Baada ya Kifo cha Rais Magufuli: Nani anafaa kuwa Makamu wa Rais Tanzania?
Dini inamwangusha Bashiru japo anafit, ikiwa hivyo kelele zitakuwa nyingi huku chini, elewa kuwa hakuna mtu anapenda kuongoza huku akipigiwa kelele, ni jpm pekee ambaye hakujali sana kelele za wananchi wake, ndio maana alikuwa akisema yeye hapangiwi.
Bashiru hana sifa ya kuwa VP, hana tena hana kabisa .

Haiwezekani rais alikuwa huko kanda ya ziwa alafu tena vp atoke huko
 
MTAKA sina shaka,ila nchimbi hakuna kitu mule.aliishashika nyazifa kibao ikiwapo mambo ya ndani hakuna alicho deliver.


huyo mtaka nafasi hiyo inamfiti sana,ila mama ndiye mwamuzi wa mwisho,kama hajamuona hakuna namna.
 
He is corrupt!! He is Rostam’s creature!! Angalieni sana influence ya Rostam katika kushawishi ccm nani awe makamu wa Rais! Kundi la Kikwete la mtandao watakuwa mstari wa mbele kutaka kuweka kinyago chao NCHIMBI!!

Hawa wanamtandao ni waporaji wa rasilimali za nchi: msisahau jinsi walivyo ifilisi nchi enzi za Kikwete na sasa watajipanga kurudi!!

Kwa wale wasiomjua Nchimbi fuatilieni historia yake akiwa kiongozi wa vijana na RUSHWA iliyoambatana na ujenzi wa jengo la vijana lililojengwa na ESTEEM construction. Pia fuatilieni uhusikaji wa Nchimbi na kifo cha ajabu cha marehemu [ IPYANA] mtoto wa John Malecela alipokuwa anagombea uongozi wa vijana!!
 
Kwani akiapishwa Mama Samia anaanza uteuzi upya wa baraza la mawaziri?
Hiyo itategemea umakamu wa rais ataupata nani. Kwakuwa huku bara idadi ya Waislamu na Wakristo ni nusu kwa nusu, inawezekana kabisa kukawa na shinikizo kwamba makamu wa rais awe Mkristo ili kubalance na rais ajaye ambaye ni "Muislamu."

Tukumbuke kwamba marais watatu waliopita kuanzia Mkapa wametoka bara, na hivyo ilikuwa umakamu kutoka ZNZ anaangukia kwa asilimia kubwa kwa Muislamu kutokana na wingi wa dini hiyo kule visiwani. Ila kwa bara hali ni tofauti. Sasa basi, ikiwa makamu atakuwa Mkristo, basi waziri mkuu anaweza kuwa Muislamu au Mkristo, lakini Wakristo watapendelea zaidi awe wao kwasababu miaka 5 iliyopita amekuwa "Muislamu."

Kujibu swali lako kuhusu baraza la mawaziri, sio lazima avunje baraza lote na kuteua upya, ila anaweza kuondoa waziri mmoja mmoja na kuweka anaewataka yeye. Yaani atakuwa anapanga na kupangua kwenye wizara, mikoa, wilaya, na kwingineko...
 
Samia anahitaji msaidizi makini na sio mbabaishaji na mtu mnafiki kama NCHIMBI!!
ccm imuangalie kwa jicho la karibu huyo waziri wa usafirishaji Dr. Chamriho; huyu ni mtendaji mzuri asiye na makuu wala makundi! Sio mtu wa kujikweza na mtu rahimu. Ni mtendaji mithili ya marehemu Magufuli. Chumguzeni utendaji wake.
Ni mtu safi hana makandokando kama Nchimbi kwa muda mfupi tu alipokuwa waziri wa Mkwere!
Hao watu wa ujenzi ndio wezi toka 1995 hadi leo. Ni team JPM
 
Hapo yule jamaa wa ardhi anawaangalia kwa mbali alafu anawacheka hi hi hii
 
Umewaza kama mimi Chief, namuona January akienda kushine tena, japo inaweza isiwe kirahisi sana.
Hawa jamaa huwa wana namna ya Ku balance dini ingawa si kigezo rasmi,manake hawana dini.Ila January Muisalmu pamoja na mama sidhani kama wakatoliki watakubali!
 
Back
Top Bottom