LGE2024 Baada ya kupuuza Ule msemo wa jinsi ya kula na kipofu, Leo wanatafutwa wananchi wa kujiandikisha Kwa tochi ili kura ziibwe!

Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024
walikojiandikisha kupiga kura Serikali za mitaa wajaa sana kwenye kampeni za CCM,

wachache ambao hawakujiandikisha kwasabb za ushirikina wao, wakua kwenye kampeni za upinzani wakipeana matumaini na muujiza wa kushinda uchaguzi 🤣
 
Wananchi wengi wamejiandikisha tayari kukipa chama CCM ushindi wa kishindo. Huu uzi wenu ni wa kujifariji.
 
Hovyo sana.
 
Hawaamini macho yao. Naona baadhi ya watumishi wa umma wanaposti poster za kuamashisha watu kujiandikisha. Nadhani watakuwa wamewalazimisha kufanya hivyo. Vituoni hali ni mbaya.
Wanadhani tatizo ni matangazo ya kuhamasisha, bila kujua watu wameamua hawataki upuuzi tena.
 
😁😁😁

Tanzania ni channel ya comedy kule mbinguni
 
Leo nimewaona watumishi wa manispaa fulani Dar wanavyohangaika kuhamasisha. Zimemwagwa 'reflectors' kibao mpaka kwa bodaboda.Na hapa pia lazima kuna wizi kama kawaida.
 
Wameamua kuwaangushia jumba bovu viongozi wao wanaomaliza muda wao kuwa ndiyo wanaovuruga zoezi la uandikishaji wapiga kura wakati ni wao wenyewe walioratibu uhuni huu ili kuficha aibu ya watu kususia kujiandikisha.
Spana zimekuwa Kali, wanataka kujisafisha kiaina.
 
Wenyewe waliojikoni walishasema kupiga kura na kuhesabu vitu viwili tofauti.
 

Elimu ya uraia inahitajika sana, ili raia wajue na kusimamia HAKI na WAJIBU wao.
Ikiwemo hii ya kushiriki katika kuchagua viongozi
 
Hiyo KAZI mnayofanya ni kama tu ulozi,

Ukitafuta sababu na faida ya kuwafanya watu kama wajinga huioni.

Ndio maana Hayati Nyerere alitishia kurudisha Kadi!
 
Sasa mtamtoaje na hamjajiandikisha? Na hata mkimkataa, anaiba kura,

Njia mbadala ni ipi?
 
Elimu ya uraia inahitajika sana, ili raia wajue na kusimamia HAKI na WAJIBU wao.
Ikiwemo hii ya kushiriki katika kuchagua viongozi
Sasa umejiandikisha halafu unamsikia mgombea anaongea Kwa dharau kuwa, hata msiponichagua,

Mimi ndiye nitakayeshinda uchaguzi na hachukuliwi hatua yeyote,

Nini kinajengeka akilini mwako?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…