Baada ya kulipa Mahari kwao Ndipo nimegundua ana Majini

MUACHE.
 
Iko hiv ongea nae kwanza huyo bint je ana muda gani hayo majini yana msumbua ?na je yupo tatari kuyatoa ?Akisema yupo tayari mpeleke akapate Tiba ni haram mwanadam kumiliki jini
Anasema toka alipokuwa mdogo alikua ana iyo hali, pia akiwa na hasira/ghazabu ndio inatokea mara Kwa mara.
Sasa mi nimemuona iyo mara moja tu na tulikuwa tupo very peaceful tunakula na kupiga story mbili tatu
 
mpeleke wa watumishi wamchomoe hayo majini, na dini apadilishe, utaishije na mwenye majini? kuna majini mengine yanafisha hali yako ya kiuchumi, au utajikuta hampati watoto, anazaa na hayo majini
 
Mkuu hata Mimi nilikuwa nachukulia mambo kimasihara hivi hivi humu jamvini kama wew, paka pale yamenikuta ndio Naona kumbe kuna kupatwa na maswahibu
Mkuu mimi unipe Cardi B sijui Beyonce sijui Miss World nakuwachia mwenyewe, Mimi nachukuwa mwanamke mlevi au mwenye mashetani tu.

Hawa wanawake wana raha zao kama kuku choma mwenye pilipili(periperi)😋😂😂
 

Kinachokuuma ni hiyo mahari
Sasa chagua moja...uoe na majini yake ama usamehe hela uliyotoa

Sisi mahari hatukurudishii
 
Kuna classmate wangu wakati nipo chuo alikutana na kitu kama hii, mtiti wake ilikuwa ni kisanga, hostel nzima tulikuwa tunaenda kumuamulia pale anapokabwa, cha ajabu sasa jamaa alikuwa anampenda demu vibaya sana
 
Hao wazee wa kanzu wamekuruhusuje kirahisi hvyo umchukue binti yao pasipo kugusia swala la dini. Walikua washajua mchezo mzima. Wenyew wameshindwa ku deal nae tangu ypo mdogo wameona ww ndo mkombozi. Hao wazee kabis wa dua hio ishu imewashindaje.

Iyo ishu lazima uwe na roho ngumu. Bora ku deal na majambazi ( physically) vitu unavyoviona kuliko na majini ( spiritual) usio yaona, utapigw matukio kiuchumi, kimaendeleo nk

Mrudishe kwao waambie wa deal nae akikaa saw atarud. Utatoaje kitu amacho hujui ata chanzo chake kimeanzia wap
 
Kulioa mahari kwa yeyote ni upuuzi.

Na majini hayapo, hao wengine wana matatizo ya afya ya akili pengine, ila kwa sababu hatuna wataalam wa mambo hayo tunaita majini tu.
 

Inawezekana lipo kusudi la kukutanishwa nae.
Kama umempenda unaweza kumsaidia kwani hakuna kinachoshindikana kwa MUNGU ila kabla ya kuanza kumsaidia hakikisha unakuwa na vitu vifuatavyo
1. Uwe vizuri kiimani yaani uwe unajua kuomba vizur, Kusali na kutoa sadaka.
2. Uwe jasiri na mwenye msimamo USIOGOPE kwani Kuna muda atakua anabadilika zaid ya hapo unaweza kufikiri unaongea naye au unagombana naye kumbe ni PEPO
3. Usitende dhambi kabisa hasahasa KUZINI kwani mwenyeew utakua unajisindika kaburini kwa kuruhusu mashambulizi.
4. Funga ndoa ya kiimani kama kanisani sio Bomani kwani hyo ya Bomani Haina ulinzi wowote wa kimungu MNAZINI hapo tambua.
5. Uwe mtu wa kufunga at least kwa mwezi mara 3 ili ukae vizuri

MWISHO
Mara nyingi wazazi Huwa wajua haya mambo na Huwa wanawawekea watoto wao ulinzi wa majini pasipo kujua madhara ya baadae kama mikosi,kutoshika ujauzito,mzunguko wa hedhi usio na mpangilio ukiambatana na maumivu makali,kutofanikiwa kiuchumi na mahusiano na kuota ndoto mbaya alafu wenyewe wanaita MAJINI WAZURI.
Hivo kama utaweza kufata ushauri wa hapo juu utamkua mshindi na mtu mwenye mafanikio kama huwezi ACHA kwani vita ya kutoa Hayo madude na huku MNAZINI ni Kali sana utakufa siku sio zako.
KILA LA KHER I!!
 
Kinachokuuma ni hiyo mahari
Sasa chagua moja...uoe na majini yake ama usamehe hela uliyotoa

Sisi mahari hatukurudishii
Pesa sio kila kitu, msaada
Mkuu Hilo ndio namimi nalihofia, ku deal na vitu visivyoonekana ni jambo lisilomithilika. Hofu yangu ni kwamba ikitokea akajua ninamwacha kwa sababu ya hayo mavitu je hawezi yatumia dhidi yangu kunidhuru? Ukizingatia ni MTU anayenipenda sana kwaio atafanya kisasi namm kuona nimemwacha
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…