Baada ya kulipa Mahari kwao Ndipo nimegundua ana Majini

Baada ya kulipa Mahari kwao Ndipo nimegundua ana Majini

Huko bomani unafata nini sasa ina maana ukilipa mahali bila kwenda huko haiwi ndoa? Hayo mavyeti mnayoyakimbilia huko ndio yanawaponza alafu mnarudi hapa kutia huruma
 
Huyo hana majini wala nini,hakutaki tu kua Mume wake,umechezewa game na wewe ukaingia Kingi,

Miaka 3 ungekua umeshamjua au watu wa Nyumbani kwao wangekua wamesha kuambia.
Nakazia hapa aisee. Ni juzi au Jana nilikuwa napita mahala nikaona kihoja Cha mwanamke kaketi koridoni Kwenye kijumba anawapazia sauti wapita Njia eti udugu uduguuu udugu wangu.. anaeitwa ndio kwanza akawa anaongeza mwendo kuonesha kakerwa. Nikawambia niliokuwa nao uswahili ni kirusi kipya kitafutiwe chanjo mapema. 😂
 
Pole sana, kuwa nae au kumuacha ni maamuzi yako. Ila ukiwa nae lazima utambue kuwa mkeo ana tatizo la ugonjwa wa majini ili umtafutie tiba au uishi nae hivyo kwa hali hiyo.
 
Majini yanaondoka kirahisi kwa maombezi. Dua zinayatuliza yanabaki humohumo na Siku moja yatalipuka tena.
Kama hutaki kimpeleka kanisani kuombewa inawezekana kifo kinakutafuta, usifikiri hilo jini linapotulia linaondoka la, linaishi nae mchana na usiku, ni kiti chake, wewe umechumbia kiti cha majini,
Kumbuka yeye majini yanaendana na Imani yake, wewe Imani ya kikristo Ina uadui na majini, halafu unajilengesha..
 
Wakuu kwema?
Ipo hivi, nimekuwa kwenye mahusiano na binti fulani Kwa muda wa miaka mitatu.

Mwanzoni mwa mwaka huu nikasema sasa ni muda muafaka wa Mimi kwenda nyumbani kwao nikatoe mahari ili nimiliki mke rasmi.

Kweli tarehe za mwanzo wa mwezi January mwaka huu, nilipeleka ujumbe wangu kwao na binti, tukakubaliana mahari, nikalipa kiasi chote cha mahari tulichokubaliana.

Sasa wakati tukiwa tumeanza taratibu zingine ili tufunge ndoa ya bomani kwa maana tunatofauti ya kiimani Kati yetu, Ndipo nimegundua hii kitu.
Binti ana maruhani/majini, nimeshuhudia kwa macho yangu akifanya jambo lisilo la kawaida.

Tulikiwa tunakula chakula wote, mara gafla akaanza kudai kifua kinamuuma na akaanza kujishika kifua chake karibu na shingo na kujibana.

Kwakuwa sikuwahi kumuona kwenye hali hiyo, Nilinyanyuka gafla kutoka kweny kiti nilichokuwa nimekaa ili kumpa msaada Lakini nilikutana na upinzani wa hali ya juu sana kutoka kwake. Niliomba msaada kwa majilani ndipo walitokea watu wa wakunisaidia na hapo hapo nikapiga simu kwao ili nipate ufafanuzi labda hii hali wanaijua, wakaniambia nimwache atatulia mwenyewe.

Baada ya siku mbili kupita nimekaa nae chini kumuuliza kwanini alikuwa vile majibu yake ni kuwa ana Majini, nimejaribu kuuliza baadhi ya ndugu zake nao kumbe wanafahamu.

Nimemuuliza kwanini hakuniambia mapema majibu yake eti ningemuacha, sasa nifanyeje ndugu zangu na mahari nimeshalipa?
Napata shida kuelewa jambo hapa ina maana ndani ya miaka yote 3 hkujua chochote au mlikuwa mnaishi mbali mbali lakini hatakama bado hainingi akilini kusema baada ya kulipa mahari ndo ukagundua kama ana majini
 
Majini yanapaswa yabomolewe kinyeo vizuri tena Ile staili ya chumba magimbi mbona yatakimbia yenyewe 😅wewe unapiga kimoko wa Do you expect
 
Watu wakifanya mapenz Huwa yanachungulia au😃
Nimemkumbuka jirani yangu yeye akitaka kuchepuka anapandisha huko huko hata km ni guest na anarudi nyumbn ivoivo km alikuwa kaanza kuvua ni anatoka hivohivo anakuja Kwa mumewe 🤣🤣🤣🤣
Hao wapuuzi huwa asilimia kubwa hawapendi uzinifu au uchepukaji😁
 
Napata shida kuelewa jambo hapa ina maana ndani ya miaka yote 3 hkujua chochote au mlikuwa mnaishi mbali mbali lakini hatakama bado hainingi akilini kusema baada ya kulipa mahari ndo ukagundua kama ana majini
Ni kwamba iyo miaka mitatu ni long distance relationship, hatukuwahi kukaa nyumba moja hata Kwa siku tatu. Nadhani nilifanya makosa kwa kushindwa kupeleleza kiundani zaidi kuhusu familia yake, na hii ilisababishwa na mapenzi makubwa aliyonayo kwangu kwaio sikujishughulisha Sana kumfatilia. Sasa baada ya kuwa nimeshatoa mahari Ndipo nilimtoa nyumban kwao ambapo ni mkoa tofauti nikasafiri nae paka mkoa ninakoishi Mimi, Ndio nimejionea hii Hali na kuamua kumuuliza na jibu lake ndio hilo
 
Wewe ni mtu wa Imani Gani? Na yeye je?

Kuna njia tatu ila nitasema mbili tu.

1. To cast out all demon by the power of the Holy Spirit na Kwa jina la Yesu ... Tafuta madhabahu yenye watumishi WA kweli

Ila hii ni mpaka muhusika awe tayari!

2. Hii kutuliza majini kwa kuagua ... Kule kwetuu Tanga tunafanya sana! Huondoi jini ila unalituliza tu

Maamuzi ni yako!.

Mh. Mwenyekiti TUNDU LISU anakupa pole
Ila unajua kufukuza jini Moja yanaweza kuleta tisa😂😂
Bora tu akae na huyo jini mmoja
 
Huko bomani unafata nini sasa ina maana ukilipa mahali bila kwenda huko haiwi ndoa? Hayo mavyeti mnayoyakimbilia huko ndio yanawaponza alafu mnarudi hapa kutia huruma
Kwa hiyo ukitoa mahari ndo ushaoa, utaratibu mpya huu
 
Ni kwamba iyo miaka mitatu ni long distance relationship, hatukuwahi kukaa nyumba moja hata Kwa siku tatu. Nadhani nilifanya makosa kwa kushindwa kupeleleza kiundani zaidi kuhusu familia yake, na hii ilisababishwa na mapenzi makubwa aliyonayo kwangu kwaio sikujishughulisha Sana kumfatilia. Sasa baada ya kuwa nimeshatoa mahari Ndipo nilimtoa nyumban kwao ambapo ni mkoa tofauti nikasafiri nae paka mkoa ninakoishi Mimi, Ndio nimejionea hii Hali na kuamua kumuuliza na jibu lake ndio hilo
Una haki y kurudishiwa mahari yako na kama itashindikana samehe fungua ukurasa mwingine wahenga walisema ukikosea kujenga utabomoa ila cyo kuoa
 
Wakuu kwema?
Ipo hivi, nimekuwa kwenye mahusiano na binti fulani Kwa muda wa miaka mitatu.

Mwanzoni mwa mwaka huu nikasema sasa ni muda muafaka wa Mimi kwenda nyumbani kwao nikatoe mahari ili nimiliki mke rasmi.

Kweli tarehe za mwanzo wa mwezi January mwaka huu, nilipeleka ujumbe wangu kwao na binti, tukakubaliana mahari, nikalipa kiasi chote cha mahari tulichokubaliana.

Sasa wakati tukiwa tumeanza taratibu zingine ili tufunge ndoa ya bomani kwa maana tunatofauti ya kiimani Kati yetu, Ndipo nimegundua hii kitu.
Binti ana maruhani/majini, nimeshuhudia kwa macho yangu akifanya jambo lisilo la kawaida.

Tulikiwa tunakula chakula wote, mara gafla akaanza kudai kifua kinamuuma na akaanza kujishika kifua chake karibu na shingo na kujibana.

Kwakuwa sikuwahi kumuona kwenye hali hiyo, Nilinyanyuka gafla kutoka kweny kiti nilichokuwa nimekaa ili kumpa msaada Lakini nilikutana na upinzani wa hali ya juu sana kutoka kwake. Niliomba msaada kwa majilani ndipo walitokea watu wa wakunisaidia na hapo hapo nikapiga simu kwao ili nipate ufafanuzi labda hii hali wanaijua, wakaniambia nimwache atatulia mwenyewe.

Baada ya siku mbili kupita nimekaa nae chini kumuuliza kwanini alikuwa vile majibu yake ni kuwa ana Majini, nimejaribu kuuliza baadhi ya ndugu zake nao kumbe wanafahamu.

Nimemuuliza kwanini hakuniambia mapema majibu yake eti ningemuacha, sasa nifanyeje ndugu zangu na mahari nimeshalipa?
Ishi naye tu ila kama hayo majini ni ya kiume ujiandae kuwa unapigwa miti ukiwa usingizini
 
Back
Top Bottom