Baada ya Lissu kutwaa madaraka, wale waliotenda makosa wakiwa madarakani wasamehewe tuanze upya au Sheria ifuate mkondo wake?

Mkuu Erythrocyte baada ya October 2020 Nahisi tutatofautiana iwapo tu sheria ikipindishwa kuwasamehe wahalifu wa awamu ya5 na wale waliowatangulia huko nyuma. Rais mtarajiwa TAL akiwasamehe wahalifu waliotangulia nyuma yake hakika hatakuwa na utofauti wowote na hao wahalifu, anatakiwa awe mfano wa utawala wa sheria ambao amekuwa akituhubiria kila siku, AWAHUKUMU KWA MUJIBU WA SHERIA!

List ni ndefu kidogo, kila mtu ahukumiwe kadiri ya uhalifu alioufanya
 
Lisu na Chadema hwafai kuongoza watajishughulisha na visasi zaidi. Ni hatari na nchi itayumba. Hatujapata chama pinzani komavu.
 
Lissu atakuwa rais lini??
 
Kitawekwa kipengele cha Tume ya Maridhiano ndani ya Katiba Mpya,lakini kwa wale watakaokiri kutenda uhalifu,ila vichwa ngumu wapambane na sheria ambazo zingine wao wenyewe walishiriki kuzishabikia na kuzipitisha kwa mbwe mbwe hata wakati mwingine usiku wa manane kwa kura ya ndiyooo!
 
Fisi alimfuata binadamu akifikiria mkono utadondoka autafume akaishia kumsindikiza mpaka mlangoni akaingia ndani na fisi akarudi na uchu wa nyama.
 
Tulishatoka huko ndio maana awamu ya Tano ikaanzisha mahakama ya mafisadi.

Msitupotezee muda njooni ni sera mpya.
 
Huu utoto wenu unaompa kichwa Lissu kuropoka ovyo ndio utakao mponza na mnamfanya aishi kwa hasira kila siku kwa kumkumbushia masahibu yaliyo mkuta. Jamaa anabaki kuangalia nyuma badala ya ku move on na maisha.

South Africa awakuwa wajinga baada ya kutoa apartheid kuanzisha ‘Truth and Reconciliation Council’ ili wasamehe ya kale na yapite vinginevyo nchi yao isingekuwa na amani.

CDM kila kukicha mnamchochea Lissu na yeye anaripuka tu ovyo hata anachoongea saa zingine uelewi na deep down mnajua awezi shinda, sasa hizo hasira zake asipozituliza ipo siku atazungumza mambo ya nchi sensitive ya National security jamaa wakashindwa mvumilia tena.
 
Mkuu kila mtu ataenda kula alipopeleka mboga ,kumpiga tundu lissu risasi 16 , unamuua ben saa8 , unamuua azory halafu useme tukusamehe wakati wanajulikana waliofanya hivyo? Sheria lazima ichukue mkondo wake hakuna namna kuna vitu vya kusamehe lakini sio unyama huu walioufanya.

Ingekuwa wizi ni tungetaifisha mali zao ila kuua lazima nao wauawe "ilaji ilaji" dawa ya moto ni moto.
 
Kinachotakiwa audio clips za Lissu zitolewe tujue alikuwa anafanya uhaini gani nyuma ya pazia. Sio kumfichia siri.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…