Safi sana,huu ndio utumishi wa Mungu tunaouhitaji.
Better late than never.
Waumini katika maeneo mengine, mjiongeza,msisubiri taarifa kama hii kwani si kila kiongozi wa dini atafanya hivi katika maeneo yenu.
Viongozi wa madhehebu mbalimbali(RC,KKKT.n.k) wanaokutana kutoa matamko ya pamoja(waraka) kama ya kukemea maovu,kukemea wanasiasa,n.k,walipaswa kuwa wamekutana na kuja na tamko kama hili; hivyo, tunatumai tangazo hili litatumika kama mfano kwa viongozi wengine wa dini waliobaki.
Baba Askofu,katika hili,umevaa viatu vilivyowapwaya wengi wakiwemo viongozi wa dini na wasio viongozi wa dini.
Hongera sana Baba Askofu!