Baada ya njia za giza kugonga mwamba kwenye kusaka utajiri, nimeamua kufanya hivi

Baada ya njia za giza kugonga mwamba kwenye kusaka utajiri, nimeamua kufanya hivi

Hii episode ya mwisho imeniudhunisha sana.. Nimejikuta naumia sana aiseee...
Kweli wanaume tumeumwa mateso...
Baada ya kufuta lile tope mdogo mdogo nikaanza kupandisha kimpando cha kuelekea kwa babu nikafika pale nikazuga kama nimeenda kuomba ganja akaanza kusema asubuhi yote umekuja kufanya nini nikamwambia nimekuja kufata dawa.
Akaniambia yamebaki makapi , kisha akaniuliza yule mwenzako agustino mzigo amesha leta nikasema hapana.

Ikabidi aingie ndani aniletee yaleyale makapi

Nilitoka pale kwa babu nikijua agustino hakuuza mtu yoyote kwa polisi basi nikaanza kutembea kurudi shuleni kwa yale mavazi nilishindwa nitarudi vipi ikabidi nitafute sehemu nikae nitulie nione jinsi gani nitatunga hoja .


Nilikaa mahali nikawaza agustino hana ndugu mahali pale nikasema nitafanyaje niende hata kumuona kituoni nikakosa jibu maana na mimi nilikuwa na hofia usalama wangu nilimpigia tena ndugu yake yule nikamwambia awaambie wazazi wake hata na yeye pia aje kumuona maana haikuwa mbali sana

Nilimwambia pia aje niwaoneshe getto ikiwezekana wachukue vitu vyake vya muhimu wa mtunzie jamaa aliniambia yeye anatangulia kashamwambia baba yake atakuja kesho

Basi alivyofika nilienda kumpokea pale centre tukaenda hadi getto jamaa akajitambulisha kuwa nikakaake tukavunja kufuli tumeingia ndani tafuta vitu muhimu kama simu, kadi ya banki,walet vyote hakuna na baadhi ya vitu vingine sivikumbuki

Basi yule kaka yake japo wakuvuta na kamba kesho yake akasema nije nimpeleke kituoni tumpelekee msosi mimi nilikubali ila nikamwambia nitabaki mbali kabisa usikie maafande watakwambiaje.

Kweli kesho yake nilivunja vipindi nikamsindikiza Yule jamaa alivyorudi akaniambia walimuoji ikabidi awaambie yeye ni kaka yake alitokea wilaya nyingine kuja kumletea msosi, Jamaa aliulizia kama anaweza muwekea dhamana ya pale kituoni maafande walikataa wakasema tena jarada lake linapelekwa mahakama ya wilaya

Daa jamaa alichoka tulirudi nae hadi getto kesho yake tena tukaenda kumuona na yule jamaa ndio nikajua kweli bongo nyoso yani hawakupi nafasi ya kuongea na mtu ukishapeleka msosi unaonja askari wanachukua unatembea mbele huwezi ongea hata siri na mtuumiwa , Halafu kituoni kumbe hawapiki sasa nikawa najiuliza hivi waliokamatwa na hawana ndugu karibu huwa wanakula nini kabla hawajapelekwa magereza


Kiufupi agustino kesi yake ilipelekwa mahakama ya wilaya, tena alishitakiwa na jamuhuri kwa kosa la kukamatwa na zaidi ya kili 100 za bangi tena alikamatwa na ushahidi kabisa boda boda wake kwa kujitetea ikabidi amchomee kabisa alisimama kama shahidi wa mwisho

Kulingana na mapambano ya bangi kipindi kile bila huruma hakimu alimtundika miaka 30 jela. Nimechoka kutype

Oky ngoja niendelee nakumbuka siku ya mwisho nimeenda kumuona pale magereza nikiwa nimeshika mkate na vipande vya sabuni + wembe nikajua labda kidogo kule magereza kutakuwa na utaratibu mzuri wa kuongea na mfungwa asee kufika tuliruhusiwa raia kama 20 hivi kwa mkupuo eti tuongee na wafungwa wetu kwa zile kelele sikuweza kumsikia vizuri neno nililolisikia kutoka kwake ni MWANANGU ENDELEA KUKOMAA

Na hapo nilikuwa nimetoka shuleni wilaya nyingine wakati natoka kwenye lile gereza nilijisikua huzuni sana kiasi kwamba nilijikuta na bubujikwa na machozi baada kama ya mwaka na nusu kupita nikiwa chuoni niliongea na yule kaka yake akaniambia agustino alihamishwa butimba mwanza

Kunakipindi niliona magufuli ameenda pale niliangaika sana kumtafuta agustino kwenye zile camera lakini sikufanikiwa kumuona rafiki yangu kipenzi now kamanda agustino amemaliza miaka 5 gerezani. kwa kifungo cha miaka 30 kwa jinsi wanavyo hesabu amebakiza miaka 15 gerezan

Mimi bado nikijana sana mwaka huu mwezi fulani na fikisha 24 yrs damu bado inachemka naendelea kupambana rafiki yangu mpambanaji agustino, kufa na kupona, kwa hali na mali nijipanue kiuchumii ili siku ukitoka gerezani husije kunicheka eti nilikuwa napoteza muda kitaa

Nataka uje unikute nimesha tengeneza bara bara nzuri ya kiuchumi uje tuishi maisha ya kidoni kama zilivyokuwa ndoto zako.

Nilichojifunza urafiki bora haupimwi kwa muda unapimwa kwa matendo maana niliishi na agustino katika kipindi kifupi sana lakini ameacha historia kubwa sana ndani ya maisha yangu

Nineandika kwa haraka vibaya vibaya kama kutakuwa na makosa tusameeane

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hapana mkuu sio ubakaji ni hilo hilo la bangi sema tu sikutaka kufunguka saana kuhusiana na agustino. Nilikuwa na elezea maisha yangu binafsi

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu tukio kama hili limewahi kumtokea ndugu yangu kabisa wa baba yangu mkubwa akiwa na rafiki yake, walianzia kwa mganga ili kupata utajiri wakafuata masharti yote kabisa na sharti la mwisho wakapewa kamba za katani na kuambiwa waende nje kidogo ya kijiji (ni jirani na mbuga ya serengeti) watawakuta ngo'mbe wawafunge na zile kamba na kuwaleta kwa mganga baada ya hapo pesa itakuw ni ya kumwaga. Walipofika pale walichokiona kwanza ni vumbi linatimka na muda si mrefu Nyati wawili walioshiba wako vichwa chini spidi 240 km/h. Ndugu yangu anasema mbio alizotimka siku hiyo si za dunia hii. Hii si hadithi na mimi si muumini wa mambo hayo lakini tulikuwa tunajua katumwa kwenda kuleta ng'ombe na mganga na miaka ile mgodi wa Nyamongo (sasa North Mara) ulikuwa chini ya wenyeji na mambo ya ushirikina yalikuwa mengi sana.
 
Duh labda Jooh kajikuta kwenye ule mwembe na simu haiwaki!!![emoji32], mida hii huwa tushakutana na "oooooky inaendelea....."
[emoji2][emoji2]Mama mwenye nyumba!Tunaomba wajihi wake,maana mtaani hapa kuna mama anasadikika ni witch ila "mzigo" wake looh,nikikutana nae night na manyanga yake nakuwa na roho ya jooh na mbegu zake,namg'oa[emoji2][emoji2]
Nipe namba mkuu[emoji1787]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu swali la kwanza kuhusu zile damu mimi mwenyewe nilikuwa na muhisi agustino lakini mara ya kwanza nikijua atakuwa na tatizo kiafya hata alikuwa akivua shati nilikuwa najaribu kumchunguza, wakati mwingine nilikuwa nikimuuliza anasema anaziona lakini hajui zinapotoka, pia muda mwingine nilikuwa nikizikuta nikaondoka kurudi nikimuuliza anasema hajaona kitu yaani mambo haya ya ushirikina yanachanganya sana

siku nilipo muamini kuwa sio yeye niilesiku tumekuta damu zimetapakaa kuchumbani ikabidi tumuite mama mwenye nyumba ili tumueeleze chaajabu alipokuja sikuona wote hatukuziona

Pia hata wakati namwabia agustino acheki kile kimkono chini ya kitanda akaniambia haoni kitu.
Pia na wanakijiji walivyoingilia kati nikajua atakuwa ni yule yule mama maana wakati ameamia kwenye getto lingine sikuwahi shuhudia mauza uza kama yale

Swali la 2 yule mama hakumkimbiza Agustino siku ile agustino alirudi asubuhi akaniambia alikuwa zake njee usiku kugeuka akamkuta mama mwenye nyumba yuko nae zero distance ikabidi atimue mbio nikamuuliza au ni bangi zimekuchanganya

Pia hata mimi nilivyo eleza kwenye story yote kulitokea na matukio tofauti tofauti usiku nikawa na muona live kipindi hata naenda kuke kwenye muembe nikiwahi kumuona

Kuhusu agustino kusita sita kuondoka pale nadhani ilikuwa mazingira maana tulikuwa tunajitawala wenyewe pale chumba kilikuwepo pembeni yetu lakini kilikuwa hakina mtu

Swali la mwisho Mimi niliamin amini kuna nguvu za maganga zinatumika kwa kiasi kukubwa siku ile nimeenda kuchimba mbegu nikakuta geneza mauza uza mengine yalikuwa chanzo ni kule tulikotoka nadhani walikuwa wanatupima imani



Sent using Jamii Forums mobile app
Ila mkuu inaonekana huyo mganga alikuwa kiboko haswaa.
 
Ila mkuu inaonekana huyo mganga alikuwa kiboko haswaa.
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]sema mganga kazingua sasa angewapa hata nusu hasara..

Ila nawaza vipi kama joooh saivi akienda tena kwa mganga huyohuyo kumwambia afanye mautundu amtoe mwanetu agustino?

Ila jooohs hili wazo akikumbuka yale mawe yaliyokuwa yanaongezwa lazima aseme tuende na mtu[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Msimuliaji Jooohs akiwa shule boarding alipata rafiki aitwaye Augustino ambaye pia alisoma naye shule moja, Augustino alikuwa Mwanafunzi wa day

Katika urafiki wao Augustino alionesha kutaka kuwa Tajiri kwa udi na uvumba, hali iliyosababisha ajiingize kwenye biashara ya bangi na baadae kwenda kwa mganga ili apate utajiri, katika hizi harakati Augustino alimshirikisha Jooohs

Walienda kwa mganga, wakafanyiwa dawa lakini wakaja kugundua kuwa ili pesa zianze kumiminika inabidi watoe kafara wazazi wao, hivyo jamaa wakaghairi. Kumbuka wakati huo wote walikuwa wanaendelea kuuza ganja.

Kwenye gheto la Augustino ambapo alipanga, palikuwa na matukio mfano mara kwa mara Jooohs alikuwa anakuta damu magetoni na kuna siku walikuta viganja vya mikono vya watoto wachanga.

Majirani wa mama mwenye nyumba wote walijua kuhusu uchawi wa huyu mama, na walimchoka mpaka walipokuja kumchomea moto nyumba yake lakini kipindi hicho akina Augustino walishahamia nyumba nyingine kumkimbia mother mchawi

Katika maisha yao ya utafutaji kupitia ndumu walikuwa na upinzani na ma pusher wengine ambao ni wazawa wa pale, hawa jamaa walishamuonya Augustino, lakini Augustino aliendelea na biashara ya ndumu.

Kama kawaida Serikali iliendeleza kubana mianya ya biashara ya bangi, hivyo ma dealers waligundua mbinu ya kusafirisha bangi ndani ya madumu. Biashara iliendelea kwa muda, siku moja katika harakati za kupokea mzigo Augustino alikamatwa na polisi akiwa na madumu yake akapelekwa mahakani akahukumiwa miaka 30 jela na kwa sasa yupo gereza la Butimba.

Augustino ambaye ameshatumikia kifungo miaka 5 na amebakiza miaka 15 (miaka ya jela) , alitembelewa na Jooohs siku moja, Jooohs ambaye kwa sasa ni graduate alikwenda kumsalimia Augustino, na Augustino alimsisitiza Jooohs aendelee kukomaa mpaka atusue maisha.

Tayari summary mkuu, usije sema nikusomee [emoji23][emoji23], acha uvivu
Ambaye anaweza kunipa kifupisho cha hili swala anionee imani anipe. Naona mnauliza habari za Augustine kua gerezani lakini mi nipo page ya 26 na zipo zaidi ya 50.

msaada wakuu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu wazo lako ni zuri sana

Ila kwa haya nilio yazungumza hapa kama kuna baharia

Atajipeleka kwa mganga kusaka pesa yaani omba ukakutana na mganga uchwara maana atakuibia pesa lakini sio nafsi

Lakini usikutane na wale wanaoiweza kazi kama unaroho ya panzi cha moto utakipata

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu mbona huku uliandika jamaa alifungwa kwa kubaka,afu huku amefungwa kwa bangi au ni watu wawili tofauti
Screenshot_20200410-211439.jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huyu jamaa naona ni mtunzi wa stori make kuna nyuzi zake nyingi sanaaa
Mkuu unajua unachekesha sana

Wewe umejiunga jamii forum Jana una nyuzi tano

Mimi huu mwaka wa 4 na nyuzi tano

Kati yangu na yako nani ananyuzi nyingi??

Unajua kabla hujahukumu mtu jiangalie wewe kwanza huko salama

Mimi sii mwandishi wa story za udaku ningekuwa nataka ningekuwa kila siku nafyatua uzi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom