naomba na mimi nitoe shukrani zangu kwa Jakaya kikwete kwenye uzi wako
Kiukweli nimeshindwa kujizuia kutoa shukrani za dhati kwa Jakaya Kikwete kwa uzalendo wake katika hii nchi. Kikwete wewe ni jabali, mwanajeshi wa ukweli bila magwanda.Watu wanasema huna akili na wanasahau wewe umelamba digrii UDSM kipindi hakuna google wala wikipedia.
Tena digrii ya nguvu ya uchumi sio ya sociology wala PSPA, huku wao wanaokuponda wamesoma miaka ya google ila UDSM tu wameshindwa kusoma kwa kukosa vigezo wameishia vyuo ulivyowaletea vya msaada.
Mtu amesoma Sauti au Jordan tena digrii ya ualimu, sociology au development studies. Halafu linaponda eti JK hana akili.Lenyewe UDSM tu limeshindwa kufika hii internet era.
Umefanya mengi sana makubwa hii nchi. Shule za kata leo house girl tu kumpata shida. Kila mtoto anafika sekondari.
UDOM ambayo ni jengo la CCM chimwaga ndio lililoanzisha chuo leo watu walioshindwa kufika UDSM wanapata nafasi ya kusoma nao chuo kikuu ila kwa kukosa shukrani wanakutukana.
Mabasi ya mwendokasi ni uroda. Asante sana Kikwete kuna mijinga inakuponda hujafanya kitu huku inapanga foleni kila siku na kadi zao za malipo kusubiri mabasi ya mwendo kasi. Kikwete unawacheka tu ukiwa Msoga na majuu kwenye trip zako zile.
Muhimbili heart institute, barabara leo Mwanza tunaenda siku moja tu full lami na bus luxury kama Dar lux, Green star, na mengineyo kiyoyozi from Dar to Mwanza kisa uzuri wa bara bara ulizojenga. Kuna wajinga wanasema hujafanya kitu huku inacharge simu zao kwenye hizo bus ikiwa safarini ( wanafikiri bila uzuri wa bara bara ni mtu gani angeweka ma bus mazuri kama hayo?)
Daraja la Kigamboni, Terminal 3 new airport DSM. Kitu JK Nyerere kama Dubai vile.
Mwisho kabisa kumpa nchi Rais Magufuli jembe ni bonge la zawadi kwa watanzania wote wapenda maendeleo ya nchi yao.
Mafisadi wanahaha kila siku wanadata kwa kasi ya Rais Magufuli na nina amini Tanzania mpya imeshazaliwa.
Ila Kikwete umetisha sana hasa style yako ya majina mfukoni na kumtanguliza Membe kama fake choice na kuweza kuwafool wana CCM 3000.
Barcelona walitawala mpira kwa style ya fake no 9 na Kikwete umeweza mpitisha Rais Magufuli wa style ya fake no 9 pia kwenye siasa.
Yaani unaudanganya uma kwa kumtanguliza mtu asiyefaa ili mabeki wamkabe asiwafunge kumbe mfungaji yupo nyuma. Anawafunga kiulaini tu.