Uchaguzi 2020 Askofu Niwemugizi ataka walioenguliwa wote warejeshwe kwenye kinyang’anyiro, Uchaguzi uwe wa Haki

Uchaguzi 2020 Askofu Niwemugizi ataka walioenguliwa wote warejeshwe kwenye kinyang’anyiro, Uchaguzi uwe wa Haki

Return Of Undertaker

JF-Expert Member
Joined
Jun 12, 2012
Posts
4,572
Reaction score
26,885
ASKOFU NIWEMUGIZI ATAKA WALIOENGULIWA WARUDISHWE WOTE, UCHAGUZI UWE WA HAKI

Mimi naamini kwamba amani msingi wake ni haki. Pale ambapo kuna haki, amani itatawala." Askofu Niwemugizi aiomba Tume ya Taifa ya Uchaguzi NEC kutenda haki kwenye mchakato mzima wa kupata viongozi wa nchi oktoba 28,2020.

Wale wanaoenguliwa waenguliwe kwa misingi sahihi, sio kwa sababu za ovyoovyo. Lakini, kwa bahati mbaya picha tunayoiona upande fulani umeathirika sana na hii engua engua, wakati upande mwingine hamna.Hii inaweza kuleta doa katika mchakato mzima wa uchaguzi huu.

Upande flani unaonekana hakuna walioenguliwa, wameenguliwa wa upande mmoja. Tulitarajia mchakato uonekane ni wa haki kabisa tangu wakati wa watu kutafuta kuteuliwa, ionekane kweli watu wameteuliwa kwa haki, na wale wanaoengeuliwa waenguliwe kwa misingi inayokubalika

Ni vizuri wadau wote wahusika wa mchakato wa uchaguzi, kila mmoja afanye wajibu wake, sasa ni bahati mbaya kidogo kwamba tunaongea wakati matayarisho ya awali ya uchaguzi yamekamilika.


 
Natanguliza shukrani zangu za dhati kwetu ninyi nyote mnaosoma uzi huu ama kijiswali hicho kidogo. Asalaam alaykm!

Nataka niulize kajiswali kadogo. Je, kazi za wasimamizi wa uchaguzi ni kuwaengua wagombea kwa mitego midogo midogo au kuwasaidia ili wapate sifa za kugombea?

Ni kwanini wasimamizi wa uchaguzi anapoona mgombea amekosea kujaza form au kuna kitu amekisahau asichukue nafasi yake kama kiongozi kumwelekeza ajaze vizuri? Anashindwa nini kumpigia simu kamaameondoka arudi ili aijaze vizuri?

Kwanini refa ndio anakua adui wa mchezaji badala ya kumwelekeza kufuata utaratibu?

Kwanini refa ndio anamtegeshea penati mchezaji?

Nia ni kuwaengua au kupata wagombea watakaoshindana ili mshindi apatikane kwa njia halali?

Ni sahihi kuwachagulia wananchi mgombea badala ya wao?
 
Angekuwa Ponda Issa Ponda saa hzi anayea debe, mukiambia hii nchi ni mfumo galatia mnakataa
Acha uduanzi, yaani askofu anakuteteeni bado mnashupaza shingo na kuropoka utopolo.

Kule south Africa haohao mnaowaita magaltia wanawapigania adhana yenu iendelee kulizwa baada ya mamlaka kuipiga 'bani'

Muwe waungwana,Askofu anapigania maslahi ya wote acha uzwazwa!
 
NEC walitakiwa wawasaidie kujaza form wagombea na si kuwazuia kugombea. Mbona tukienda kupata huduma sehemu zinazotuhitaji kujaza form kama huelewi jambo kwenye form unarudi kwa wahusika kuwauliza namna sahihi ya kujaza form na unapewa maelekezo ili form yako ikamilike vizuri.

Mfano umeacha tarehe, hujaandika labda mwaka wa kuzaliwa, hujaweka picha nk. Vyote utaambiwa kuvikamilisha ili swala lako likamilishwe.

LAKINI NEC wamefanya kugombea kama mashindano ya kufanya mtihani kumbe ni swala la kikatiba na mtu hawezi kuenguliwa kwa sababu ya kukosea kujaza form labda asiwe na sifa ya kugombea.
 
Back
Top Bottom