Atakayeweza kuniloga nitamlipa Milioni 25

Atakayeweza kuniloga nitamlipa Milioni 25

Hujawahi kupigwa ukapigika hujawahi kuteseka siku ukinyonywa damu ingali bado upo hai ndio utaelewa, tren linagonga Gari ndani kuna baba mama na mtoto mdogo, baba Mama wanakufa papo hapo Ila mtoto anatoka mzima bila hata jeraha moja Wala kuvunjika pahala, niulize Mara 3
Aniroge nani mnarogwa nyinyi wenye Imani haba hakuna uchawi mbele ya YAKOBO
 
Anipige nani mnarogwa nyinyi mliekuwa na iman haba hakuna uchawi mbele ya Yakobo 😂😂
Haujui kwanini kanisani kuna kengele na haujui kwanini msikitini kuna sipika kubwa za kupiga kelele za Azana, utajulia wapi masuala ya wachawi ?
 
Haujui kwanini kanisani kuna kengele na haujui kwanini msikitini kuna sipika kubwa za kupiga kelele za Azana, utajulia wapi masuala ya wachawi ?
Ukiwa na Imani kubwa huwezi rogwa watu wasingehangaika kuwauwa watu wasumbufu kama Lissu badala yake wangetumia uchawi ukiona unarogwa ujue hauna Imani nakupa hii chukua itakusaidia 😁 😁
 
Eti bila majina matatu hawawezi kuniloga.
Wengine wanadai sina vigezo vya kuvutia wachawi waniloge[emoji1787]
Mmoja tu ndo kasema anaweza kuniloga bila majina yangu.
Niko hapa namsubiri.
Msiponioma kesho nzima kwa huu uzi mjue washapita na mim usiku[emoji23]
Aah wapiiii hawana lolote, unakumbuka yule aliyekua Sheikh mkuu wa Dar alimwambia Mange hatoboi huu mwaka wa pili naona Mange anazidi kudunda,

Uchawi hauendi kwa Mentali [emoji38]
 
Hello Africans.

Hakuna binadamu ninaowadharau kama wanaoamini mauchawi na mauganga.

Huwa nawaona ni watu wenye kasoro kubwa kichwani na wameoza kiasi kwamba hata uwaambie nini huwezi kuwabadili imani.

Hizi imani pumbavu zinaonesha vile Africans tuko na IQ ndogo.Na ndio maana pamoja na utajiri uliopo ktk hili bara tunateseka na shida karne kwa karne huku wenzetu wasioamini haya maujinga wakituacha mbali kwa maendeleo. (Najua kuna wazungu wachache vichaa pia wanaamin ushirikina).

Ukweli hizi imani zinanikera sana maana mbali ya kuchelewesha maendeleo ya hili bara pia ni hatari.Tushaua sana wenzetu wasio na hatia sbb ya hizi imani pumbavu.Albino,Vipara,wazee with red ayes na wengine wengi.Upumbavu mtupu.

Mimi binafsi nilishahama sehemu kwa kusingiziwa eti mimi ni freemason.Nilifanya kosa nikaporomosha hekalu wanakoishi wajinga.Mjengo wetu uko tofaut by far na nyumba zingine zote.

Wale wapuuzi walishindwa kujua kuwa kufanikiwa hakuna uchawi bali janja janja na timing kwenye fursa,basi yenyewe yakajiongoza eti hapa ni masonic na makafara tu.

Mwanzoni niliwapuuza ila badae kuna kitu ilitokea nikaona hawa wapuuzi kuna siku wanaweza wakajiunga wakanichoma mle ndani wakiamin mie natoa damu za watu kafara.Ikabidi niondoke.

Yupo mfanyakazi wangu alinichana Live kuwa "boss najua huwez kutoa siri zako ila siwez amini umefika hapa ulipofika bila ndumba kuhusika"

Mimi siamini kama kuna mtu yeyote anayeweza fanya kitu digits zangu bank zikaongezeka.Siku zote ninaamini katika kutumia akili ktk kutafuta.

Pia siamini kama kuna mjinga yeyote anayeweza kuniloga kitu kibaya kikanipata sbb havifanyi kazi.Mnadanganywa tu.

UCHAWI NA UGANGA NI UONGO havipo na havifanyi kazi.
Mpo wengi humu mnaoamini hayo matakataka sasa nawapeni ofa ya 25M kwa atakayeweza kuniloga.

Nifanyeni chochote kibaya na mhakikishe hamnisamehi mpaka nije hapa niandike uzi wa kuomba msamaha na kukiri kuwa kweli uchawi upo nimelogwa na pia nilipe hiyo 25M kwa mchawi wangu.

Mkitaka niwatukane babu na bibi zenu wanaoogopwa kwa uchawi ili hasira ziwapande mniloge vizuri semeni.Nitawavurumishia mitusi hao babu/bibi zenu hamjapata kuona.Nitawatukana na kuwakashifu ma hawatanifanya chochote wajinga hao😂

Haya kazi kwenu.

NILOGENI

UPDATE:Mnaotaka jina ili mniloge siwezi kuwapa sbb ua Privacy ila nawawekeeni picha yangu muitumie kuniloga.Kateni mikono,vidole,nifanyeni niwe na miguu 4 kama.ng'ombe vyovyote.
mtoto we si haba🤩
 
Mitusi na hiyo imani vimekupendezea kweli.
Majina yako matatu
Majina ya Mama yako matatu

Kabizi hivyo vitendea kazi mezani subiri uje uchezee viwembe yaan mtu hata hujalowekwa kwenye chungu chenye dawa unajifanya kutamba km umechanjiwa kucha ya Simba kumbe kima tu
 
Majina yako matatu
Majina ya Mama yako matatu

Kabizi hivyo vitendea kazi mezani subiri uje uchezee viwembe yaan mtu hata hujalowekwa kwenye chungu chenye dawa unajifanya kutamba km umechanjiwa kucha ya Simba kumbe kima tu
Sa matusi ya nin🤣
 
Back
Top Bottom