Askari aliyempiga mwanafunzi wa IAA asimamishwa kazi, SUMA JKT kufidia gharama za matibabu

Askari aliyempiga mwanafunzi wa IAA asimamishwa kazi, SUMA JKT kufidia gharama za matibabu

BARD AI

JF-Expert Member
Joined
Jul 24, 2018
Posts
3,591
Reaction score
8,826
Chuo cha Uhasibu Arusha kimethibitisha tukio la Askari wa SUMA JKT kumshambulia mwanafunzi wa chuo hicho baada ya kujibizana kwa madai ya kutokuwa na Kitambulisho.

Askari huyo amesimamishwa kazi huku Uongozi wa Chuo ukiagiza achukuliwe hatua zaidi za kiutendaji na kijinai, pia, Mwajiri wake (SUMA JKT) agharamie matibabu ya mwathirika pamoja na kuomba radhi kwa kitendo hicho.

Askari wa SUMA JKT wamekuwa wakilalamikiwa kwa kujichukulia Sheria mkononi na kuwashambulia watu mbalimbali katika maeneo wanayotoa huduma za ulinzi.

=========================

Chuo cha Uhasibu Arusha (IAA) kinapenda kutoa ufafanuzi juu ya taarifa inayosambaa kwenye mitandao ya kijamii kuhusu mmoja wa wanafunzi wa Chuo cha Uhasibu Arusha kupigwa na Askari wa SUMA JKT katika eneo la Chuo siku ya Jumanne tarehe 22/11/2022.

Uongozi wa Chuo kwa masikitiko makubwa unakiri kutokea kwa tukio hilo katika Kampasi yetu kuu ya Arusha na umelaani kitendo hicho kilichotokea baada ya majibizano kati ya Askari wa SUMA JKT na mwanafunzi ambayo yalipelekea kitendo hicho.

Baada ya kutokea kwa tukio hilo Uongozi wa Chuo umekutana na Uongozi wa SUMA JKT na kukubaliana kuchukua hatua zifuatazo:-

i) Askari husika amesimamishwa kazi mara moja mara baada ya tukio hilo
ii) Askari husika achukuliwe hatua za kisheria (kiutendaji na kijinai) juu yake
iii) SUMA JKT kufidia gharama za matibabu pamoja na kutoa fidia ya fedha kwa mwanafunzi husika
iv) SUMA JKT wameahidi kutoa tamko la kuomba radhi kwa kitendo kilichotokea cha Askari wake kukiuka taratibu za kiutendaji

Tunasikitika sana kwa kitendo hiki na tunaahidi kuhakikisha haya hayajitokezi tena ikiwa ni pamoja na kuendelea kutoa elimu ya mahusiano mazuri katika jamii yetu.
 

Attachments

Ni hatari sana kuwatumia hawa askari kwenye ulinzi wa mageti kwenye sehemu ambazo wanakutana na watu wa kawaida.

Wanapaswa kuajiriwa na Polisi kulinda mabank na si kukaa mapokezi.
Wanapaswa kulinda sensitive areas usiku na si kuwa sehemu ya mapokezi.
 
Kitu ambacho sielewi hadi leo kwa nini wanawake wanazuiliwa kuvaa suruali za jeans wakiwa maeneo ya shule au kazi. Ni kitu ambacho bado kinatafakarisha maana asipo vaa huko atavaa uraiani hakuna kinacho badirika katika tabia ya mtu.

Jambo lingine linalo shangaza kuelekea ulimwengu wa 2023 ni wanafunzi wa kike kuzuiliwa kusuka nywele zao. Pia wanafunzi kupewa ulazima kuvaa viatu vyeusi kama vile mavazi ndio chanzo cha akili au ufaulu
 
Kitu bikra 14 yrs
hapana, mie natumia

baby.jpg


mchawi 5k tu mwaka mzima
 
Kitu ambacho sielewi hadi leo kwa nini wanawake wanazuiliwa kuvaa suruali za jeans wakiwa maeneo ya shule au kazi. Ni kitu ambacho bado kinatafakarisha maana asipo vaa huko atavaa uraiani hakuna kinacho badirika katika tabia ya mtu.

Jambo lingine linalo shangaza kuelekea ulimwengu wa 2023 ni wanafunzi wa kike kuzuiliwa kusuka nywele zao. Pia wanafunzi kupewa ulazima kuvaa viatu vyeusi kama vile mavazi ndio chanzo cha akili au ufaulu
Wanashindwa kuboresha elimu, wanajificha kwenye mambo yasiyo na msingi. Wanafunzi hawakidhi matakwa ya taaluma, mfano jinsi wanasheria walivoshindwa kufaulu mtihani wa taaluma yao Tz.
 
Back
Top Bottom