Baada ya Malalamiko ya wananchi, Serikali yasitisha bei mpya za vifurushi

Baada ya Malalamiko ya wananchi, Serikali yasitisha bei mpya za vifurushi

IMG_20210402_201224.jpg
 
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano kwa Umma wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Semu Mwakyanjala, amesema matumizi ya bei mpya ya vifurushi yamesitishwa kwa muda....
Je ni kutokana na ombi la DC wa Kisarawe?

Au anapingana na yule Waziri wa vifurushi aliyesema anaanza kuitoza kodi whatsapp
 
Walizuia sherehe za pasaka zisiwepo, watu walipolalamika wakaruhusu ziwepo.Wakapandisha bei za vifurushi, watu walipolalamika wamesitisha.Naona umakini wa viongozi wa awamu hii katika kufanya uamuzi si wa kujiamini.
 
Angekuwa fulani angesema tunapoteza muda wa kulima kwenye mitandao hivyo tutwangwe haswaaa na angeungwa mkono. Haya mzee Slaa tayari tangazo lingine limetoka wahi ukapongeze. Yani ukimaliza huu mwezi ukiwa balozi nenda katambike!

Hii kodi ilipendekezwa kuendana na utashi wa jiwe, saa hii watu wamepinga na kwa vile hayuko yule dhalimu, ndio wanapotezea.
 
Inasitisha ?, Aliyeleta hizi Bei Elekezi na kupelekea huu Utani kutokea ni nani?

Wamewapangia bei elekezi na wao wakaondoa offer zote wakacheza mule mule kwenye uelekezi.......

Hawa TCRA hawa...., Bure Kabisa....
 
Dar es Salaam. Saa chache baada ya kutangazwa kwa bei mpya za vifurushi, Serikali imetangaza kusitisha kutumika kwa gharama hizo hadi hapo itakapotangazwa baadaye.

Uamuzi huo unaweza kuwa habari njema kwa watumiaji wa mitandao ya simu ambao, tangu kutangazwa kwa bei hizo mpya mapema leo Ijumaa ya Aprili 2, 2021, wamekuwa kwenye mjadala mzito kwani, matarajio ya wengi ilikuwa ni kushuka kwa gharama hizo.

Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano kwa Umma wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Semu Mwakyanjala, amesema matumizi ya bei mpya ya vifurushi yamesitishwa kwa muda.

Hata hivyo, amesema uamuzi huo utahusu vifurushi vya data pekee huku vile vya ujumbe mfupi wa maneno na kupiga zitaendelea kama ilivyotangazwa mapema leo Ijumaa.

“Tumesitisha matumizi ya gharama mpya za vifurushi hadi hapo itakapotangazwa baadaye. Lakini, hili litahusu vifurushi vya data pekee na vile vya sms na kupiga vitaendelea kama kawaida,” amesema Mwakyanjala alipozungumza na Mwananchi kwa njia ya simu dakika chache zilizopita.

Kanuni ndogo za gharama na tozo za vifurushi, utangazaji wa huduma na ofa maalum zilizotungwa na TCRA, zimeanza kutumika leo ambapo, matumaini ya wengi ilikuwa ni bei za vifurushi kupungua lakini ikawa tofauti.
 
Hili linajulikana
Wanampima madam president
Sijui kama j4 kumekucha salama kwa waziri huyu

Hujuma ndani ya serikali, hawataki kushirikiana asema Katibu Mkuu Kiongozi Hussein Katanga na akashangaa wizara kutofanya kazi kama serikali moja.

TCRA na wizara ya Tekenolojia Hawajui bando hutumika hata vyuoni wanafunzi kupata lecture na material, tele-health video conferencing kwa huduma za afya n.k

Hivi TCRA na wizara mama ya Tekenolojia waliwasiliana na wizara ya elimu, elimu ya juu au wizara ya afya, Wizara ya Biashara na Mapinduzi ya Nne ya Viwanda / Fourth Industrial revolution ktk uzalishaji, masoko , uendeshaji viwanda n.k na kujua umuhimu wa bando nafuu au waliangalia tu Idara ya Maelezo propaganda ya Dr. Abbas ilivyonuia na inavyotaka kama ktk utawala wa mwendazake John Magufuli (RIP) kubana tu maoni ya wananchi ktk kupashana habari na medani ya siasa?

Wanataka kutuchelewesha hawa wafuasi wahafidhina wa mwendazake waliobaki kina Dkt. Hassan Abbas, Msemaji Mkuu (MAELEZO), TCRA, wizara mama na wale makada wa mtaa wa Lumumba Ofisi Ndogo.

Imagewww.cnn.com
Africans face most expensive internet charges in the world, new report ...
DR Congo has the cheapest internet service charges from amp.cnn.com
22 Oct 2019 — Citizens of Chad, DR Congo, and the Central African Republic must all pay more than 20% of average earnings
.................................................................

Mbinu za maendeleo katika mapinduzi ya nne ya viwanda : Total Change

5 Dec 2019
Kongamano la vijana katika ushiriki wa mapinduzi ya maendeleo ya nne ya viwanda ambapo wameseme vijana wanatakiwa kuona fursa za maendeleo na kuwa wabunifu katika kutumia Teknolojia hasa katika viwanda. Kwa habari za uhakika kutoka nyanja mbali mbali tembelea www.dar24.com
 
Back
Top Bottom