Uchaguzi 2020 Askofu Gwajima atangaza nia ya kugombea ubunge jimbo la Kawe

Uchaguzi 2020 Askofu Gwajima atangaza nia ya kugombea ubunge jimbo la Kawe

Kama Msukuma na Kibajaji wameingia mjengoni tena zaidi ya mara moja ndo uone ajabu kwa Gwajima?
 
Ukiona kiongozi wa dini anaanza kugombea nafasi za kisiasa changanya na zako
 
Uchaguzi wa mwaka huu hautegemei sanduku la kura
 
Katika watu niliokuwa natamani siku moja aingie bungeni ni Gwajima.

Anakuaga na point sana za maswala mbalimbali yahusuyo nchi coz ana exposure kubwa ya nje.
Hizo point zake unafikiri zinatakiwa kwenye siasa! Pale alipo kama mchungaji yeye ndiye kiongozi na hakuna wa kumpinga, akisema wote wanaitikia Amen. Kwenye siasa kwanza atakuwa chini ya chama cha siasa ambacho kina uongozi; ni lazima sasa yeye ndiye aseme Amen vinginevyo.

Pili ajue kuwa atakapozungumza kuna watakaomwambia hapo siyo, jambo ambalo kwake hakulizoea.
Mimbari ya kidini ni tofauti sana na mimbari ya kisiasa!
 
Labda tunajifariji tunaojaribu kumbeza huyu Baba Askofu, Achilia mbali tunayosikia kumhusu yeye, lakini ukweli kabisa, iwe mvua liwe jua, Mdee Kwa heri
 
View attachment 1494766

Askofu Josephat Gwajima ametangaza nia ya kugombea ubunge Jimbo la Kawe kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM) na leo amefika kwenye ofisi za chama hicho kupewa utaratibu.

Kuhusu kuunga mkono UKAWA mwaka 2015, amesema hajawahi kuwa mwanachama wa CHADEMA, ila hutetea haki wakati wote.

===
Aliingia Ofisi ya CCM Wilaya ya Kinondoni

Amesema alikwenda pale baada ya kumsikia Rais na Katibu mkuu wa CCM aliyetangaza kuwa wale wenye nia ya kumsaidi rais achukue fomu, na yeye ameona awezekwenda ofisini kujua utaratibu wa kugombea

Amesema inaweza kuwa mtu mchungaji haimzuii kuwa mbunge kwa kuwa wako viongozi wa dini ambao pia ni viongozi kisiasa, amesema hajawahi kuwa mwananchama wa chadema

Amesema amekuwa mwanachama wa CCM tangu mwaka 1994, aliipata katika mkoa wa Mwanza, Wilaya ya Misungwi, kata ya Buhingo kijiji cha Kabale na alipewa kadi na mzee Kasmiriki Futumo, alikuwa ni mwenyekiti wa ccm ambaye katibu wake alikuwa Leoneidas Masungwa

Kadi yake amesha-upgrade kuingia mfumo mpya, amesisitiza hajawahi kuwa mwanachama wa CHADEMA, ila anapenda kutetea haki na tatatetea haki siku zote. Amesema anatetea haki sehemu yoyote, iwe ccm au kokote pale atatetea haki

Hajasema kitu ambacho anaweza kwenda kuwafanyia watu wa Kawe. Aidha ilionekana kuwa angeweza kugombea Misungwi, lakini amesema Misungwi ni sehemu aliyozaliwa lakini maisha yake yamekuwa Kawe kwa hiyo atagombea Kawe

View attachment 1495050
Amemrahisishia Halima Mdee kazi asante sana.
 
Viongozi wa dini na wale wa kisiasa wanafanana katika jambo moja kuu, ambalo ni kuishi kwa jasho la mlalahoi. Tangu enzi na enzi, mlalahoi amefungwa nira za siasa na dini (unyonyaji uliohalalishwa).

Kiongozi anayetafuta madaraka ya kidini na kisiasa kwa wakati mmoja ni mlafi anayepaswa kuogopwa kuliko ukoma. Kwa mustakabali mwema wa nchi, CCM ikiwa ni chama kilichoshika hatamu za uongozi, kina umuhimu wa kutowahusisha viongozi wa dini kwenye siasa zake, ikiwa ni njia ya kupunguza unyonywaji wa wanyonge.

Mchungaji Gwajima analo jukwaa (kanisa lake) la kuzungumzia na kutetea haki, hivyo kutafuta tena jukwaa la kisiasa (ubunge) siyo muhimu kwa mtu asiye na tamaa ya madaraka.
 
Back
Top Bottom