Baada ya kubainika ufisadi wa kutisha, anataka kujifichia kwenye Mradi Bandari ya Bagamoyo?

Baada ya kubainika ufisadi wa kutisha, anataka kujifichia kwenye Mradi Bandari ya Bagamoyo?

Kwa kumbukumbu zangu Ndugai alisema bungeni akiwa ktk kiti cha spika kwamba mradi wa Bagamoyo ni wa faida sana ameupitia kwa kina Mpaka huko China.

Baada ya muda mfupi Hayati akaukandia kwa kutoa nukuu ya vipengele kadhaa vya kiunyonyaji ambavyo sisi wananchi hatujui kama ni kweli au sivyo.Hapo ndipo Ndugai ikabidi atumie kanuni ya The boss is always right

Binafsi Siamini yale yaliyosemwa na JPM juu ya mradi huo wala yanayosemwa na wanaoutaka sasa Mpaka nipate "bahati"ya kusoma mkataba huo.

Serikali iruhusu mikataba yenye mivutano kama huu upelekwe bungeni kwa mjadala hapo sisi wananchi tutajua mbivu na mbichi
Watakaoujadili ni wabunge gan labda?,labda bunge livunjwe uchaguzi urudiwe upya tena chini ya tume huru ya uchaguzi
 
Hivi huyo siejii ametoa pia na taarifa ya matibabu ya huyo spika kweli kipindi kile wakati anaumwa??

Manake napo pesa zilizotumika nasikia ni balaa
Huyo mgogo dhaifu kaona ahamishe magoli, atutoe kwenye madudu ya wizi, maana watu wanaweza kukumbushia aliyeweka record ya kuwa mgonjwa ghali nchini.

Everyday is Saturday............................... 😎
Na kweli tunahitaji
CAG atuweke wazi gharama za matibabu ya huyy spekear
 
Hakuna kiongozi ambae simuelewagi kama huyu, hana analolisimamia hana analoliamini, anajazwa.kila kitu. Sijui alikuwaje na hiyo nafasi.
 
Wanataka kuanzisha mradi mwingine halafu wapige. Nchi imejaa watumishi wa aina yake. Hawaogopi kusema uongo hadharani wala kupiga mali ya umma.
 
Eti, Raisi hakushauriwa vizuri kuhusu mradi wa ujenzi bandari ya Bagamoyo, Wakati huohuo yeye ndiye mshauri mkuu wa serikali, alikuwa wapi?

Raisi wetu amefariki ndo kunakupa mwanya wa kumwandama na kumkandia kila Neno Baya, sasa tunataka mtwambie kama Kweli kazi yenu ni kuishauri serikali na kuisimamia

Kabla ya tamko lake Jana kuhusu ujenzi na uwekezaji wa bandari ya Bagamoyo, aliwahi pia kutamka kwamba, mradi huo ni hasara Kwa Serikali Kwa jinsi Mkataba wake ulivyokaa, na kama ndivyo, yeye ndiye ametufanya kama Taifa tuchelewe kuwa na mradi huo,

Sasa Sisi tushike lipi?

Najiuliza, Yeye kama mkuu wa mhilimili huo, anaongoza chombo chenye kazi ya kuishauri na kuisimamia serikali, Alikuwa wapi, mbona alitaka Raisi aongezewe muda wa kutawala? Si ni yeye jamani au ni mwingine!! Je, hakuwa analiona tatizo la ufisadi uliokuwa unaendelea?

Kwa tarifa ya CAG imeibua madudu makubwa na ufisadi wa kutisha, badara ya yeye na mawaziri wote kama sio Bunge loote kuwajibike Kwa kushindwa kuisimamia serikali anaibuka na Jambo la ajabu tu ili kutuondoa kwenye Hilo la ufisadi, hivi mnaaibu kweli nyinyi watu!

Tukionyesha hasira zetu wananchi tuliowatuma kwenda kusimamia rasilimali zetu mnatutumia wasiojulikana, ni Sawa Kwani kufa ni kutangulizana Tu

Tunalitaka Bunge liwajibike katika hili, la sivyo mtuambie ni Kwa nini mlitaka Raisi aongezewe muda

Tunataka pia, mradi wa Ujenzi bandari ya Bagamoyo, Mkataba wake uwekwe mezani tuambie yaliyomo na Kisha Bunge loote livunjwe, Kwani ni hasara tupu!!

Acha tupige 🏋️🏋️🏋️

Kumbe hamuaminiki tena!!

NDUGAI NA BUNGE LAKO MNA KILA SABABU YA KUWAJIBIKA KWA MAPUNGUFU YOTE YALIYOAINISHWA NA REPORT YA CAG KWANI KAZI YENU KAMA BUNGE NI KUISIMAMIA NA KUISHAURI SERIKALI , KAZI AMBAYO HAMKUITIMIZA KWA UFANISI!! NI LAZIMA MUWAJIBIKE.
 
Hili la bandari mtamuenea tu speaker , pamoja na kwamba simpendi Ndugai lakin kwa hili hapana alishawahi liongelea bungeni kuwa huu mradi una faida nyingi kuliko hasara ,gafla mwenda zake akaanza kebeh juu ya mradi huo ,basi kwakuwa mkubwa ni mkubwa ikabid akubaliane nae tu kishingo upande lakin kwa hil job hakuweka unafki kabisa.

Hata Kama mtu Ana mapunguf basi asibebeshwe lawama pale anaposema ukwel ,job yuko sahihi kbs na kwahil ntampambania kabisa tofaut na wengine ambao hawakuwah sema lolote kipind uchwara akiwa hai

Faida na hasara ni Mkataba Kiongozi, sio maneno ya Spika wa Bunge. Kumbukumbu zangu sijawahi kusikia huo Mkataba ukijadiliwa Bungeni.
Aache uhuni huyo jamaa, kama kapokea rushwa tujue pia. Kwa jicho la tatu, huu mradi kung’ang’aniwa kurudishwa sio bure. Ukizingatia kwa wahuni walewale ambao hawajawahi kuisimamia Serikali kikamilifu.
Sasa tunaanzaje kuwa na imani na watu hao wa calibre ya Spika wetu?
 
Faida na hasara ni Mkataba Kiongozi, sio maneno ya Spika wa Bunge. Kumbukumbu zangu sijawahi kusikia huo Mkataba ukijadiliwa Bungeni.
Aache uhuni huyo jamaa, kama kapokea rushwa tujue pia. Kwa jicho la tatu, huu mradi kung’ang’aniwa kurudishwa sio bure. Ukizingatia kwa wahuni walewale ambao hawajawahi kuisimamia Serikali kikamilifu.
Sasa tunaanzaje kuwa na imani na watu hao wa calibre ya Spika wetu?
Ndugaye ang'olewe pale
 
NDUGAI NA BUNGE LAKO MNA KILA SABABU YA KUWAJIBIKA KWA MAPUNGUFU YOTE YALIYOAINISHWA NA REPORT YA CAG KWANI KAZI YENU KAMA BUNGE NI KUISIMAMIA NA KUISHAURI SERIKALI , KAZI AMBAYO HAMKUITIMIZA KWA UFANISI!! NI LAZIMA MUWAJIBIKE.
Ndugaye, ang'oke
 
Eti, Raisi hakushauriwa vizuri kuhusu mradi wa ujenzi bandari ya Bagamoyo, Wakati huohuo yeye ndiye mshauri mkuu wa serikali, alikuwa wapi?

Raisi wetu amefariki ndo kunakupa mwanya wa kumwandama na kumkandia kila Neno Baya, sasa tunataka mtwambie kama Kweli kazi yenu ni kuishauri serikali na kuisimamia

Kabla ya tamko lake Jana kuhusu ujenzi na uwekezaji wa bandari ya Bagamoyo, aliwahi pia kutamka kwamba, mradi huo ni hasara Kwa Serikali Kwa jinsi Mkataba wake ulivyokaa, na kama ndivyo, yeye ndiye ametufanya kama Taifa tuchelewe kuwa na mradi huo,

Sasa Sisi tushike lipi?

Najiuliza, Yeye kama mkuu wa mhilimili huo, anaongoza chombo chenye kazi ya kuishauri na kuisimamia serikali, Alikuwa wapi, mbona alitaka Raisi aongezewe muda wa kutawala? Si ni yeye jamani au ni mwingine!! Je, hakuwa analiona tatizo la ufisadi uliokuwa unaendelea?

Kwa tarifa ya CAG imeibua madudu makubwa na ufisadi wa kutisha, badara ya yeye na mawaziri wote kama sio Bunge loote kuwajibike Kwa kushindwa kuisimamia serikali anaibuka na Jambo la ajabu tu ili kutuondoa kwenye Hilo la ufisadi, hivi mnaaibu kweli nyinyi watu!

Tukionyesha hasira zetu wananchi tuliowatuma kwenda kusimamia rasilimali zetu mnatutumia wasiojulikana, ni Sawa Kwani kufa ni kutangulizana Tu

Tunalitaka Bunge liwajibike katika hili, la sivyo mtuambie ni Kwa nini mlitaka Raisi aongezewe muda

Tunataka pia, mradi wa Ujenzi bandari ya Bagamoyo, Mkataba wake uwekwe mezani tuambie yaliyomo na Kisha Bunge loote livunjwe, Kwani ni hasara tupu!!

Acha tupige [emoji2484][emoji2484][emoji2484]

Kumbe hamuaminiki tena!!
Yaani huyu Ndungai ni wa kuchapwa viboko kabisa
 
Kama nchi yetu kila Chama ni cha majambazi, tufanye nini sasa?
 
Haitakiwi kuwalaumu viongozi wa kipindi cha Jiwe wengi walitetea matumbo yao, hawakutaka kuacha kazi na kwenda kujiajiri, ila walisema vijana wa graduate tujiajiri.
Kutetea matumbo yao je -hata spika? Kiongozi wa muhimili no way. Unatania
 
Ndugai ni spika wa bunge letu ana mamlaka ya kuomba mkataba ukajadiliwa bungeni na Watanzania wakausoma na kuuelewa ila kitendo cha kusema alienda China sijui balozi Kaituki aliwapeleka Shenzein ilipo hiyo kampuni na walipata presentation nzuri mimi binafsi sijamuelewa hao wachina angalieni Zambia wanavyoteseka kwa sababu ya kuwapa kila kitu haijatosha huko Zambia kumekua na polisi wa kichina wakilinda Mali walizochukua kwenye serikali sio watu hao huko Zimbabwe wanapata tabu na mikataba mibovu waliyoingia ya madini na makampuni kutoka China...
 
Msimamo wa Ndilugai toka mwanzo ni kuwa mradi wa bandari ya Bagamoyo ulikuwa mzuri na ulikuwa na faida kubwa kwa nchi. Lakini sijui kulikuwa na mazingira gani, ilimlazimu kubadili msimamo wake baada ya Rais kutoutaka huo mradi.

Kosa kubwa la awamu ya 5 ilikuwa ni kuminya uhuru wa maoni na uhuru wa vyombo vya habari. Kama laiti uhuru wa maoni na wa vyombo vya habari ungelindwa kwa matakwa ya katiba, ni dhahiri watu wengi wangeweza kuuchambua huo mkataba wa ujenzi wa bandari ya Bagamoyo, na kisha hata ambao tusiojua content ya huo mkataba, tungejua kwa uhakika kama mkataba ulikuwa mbaya au mzuri.

Serikali awamu ya 6, lindeni kwa nguvu zote uhuru wa maoni na uhuru wa vyombo vya habari. Kunabfaida nyingi kufanya hivyo kuliko hasara.
 
Back
Top Bottom