Uchaguzi 2020 Askofu Niwemugizi ataka walioenguliwa wote warejeshwe kwenye kinyang’anyiro, Uchaguzi uwe wa Haki

Uchaguzi 2020 Askofu Niwemugizi ataka walioenguliwa wote warejeshwe kwenye kinyang’anyiro, Uchaguzi uwe wa Haki

The most civilized Askofu in Tanzania. Ana sifa za kuwa kiongozi hata wa kitaifa huyu Askofu. Ni fluent wa lugha na very logical man. Vitabu vyote vya dini vinahimiza HAKI na kamwe HAKI isichanganywe na batili.
 
NEC walitakiwa wawasaidie kujaza form wagombea na si kuwazuia kugombea. Mbona tukienda kupata huduma sehemu zinazotuhitaji kujaza form kama huelewi jambo kwenye form unarudi kwa wahusika kuwauliza namna sahihi ya kujaza form na unapewa maelekezo ili form yako ikamilike vizuri, Mfano umeacha tarehe, hujaandika labda mwaka wa kuzaliwa, hujaweka picha nk. Vyote utaambiwa kuvikamilisha ili swala lako likamilishwe. LAKINI NEC wamefanya kugombea kama mashindano ya kufanya mtihani kumbe ni swala la kikatiba na mtu hawezi kuenguliwa kwa sababu ya kukosea kujaza form labda asiwe na sifa ya kugombea.
NEC imejaa washenzi na wahuni watupu itaweza kutenda haki ?
 
nakusoma ila ngumu kuwagundua kaka...

Unakumbuka ya Mb Nassari.... Anaitwa afanye press conference kulalamika anajichelewesha kijanja ....

leo kijani....
Hata kama ni ngumu kuwagundua NEC kunyamazia hili ni kama inasapoti uhuni,ila NEC ina dawa rahisi ya kukomesha uhuni huu, dawa rahisi ni tume kuja na utaratibu wa wagombea kujaza fomu ndani ya ofis ya msimamiz hao wanunuzi tutakuwa tumewakomesha make chanzo cha yote hayo ni wanunuzi,
 
Hata kama ni ngumu kuwagundua NEC kunyamazia hili ni kama inasapoti uhuni,ila NEC ina dawa rahisi ya kukomesha uhuni huu, dawa rahisi ni tume kuja na utaratibu wa wagombea kujaza fomu ndani ya ofis ya msimamiz hao wanunuzi tutakuwa tumewakomesha make chanzo cha yote hayo ni wanunuzi,
Siyo wanunuzi ni walanguzi
 
Siyo wanunuzi ni walanguzi
Wasimamizi wakiwabana wagombea wajaze fomu ndani ya ofisi kwa kuongozwa na msimamizi then fomu inabaki kwa msimamizi, halafu mgombea akishateuliwa na tume hata akijiondoa tume isifute jina lake, hakika walanguzi tutakuwa tumewakomesha
 
Safi kabisa tuondokane na jiwe anatupeleka pabaya kwa ukabila na mambo mengine ya hovyo anayofanya.
 
Kwamba kamanda Askofu anataka kuwapangia NEC, kama mtu hana umakini kwenye kujaza tu fomu hawezi pia kuwa na umakini kwenye mambo muhimu mengine ya uongozi.
Acha ubinafsi. Hizo fomu ziliandikwa lugha ya ki-ccm? Mbona walioenguliwa wote ni wapinzani?
 
NEC walitakiwa wawasaidie kujaza form wagombea na si kuwazuia kugombea. Mbona tukienda kupata huduma sehemu zinazotuhitaji kujaza form kama huelewi jambo kwenye form unarudi kwa wahusika kuwauliza namna sahihi ya kujaza form na unapewa maelekezo ili form yako ikamilike vizuri.

Mfano umeacha tarehe, hujaandika labda mwaka wa kuzaliwa, hujaweka picha nk. Vyote utaambiwa kuvikamilisha ili swala lako likamilishwe.

LAKINI NEC wamefanya kugombea kama mashindano ya kufanya mtihani kumbe ni swala la kikatiba na mtu hawezi kuenguliwa kwa sababu ya kukosea kujaza form labda asiwe na sifa ya kugombea.
Mkuu huu ni uhuni tu. Wewe unaamini kwamba wagombea wa cccm wote hawakusahau au kukosea baadhi ya mambo? John mwenyewe alikosea akawekewa pingamizi lkn likafunikwa funikwa tu. Hawa ni wahuni kama wahuni wengine tu.
 
Asante baba Askofu....kutimiza wajibu wako kama kiongozi mkuu wa dini ni karama kubwa...wengine wako busy kukusanya sadaka na fungu la kumi bila kujua hao wanaozileta kanisani wanahitaji Haki na Usawa ili kuzileta sadaka hizi zenye upako mkubwa kwa mwenyezi Mungu bila kinyongo
 
Natanguliza shukrani zangu za dhati kwetu ninyi nyote mnaosoma uzi huu ama kijiswali hicho kidogo. Asalaam alaykm!

Nataka niulize kajiswali kadogo. Je, kazi za wasimamizi wa uchaguzi ni kuwaengua wagombea kwa mitego midogo midogo au kuwasaidia ili wapate sifa za kugombea?

Ni kwanini wasimamizi wa uchaguzi anapoona mgombea amekosea kujaza form au kuna kitu amekisahau asichukue nafasi yake kama kiongozi kumwelekeza ajaze vizuri? Anashindwa nini kumpigia simu kamaameondoka arudi ili aijaze vizuri?

Kwanini refa ndio anakua adui wa mchezaji badala ya kumwelekeza kufuata utaratibu?

Kwanini refa ndio anamtegeshea penati mchezaji?

Nia ni kuwaengua au kupata wagombea watakaoshindana ili mshindi apatikane kwa njia halali?

Ni sahihi kuwachagulia wananchi mgombea badala ya wao?

Tume imejivika u-baraza la mitihani hili Taifa limekuwa la kijinga sana. Kuna kisa nilikisikia eti mgombea alienguliwa sababu hakimu alisaini akaandika kifupi alisaini akiwa DSM badala ya Dar es Salaam na hii ikawa sababu tosha ya kumuengua mgombea. Halafu aibu nyingine kubwa Zaidi ni wagombea aina moja ndiyo wanakosea kujaza form ule upande mwingine hata kama hajawahi kuingia darasani hata siku moja hawezi kukosea kujaza form-ujinga mtupu.
 
Back
Top Bottom