Askofu Kilaini: Nyerere alikuwa Mtu Mwema. Mwana wa Kanisa, Baba wa Taifa na mwanadamu mwenye harufu ya Utakatifu

Akili zingine bana! Kuwa ni tukio kubwa la kumbukizi ndiyo iwe sababu ya kuhalilisha gharama kubwa. Ndiyo! Viongozi kitaifa huwajibika kusafiri kwa kuwa hayo ni majukumu yao ya kila siku.

Basi, napendekeza siku ya kumbukizi ijayo ije kufanyika huko kijijini kwenu kwa kuwa ni tukio kubwa la kitaifa.
 
Hivi huwa tunamuombea nini mtu ambaye mema au mabaya yake yamekwishaandikwa, kwanini tusiitumie nafasi hiyo kufanya wema sisi wenyewe? Je, sisi ni wema kiasi gani mpaka tuweze kuwaombea wenzetu?
Hivi huyo Askofu Kilaini sio yule ambaye, naye alipata mgao wa pesa za Escrow wakati ule??? Kaazi kwelikweli
 
Ila kule Pemba nimeona eti hawataki lijengwe kanisa
 
Hivi huwa tunamuombea nini mtu ambaye mema au mabaya yake yamekwishaandikwa, kwanini tusiitumie nafasi hiyo kufanya wema sisi wenyewe? Je, sisi ni wema kiasi gani mpaka tuweze kuwaombea wenzetu?
Hii tuachie sisi wakristo wakatoliki. Itakuchukua muda mrefu mno kujifuñza, kuelewa- imani yetu.
 
Kikwazo alikuwa ni Mama NYERERE na familia yake kuna jinsi ambavyo walisema japo NYERERE katenda Mengi mema basi achukuliwe tu mtu wa kawaida !
 
Mchakato unaofanyika kwa Nyerere ni sehemu ya imani ya kanisa Katoliki sasa wewe unataka kulifundisha kanisa katolikii mambo ya imani? Wewe endelea kuamini unavyoona sawa na kanisa liache liamini linavyoona sawa.
 
Swala la mwalimu Nyerere kura mtakatifu sio rahisi achilia mbali juwa mwenye heri.

Vigezo vya kufanywa kua mtakatifu ni ngumu sana kupatikana kwa mwana siasa tena mwafrika ,tena chini ya jangwa la Sahara .

Hii ikiwezekana kwa wanasiasa wa Kirumi tu enzi hizo.
 

Papa John Paul ii alipokuaja mwaka 1991, alisema hajaona nchi kanisa Lina wasaa mzuri kuzidi Tanzania, architect wa Hilo anajulikana, kwenye kitabu Cha van Bergen alinukuliwa akisema atalipa kanisa lake a better chance...huo mchakato haujaanza kwa bahati mbaya ,utakatifu si tu ulikua mchamungu kiasi gani Bali pia umelifanyia nini kanisa
 
Ni fumbo kubwa sana mkuu,

Hatima ya mtu aijuaye ni Mungu pekee na baadhi ya wapendwa wake atakao wafunulia kama apendavyo, yeye pekee ndo mwenye uweza wa kuhukumu na pia kutakatifuza.

There is no way way to enter heaven without being a Saint.

Kama mimi, wewe, na wengine tunatamani kuingia mbinguni, ni lazima tutakatifuzwe kwanza pasipo kujali imani au dini zetu. Na baada ya kutakatifuzwq tunageuka na kuingia kwenye umoja wa watakatifu.

Ingawa nina bad feelings na Nyerere, lakini sijui dakika ya mwisho ya uhai wa Nyerere aliyaweka vp sawa maisha yake na Mungu.

Kiimani, Kwa waislam au wakristo, wanaambiwa sekunde chache za toba ya kweli kwa Mwenyezi Mungu zinaweza kubadilisha hatma nzima ya mtu.

Kama wote wanatamani kuingia heaven, why not Nyerere as long ame-qualify criteria zote?

Binafsi siyo Mungu, hivyo siwezi kusema kwa usahihi zaidi maana tumeambiwa tusihukumu tusije tukahukumiwa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…