Askari JWTZ apewa kichapo baada ya kutomlipa bodaboda Mafinga

Askari JWTZ apewa kichapo baada ya kutomlipa bodaboda Mafinga

Dogo GSM

Member
Joined
Jul 31, 2021
Posts
65
Reaction score
91
Wakuu nchi imekuwa ngumu hii nahisi kila mtu amevurugwa, imetokea jana asubuhi kuna jamaa anasemekana ni mjeda amepewa kichapo na vijana hao wenye hasira kali.

Chanzo ni baada ya bodaboda kumpeleka mjeda huyo kazini..inasemwa mjeda huyo alifika kijiweni juzi asubuhi na kumchukua boda mmoja ampeleke kambini ila walipokaribia mjeda huyo alihamaki na kumtaka boda amshushe kwa kuwa anaendesha hivyo hivyo hatoi hela na akiendelea kumfwata atamuitia wenzie.

Basi jana mjeda huyo alionekana maeneo ya kijiweni ndipo boda wakamuamuru alipe hela ya kusafirishwa na riba juu ndipo akagoma basi vijana wakaanza kumshambulia lakini kwa bahati nzuri polisi walikuwa doria ndipo wakawahi kumuokoa na kumtoa katika tukio haraka sana.

4bpn7318071cf4130wz_800C450.jpg
 
Sasa hicho kijiwe kisubiri kuvamiwa na kambi nzima.

Maana hawa jamaa wanaamini wao ni miungu watu hivyo hawapaswi kupigwa, japo wwnyewe ni waonevu wakubwa.

Ila daima ujanja wao wakiwa wengi, wakifumwa mmoja mmoja wanadundwa mpaka kuvuliwa nguo.
 
Wakuu nchi imekuwa ngumu hii nahisi kila mtu amevurugwa..imetokea jana asubuhi kuna jamaa anasemekana ni mjeda amepewa kichapo na vijana hao wenye hasira kali.

Chanzo ni baada ya bodaboda kumpeleka mjeda huyo kazini..inasemwa mjeda huyo alifika kijiweni juzi asubuhi na kumchukua boda mmoja ampeleke kambini ila walipokaribia mjeda huyo alihamaki na kumtaka boda amshushe kwa kuwa anaendesha hivyo hivyo hatoi hela na akiendelea kumfwata atamuitia wenzie.

Basi jana mjeda huyo alionekana maeneo ya kijiweni ndipo boda wakamuamuru alipe hela ya kusafirishwa na riba juu ndipo akagoma basi vijana wakaanza kumshambulia lakini kwa bahati nzuri polisi walikuwa doria ndipo wakawahi kumuokoa na kumtoa katika tukio haraka sana.

Wanakuja wale waathirika wa siasa uchwara wa mitandaoni kubeza Akari wetu wote wa JWTZ sababu ya kosa 1 la huyo Askari.
 
Na wanajeshi walishafanikiwa kuwaaminisha watu kua wao wanapiga sana na wanaogopeka kutokana na mzoezi yao huko kambini.

Imefika hatua sasa kila mtu anataka kuvaa gwanda ili awe tishio aogopeke na watu

Ishini na watu vizuri kudadeki huku mtaani watu hawaelewi huku kila mtu ninja, dhulma haijengi
 
Na wanajeshi walishafanikiwa kuwaaminisha watu kua wao wanapiga sana na wanaogopeka kutokana na mzoezi yao huko kambini.

Imefika hatua sasa kila mtu anataka kuvaa gwanda ili awe tishio aogopeke na watu

Ishini na watu vizuri kudadeki huku mtaani watu hawaelewi huku kila mtu ninja, dhulma haijengi
Inatakiwa umuogope,umtii mwanajeshi siku zote za maisha yake.wazii!
 
Back
Top Bottom