Mwambie Gwajima Samia kawaona wanafaa ndio maana amewaacha kwenye nafasi zao, kama tatizo lipo basi linaanzia kwenye mamlaka ya uteuzi, na kuhusu chanjo kuwa na madhara baada ya miaka mitano ametumia kipimo gani? kwenye maabara ipi? au ni yale maigizo yake aliyotuambia Corona haitakuja Tanzania na ikaja? huyu ni tapeli.
Zaidi, Gwajima anaonekana akiwa kwenye madhabahu yake anajisahau kama na yeye ni mwanasiasa, sijui nani alimtuma aibe zile kura, kwa kufanya vile sasa ajue anabanwa na taratibu za chama, makubaliano ya chama chake kwenye vikao halali lazima ayatii, kama hawezi asisubiri kufukuzwa, aondoke chamani abaki kanisani, kinyume na hapo ni kumdharau mwenyekiti wa chama chake, asilete unafiki wa kumpinga Dr. Gwajima na kumsifia Samia.