Askofu Bagonza: Jakaya Kikwete hana ushawishi wowote kwenye Awamu ya Sita

Askofu Bagonza: Jakaya Kikwete hana ushawishi wowote kwenye Awamu ya Sita

Wapinzani wa nchi hii wamejaa "siasa za kufikirika"....

Ndio ninaziita za kufikirika kwani "wao ni waafrika" na "wako afrika"....

Wapinzani wa nchi hii wengi hawajui walitakalo.....

Kipindi cha JK akina Mnyika walimwita Legelege.....

Kipindi cha JPM Chadema wakamuita Dikteta......

Amekuja kipenzi chetu mh.SSH naye kwa muda mfupi mno WANAMDOGOSHA/WANAMDHIHAKI/ mbaya zaidi wanamuita Dikteta.......

Dawa ya ndugu hawa ni hii COMMENT hapa chini......


#Siempre JMT
#NchiKwanza
#Kazi Iendelee Kwa Kasi & Weledi Zaidi
FB_IMG_16307140795615105.jpg
 
Hata mimi nashangaa ni sawa na mwenda zake badala angekua padri yeye akawa rais afu kila jumapili yupo madhabahuni anapiga vijembe na kukoromea watumishi wa Mungu
Mie naongezea. Bagaonza na wenzako wanaojificha kwenye majoho anzisha chama badala ya kujiingiza kwenye siasa kwa mlango wa nyuma. Kikwete alikuwa bomu kuliko rais yeyote aliyewahi kuumbwa. Alikuwa rahisi na siyo rais. Alikuwa mzururaji na mtupu upstairs.
 
Huko siko kujikomba mjomba.

Kenya, Zambia, Malawi, SA hakuna uhasama kati ya vyama madarakani na vyama vya upinzani.

Uhasama baina ya vyama tawala na vyama vya upinzani nyumbani kwao ni Uganda, Burundi, Rwanda, Zimbabwe, Mozambique na Tanzania kutokea awamu ya tano.

Bado haikufikirishi?

Awamu #5 na #6 ni machukizo hata kwa Mola.

JK alikuwa Jembe. Viva JK!
Viva JK wapi wakati aliwatendea vizuri upinzani na upinzani mkamjibu kwa kumtendea mabaya? Kama siasa sio uadui kwa Nini mliitisha migomo ya madaktari watu wakafa Kama kuku kipindi Cha Kikwete mahospitalini? Mkaitisha migomo ya madereva wa mabasi nchi nzima mnyika akiwa ndie kinara wa kusimamia migomo ile?

Mlivuruga na kuchafua nchi isitawalike kipindi Cha Kikwete pamoja na uzuri Kumbe CCM tulikuwa tunawaangalia tu majibu yenu mliyapata kwa Magufuli mtarudia Tena ule ushenzi mlimfanyia Kikwete semeni mtarudia au mumekoma hamrudii Tena? Tubuni kwanza ushenzi mlifanyia Kikwete Ndipo tuelewane

Kikwete alikuwa Yuko Tayari ku sacrifice hata kura ili mpate lakini wapi mitusi kwake kibao.Baada ya kunyooshwa na Magufuli naona Sasa vichwa vyenu akili zinaanza kuwarudia mnaanza kujua siasa safi ni Nini baada ya Magufuli kuponda vichwa vyenu barabara

Na Mama Samia msimzengue alushatamka wazi kabisa .CCM hatutakubali yajirudie mliyomfanyia Kikwete baada ya kuwafanyia mema .So behave yourselves
 
Viongozi wa dini ni wananchi kama wengine!
Viongozi wa dini wanaongoza wenye itikadi na wasio na itikadi za kisiasa!
Viongozi wa dini ni kimbilio kwa wanasiasa mambo yanapokuwa magumu!
Viongozi wa dini wanatakiwa kuwa wa kweli na kuwaongoza waumini wao katika ukweli!
Viongozi wa dini wanatakiwa kukemea maovu!
Viongozi wa dini wanapaswa kujihusisha kikamilifu na siasa kwa sababu siasa hutumika kufanya maamuzi ya uendashaji wa nchi!
Viongozi wa dini wanapaswa kusimama kidete ili wapatikane viongozi wa kisiasa wenye utashi na nia ya dhati kuwatumikia wananchi ambao ni waumini wao!
Viongozi wa dini wanaosapoti wanasiasa waovu, wenye hila, wanafiki na wakandamizaji ni wabaya sana kwa mustakabali wa Ustawi wa jamii!
Kama wanavyosisitiza kwa waumini wao kuwa wakamilifu na waadilifu; hawana budi kuwaambia ukweli wanasiasa!
Siasa inatakiwa ishikamane pamoja na hofu ya Mungu!
Kiongozi wa dini hasa ya Kikristo Yesu kawatuma ulimwenguni kwenda kuhubiri Injili hakuna mahali Yesu aliwatuma wakahubiri Siasa hakuna popote Agano Jipya.

Hawa ni majobless waliojiunga na dini wapate sehemu ya kupata maisha sio vio gozi waliotumwa na Yesu kuhubiri injili ndio maana waweza kuta wanahubiri katiba mpya au tume huru badala ya injili!!!

Badala ya kufungua Biblia kuhubiri Injili unawakuta wameshika katiba wanasema tufungue katiba kifungu Cha ngapi huko!!!

Tatizo la Tanzania kutoendelea ni kuwa watu hawajiliti kwenye fani zao kuepuka mwingiliano.Kiongozi wa dini ana nafasi kubwa akisimama eneo lake kuleta mageuzi makubwa hata ya kiuchumi kupitia eneo lake tu mfano tulikuwa na yule mzee mchungaji Mwasapile mzee wa kikombe Cha Babu Hakuwa mwanasiasa akaema Mungu kamuonyesha kitu dawa.Akaanza kutumia kikombe chake kule
porini kabisa .Mamilioni ya watu walienda kutoka ndani na nje ya nchi na kwa kuwa lile eneo ni la hifadhi walilipa viingilio .Halmashauri kwa mwezi kwenye eneo Hilo kwa mwezi mapato yalikuwa milioni 15 Mwasapile akayapaisha kufikia bilioni moja kwa mwezi kwa wageni walioingia simu zilikuwa hazidaki kule makampuni ya simu yakaweka minara kuhudumia Mamilioni ya watu waenda kule, barabara ilikuwa mbaya ikatengenezwa, kampuni za kubeba abiria zikapata pesa hasa,hoteli zikafurika wageni nk lakini alisimama eneo lake tu

Hawa akina Bagonza ni weupe ndio maana hawajui wafanye Nini ndani ya wito wait
TB Joshua kule Nigeria alitunukiwa Hadi Nishani na serikali kwa kuiza religious tourist wengi walioingizia mapato serikali ya Nigeria kupitia Visa kuliko sekta yeyote na kuchangamsha uchumi wa Nigeria na image kupitia wageni wake na huduma yake.Watu kutoka mataifa mengi duniani walienda kwa TB Joshua!!! Bagonza watu toka taifa gani wanaenda kwake wageni wake labda Askofu mwamakula asiye na waumini akitokea kimara kwenda kumtembelea Bagonza ,!!!
 
Kikwete alijitahidi sana kujikomba kwa wapinzani Hadi kuwa anawaalika kunywa chai na vitafunwa ikulu lakini malipo upinzani waliyomlipa ni matusi kutwa kuwa ni Raisi dhaifu kuwahi tokea Tanzania ni mpole mno na kazi yake kucheka cheka tu

Wakafikia hatua Hadi ya kumwita Vasco da Gama kuwa sijui kala miguu ya kuku ndio maana hatulii nchini kutwa kusafiri wakasema Raisi hatakiwi kuwa mtu mpole na wa kucheka cheka.Ok Mungu akaona na akasikia na CCM tukasikia kilio chao Cha kutaka Raisi Mkali asiyecheka cheka na asiye mpole.Naona Sasa Askofu wa Chadema Bagonza na Chadema mnamwamkia Shikamoo Kikwete baada ya kushikishwa adabu na Marehemu Magufuli.

Haya Bagonza na Chadema niwaulize swali mnataka Raisi mpole na anayecheka cheka au Bado mko msimamo ule ule mliokuwa nao kabla Magufuli kuingia kuwa mnataka Raisi serious,Mkali asiyecheka cheka?

Kikwete pokea Shikamoo kutoka kwa Askofu Bagonza na Chadema .Usisite kuwajibu marahaba walishanyooka hao.Hata ulipohutubia kuwa huyu anayekuja sio mpole walizomea na kusema kwenda zako huko Hadi humu wakaandika Siku ukiondoka watafanya sherehe Leo wanalia Lia ohh Kikwete the best!!!!

Sasa Askofu Bagonza nenda kaungame dhambi kwa Kikwete mwende na Chadema wenzio na kabla ya kuungama dhambi mwamkieni kwanza Shikamoo
utopolo
 
Kiongozi wa dini hasa ya Kikristo Yesu kawatuma ulimwenguni kwenda kuhubiri Injili hakuna mahali Yesu aliwatuma wakahubiri Siasa hakuna popote Agano Jipya.

Hawa ni majobless waliojiunga na dini wapate sehemu ya kupata maisha sio vio gozi waliotumwa na Yesu kuhubiri injili ndio maana waweza kuta wanahubiri katiba mpya au tume huru badala ya injili!!!

Badala ya kufungua Biblia kuhubiri Injili unawakuta wameshika katiba wanasema tufungue katiba kifungu Cha ngapi huko!!!

Tatizo la Tanzania kutoendelea ni kuwa watu hawajiliti kwenye fani zao kuepuka mwingiliano.Kiongozi wa dini ana nafasi kubwa akisimama eneo lake kuleta mageuzi makubwa hata ya kiuchumi kupitia eneo lake tu mfano tulikuwa na yule mzee mchungaji Mwasapile mzee wa kikombe Cha Babu Hakuwa mwanasiasa akaema Mungu kamuonyesha kitu dawa.Akaanza kutumia kikombe chake kule
porini kabisa .Mamilioni ya watu walienda kutoka ndani na nje ya nchi na kwa kuwa lile eneo ni la hifadhi walilipa viingilio .Halmashauri kwa mwezi kwenye eneo Hilo kwa mwezi mapato yalikuwa milioni 15 Mwasapile akayapaisha kufikia bilioni moja kwa mwezi kwa wageni walioingia simu zilikuwa hazidaki kule makampuni ya simu yakaweka minara kuhudumia Mamilioni ya watu waenda kule, barabara ilikuwa mbaya ikatengenezwa, kampuni za kubeba abiria zikapata pesa hasa,hoteli zikafurika wageni nk lakini alisimama eneo lake tu

Hawa akina Bagonza ni weupe ndio maana hawajui wafanye Nini ndani ya wito wait
TB Joshua kule Nigeria alitunukiwa Hadi Nishani na serikali kwa kuiza religious tourist wengi walioingizia mapato serikali ya Nigeria kupitia Visa kuliko sekta yeyote na kuchangamsha uchumi wa Nigeria na image kupitia wageni wake na huduma yake.Watu kutoka mataifa mengi duniani walienda kwa TB Joshua!!! Bagonza watu toka taifa gani wanaenda kwake wageni wake labda Askofu mwamakula asiye na waumini akitokea kimara kwenda kumtembelea Bagonza ,!!!
utopolo
 
Udhaifu wa akili yako hauwezi kufanya wengine wasione usahihi wa maoni ya Bagonza.
Nayaheshimu maoni yako kwangu kama ninavyoyaheshimu ya akina Bagonza.....

Maoni ya mtu si lazima yawe sahihi na yenye UHALISIA...
 
Viongozi wa dini ni wananchi kama wengine!
Viongozi wa dini wanaongoza wenye itikadi na wasio na itikadi za kisiasa!
Viongozi wa dini ni kimbilio kwa wanasiasa mambo yanapokuwa magumu!
Viongozi wa dini wanatakiwa kuwa wa kweli na kuwaongoza waumini wao katika ukweli!
Viongozi wa dini wanatakiwa kukemea maovu!
Viongozi wa dini wanapaswa kujihusisha kikamilifu na siasa kwa sababu siasa hutumika kufanya maamuzi ya uendashaji wa nchi!
Viongozi wa dini wanapaswa kusimama kidete ili wapatikane viongozi wa kisiasa wenye utashi na nia ya dhati kuwatumikia wananchi ambao ni waumini wao!
Viongozi wa dini wanaosapoti wanasiasa waovu, wenye hila, wanafiki na wakandamizaji ni wabaya sana kwa mustakabali wa Ustawi wa jamii!
Kama wanavyosisitiza kwa waumini wao kuwa wakamilifu na waadilifu; hawana budi kuwaambia ukweli wanasiasa!
Siasa inatakiwa ishikamane pamoja na hofu ya Mungu!
Ilisemwa ya Kaisari mpe kaisari ya Mungu mpe Mungu. Fullstop.
 
Nikisikia kiongozi wa dini anajihusisha na masuala ya siasa huwa nakwazika sana.

Sana sana nafarijika napoona anahimiza waamini wajikite katika kufuata misingi yote pasipo kuvunja sheria za nchi.
Hasa kule babeli waliokuwa wanapingana na Mungu
 
Askofu mpumbavu
Askofu aliyefunga kanisa wakati wa korona watu wasali majumbani mwao halafu huyohuyo hajawahi hata kuwaza kufunga milango ya kanisa kwa kirusi kikali zaidi cha delta...ni mpumbavu kweli kweli huwezi wanyima watu haki ya kusali kisa tu ati wewe ni askofu
 
Maneno ya hekima kabisa haya ya baba askofu. Kwa hakika Askofu Bagonza ana hoja nzito:

View attachment 1983684

View attachment 1983686

View attachment 1983687

Kwa hakika kumvisha JK yanayojiri awamu ya sita ni kumkosea sana. Anamalizia baba askofu kwa kusema:

View attachment 1983688

Barikiwa sana baba askofu kwa kuendelea kutuchotea busara na uzoefu uliopewa na Mola wetu kila inapowezekana.
Serikali ya awamu ya 4 ilikuwa haina muda wa kukaa nchini na kuongoza nchi.
 
Back
Top Bottom