Asiyoyajua Yericko Nyerere katika utafiti wa historia ya Mapinduzi ya Zanzibar

Narudia tena mzee Mohamed acha unafiki, ukiwa mzee unafiki ni uchawi.....

Wasomaji gani waliokufuata wewe wakakulalamikia juu ya kitabu changu?

Narudia tena, Mohamed hujakisoma kitabu changu, ili uweze kujadili jambo lilolote toka kitabuni ni vema ukakisoma na kuacha chuki za kipuuzi zisizo na maana....
 
Yericko,
Kuwa na subira unapojadili jambo.

Ungekuwa na subira na kuniuliza usingetumia lugha hiyo kali ya "utoto," nk.

Mimi sijasoma kitabu chako lakini hayo niliyonakili wewe mwenyewe umesema ni kutoka katika kitabu chako.

Ikiwa haya ni tofauti na yaliyomo katika kitabu chako hili halina shida kwangu ni kueleza tu tukajua.
 
Unapotosha na kunilisha maneno mzee, hakuna mahali katika kitabu changu chote cha kurasa 715 paliposemwa kwamba TANU iliundwa na Kanisa Katoliki, kinachohusishwa na kanisa katoliki ambacho ndicho nimekifanyia utafiti kwa ushahidi wa nyaraka ni Kanisa Katoliki kumwibua Nyerere, kumlea na kusimamia Uhuru wa Tanganyika.

Hayo mengine porojo zako peleka kariakoo na magomeni
 
Unaitambua subira sasa? Kwanini hukuwa na subira ukakisoma kitabu kwanza kuliko kukurupuka na kuja kunitusi na kunidhihaki hapa kwa kuanzisha uzi huu? Ulijua sitakuja kujitete na kujibu hoja zako na viroja vyako mzee?

Nasisitiza mzee acha unafiki, uzandiki na uongo.... Huo ni uchawi mbaya....
 
Yericko,
Unanitukana ilhali mimi nakisema kile ninachoona katika uandishi wako.

Hii si haki.

Mimi sijavutiwa na uandishi wako ndiyo maana sijasoma kitabu chako.

Haya niliyosoma hapa JF yamenitosha.
Mimi ni publisher, mhariri, mtafiti, broadcaster, public speaker, mfasiri na mwandishi niaijua biashara ya vitabu na yote yanayohusiana na tasnia hii.

Kitabu kikiwa cha maana utaona haijifichi.

Sijui kama kitabu chako kimeshapata review yoyote katika gazeti sisemi kwenye academic journals.

Wala sijui kama umepata wewe mwenyewe kukizungumza popote hadharani ukiacha huu uwanja wetu wa JF ambao ni wetu sote.

Mwisho jifunze maana ya neno, "unafiki."
 
Baba yangu nimesema tokea mwanzoni kabisa kwamba una chuki binafsi na Yericko.

Na nilisema tumia taaluma yako vema ili kuwafanya waandishi wengine vijana wasifanye makosa unayoyaonyesha na kama aliyoyafanya Yericko ..anzisha darasa tujifunze lkn hiki unachokifanya sicho.

Amekujibu vema kila hoja uliyoleta lkn kila jibu unaligeuza swali au unazalisha maswali yasiyoisha.

Kumbe sasa hivi unakiri kwamba hicho kitabu haujakisoma na unasema haukisomi kwa kua aliendika Yericko,sasa unajipa shida ya nini baba yangu?
.Kama haujakisoma hii haki ya kukosoa na kumshambulia mtu personal unaitoa wapi?
Unachukua nukta nukta unazichambua kwamba hicho ni kitabu.
Mzee jitendee haki wewe mwenyewe,itendee haki taaluma yako na mtendee haki unae mshambulia.

Nilisema, soma kitabu chake fanya uchambuzi wa kina ulete ili sote tufaidike lkn unaleta blaablaa nyingi hapa na kujisifu "Mm Editor,mm publisher,mm speaker n.k hivyo vyote havina maana endapo hautovitumia ipasavyo kama ufanyavyo hapa.

Sasa hivi unalalamika anakutukana ulitaka afanye nini zaidi ya hapo.Uvumilivu una kikomo chake na hasa kwa kua huu si mjadala bali ni shambulio.

Hakuna asiejua kwamba ww unajua lkn unaona bado haitoshi,ukiaga unaenda library basi unarudi na sifa ulizotunukiwa,mara ulete fax ya Prof. Mazrui,mara ulete picha ulizopiga Oman sijui na nani,mara sijui kitabu kilisifiwa wapi.Hata Uislam unakataza "RIIIYA" (Kufanya kitu kwa nia ya kutafuta sifa,ili watu wakuone unajua).

Fanya makubwa kuliko unalofanya hapa.
 
Ridhiwani,
Unaweza kusema unachopenda kuhusu mimi.

Wala hayo usemayo hayamo katika riya unaweza kufanya rejea katika Riyadh Salihin ukipenda.

Vielelezo ni muhimu na naviweka siku zote kukazia hoja ingawa najua vinawachoma wengi.

Oman picha ile na Dr. Harith Ghassany mwandishi wa Kwaheri Ukoloni Kwaheri Uhuru naamini unakijua kitabu hiki.

Mimi Yericko kaniita mwenyewe kwa kunitaja katika historia ya TANU na Mapinduzi ya Zanzibar.

Sikuwa najua kama wewe unajua kuwa mie najua.

Labda umesahau.
Kwa kejeli ulinipa changamoto.

"Andika kaka andika."
Nikakushangaza.

Mwambie Yericko asinitaje.

Mwambie Yericko asiandike uongo katika historia ya AA, TANU, uhuru wa Tanganyika na Mapinduzi.

Mimi nitakuwa kimya.
 
Wee mzee acha blahblah zako. Asikutaje kwani wee mwali wa kimanga?
 
Nilijua hotofika mbali.
Wewe ndiye kwa Kiingereza anafahamika kama "one-trick pony". Huna jipya other than the usual name-dropping of long dead or dying Muslimans, and reminding everybody how well-learned, talented and sophisticated you supposedly are. Same ol' shit year-in, year-out.
 
Ndjabu,
Mwalimu wangu aliyenisomesha ilm ya mnakasha yaani majadiliano, marehemu Sheikh Haruna alikuwa akisema kuwa ukiona mtu anakutukana jua ushamshinda.

Akaendelea akasema ikifikia hali hiyo basi sitisha mjadala hadi ghadhabu zake zipoe.

Nashauri tusubiri kidogo fahamu zirejee.
 
Nilishasema tangu mwanzo kwamba wewe lizee ni linafiki na zandiki kwelikweli, huna tofauti na wachawi halisi, kibaya zaidi unautusi uislamu kujifanya muislamu safi wakati matendo yako yote ni yakishetwani kabisa...

Unapata wapi kibri cha kuchambua kitabu ma kukibeza wakati hujakisoma? Na hili umekuja kukiri wazi baada ya mimi kukubana kwamba hujasoma kitabu...

Leo unakosoa nini hasa? Nini hukitaki mtu mwingine akiandike?

Sijui hata wanaokuunga mkono wanakuelewa au wanakusanifu tu?

Mbona mimi nilisoma kwanza kitabu chako ndipo nikapata uhalali wa kukisema ndani ya kitabu changu na nikaweka marejeo kwamba ni kutoka kitabu cha Kwaheri Ukoloni, Kwaheri Uhuru kilichoandikwa na Dr Ghasany akisaidiani na Mohamed Said?

Unazeeka vibaya mzee.....
 
Usitajwe wewe nani? Ikiwa umeandika kitabu na mimi ni mmoja wa waliokisoma lazima nikutaje utake usitake....

Uongo upi niliouandika? Hebu uanishe hapa mzee....
 
Daaah aisee nakushukuru sana kwa kumjibu kwa hekima huyu mzee, kwakweli mimi ninahasira....
 
Mzee Mohamed Said naomba ujibu maswali yangu hapo nyuma ili niweze kukujibu, naona unaruka na kuendelea na soga ukiacha maswali yangu
[emoji16] [emoji16] [emoji16] [emoji16] mzeee wa mbutu,umeingia ulingoni rasmiii
 
Mzee naona alighagilika hapo
 
Daaah aisee nakushukuru sana kwa kumjibu kwa hekima huyu mzee, kwakweli mimi ninahasira....
Yericko,
Mimi nina kitu kimoja.
Mtu akinitaja humjibu tukafanya mjadala.

Tusiwe na hasira tufanye tu mjadala wa kiungwana.

Ukikasirika ndipo utatoa lugha isiyopendeza na kama
Maalim Haruna alivyonifunza anasema ukiona mtu
kaghadhibika basi ujue ushamshinda.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…