AZAM na Baraka Mpenja punguzeni mahaba kwa Yanga, kuweni professionals

AZAM na Baraka Mpenja punguzeni mahaba kwa Yanga, kuweni professionals

Jana nilipokuwa nafuatilia gemu ya Yanga, nilikuwa nasikia mahaba ya kupitiliza kwa timu ya Yanga kutoka kwa mtangazaji Baraka Mpenja na hii siyo mara ya kwanza kuliona hili.

Jana alikuwa anatoa kauli kama "upande wa pili nao watakuwa wakienda chooni wanasema Yanga kweli anapiga mpira mwingi" na kauli aliyokuwa anairudia mara nyingi ni "huu ni mpira wa kitabuni, siyo mpira wa papatu papatu". Ulikuwa unawalenga kina nani kwa kauli hizo?

Viongozi wa Simba nao waamke, hali iliyokuwepo msimu uliopita ya kuishi kinyonge haitaifikisha hii timu popote. Karibia media zote sasa hivi ziko kwenye payroll ili kuichafua Simba. Mnaweza kuyaona haya mambo ni madogo ila media ina nguvu sana inaweza kuupamba uongo hadi ukaonekana kweli.

Azam kiujumla ni kama wamekuwa na bifu na Simba ndiyo maana wanasimba wengi wanafurahi mnapofanya vibaya. Uwanjani mnaikamia Simba halafu Yanga wanajipigia wanavyotaka.

Mechi zinazochezwa uwanja wa Uhuru hawafanyi coverage nzuri, Camera ya muhimu inawekwa chini na muda wote unaona kwanza mabenchi na nguzo kabla haujawaona wachezaji waliopo uwanjani. Mechi za mikoani hawaweki camera za kuonyesha offside, matokeo yake minong'ono kuwa Simba inabebwa na marefa inakuwa na nguvu bila ushahidi wa kutosha. Inabidi wawepo watu ndani ya Simba kuhakikisha mechi zake hasa zile za nyumbani zinatangazwa ipasavyo.

Kwa ujinga huu ndiyo maana wengine ikifika makundi tu ya CAF tunaswitch DSTV. Watangazaji wa nje wanatoa facts siyo mahaba binafsi na pia hawatangazi mpira kama wako redioni.

Nimemaliza.
Ameongea UKWELI [emoji1787]
 
Mechi ipi Yanga amecheza halafu dstv wamefanya production.?
Mkuu ulikuwa unafatilia kweli mechi za kimataifa za yanga au ulikuwa unaulizia matokeo, mbona mechi nyingi sana dstv kafanya production, au hata fainal hukuangalia kutokana na wivu wako juu ya yanga?. Muda mwingine tuwe tunabishana kwa hoja mkuu siyo kelele za vijiweni
 
Mkuu ulikuwa unafatilia kweli mechi za kimataifa za yanga au ulikuwa unaulizia matokeo, mbona mechi nyingi sana dstv kafanya production, au hata fainal hukuangalia kutokana na wivu wako juu ya yanga?. Muda mwingine tuwe tunabishana kwa hoja mkuu siyo kelele za vijiweni
Kuna utofauti kati ya kufanya production na kuonyesha, dstv kuonyesha haina maana kwamba yeye ndie kafanya production. Mechi zote za yanga, simba na wengineo walizocheza hapa nchini production imefanywa na azam hadi hy fainali, mechi za yanga, simba na wengineo nje ya nchi zimefanywa na kampuni tofauti kabisa ila sio dstv. Kinachofanyika ni dstv anapewa clear feed tuu ndipo anaonyesha. Tafuta mtu anayefanya kazi kwenye tv atakupa hy elimu.
 
Kuna utofauti kati ya kufanya production na kuonyesha, dstv kuonyesha haina maana kwamba yeye ndie kafanya production. Mechi zote za yanga, simba na wengineo walizocheza hapa nchini production imefanywa na azam hadi hy fainali, mechi za yanga, simba na wengineo nje ya nchi zimefanywa na kampuni tofauti kabisa ila sio dstv. Kinachofanyika ni dstv anapewa clear feed tuu ndipo anaonyesha. Tafuta mtu anayefanya kazi kwenye tv atakupa hy elimu.
Nimekupata mkuu
 
Hivi TFF wanakamati ya kuhakiki ubora wa matangazo ya Azam kweli?

Kama hawana nawashauri waiunde haraka sana na kila wiki wawe wanatoa ripot iwekwe wazi ili tujue wanashauri nini.

Ubora wa matangazo ya Azam ni hovyo sana. Miaka inaenda lkn hawataki kujirekebisha.

Azam wakiweza hilo watauza sana visimbuzi vyao.
 
Hivi TFF wanakamati ya kuhakiki ubora wa matangazo ya Azam kweli?

Kama hawana nawashauri waiunde haraka sana na kila wiki wawe wanatoa ripot iwekwe wazi ili tujue wanashauri nini.

Ubora wa matangazo ya Azam ni hovyo sana. Miaka inaenda lkn hawataki kujirekebisha.

Azam wakiweza hilo watauza sana visimbuzi vyao.
Wazo zuri. Kuna maboresho mengi yanaweza kufanyika mbali na haya. Mfano, huwa nashangaa kwa nini mechi ikiisha hawafanyi marudio ya magoli yote ya mechi hiyo kabla ya kurudi studio au kuanza mahojiano pale uwanjani. Nadhani hii ni standard inayotumika na media zingine za nje zinazotangaza mpira.
 
Back
Top Bottom