Baada ya Malalamiko ya wananchi, Serikali yasitisha bei mpya za vifurushi

Baada ya Malalamiko ya wananchi, Serikali yasitisha bei mpya za vifurushi

#BREAKINGNEWS Serikali imesitisha gharama mpya za vifurushi hadi hapo baadae.Imeangiza vifurushi vya zamani kuendela kutumika.

20210402_221643.jpg
 
katika hili la kupandishwa kwa gharama za vifurushi wa kilaumiwa sio mama samia, ni mwendazake.

Mwendazake alikuwa hapendi kukosolewa, alionyesha chuki ya wazi kabisa kwa watu waliokuwa wanamkosoa kupitia mitandao ya kijamii. Akafikia hatua ya kutamani malaika washuke wazime mitandao yote.

washauri wake kwa kutambua chuki ya wazi ya boss wao kwenye mitandao, wakaona bora wamfurahishe, wakaja na idea za kutumia vpn kwa upande wa twitter (japo haijasaidia) na kuongeza gharama za vifurushi.

Matokeo ya idea hizo ndio hii bei mpya ya kikatili ya vifurushi. ndungulile na team yake walisukumwa zaidi na utashi wa kisiasa kuliko utu ili wamfurahishe boss wao ambaye kwa sasa ni marehemu.

sina shaka na Mama Samia, najua atafikishiwa malalamiko kuhusu vifurushi hivi vya sasa ambavyo sio rafiki kwa mwananchi mwenye kipato cha chini na haraka sana atatoa amri ya kuvisitisha.

asante mama samia kwa kusikiliza kilio chetu.
IMG-20210402-WA0019.jpg
 
Friday April 02 2021

Mwananchi Gazeti

Dar es Salaam. Saa chache baada ya kutangazwa kwa bei mpya za vifurushi, Serikali imetangaza kusitisha kutumika kwa gharama hizo hadi hapo itakapotangazwa baadaye.

Uamuzi huo unaweza kuwa habari njema kwa watumiaji wa mitandao ya simu ambao, tangu kutangazwa kwa bei hizo mpya mapema leo Ijumaa ya Aprili 2, 2021, wamekuwa kwenye mjadala mzito kwani, matarajio ya wengi ilikuwa ni kushuka kwa gharama hizo.

Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano kwa Umma wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Semu Mwakyanjala, amesema matumizi ya bei mpya ya vifurushi yamesitishwa kwa muda.

Hata hivyo, amesema uamuzi huo utahusu vifurushi vya data pekee huku vile vya ujumbe mfupi wa maneno na kupiga zitaendelea kama ilivyotangazwa mapema leo Ijumaa.

“Tumesitisha matumizi ya gharama mpya za vifurushi hadi hapo itakapotangazwa baadaye. Lakini, hili litahusu vifurushi vya data pekee na vile vya sms na kupiga vitaendelea kama kawaida,” amesema Mwakyanjala alipozungumza na Mwananchi kwa njia ya simu dakika chache zilizopita.

Kanuni ndogo za gharama na tozo za vifurushi, utangazaji wa huduma na ofa maalum zilizotungwa na TCRA, zimeanza kutumika leo ambapo, matumaini ya wengi ilikuwa ni bei za vifurushi kupungua lakini ikawa tofauti.

Mwanzoni mwa Machi, 2021 Mkurugenzi Mkuu wa TCRA, James Kilaba aliahidi utekelezaji wa kanuni hizo za kukabiliana na malalamiko juu ya huduma ya vifurushi yaliyotokana na maoni 3, 278 yaliyotolewa na wananchi.

Baadhi ya changamoto ambazo watumiaji wa huduma za simu walikuwa wakikutana nazo na kuzilalamikia ni pamoja na gharama za vifurushi kuwa juu na vifurushi vya data kubadilika mara kwa mara.

Jana mitandao ya simu iliwataarifu watumiaji wake juu ya mabadiliko hayo, lakini jambo ambalo limewaibua wengi hususani katika mitandao ya kijamii ni kuminywa kwa vifurushi hivyo kuliko hata ilivyokuwa awali wakati wanatoa malalamiko hayo.

Katika makundi ya mtandao wa kijamii wa WhatsApp na mitandao mingine ya kijamii inayokutanisha watu kama Twitter, Instagram na Facebook mjadala ni vifurushi ambavyo vimebadilika katika mitandao yote ya huduma za simu wengi wanaomba walau hali irudi kama ilivyokuwa.

Mitandao mbali ya simu kama ilivyo ada katika sikukuu mbalimbali ilituma salamu zao za sikukuu kupitia kurusa zao za mitandao ya kijamii, lakini maoni ya wananchi wengi si kupokea salamu hizo bali ilikuwa ni kulalamikia mabadiliko yaliyofanywa katika vifurushi.

Zaidi, soma: Tanzania na Vifurushi vipya vya Data na Sauti (Aprili 2021) - Mwitikio wa wananchi
View attachment 1741566

Kwa hili kosa ilitakiwa Dr Faustine Ndugulile ajiuzulu mara moja kwa kudanganya umma ,alishupalia kwamba gharama zitashuka za data kutoka sijui Tsh 50 hadi 2 mpaka 9 Tsh ,cha ajabu gharama zime double , yaani 1000 napata MB 350??? 10000 GB 4 kutoka GB 12? TCRA inabidi wakusanye maoni upya maana tunarudi nyuma ,nchi nyingi gharama za internet zipo chini sana ila huku wanazidisha.

Na pia wasiangalie gaharama kubwa za data ,waangalie pia Mobile Money ,tozo za kutuma na kutoa pesa ni kubwa sana ,kila siku tunaona makampuni wanatoa records zao za faida kwa kuwakamua wananchi...imagine voda inaingiza mabilioni ya shillingi kwa mwezi kutoka kwenye Mpesa yaani wanatengeneza faida maradufu kwenye Mpesa,why TCRA wasi regulate faida kama EWURA wanavyoregulate price ya mafuta? How Mpesa waingize faidi ya zaidi ya bilioni 15 kwa mwezi? Huo si wizi? Kwanini gharama za kutuma na kutoa wasipunguze?
 
Friday April 02 2021

Mwananchi Gazeti

Dar es Salaam. Saa chache baada ya kutangazwa kwa bei mpya za vifurushi, Serikali imetangaza kusitisha kutumika kwa gharama hizo hadi hapo itakapotangazwa baadaye.

Uamuzi huo unaweza kuwa habari njema kwa watumiaji wa mitandao ya simu ambao, tangu kutangazwa kwa bei hizo mpya mapema leo Ijumaa ya Aprili 2, 2021, wamekuwa kwenye mjadala mzito kwani, matarajio ya wengi ilikuwa ni kushuka kwa gharama hizo.

Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano kwa Umma wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Semu Mwakyanjala, amesema matumizi ya bei mpya ya vifurushi yamesitishwa kwa muda.

Hata hivyo, amesema uamuzi huo utahusu vifurushi vya data pekee huku vile vya ujumbe mfupi wa maneno na kupiga zitaendelea kama ilivyotangazwa mapema leo Ijumaa.

“Tumesitisha matumizi ya gharama mpya za vifurushi hadi hapo itakapotangazwa baadaye. Lakini, hili litahusu vifurushi vya data pekee na vile vya sms na kupiga vitaendelea kama kawaida,” amesema Mwakyanjala alipozungumza na Mwananchi kwa njia ya simu dakika chache zilizopita.

Kanuni ndogo za gharama na tozo za vifurushi, utangazaji wa huduma na ofa maalum zilizotungwa na TCRA, zimeanza kutumika leo ambapo, matumaini ya wengi ilikuwa ni bei za vifurushi kupungua lakini ikawa tofauti.

Mwanzoni mwa Machi, 2021 Mkurugenzi Mkuu wa TCRA, James Kilaba aliahidi utekelezaji wa kanuni hizo za kukabiliana na malalamiko juu ya huduma ya vifurushi yaliyotokana na maoni 3, 278 yaliyotolewa na wananchi.

Baadhi ya changamoto ambazo watumiaji wa huduma za simu walikuwa wakikutana nazo na kuzilalamikia ni pamoja na gharama za vifurushi kuwa juu na vifurushi vya data kubadilika mara kwa mara.

Jana mitandao ya simu iliwataarifu watumiaji wake juu ya mabadiliko hayo, lakini jambo ambalo limewaibua wengi hususani katika mitandao ya kijamii ni kuminywa kwa vifurushi hivyo kuliko hata ilivyokuwa awali wakati wanatoa malalamiko hayo.

Katika makundi ya mtandao wa kijamii wa WhatsApp na mitandao mingine ya kijamii inayokutanisha watu kama Twitter, Instagram na Facebook mjadala ni vifurushi ambavyo vimebadilika katika mitandao yote ya huduma za simu wengi wanaomba walau hali irudi kama ilivyokuwa.

Mitandao mbali ya simu kama ilivyo ada katika sikukuu mbalimbali ilituma salamu zao za sikukuu kupitia kurusa zao za mitandao ya kijamii, lakini maoni ya wananchi wengi si kupokea salamu hizo bali ilikuwa ni kulalamikia mabadiliko yaliyofanywa katika vifurushi.

Zaidi, soma: Tanzania na Vifurushi vipya vya Data na Sauti (Aprili 2021) - Mwitikio wa wananchi
View attachment 1741566

Walitaka to Kumfitinisha ( Kumgombanisha ) Rais Mheshimiwa Mama Samia Suluhu Hassan na Watanzania ili aonekane mbaya na hafai kisha sababu ipatikane.

Wakasahau kuwa huyu Mama ni Mwanamke Mwerevu, Mjanja, ana Exposure Kubwa, Mtoto wa Mjini vile vile halafu siyo Mshamba ( Mbwiga ) kama wengineo hivyo nae kawawahi mapema mno.

Na kutokana na Upuuzi huu huenda Siku ya Jumanne ijayo Mtu au Watu yakawakuta makubwa kiasi hata cha kuweza Kugharimu Vyeo vyao kwani Kitendo walichokifanya Leo kilikuwa ni Kuwakomoa na Kuwakandamiza Watumiaji Simu Wanyonge wa Tanzania.
 
Samia oyeee.Ndugulile ondoa idea za Magufuli. Magufuli alitaka kupandisha vifurushi ili watu wasiingie mitandao ya jamii,ili wasihabarike. Maana mitandao ya jamii ndo source ya habari. Magufuli kafa. Acheni kufufua idea zake za kijinga.
 
Aisee!!

Sema tu kwamba, kutukana ni Matumizi mabaya ya akili!!

Serikali hongereni kwa hili
 
Back
Top Bottom