Askofu Niwemugizi amuomba Rais Samia asikubali kufananishwa na Mungu

Askofu Niwemugizi amuomba Rais Samia asikubali kufananishwa na Mungu

“Nikikuombea uwe na afya njema na uwe mnyenyekevu lakini pamoja na madaraka hayo makubwa uliyonayo usikubali kamwe kulinganishwa na Mungu kwa namna yoyote ile usikubali."
Askofu ungemwambia tu bila kumficha, kuna watu wengi mno wamefungwa hadi maisha, wengive vifungo virefu na wengine wanasota magelezani - mambo ya UCHAGUZI Mkuu uliopita- ameshaombwa haya mambo kwa muda mrefu sana ila sijui nini kinamkwambisha.

Kuachilia ni sehemu ya ibada kwa mwanadamu, sijajua ugumu anaupata wapi, kama kuwaibia kura mmeiba, kama madaraka mnayo sasa jamani ndiyo muwatese hivi ?
 
hapa Tanzania ni vigumu ukiwa kiongozi ukatae misifa kwa sababu watu wengi wanafiki sana
hata Nyerere alisema kuna kipindi walimuingiza kingi, "Mwalimu ukistaafu nchi itabaki na nani ?"mwisho wa siku anasema aligundua walikuwa ni wachumia tumbo
Brother una akili sana hongera, Nyerere aliwahi kusema kabisa kwamba aliingizwa Chaka na wasaka fursa na hili lilimpata Magu alikuwa akizungukwa na machawa hadi kero
 
Nyerere hakuitwa mtukufu.
Enzi za Nyerere viongozi na watu wote walikuwa wanaitwa Ndugu.
Mtukufu na waheshimiwa mlianza kipindi cha Mkapa.
Hapana. Neno Mtukufu lilitumika sana kipindi cha awamu ya pili. Nakumbuka mwaka 1995 tena ilikuwa mwezi November kama sikosei siku Rais Mkapa (RIP) anataka kutangaza Baraza lake la Mawaziri la kwanza ndiyo ametoka tu kuchaguliwa October 1995 ndipo ALIPOLIPIGA MARUFUKU neno MTUKUFU baada ya MC (yule aliyekuwa anaendesha hiyo event sijui hata anatakiwa kuitwaje) alivyomuaddress kama Mtukufu Rais. MC alikuwa anamkaribisha ili ahutubie na kutangaza Baraza la Mawaziri.

Ndipo Mkapa aliposimama akasema kuanzia siku hiyo hataki kuitwa Mtukufu kwa sababu Mtukufu ni Mungu peke yake!!!. Since then hakuna Rais aliyetumia neno hilo ndipo tulipoanza kutumia MHESHIMIWA
 
Nani aliwahi kujifananisha na Mungu Tz?

Magufuri. Aliwahi kuitwa Mungu na Waziri Fulani na Wala hakukanusha. Pia amewahi kuitwa Yesu na mbunge mmoja wa CCM , tena kwa kusema jina la Magufuri libarikiwe.
 
Niwemugizi ni Desmond Tutu mwingine - ni mnyoofu kama rula. SSH hebu plz fanyia kazi ushauri wake upate thawabu
 
... kizazi cha lini wewe? Official salutation ya Nyerere ilikuwa Mwalimu or Ndugu or (rarely) Mheshimiwa na sio vingenevyo!
Mheshimiwa Nyerere alikataa, ilirudi wakati wa mkapa.
Ila Kuna hii wakati wa mawaidha... "Watukufu waislam"! Hii ni sawa?
 
Askofu severine kachanganyikiwa yeye kwanza ajitambue asimuite yesu mungu. anajua yesu hataki kuitwa mungu na ndani ya biblia yesu kawaeleza wazi kuwa mungu yupo.

Lakini askofu bado anamwita binadamu mungu halafu leo anakuja kusema mbele ya mama samia usifananishwe na mungu. binadamu hawezi kuumba mbingu wala hawezi kulipeleka jua au kulizuia jua lisitoke mnaenda kumuita mungu askofu sahihisha kwanza hapo

Doctrine ya ukristo Ni utatu Mtakatifu. Mungu Baba, Mungu Mwana na Roho Mtakatifu.
 
Magufuri. Aliwahi kuitwa Mungu na Waziri Fulani na Wala hakukanusha. Pia amewahi kuitwa Yesu na mbunge mmoja wa CCM , tena kwa kusema jina la Magufuri libarikiwe.
No hiyo sidhani kama yeye alipenda. Ni kama Mama alivyokaa kimya kuacha Dkt Magufuli adhalilishwe sidhani kama anamaanisha hakumpenda
 
Baada ya jubilee Rais ataenda chato, mwenye akili na atambue
 
Mheshimiwa Nyerere alikataa, ilirudi wakati wa mkapa.
Ila Kuna hii wakati wa mawaidha... "Watukufu waislam"! Hii ni sawa?
Nadhani kwa mazingira ya ibada haina tatizo kuwa-address hivyo kwa ujumla wao (the people) ila sio mmoja mmoja.
 
Nyerere alitwa mtukufu rais mpk anang'atuka na hakuna lolote lililompata.

Ni unafiki wetu tu wanadamu tunaweza kutukuza kitu kwa mdomo lakini moyoni hakuna kitu.

Uzuri hilo neno liliisha ondolewa tangu awamu ya tatu.
Wakati wa Nyerere ilikuwa ni NDUGU
 
Hakuna binadamu asiyependa kutukuzwa awe mbunge au mchungaji,padre ,askofu ,shehe nk au mtu wa kawaida ndio maana hata maaskofu husujudiwa watu wanapobusu Pete yake hupiga magoti kuibusu Pete

Hivi sahihi mwanadamu kumpigia magoti mwanadamu mwenzie ville?

Na hupenda kuitwa Baba Askofu,baba padre au Baba mchungaji wakati hawakuwazaa
 
Hakuna binadamu asiyependa kutukuzwa awe mbunge au mchungaji,padre ,askofu ,mbunge,shehe nk au mtu wa kawaida ndio maana hata maaskofu husujudiwa watu wanapobusu Pete yake hupiga magoti kuibusu Pete

Hivi sahihi mwanadamu kumpigia magoti mwanadamu mwenzie ville?

Na hupenda kuitwa Baba Askofu,baba padre au Baba mchungaji wakati hawakuwazaa
[emoji38][emoji38][emoji38] we jamaa kichwani mwako hamna kitu
 
Kwanini usiendelee kufuatilia singeli mkuu. Yani hujui Jiwe alivyokuwa anamchukia Askofu Niwemugizi mpaka akaitwa sio raia uhamiaji wakamchunguza. Tanzania hii kuna maaskofu wawili walikuwa strong ni Askofu Niwemugizi na Askofu Bagonza, wote majirani ila makanisa tofauti
Mkuu Achana naye huyo, ukute Anataka kupima watu watasemaje.
 
Ameyasema hayo leo katika Jubilee inayofanyika Mkoani Kagera, ambayo pia imehudhuriwa na Mh Rais

===

skofu wa Jimbo Katoliki la Rulenge-Ngara, Severine Niwemugizi amemuomba Rais Samia Suluhu Hassan kutokubali kulinganishwa na Mungu kwa namna yoyote ile.

Amesema hayo leo Jumanne Februari 22, 2022 katika sherehe za Jubilee ya miaka yake 25 inayofanyika wilayani Ngara mkoani Kagera.

“Nikikuombea uwe na afya njema na uwe mnyenyekevu lakini pamoja na madaraka hayo makubwa uliyonayo usikubali kamwe kulinganishwa na Mungu kwa namna yoyote ile usikubali."

"Ninakumbuka sana Hayati Benjamini Mkapa najua huko mlikuwa mmezoea mtukufu rais, mtukufu rais alifika mahali akawa mkali kabisa mtukufu ni Mungu tu naomba hilo liwe neno kwako, " amesema Askofu Niwemuguzi.

Huku akiwa makini amesisitiza,"basi nakuombea Mungu akusaidie kukuza upendo kati ya Watanzania unaotuongoza, ukuze haki nayo haki izae amani na utulivu na kukuza demokrasia katika nchi yetu."

“Ukuze upendo na mshikamo wa Watanzania ili hatimaye utumishi wako utukuke na kuacha alama itakayoonwa kwa vizazi vingi.
Mungu akujalie hekima na uvumilivu wa kusikiliza hata yale yanayokela masikio yako, unajua sisi watoto wako tuko wakorofi, Mungu akujalie tu hekima na uvumulivu hasa pale unapokuwa ni ushauri wenye nia njema ya kulijenga Taifa letu liendelee kuheshimika ndani na nje.”

PIA SOMA
- Rais Samia akataa kutukuzwa, asema yeye hawezi kujilinganisha na Mungu



View attachment 2127421
Huyu ni baadhi ya Maaskofu wachache sana Wakatoliki ninao wakubali wanajitambua.
 
Nyerere alitwa mtukufu rais mpk anang'atuka na hakuna lolote lililompata.

Ni unafiki wetu tu wanadamu tunaweza kutukuza kitu kwa mdomo lakini moyoni hakuna kitu.

Uzuri hilo neno liliisha ondolewa tangu awamu ya tatu.
Lakini mkuu, Nyerere aliikataa ile kauli mbiu ya 'Zidumu fikra za mwenyekiti'.
 
Back
Top Bottom