Baada ya muhula huu, Rais Samia Suluhu Hassan anaweza kuchaguliwa kushika kiti hicho mara moja

Baada ya muhula huu, Rais Samia Suluhu Hassan anaweza kuchaguliwa kushika kiti hicho mara moja

2025 wingi ni kubwa mno. Ccm wanatunga yao, ulifika muda huo utaona wagombea 150 wanautaka urais. Wa kwanza M. M yule wa fedha
Ikifika 2025 kale kautamaduni ka ccm kakuprint fomu moja ya mgombea rais watajifanya hawakajui.
 
Kulingana na katiba SSH hawezi kukaa madarakani miaka 14 ,
Ingewezekana kama magufuli angefariki madarakani amebakiza miaka 3 kushuka chini.
Maximum yake ni 9 years
 
Miaka 14 kutoka sasa. Soma ibara ya 40 (2).

Kama unayo ibara nyingine ya kuonesha miaka 9 naomba ilete hapa tuijadili.
Kutoka sasa hadi 2025 ni kipindi cha miaka minne.

Kwa mujibu wa Katiba ibara ya 40(4) hapa chini; anaruhusiwa kugombea Urais mara moja kwa kipindi cha miaka mingine mitano tu.

Kama atashida atakuwa na jumla ya miaka tisa tu. Umechemka Mkuu.
IMG-20210419-WA0008.jpg
 
Kutoka sasa hadi 2025 ni kipindi cha miaka minne.

Kwa mujibu wa Katiba ibara ya 40(4) hapa chini; anaruhusiwa kugombea Urais mara moja kwa kipindi cha miaka mingine mitano tu.

Kama atashida atakuwa na jumla ya miaka tisa tu. Uzi ufungwe.
View attachment 1756505
Nilisoma 40(2) naona huko chini wanefafanua zaidi. Shukurani.


Katiba imeeleweka na atagombea kipindi kimoja.

Lakini uzi kufungwa ni jambo tofauti kwa sababu katiba inaweza kujadiliwa kwamba iko arbitrary.

Mfano, miaka mitatu umepatikanaje? Maana hata ukisema nusu ya muhula ni miaka miwili na nusu si mitatu.

Naona mabadiliko ya katiba chini ya Rais Samia yatakuwa topic ngumu sana.
 
Usiogope
Uhai wetu sote ni mali ya Mungu

Mi10 tena kwa mama rais Samia Suluhu Hassan[emoji1241][emoji95]
Kwa mama hapa tunakubaliana ,,siyo yule mtesaji ,, nilikuwa sikwelewi kabisa.
 
Mkimnyima fomu chama chenu kitaingia kwenye uchaguzi mkiwa na Mkuu wa kaya na mwenyekiti asiye na hamasa ya kutumia dola kufanikisha ushindi wenu kama ambavyo imezoeleka.

Mkumbuke yeye bado ndiye mpangaji wa tume ya uchaguzi. Kama bado atataka kutawala na mkanyima fomu mtamuambia nini asiweke tume huru itakayomtangaza yeyote atakayeshinda.Hapo ndipo utabiri wa Pole pole utakapotimia.

Mtajua hamjui.
Kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya 1977 na marekebisho yake yote, baada ya mhula huu mfupi wa urais wake wa kurithi kwa mujibu wa masharti ya Ibara ya 37(5), Rais Samia Suluhu Hassan anaweza kuchaguliwa tena kwa mhula mwingine mmoja. Ibara ya 40(4) ambayo ndiyo inahusika inasema hivi:

Endapo Makamu wa Rais anashika kiti cha Rais kwa mujibu wa masharti ya ibara ya 37(5) kwa kipindi kinachopungua miaka mitatu ataruhusiwa kugombea nafasi ya Rais mara mbili, lakini kama akishika kiti cha Rais kwa muda wa miaka mitatu au zaidi ataruhusiwa kugombea nafasi ya Rais mara moja tu.

Obviously, kulikuwa na sloppiness katika uandishi wa Ibara ya 40(4). Limit ni ya kuchaguliwa sio kugombea. Kama hujachguliwa unaweza kugombea hata mara tano kama alivyofanya Hayati Maalim Seif kule Zanzibar. Ukiisoma ibara hii sanjari na ibara ya 40(1), utabaini kwamba walichokusudia kuweka katika ibara ya 40(4) ni ukomo wa kuchaguliwa na sio ukomo wa kugombea kama waandishi wa Katiba walivyoandika!

Kwa kuwa mhula huu mfupi unazidi miaka mitatu, Rais Samia Suluhu Hassan anaweza kugombea na kuchaguliwa tena kushika kiti hicho mara moja tu, baada ya mhula huu.

Tofauti na ilivyozoeleka, kwa uchaguzi wa 2025, Lissu na wafuasi wake (na Kambi ya Upinzani kwa ujumla) wajiandae kukimbizwa mchakamchaka na mwanamama (iwapo ataamua kugombea).
 
Back
Top Bottom