Baada ya njia za giza kugonga mwamba kwenye kusaka utajiri, nimeamua kufanya hivi

Baada ya njia za giza kugonga mwamba kwenye kusaka utajiri, nimeamua kufanya hivi

ok mkuu kabla hujafunga mahesabu hebu tueleze sasa umeamua kufanya nini kuusaka utajiri baada ya njia za giza kugoma...
shukurani na asante kwa stori nzuri yenye kufurahisha ,kuhuzunisha na mafundisho ya kutosha,,
 
Umenikumbusha niliwahi kumtembelea rafiki yangu Magereza ya Butimba Wakati fulani..
Nilichokiona ndicho ulichoandika.. Watu mnaingia wengi,mnaongea kwa nguvu kwenye nyavu.. hakuna kusikilizana.. Sikuwahi kuingia.. Nikivyotoka pale nililia njia nzima.. Wafungwa wanateseka sana.

Sent using Jamii Forums mobile app
Inatakiwa wabadilishe mfumo uwe hata wa kiistaarabu kidogo

Ndomaana trump alituita shithole hakukisea

Sent using Jamii Forums mobile app
 
ok mkuu kabla hujafunga mahesabu hebu tueleze sasa umeamua kufanya nini kuusaka utajiri baada ya njia za giza kugoma...
shukurani na asante kwa stori nzuri yenye kufurahisha ,kuhuzunisha na mafundisho ya kutosha,,
Nitaandikia mada nyingine nieleze kila kitu

Nilikuwa nataka nieleze humu lakini lengo linesha haribika

Hii mada inatakiwa ikae kwenye jukwaa la hoja na habari

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Baada ya kufuta lile tope mdogo mdogo nikaanza kupandisha kimpando cha kuelekea kwa babu nikafika pale nikazuga kama nimeenda kuomba ganja akaanza kusema asubuhi yote umekuja kufanya nini nikamwambia nimekuja kufata dawa.
Akaniambia yamebaki makapi , kisha akaniuliza yule mwenzako agustino mzigo amesha leta nikasema hapana.

Ikabidi aingie ndani aniletee yaleyale makapi

Nilitoka pale kwa babu nikijua agustino hakuuza mtu yoyote kwa polisi basi nikaanza kutembea kurudi shuleni kwa yale mavazi nilishindwa nitarudi vipi ikabidi nitafute sehemu nikae nitulie nione jinsi gani nitatunga hoja .


Nilikaa mahali nikawaza agustino hana ndugu mahali pale nikasema nitafanyaje niende hata kumuona kituoni nikakosa jibu maana na mimi nilikuwa na hofia usalama wangu nilimpigia tena ndugu yake yule nikamwambia awaambie wazazi wake hata na yeye pia aje kumuona maana haikuwa mbali sana

Nilimwambia pia aje niwaoneshe getto ikiwezekana wachukue vitu vyake vya muhimu wa mtunzie jamaa aliniambia yeye anatangulia kashamwambia baba yake atakuja kesho

Basi alivyofika nilienda kumpokea pale centre tukaenda hadi getto jamaa akajitambulisha kuwa nikakaake tukavunja kufuli tumeingia ndani tafuta vitu muhimu kama simu, kadi ya banki,walet vyote hakuna na baadhi ya vitu vingine sivikumbuki

Basi yule kaka yake japo wakuvuta na kamba kesho yake akasema nije nimpeleke kituoni tumpelekee msosi mimi nilikubali ila nikamwambia nitabaki mbali kabisa usikie maafande watakwambiaje.

Kweli kesho yake nilivunja vipindi nikamsindikiza Yule jamaa alivyorudi akaniambia walimuoji ikabidi awaambie yeye ni kaka yake alitokea wilaya nyingine kuja kumletea msosi, Jamaa aliulizia kama anaweza muwekea dhamana ya pale kituoni maafande walikataa wakasema tena jarada lake linapelekwa mahakama ya wilaya

Daa jamaa alichoka tulirudi nae hadi getto kesho yake tena tukaenda kumuona na yule jamaa ndio nikajua kweli bongo nyoso yani hawakupi nafasi ya kuongea na mtu ukishapeleka msosi unaonja askari wanachukua unatembea mbele huwezi ongea hata siri na mtuumiwa , Halafu kituoni kumbe hawapiki sasa nikawa najiuliza hivi waliokamatwa na hawana ndugu karibu huwa wanakula nini kabla hawajapelekwa magereza


Kiufupi agustino kesi yake ilipelekwa mahakama ya wilaya, tena alishitakiwa na jamuhuri kwa kosa la kukamatwa na zaidi ya kili 100 za bangi tena alikamatwa na ushahidi kabisa boda boda wake kwa kujitetea ikabidi amchomee kabisa alisimama kama shahidi wa mwisho

Kulingana na mapambano ya bangi kipindi kile bila huruma hakimu alimtundika miaka 30 jela. Nimechoka kutype

Oky ngoja niendelee nakumbuka siku ya mwisho nimeenda kumuona pale magereza nikiwa nimeshika mkate na vipande vya sabuni + wembe nikajua labda kidogo kule magereza kutakuwa na utaratibu mzuri wa kuongea na mfungwa asee kufika tuliruhusiwa raia kama 20 hivi kwa mkupuo eti tuongee na wafungwa wetu kwa zile kelele sikuweza kumsikia vizuri neno nililolisikia kutoka kwake ni MWANANGU ENDELEA KUKOMAA

Na hapo nilikuwa nimetoka shuleni wilaya nyingine wakati natoka kwenye lile gereza nilijisikua huzuni sana kiasi kwamba nilijikuta na bubujikwa na machozi baada kama ya mwaka na nusu kupita nikiwa chuoni niliongea na yule kaka yake akaniambia agustino alihamishwa butimba mwanza

Kunakipindi niliona magufuli ameenda pale niliangaika sana kumtafuta agustino kwenye zile camera lakini sikufanikiwa kumuona rafiki yangu kipenzi now kamanda agustino amemaliza miaka 5 gerezani. kwa kifungo cha miaka 30 kwa jinsi wanavyo hesabu amebakiza miaka 15 gerezan

Mimi bado nikijana sana mwaka huu mwezi fulani na fikisha 24 yrs damu bado inachemka naendelea kupambana rafiki yangu mpambanaji agustino, kufa na kupona, kwa hali na mali nijipanue kiuchumii ili siku ukitoka gerezani husije kunicheka eti nilikuwa napoteza muda kitaa

Nataka uje unikute nimesha tengeneza bara bara nzuri ya kiuchumi uje tuishi maisha ya kidoni kama zilivyokuwa ndoto zako.

Nilichojifunza urafiki bora haupimwi kwa muda unapimwa kwa matendo maana niliishi na agustino katika kipindi kifupi sana lakini ameacha historia kubwa sana ndani ya maisha yangu

Nineandika kwa haraka vibaya vibaya kama kutakuwa na makosa tusameeane

Sent using Jamii Forums mobile app
AGUSTINO HAS FALLEN[emoji31][emoji31]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Dah mwanangu nusu nitoe chozi ....afu nipo na manzi na nlimwambia natokea bara sasa ningetoa chozi nahisi angejua uhalisia wangu kuwa mwanaume wa Dar...

Ila mkuu tuambie sasa zile damu ni nini?[emoji848][emoji848][emoji848][emoji848]
 
Oooky Inaendelea..................



Wakati naendelea kujiuliza huyu agustino atakuwa kaenda wapi wazo likaniijia nimpigie tena yule ndugu yake labda atakuwa kapata baadhi ya information nikampigia tena akaniambia bro siumetoka kunipigia sasa muda si mrefu nimekwambia sina taarifa yake akinitafuta tu nitakupigia basi nikatoka pale getto nikaanza safari kuelekea centre pengine nikae pale naweza kumuona labda anapita na madumu nikampokee

Muda ulikuwa unayoyoma jua linaelekea kuzama nikaanza mwendo ukumbuke hapo alipokuwa anakaa ilikuwa kunaka umbali hadi kufika centre ikabidi nitembee haraka haraka hadi kufika pale nikakuta maboda boda kibao wamekaa wanapiga story, wengine wanakunywa uji kulikuwa kunamama anapika pale centre.

Mimi muda huo nimechanganyikiwa kila muda napiga simu ya agustino lakini haipatikani nikajipa moyo labda simu yake itakuwa imezima maana alikuwa anakatecno kadogo sana lakini touch screen. Basi nikaendelea kuzuga pale huku nikiendelea kusikiliza sauti za wale boda boda wa kibishana kuhusu simba na yanga, wengine wakiongea lugha za kienyeji

Wakati na zidi kutafakari huku nikikodolea macho kila piki piki inayopita pale nikawa na matumaini labda itakuwa ni agustino lakini nilikuwa naambulia patupu daa nikiangalia muda unazidi kwenda nikipiga simu haipokelewi mara muda kidogo naona message kutoka voda kifurushi chako kimeisha.

Ikabidi nisimame nitazame kibanda ambacho kiko karibu nikaona kimoja kiko upande mwingine nikavuka upande wa pili wa bara bara nikaenda kibandani nikatoa noti ya elfu moja nikapewa vocha ya mia tano nukarudishiwa mia tano
huku nikiendelea kukodolea macho kila usafiri unaopita pale

Ikabidi nivuke tena bara bara niende kukaa ile sehemu niliokuwa nimekaa kufika nataka kukwangua vocha mkononi siioni kusachi mfukoni na ile jero peke yake nikaanza kurudi kukagua pale chini labda nitakuwa nimedondosha wapi nikafatilia barabara yote hadi pale kibandani sikuona kitu.

Nikatoa tena ile 500 nikanunua vocha nyingine kuweka nampigia jamaa bado simu haipatikani daa nikaendelea kukaa pale hadi giza kabisa likaingia nikawaza huyu jamaa atakuwa yuko wapi nilikaa pale hadi wauza mboga kina mama kila mmoja akaanza kubeba sinia anaondoka zake

Daa nikapiga mawazo au kati ya zile taxi zilizokuwa zinapita hapa moja kati yake atakuwa alikuwa ni agustino ngoja nirudi getto kwake kufika pale nikakuta baadhi ya wapangaji pale kuwauliza wanasema bado jamaa hajarudi labda atakuwa yuko shuleni.

Asee niliondoka huku nimechoka hata nguvu za kutembea nilikuwa sina nilitembea hadi nikafika pale hostel nikamwambia muddy kuwa nimeenda kwa agustino lakini sijamkuta lakini jamaa alichukulia kawaida ikabidi kwenda jikoni kwa mpishi nikapiga nae msosi maana wanafunzi walikuwa wameshamaliza kula wengine wameenda prepo ikabidi niingie hostel nianze kuuchapa usingizi

Sijui wenzangu walikuwa wananionaje, nadhani walikuwa wananiona kama mtu aliyekata tamaa na masomo halafu siko serious maana prepo nilikuwa sionekani, soma yangu ya kusua sua kila siku nasingizia naumwa kichwa kumbe hali yangu naijua mwenyewe kunasiku nilikuwa natoka darasani naenda hostel nikapita nyuma ya darasa la wanaosoma arts nikasikia wanacheka vibaya sana huku head boy anasema wale majamaa hawako serious

Kama yule anae doji prepo anasingizia kuumwa kichwa halafu jioni unamuona anaenda kuvuta bangi asee nikapita tu walivyoniona dirishani wakazuga kunyamaza kumbe baharia nimesikia kila kitu.

Wakati nimejilaza pale kitandani huku nikiendelea kupiga ile namba ya agustino bila mafanikio nikawaza sana nitafanya vipi nimpate huyu jamaa maana nilikuwa na hofu sana, niliendelea kupiga ile simu bila mafanikio kesho yake asubuhi ilikuwa ni siku ya shule nikawahi kuamka mapema sana nikajiandaa vizuri nikavaa sare za shule nikamwabia muddy ngoja niwahi kwa agustino maana ndio nilikuwa namuona kama rafiki nilie kuwa nimebaki nae wengine wote wananiona kilaza

Basi nikaanza kutembea fasta hadi nikaiacha kwa mbali mipaka ya shule nikaanza mdogo mdogo kumezwa na vichaka vilivyokuwa vimetapakaa kila sehemu ya ule mtaa basi nilitembea haraka Hadi nikafika kwenye ile nyumba kuangalia mlango umefungwa ikabidi nigonge mlango wa yule mpangaji pale nikamuuliza agustino hajarudi asee

Majibu aliyonipa yalikuwa ni yakusikitisha sana na kuniogopesha maana yule mpangaji akasema alirudi hapa usiku sana na maaskri wakafungua mlango wakapekuwa ila hawakujua walichukua nini kisha wakaondoka nae yaani nilitaka kupooza palepale ilibidi nikae chini ya udongo nikajua mambo ndio yamesha haribika kabisa.

Basi ilibidi niondoke pale nikiwa na maswali mengi , nijajiuliza nirudi shuleni au nikachukue mizigo yangu niwaambie nimezidiwa naenda kulazwa hospital, nkajiuliza tena hivi shule na maisha yangu kipi bora wakati naendelea kujiuluza nikakumbuka yule ndugu yake alietuma mzigo ikabidi nimvutie kamba alipokea nikamwambia jamaa agustino kakamatwa na maaskari jamaa kashituka sana kaniuliza mara mbili mbili nikamwambia ndio walikujanae hadi kupekuwa alipopanga jamaa akakata simu.

Kisha nikatembea fasta kurudi shuleni nikaenda kuingia hadi hosteli nikakuta jamaa ndio wanajiandaa wanavaa nguo waende kwenye ratiba za shule mimi nilipofika nikaanza kuvua yale mavazi yangu kisha nikabadili nguo nyingine za kawaida nikasepa

Nilisema ngoja kwanza niende hadi kule kwa babu labda atakuwa kupigwa kaambiwa ataje wafuasi wake nikanza mchaka mchaka haraka zangu nimefika pale mtoni navuka haraka haraka nikateleza kiatu chote kikazama ndani ya matope ikabidi nivue nikaanza kutoa yale matope kisha nikavaa hivyo hivyo kibichi nikaendelea na safari........

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu umeanza sasa ubongo movie unaadisia mpka mambo ya nilenda kbandani nkanuaa vocha sijui ya jero nkarudisjiwa jero. Mara vocha ikapotea nkarudi nkatoe ile jero. Nikascratch nkaweka vocha nkampigiia hapatikani....yanini yote hayo? Unaanza kupoteza mvuto.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu panga safari uwende kumchek mwamba usisahau kumpelekea zawadi nyingi kama box za soap, redio, nyembe n.k.

Nitajitolea box moja la sabuni kama ukitaka kwenda niPM nitachangia mkuu


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Mkuu umeanza sasa ubongo movie unaadisia mpka mambo ya nilenda kbandani nkanuaa vocha sijui ya jero nkarudisjiwa jero. Mara vocha ikapotea nkarudi nkatoe ile jero. Nikascratch nkaweka vocha nkampigiia hapatikani....yanini yote hayo? Unaanza kupoteza mvuto.

Sent using Jamii Forums mobile app
Unajua mkuu, ukiwa unaandika story ni kama uko kwenye chumba cha mtihani unashirikisha ubongo, macho pamoja na mikono

Soo kilichokuwa kunatoka kwenye ubongo ndio nilichokuwa naandika
Sorry kama huo uandishi umekukwaza

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu panga safari uwende kumchek mwamba usisahau kumpelekea zawadi nyingi kama box za soap, redio, nyembe n.k.

Nitajitolea box moja la sabuni kama ukitaka kwenda niPM nitachangia mkuu


Sent from my iPhone using JamiiForums
Sawa mkuu nikitaka siku nikitaka kwenda nitaku PM pengine yaweza kuta sumu za huu uzi zimepungua

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu narudia tena achana na mpango huo unaotaka kufanya. Acha kabisa.
Haya mambo yapo wazee. Kuna nyumba huku kwetu huwa haifahamiki mmiliki wake. Kila siku usiku watu hutoa vilio wakiwa ndani ya nyumba hiyo, ukiwa kwa nje unaona kama watu wanatembea mle ndani kupitia pazia zile za transparency. Nyumba ni kubwa haina umeme kwa hiyo mwanga unaotumika mule ni kama mwanga wa mshumaa. Eneo hilo linaogopeka sana na ukipita wakati wa mchana unakuta pako kimya kwelikweli, kuanzia usiku saa tano huwa mwanga wa mshumaa unawashwa, halafu sauti za vilio zinaanza kusikika, ni wake kwa waume huku mipishano ikiendelea mule ndani. Wanasema mwenye nyumba alishafariki miaka mingi na sijui hakuwa na familia au laa. Leo nitajiaribu kupapiga picha au kuchukua video

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nitaandikia mada nyingine nieleze kila kitu

Nilikuwa nataka nieleze humu lakini lengo linesha haribika

Hii mada inatakiwa ikae kwenye jukwaa la hoja na habari

Sent using Jamii Forums mobile app
Hata humu kwa mtazamo wangu bado inakidhi vigezo vya kubaki kwani bado inaelezea mapito wanayopitia watu kwenye utafutaji

Kwa vile moderators wameamua kuiunganisha kule juu ni vizuri sasa ukaweka mbinu mpya za halali unazotumia kwa sasa kupambana na swala zima la utafutaji baada ya mbinu zenu kugonga mwamba

Hii itaipa nguvu kubwa story yako na itabaki kuwa funzo kwa wengine wanaodhani kwa waganga kuna kupata utajiri kirahisi au wanaouza bangi na madawa mengine ya kulevya wanapata utajiri kirahisi

Ulichokieleza kinafunzo kubwa kwa watafutaji kwani katika utafutaji watu tunapitia mahangaiko mengi sana ikiwemo kuwaza hayo ya waganga

Pamoja na yote kama utakuwa umechagua kuandika hicho kipengere chako cha mwisho kinachoelezea unayo yafanya kwa sasa kwenye post hii, jitahidi kuiweka kwa kulenga pointi za msingi unazotaka watu wajifunze

Mwisho kabisa kwani tangu uzi unaanza sikuchangia popote ila nimeufuatilia vizuri tu ili kujua hatima ya Augustino, nikushauri tu kwa vile umekiri ni story ya kweli iliyokutokea mwenyewe tafuta namna ya kwenda kumuona jamaa yako huko gerezani

Ni kweli kabisa wafungwa huwa wanahamishwa hamishwa ila ukiamua utampata tu! Nenda kampe hi atajisikia faraja

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom