Askofu Mwamakula Asimulia mazito akiwa Jukwaa la Tangayika Law Society

Askofu Mwamakula Asimulia mazito akiwa Jukwaa la Tangayika Law Society

Sawa bwana mayor. Hayo yameshapitwa na Wakati chini ya Rais Dr Samia.

Ujio wa Magufuli umekuwa funzo kwa Watanzania wote hata vyombo vyenyewe vya usalama
Let’s hope so

Mama anafungua kurasa mpya ila waache kumchafua Magufuli as if huko nyuma enzi za JK mambo yalikuwa too rosy.
 
We jamaa muongo sana. Unataka kuwafanya wana JF ni wajinga? Kapumzike kama umechoka.
Nikuletee ya bomu la Soweto, Arusha (ila hilo CDM walijipiga wenyewe) ili wailaumu serikali.

Walifikia huko ndio vyombo vya ulinzi vikaona JK anawechekea sana wachukue hatua.

Magufuli alienda nao kibabe alishaona walivyomchezea JK kidogo walete madhara hasa Arusha.

Advice taken ya kupumzika 👋
 
Kaitwa lama kiongozi wa dini.Viongozi wa dini hawana mipaka kwenye mambo yanayohusu Raia na waamini wao.

Mkuu wewe ndio una misimamo ya kichama. Yeye anazungumzia mambo yanayohusu Watanzania wote. Haki amani na katiba Mpya. Hayo ta ccm na chadema umeyaandika wewe.
Sikia ukigundua mtu hamnazo usimjibu wewe mjibuji utaonekana ndo hamnazo
 
..sikiliza hotuba ya Sheikh Ponda mbele ya TLS.

..unaweza kulia kutokana na aliyoyaeleza.

..kuna mpaka matukio ya askari kuzuia mawakili wa mtuhumiwa kuingia mahakamani.

..Halafu Hakimu akaendelea kusikiliza kesi huku akijua mawakili wa mtuhumiwa wamezuiliwa kumuwakilisha mteja.
Dah!... zilikuwa enzi za giza kabisa..
 
Huyu mzee ni moja kati ya viongozi wa kidini wapumbavu,na ameitwa pale huku wakijua atakwenda kuropoka nn,na kwa taarifa yako,watu kama hao ndio wanatakiwa na utawala wa awamu ya sita,

Wewe jiuluze,ameitwa pale kama wakili au kama askofu?,je ni mwanachama wa TLS?, ili kujua kuwa ni mpumbavu,yeye ni kiongozi wa kidini,lkn anayoongea ni ya kisiasa tupu!, huo ni upumbavu,lkn pia waumini wake wanamisimamo tofauti ya kisiasa,wapo wanaccm,wanachadema,na wasio na chama,lkn yeye anawalisha tu upumbavu wake na chuki zake na jpm.
Katiba ni siasa? Hata akiongelea ya kisiasa, ni wapi viongozi wa dini walitengwa na siasa?
 
Asante sana kwa mrejesho huu.
Hii ndiyo maana halisi ya uwepo wa watu wa aina yako humu JF

Mara nyingi tunasombwa na matukio ya muda uliopo, yakishapita tunasahau kabisa kila kitu.
Hili ni tatizo mojawapo katika matatizo yetu mengi.

..mimi uonevu na serikali kutoku-deliver ni mambo ambayo nimeshindwa kuyazoea na zaidi nimeyakataa.

..kuna wachangiaji sijui ni kwa makusudi, au kwa kutokujua, wanatoa maoni yenye kuashiria kwamba kuna sehemu ya Watz inastahili kuonewa au kutokutendewa haki.

..natamani Watz wote tuwe na haki sawa. Natamani wote tuwe na fursa sawa za kujiendeleza.

..Nachukia baadhi ya Watz kujiona wana thamani kuliko wengine. Nachukia baadhi kujiona wao ndio NCHI na wana haki ya kufanya lolote kwa wale wenye mitizamo tofauti.
 
Wale wanaotumwa wamefundishwa hivyo na wameshabadilishwa mind set zao.

Kuna mada tuliwahi soma humu inaitwa Hypinotization methods zinazotumika kuwatengeneza watu kama hao. Kila kitabu sikumbuki jina kuna mdau alipost humu. Ukikisoma kinatisha. Wanafundishwa ku act kama wanyama. Ubinadamu ndani mwao unakufa. Na ni slow process wanakuwa trained hatua kwa hatua mpaka wanakua watu bora kabisa kwenye eneo hilo.
They have their theme park in hell
 
..mimi uonevu na serikali kutoku-deliver ni mambo ambayo nimeshindwa kuyazoea na zaidi nimeyakataa.

..kuna wachangiaji sijui ni kwa makusudi, au kwa kutokujua, wanatoa maoni yenye kuashiria kwamba kuna sehemu ya Watz inastahili kuonewa au kutokutendewa haki.

..natamani Watz wote tuwe na haki sawa. Natamani wote tuwe na fursa sawa za kujiendeleza.

..Nachukia baadhi ya Watz kujiona wana thamani kuliko wengine. Nachukia baadhi kujiona wao ndio NCHI na wana haki ya kufanya lolote kwa wale wenye mitizamo tofauti.
Nipo sana nawe bega kwa bega kuhusu hayo mkuu.

Kumekuwa na tabia ya baadhi ya watu kujiona wao wanayo haki zaidi ya wengine; na baadhi yao kushangilia maovu yaliyo wazi kabisa, kwa vile wanafaidika na hali hiyo.

Kuna watu siku hizi hata hawaoni aibu kabisa kushangilia au kujitangaza kabisa hata humu JF, kwamba wangeteuliwa kwenye nafasi kadhaa ingekuwa njia yao ya kupora kwa faida zao badala ya kutumikia nafasi hizo kwa manufaa ya wengi.

Kuna watu wanaamini kabisa, kujirimbikizia wao na kujenga kundi maalum la kujinufaisha ndiyo maendeleo ya nchi, bila kujali mali wanazojirimbikizia zinapatikana kihalali au kiharamu.
 
Jambo moja kubwa aliloongea askofu, ambao ni ukweli mtupu:

Nchi hii, wasomi, wakiwemo wanasheria, ndio watu waoga kuliko wengine wote. Wengine hawajaishia tu kwenye uwoga, bali wamegeuka kuwa wanafiki wakubwa.

Jingine, tufahamu kuwa, hata katika ubaya, kunaweza kuchipua mema. Yaliyotokea awamu ya 5, yachukuliwe positively. Yanatuonesha mapungufu yaliyopo kwenye mifumo yetu ya kiutawala. Sasa tuzipe hayo mapungufu. Pa kuanzia, ni katiba mpya.

Kama awamu ya 6 kweli ina dhamira njema na Watanzania, na Taifa hili, basi iende haraka, tena haraka sana kwenye taratibu za kupata katiba mpya nzuri. Vinginevyo, yote yanayofanyika itakuwa ni cosmetics, kama Askofu alivyotamka.
 
Huyu mzee ni moja kati ya viongozi wa kidini wapumbavu,na ameitwa pale huku wakijua atakwenda kuropoka nn,na kwa taarifa yako,watu kama hao ndio wanatakiwa na utawala wa awamu ya sita,

Wewe jiuluze,ameitwa pale kama wakili au kama askofu?,je ni mwanachama wa TLS?, ili kujua kuwa ni mpumbavu,yeye ni kiongozi wa kidini,lkn anayoongea ni ya kisiasa tupu!, huo ni upumbavu,lkn pia waumini wake wanamisimamo tofauti ya kisiasa,wapo wanaccm,wanachadema,na wasio na chama,lkn yeye anawalisha tu upumbavu wake na chuki zake na jpm.
Maandishi yako yote, na lugha uliyoitumia, vinaashiria tatizo kubwa akilini na moyoni mwako. Una kazi kubwa ya kufanya ili uwe binadamu wa kawaida.
 
Kuna watu wanaamini kabisa, kujirimbikizia wao na kujenga kundi maalum la kujinufaisha ndiyo maendeleo ya nchi, bila kujali mali wanazojirimbikizia zinapatikana kihalali au kiharamu.
Bahati mbaya sana tatizo hili lipo kwenye jamii. Lipo kwa watawala, na upande wa opposition.
 
Huyu Askofu wa CHADEMA angeacha kabisa uchungaji na kuhamia kabisa kwenye siasa. Kupanda kwenye majukwaa ya kisiasa ukiwa kofia ya kiongozi wa kidini ni upuuzi mtupu. Anaweza kuwa na hoja ila analeta tu confusion. Ukimbana anajitetea yeye ni askofu.
Ongelea hoja yake. Jitahidi, ombe hekima maana unaonekana umepungukiwa.

Tangu zama za kale, manabii wa Mungu walisimama katika ukweli, wengine waliwapa maonyo makali wafalme hata kuhatarisha maisha yao.

Ni dhana dhaifu sana kusema kuwa eti mtumishi wa Mungu hatakiwi kuongelea haki, amani au kukemea maovu.
 
Bahati mbaya sana tatizo hili lipo kwenye jamii. Lipo kwa watawala, na upande wa opposition.
Sasa tatizo limejipambanua zaidi. Vurugu alizozianzisha Magufuli na kuziacha, na hizi nyingine zinazoingizwa na mrithi wake, na kuzoa upinzani; hali imekuwa wazi zaidi.

Sijui Samia na hili kundi lake watafanikiwa kwa kiasi gani? Tusubiri tuone itakavyokuwa.
 
Jambo moja kubwa aliloongea askofu, ambao ni ukweli mtupu:

Nchi hii, wasomi, wakiwemo wanasheria, ndio watu waoga kuliko wengine wote. Wengine hawajaishia tu kwenye uwoga, bali wamegeuka kuwa wanafiki wakubwa.

Jingine, tufahamu kuwa, hata katika ubaya, kunaweza kuchipua mema. Yaliyotokea awamu ya 5, yachukuliwe positively. Yanatuonesha mapungufu yaliyopo kwenye mifumo yetu ya kiutawala. Sasa tuzipe hayo mapungufu. Pa kuanzia, ni katiba mpya.

Kama awamu ya 6 kweli ina dhamira njema na Watanzania, na Taifa hili, basi iende haraka, tena haraka sana kwenye taratibu za kupata katiba mpya nzuri. Vinginevyo, yote yanayofanyika itakuwa ni cosmetics, kama Askofu alivyotamka.
Andiko lililotulia vizuri sana.
 
Ongelea hoja yake. Jitahidi, ombe hekima maana unaonekana umepungukiwa.

Tangu zama za kale, manabii wa Mungu walisimama katika ukweli, wengine waliwapa maonyo makali wafalme hata kuhatarisha maisha yao.

Ni dhana dhaifu sana kusema kuwa eti mtumishi wa Mungu hatakiwi kuongelea haki, amani au kukemea maovu.
Wale manabii wa kale hawakuwa na vyama. Hawakuwa wafuasi wa chama chochote. Ulishawahi kuona Askofu Mwamakula akimtetea yeyote aliye kinyume na itikadi ya CHADEMA? Wewe jitahidi kuwa na akili za kuwajua wachungaji wa kweli na wachungaji wanasiasa. Mbona kina Kakobe wasilaumiwe?
 
Back
Top Bottom