi mbovu kwa ujumla wa viongozi wa serikali. Si mara ya kwanza Dar es Salaam inapata mafuriko. Ni zaidi ya miaka 20 tunaishi kwa kudhani kwamba tatizo la mafuriko Dar dawa yake ni kumwomba Mungu atuepushe na vifo na upotevu wa mali, kutia ndani uharibifu wa miundombinu.

Mji wowote ulio pembezoni mwa bahari kuwa na tatizo la mafuriko yanayotokana na mvua kwa zaidi ya miaka 20 hakuna kingine zaidi ya uzembe. Serikali yetu imejisahau mno, hasa wakijua Watanzania sio rahisi kuiondoa serikali iliyopo madarakani kwa kuwa tu inafanya uzembe, ufisadi, ubinafsi nk. Kwa hiyo wanajisahau sana.

Tatizo la mafuriko linahitaji suluhisho ambalo gharama yake huenda hata isifikie gharama ya kununua ndege mbili za dreamliner, au pesa tunayolipa makampuni yanayotushitaki kukiuka mikataba.
  1. Wakusanye wataalamu wa physical geography watengeneze topographical na contour maps za Dar es Salaam na ukanda wa pwani, wakionyesha ilikupata elevation na terrain ya ukanda wote wa Dar na contour lines zinavyokwenda
  2. Kwa kutumia topographical map na contour lines, wakusanye civil engineers wachore line kupitisha maji kwa kutumia channel za ukubwa wa kiasi na kupeleka kwenye channel kubwa ambazo zitaelekeza maji baharini
Sasa, katika kufanya design ya channel za maji, factor of safety isiwe tena historical data, bali iwe projection iliyo informed na modeling za climate change impact scenarios katika masuala ya mvua, na ipigwe factor kubwa zaidi ya standard factors (najua mainjinia tu ndio wataelewa hii paragraph)

Ikibidi, baadhi ya majengo itabidi yaondoke, yabomolewe, hata kama ni mazuri kiasi gani.
View attachment 2878486
Ninatamani sana nimpigie Samia simu nimwambia nipe hii kazi nisimamie huu mkakati. Raisi Samia nakuhakikishia kwamba mji wowote uliopo kando ya bahari haupaswi kuwa na mafuriko kama tunayoona Dar. Au mwambie Prof. Tibaijuka asimamie hili.

Tatizo lililop kwako Samia ni kuteua watu ambao wanaona kipao mbele cha Dar ni kushughulika na changudoa na maandamano ya Chadema badala ya matatizo yanayoathiri wananchi na taifa kwa ujumla kwa kiwango cha juu sana. Unapewa sifa kila siku katika mambo ambayo ni routine sana, usiridhike au kudanganywa na hizo sifa. Kutoa hela za kujenga Zahanati na nini sijui sio sifa za kuwa raisi mzuri. Kwanza wengine tunaona hilo ni uongozi mbovu tu, kwa sababau pesa hizo zinapaswa kutolewa kupitia mipango ya maendeleo na bajeti za maeneo hayo. Kwa nini unakubali kuleweshwa na sifa za mambo yanayotakiwa kufanywa na wakuu wa mikoa na wakurgenzi wa miji na majiji? Fanya kazi za kitaifa tukusifie, sio mambo ya vijijini, wilayani na mikoani. Hiyo sio ligi yako.

Bado hatuoni unayofanya katika mambo makubwa ambayo yataacha legacy yako, pamoja na hili la mafuriko Dar. Japo tunaelewa ni suala la majiji haya matatu, Ilala, Kindondoni na Temeke, lakini lichukue sura ya kitaifa ili kuwe na coordination rahisi.
Well analysed and presented kudos to you fella tatizo nchi hii viongozi wana macho lakini hawaoni na wana masikio lakini hawasikii
 
Back
Top Bottom