Azam Pesa: Huduma mpya ya kifedha

Azam Pesa: Huduma mpya ya kifedha

Huduma nzuri Ila ilitakiwa ifanyiwe mabiresho ya kutosha ikiwezekana inauzwa dukani kwa kuskitratch kama vocha

Bakhresa yuko serious sana na kazi sio kama akina fulani kazi kumfuatila zeruzeru wa kariakoo
 
Kampuni kubwa na iliyoenea katika nchi ya Tanzania pamoja na nchi jirani 'Bakhresa Group' imeleta sokoni huduma mpya ya kifedha ijulikanayo kama 'Azam Pesa'.

Huduma hii ni kama zilivyo huduma nyinginezo za M-Pesa, Airtel Money, Tigo Pesa and the like.

Ili kuielewa zaidi huduma hii, nitaenda katika mtindo wa Maswali na kisha majibu.

Je, Azam wameanzisha mtandao wao wa simu?
Hapana. Azam bado hawajaanzisha mtandao wao kama zilivyo kampuni kadhaa za mawasiliano hapa nchini.

Bali AzamPesa wameingia makubaliano na baadhi ya mitandao kwa ajili ya kuwezesha upatikanaji wa huduma kupitia line za mitandao hiyo.

Mpaka sasa AzamPesa wameshakubaliana na Tigo, Airtel na Zantel. Hivyo huduma hii inapatikana katika line za mitandao tajwa.

Vodacom, Halotel na mitandao mingine bado wapo kwenye mazungumzo. Watakapokubaliana basi huduma hii itawezeshwa katika line hizo.

Je, huduma hi inahusika
na nini?
Kama ilivyo huduma zingine, huduma hii inahusika na;
1.Kutuma Pesa
2.Kutoa Pesa
3.Kulipia bili
4.Kulipia bidhaa za Azam

Je, huduma hii imeanza kufanya kazi?
Ndiyo, huduma hii imeshaanza kufanya kazi kwa wateja wote waliosajiliwa.

Je, najiungaje na huduma hii?
Fika katika duka la wakala na uweze kusajiliwa. Kinachohitajika ni namba yako ya simu pamoja na namba yako ya NIDA. Ndani ya dakika mbili tayari utakuwa umeshasajiliwa kuwa mteja wa AzamPesa.

Je, huduma naweza kupata vifurushi 'bundles' maalum vya Azam?
Hapana. Kama ambavyo nilijwishaeleza hapo juu kwamba Azam bado hawajaanzisha mtandao wao hivyo swala la vifurushi linabakia kuwa maamuzi ya mtandao husika.

Je, huduma hii naipata wapi?
Huduma hii inapatikana katika mikoa yote Tanzania. Ijapokuwa bado haijatapakaa kila mahali lakini upatikanaji wake katika maeneo mengi ya miji ni uhakika.

Je, menu 'ussd' ya AzamPesa ni ngapi?
Baada ya kusajiliwa, utabadili namba ya siri. Hivyo utabonyeza *150*08# na kuweza kupata huduma ya AzamPesa.

Kama una swali lolote kuhusiana na huduma za AzamPesa, basi karibu.

Wasalaam.
Du ila Bakhresa anajua kukaba,anakaba kila kona, ukija kwenye ubuyu yupo ,kwenye lambalamba ndio usiseme na sasa hadi kwenye pesa kiganjani.
 
Pia unaweza kutuma pesa kwenda mtandao washindani????......mfano kutuma pesa kutoka azampesa kwenda Tigo pesa au airtel money

Sent from my SM-A260F using JamiiForums mobile app
Kwa sasa ambapo huduma ndiyo imeanza, uwezo wa kutuma pesa kwenda mitandao washindani bado.

Ila kwa siku chache zijazo, uwezekano wa kutuma utakuwepo.
 
SSB kabutua hapa ,wamemuingiza chaka watu wa commercial..Azampesa ishafeli kabla ya kuanza....Bakresha kashanunua license TCRA ya mawasiliano kwanini asianzishe kampuni yake ya simu?
 
Ifike pahala serikali iwabane hawa matajiri wafanye biashara kubwa zina tija zaidi kuliko kuwaachia waue vibiashara vidogo vya wananchi wa hali ya chini.

Unataka kutuambia Airtel money, Zpesa, Tigo pesa, Halopesa na M-pesa ni watu wa hali ya chini?

Mcmpangie hela zake, hela anazo za kutosha, hata akianzisha biashara ya kuuza dagaa ni yeye mzee.
 
Isije ikawa kama wale wananunua toyota corrola halafu anaweka chata ya benz. Azam pesa ndani ya Tigopesa.

Tigo, Voda, Artel, Halotel ni washindani wenu au washirika? Anyways, wamiliki wa Azam wana akili ya biashara ngoja tuone.
 
Ninavyoijua mitandao ya simu wakiona anafanya biashara sana tena kupitia laini zao, watalemaza hiyo menu iwe ngumu ku-access. Utakuta katika attemt 5 inafanikiwa moja.

Kama amedhamiria aanzishe mtandao wa simu kabisa tuwe tunanunua na vifurushi kabisa na kujiunga intaneti na kuwapigia wake zetu kwa azam.
 
Unataka kutuambia Airtel money, Zpesa, Tigo pesa, Halopesa na M-pesa ni watu wa hali ya chini?

Mcmpangie hela zake, hela anazo za kutosha, hata akianzisha biashara ya kuuza dagaa ni yeye mzee.
Usipanick fikiria kwa taratibu utaelewa nilichomaanisha.
 
Elimu bado inahitajika tuijue kwanza hiyo azam pesa.
Na sijaona matangazo yake mkuu, imekaaje hiyo mnaitangaza vipi huenda ikaeleweka zaidi kupitia matangazo.
 
Jicho la mwewe! Hii inalenga kwenye kulipia vifurushi katika ving'amuzi vyao;
1.kutakuwa na punguzo kwa wale watakaotumia Azampesa.

2 Kwa Wateja ambao hawatatumia Azampesa watakuwa wanachewa kupata Huduma baada ya kulipia hivyo itawalazimu kujiunga Azampesa. Muda ni hakumu wa kweli.

wakati huo huo wajue kabisa dstv ni 59000tsh complete set na kuna kifurushi cha 9000tsh
 
Back
Top Bottom