Baada ya Ole Nasha kufariki ni wakati wa Mkataba wa bandari ya Bagamoyo kuwa wazi

Baada ya Ole Nasha kufariki ni wakati wa Mkataba wa bandari ya Bagamoyo kuwa wazi

Waziri Ole Nasha ndiye aliyekuwa waziri ambaye kapewa majukumu ya ufuatiliaji wa mkataba wa ujenzi wa bandari ya Bagamoyo wenye makadirio ya thamani $10B. Watanzania wengi ni lazima tujiulize huyu waziri kijana kuondoka katika mazingira haya akiwa katikati ya mkataba mkubwa hivi.

Kwa kutoa Watanzania wasiwasi na kuzingatia tajari tulisha ambiwa kuna madudu mengi sana kwenye huu mkataba. Lakini China nayo imekuwa ikisema kusuhu kuwa na base za kijeshi kwenye bandari zao ni lazima mkataba uwe wazi ili Watanzania wote tujue tunaingia kwenye mkataba wa namna gani. Wakina Samia na Kikwete hawatakuwepo pale China ikipewa bandari kwa miaka 99 na bandari kuwa kama balozi hivyo China kufanya wanalotaka.

Pamoja na mambo ambayo hatuyajui ni

1. Kuna umuhimu gani wa kuwa na bandari tatu karibu ya Tanga, Dar na hii ya Bagamoyo
2. Bandari ya Bagamoyo watarudisha vipi uwekezaji wa $10B bila kuchukuwa mizigo ya bandari ya Dar!. Je itawezekana vipi hizi bandari mbili kuongeza mizogo kwa zote!?. Na bandari ya Dar kuna mtu anafikiri watapata tena mizigo ya kutoka China?.
3 Tujue China ni kama inatawala shaba kule Zambia ndiyo mjenzi wa Tazara Je mizigo ya Zambia itaendelea kupitia bandari ya Dar au Bagamoyo?

Ukiangalia vizuri hii bandari ya bagamoyo ni mradi wa watu wachache. Hivyo viwanda wanavyosema watajenga sio viwanda ni magodauni ya kuweka mizigo huo ndiyo ukweli. Hakuna kiwanda eti kinasubiri bandari kwasababu Tanzania tuna bandari na maeneo ya ujenzi sasa hivi. Lakini kuna pesa ya mafuta na bomba linaenda Tanga ni kwanini tusikuzi pale ambapo tayari tuna uhakika wa soko kubwa na pesa? Tanga kuna umbali gani???! na hii ingefanya bandari zote bado ziwe chini ya TPA. Hii bandari ya Bagamoyo haitakuwa ya TPA tujue hilo.

Msishangae mtoto wa Kikwete kualikwa China eti kwenye mafunzo na kuacha wabunge wengine wenye uzoefu. Hii yote ni mradi wa bandari na hawa Kikwetes tuwe nao makini sana. Vilevile tusiwaamini wapinzani kwenye hili China wanauwezo wa kuhonga mpaka upinzani. Kitu kimoja tu tunaomba ni uwazi mkataba wekeni hapa na sio kutudanganya kwa mambo ya kazi. Vilevile Ole Nasha kufariki ni kitu cha kujiuliza sana maana tunasikia alianza kupinga mambo mengine.
Mkuu Kamundu , hili la uadilifu wa Comred Ole Nasha, nakuunga mkono hata mimi nimezungumzia hapa Tribute to William Ole Nasha: Alikuwa Miongoni Mwa Viongozi Wachache Bonafide Genuine Wazalendo wa Kweli waTaifa Hili. RIP Comred William Ole Nasha!
Lakini naomba usilete any conspiracy theories zozote kwenye kifo chake, kifo ni kazi ya Mungu.

Pili ujenzi wa bandari ya Bagamoyo, ilikuwa ndio iwe a feed port ya mzigo wa kushibisha SGR. Bandari ya Dar es Salaam hata iki operates kwenye full capacity, haiwezi kushibisha SGR ikajiendesha kwa faida. Reli ya SGR: Je, Tujifunze kwa wenzetu Kenya kuepusha SGR yetu kuwa ‘A White Elephant’? Wenzetu yameshawakuta...

Ujenzi wa bandari ya Bagamoyo, inakuwa ni a free port, zile yards za magari Japan, Dubai na Singapore, zinahamia Bagamoyo, hivyo nchi zote za Africa South of Sahara, wanakuja kununua mahitaji yao yote Tanzania.

Na kwa vile tunafanya miradi kibao mikubwa ya kimkakati, sijaona ukiuliza mkataba wa SGR, Stigler, Ununuzi wa Ndege, Ujenzi wa Flyovers etc, why utake mkataba wa Bagamoyo?. Mikataba yote ina confidentiality clause. Kwani umeona mkataba wa Barrick?. Why so much noise on Bagamoyo Port?.
P
P
 
Hii bandari lazima Ile vichwa vya watu tunadubiri upuuzi wa hawa kina mangungo wa msovero .kwa kweli wazarendo tuliobaki tutapambana. Yaani huyu JK sijui anafanya nini kwetu
Rais mstaafu JK anastahili heshima yake, tumuache ale pension yake kwa amani, kama una hoja kuhusu matatizo ya bandari ya Bagomoyo, itoe na hiyo ndiyo ioneshe JK ana makosa.
Siyo wewe umshambulie bila kutuelewesha.
 
Waziri Ole Nasha ndiye aliyekuwa waziri ambaye kapewa majukumu ya ufuatiliaji wa mkataba wa ujenzi wa bandari ya Bagamoyo wenye makadirio ya thamani $10B. Watanzania wengi ni lazima tujiulize huyu waziri kijana kuondoka katika mazingira haya akiwa katikati ya mkataba mkubwa hivi.

Kwa kutoa Watanzania wasiwasi na kuzingatia tajari tulisha ambiwa kuna madudu mengi sana kwenye huu mkataba. Lakini China nayo imekuwa ikisema kusuhu kuwa na base za kijeshi kwenye bandari zao ni lazima mkataba uwe wazi ili Watanzania wote tujue tunaingia kwenye mkataba wa namna gani. Wakina Samia na Kikwete hawatakuwepo pale China ikipewa bandari kwa miaka 99 na bandari kuwa kama balozi hivyo China kufanya wanalotaka.

Pamoja na mambo ambayo hatuyajui ni

1. Kuna umuhimu gani wa kuwa na bandari tatu karibu ya Tanga, Dar na hii ya Bagamoyo
2. Bandari ya Bagamoyo watarudisha vipi uwekezaji wa $10B bila kuchukuwa mizigo ya bandari ya Dar!. Je itawezekana vipi hizi bandari mbili kuongeza mizogo kwa zote!?. Na bandari ya Dar kuna mtu anafikiri watapata tena mizigo ya kutoka China?.
3 Tujue China ni kama inatawala shaba kule Zambia ndiyo mjenzi wa Tazara Je mizigo ya Zambia itaendelea kupitia bandari ya Dar au Bagamoyo?

Ukiangalia vizuri hii bandari ya bagamoyo ni mradi wa watu wachache. Hivyo viwanda wanavyosema watajenga sio viwanda ni magodauni ya kuweka mizigo huo ndiyo ukweli. Hakuna kiwanda eti kinasubiri bandari kwasababu Tanzania tuna bandari na maeneo ya ujenzi sasa hivi. Lakini kuna pesa ya mafuta na bomba linaenda Tanga ni kwanini tusikuzi pale ambapo tayari tuna uhakika wa soko kubwa na pesa? Tanga kuna umbali gani???! na hii ingefanya bandari zote bado ziwe chini ya TPA. Hii bandari ya Bagamoyo haitakuwa ya TPA tujue hilo.

Msishangae mtoto wa Kikwete kualikwa China eti kwenye mafunzo na kuacha wabunge wengine wenye uzoefu. Hii yote ni mradi wa bandari na hawa Kikwetes tuwe nao makini sana. Vilevile tusiwaamini wapinzani kwenye hili China wanauwezo wa kuhonga mpaka upinzani. Kitu kimoja tu tunaomba ni uwazi mkataba wekeni hapa na sio kutudanganya kwa mambo ya kazi. Vilevile Ole Nasha kufariki ni kitu cha kujiuliza sana maana tunasikia alianza kupinga mambo mengine.
LOoooh, hata sijui kama wewe ndiye hasa mwasisi na mwandishi wa mada hii; na kama ni kweli, basi huenda Tanzania tumekwishaingiliwa hadi mvunguni.
Hii itakuwa ni hatari kubwa sana kwa taifa hili.

Kuna kitu ambacho waTanzania wengi inapasa wakijue na wasikichanganye kabisa katika kujadili habari za uwepo wa Bandari ya Bagamoyo au nyingine yoyote mpya.
Mkanganyiko uliopo ni huu wa kuihusisha Bagamoyo na waChina, tukiondoa mkanganyiko huo nadhani wengi watakubali kwamba Bandari ya Bagamoyo au Mwambani zilizobora kabisa ni muhimu kwa taifa letu. Tunahitaji uwepo wa bandari kubwa yenye uwezo zaidi ya ule unaopatikana kwa bandari zilizopo sasa. Hili ndio takwa.
Tatizo ni mpango upi unaotakiwa tuutumie ili kupata hiyo badari. Huu wa wachina, au watu wengine wowote wenye kuhusisha kutukamua ni tatizo, bila kujali ni nani anahusika.

Tunaweza kujenga bandari mpya na kubwa taratibu kwa uwezo wetu wa ndani; mfano ni hiyo Lamu, mbona bandari imejengwa na inaendelea kujengwa kwa hatua. Maswala ya kukabidhi miradi kama hii kwa watu/makampuni/nchi zingine yana umuhimu gani kwa ufanisi wa nchi yetu?
Kwa nini ushiriki wetu kama nchi kwenye miradi ya aina hii iwe ni nongwa, mbona bomba la mafuta tunashiriki kama nchi!

Kwa hiyo, niseme tu kwa ufupi. Kuna mambo ninakubaliana nawe kuhusu huu mradi wa bandari ya Bagamoyo.
1. Ninakubaliana nawe kwamba kuna kundi la watu wanaousukuma mradi huu kwa manufaa yao binafsi zaidi kuliko manufaa ya nchi yetu, na kundi hili linaonekana wazi kuwa hatari sana kwa nchi yetu. Lisipodhibitiwa haraka tutakuwa matatani.
2. Ninakubaliana nawe kwamba hatuhitaji bandari na viwanda kushusha na kupakia bidhaa toka nje, huku tukifaidika kidogo na uwekezaji wa namna hiyo.

Nisiyokubaliana nawe ni
1. Uhitaji wa bandari kubwa yenye uwezo mkubwa kuliko unaopatikana kutokana na zilizopo sasa hivi. Ni muhimu sana tuwe na bandari ya kisasa kabisa na kubwa kuhimiri ongezeko kubwa la biashara katika ukanda huu miaka michache iinayofuata.
2. Wachina, kwani wana kizuizi gani cha kupeleka miradi yao Lamu, ambako najua wakitaka ni haraka sana wanakabidhiwa kila kitu.

Hizi 'Consipiracy theories' hizi zinazoibuka kila mahali wakati huu, ni mwanzo tu wa makubwa yatakayofuata baada ya hapa.
 
Tusisahau watanzania ni karibia mil 60. Tuache mambo ya kukopa au kuanzisha miradi ya kuneemesha watu wachache tu.
Hivi hatukomi kuanzisha kashfa zisizoisha?

Wanaofanya hivyo wanajulikana. Ukiandika kwa umoja kama wote tunahusika hututendei haki. Ni viongozi wa serikali ya CCM ndio mambo zao miaka yote katika makundi na mitandao yao. Na kwa vile wameshajihakikishia ukiritimba wa mamlaka ya kuitawala Tanzania “milele” kamwe hawatabadilika.

Hakuna tishio la kuwaondoa madarakani kiasi cha kuwatia uoga wajinyime ulaji wa wazi kabisa. Hawahitaji kura za wananchi kushika madaraka. Kila dili kubwa: EPA, ndege ya Rais, rada, Tegeta Escrow, n.k. kuna mkono wa Ikulu. Hakuna Mtanzania wa kuwarudi. Wanaojaribu wanakuwa neutralized kwa namna tofauti tofauti.

Bila demokrasia ya kweli ufisadi wa viongozi utaendelea kuwa mtindo wa maisha nchini hadi taifa lisambaratike au hadi ule mwisho. Itabidi tuzoee kuishi na ufisadi kama corona au ukimwi.
 
Sasa hivi mnaangaika sana mnazusha kila uongo ili muhalalishe mnachokizua hii haisaidii chochote zaidi ya kuchonganisha watu, halafu ebu weka angalau ile mikataba ya ununuzi wa ndege na ujenzi wa uwanja wa ndege wa Chato uliyowahi kuoneshwa na yule bwana wenu mnayempiginia wacha mikataba mingine iliyoingiwa na huyo mnayemuabudu na kumuona ni Mungu mtu halafu ndio mdai hiyo mingine.
Mkataba wa Bandari ulisainiwa wa kwanza. Huu ndio tuujadili kwa sasa. Pia hakuna mchina kwenye ununuzi wa ndege. Tupo wenyewe. Tunamudu.
 
Bandari ya Bagamoyo haina maslahi kwa Taifa. Ni shinikizo la Uchina. Ni mtindo wa ukoloni mamboleo wa Uchina. Tupanue Bandari zetu 3. DSM, Mtwara na Tanga.
Bandari ya Bagamoyo haina Maslahi kwa Taifa.
 
Nchi hii ina mambo yanakera sana. Mpaka sasa huyu aliyejiunganishia mafuta bandarini hatujui ni nani, na inaonekana kama hakuna anayejali.

Kuna wakati huwa najiuliza hivi nchi hii ikiongozwa bila kuwepo mhimili wa bunge; mwananchi atapungukiwa kitu gani!

Shida ni kuamini kwamba bila chama flani nchi haiendelei
 
Mi napata wakati mgumu hasa nikijaribu kuchungulia ambao hawapo kwenye zile nafasi ambao walikataa ile proposal ya awali.

Kamati ya majadiliano ilikuwa chini ya Prof. Kabudi wakati wajumbe wakiwa

1. Engineer Mfugale
2. Dkt. Chamuriho
3. Engineer Kakoko
4. Dkt Kilangi (Alikuwa mwanasheria mkuu wa serikali)

Ao wote hawapo leo kwenye zile nafasi na ukiangalia iyo list unaweza kuona kwanini ule mradi ulikataliwa sasa sijui wanasiasa watokaokuwa kwenye kamatu ya sasa ya mazungumzo.
What a stroke of a genius !!!
 
Hati zote za Uwekezaji ni 99 years sasa uache kuandika kabla hujatafiti!!... Haiwezekani Bandari zote zisimame kwasababu ya hii ya Bagamoyo,Ni watu wajinga na wapumbavu pekee ndio watakubali uongo huu!!.. Bandari ya Bagamoyo sio ya Kwanza (Bagamoyo inayo Bandari ya Kwanza)...Ujenzi wa Bandari hii ni kufungua nchi kuzuri!!..Sasa hivi mizigo yote ya Bagamoyo na baadhi ya mikoa ya karibu inapita Dar es salaam!!..Utakua mtu wa ajabu ukikataa Ujenzi huu kisa JK wakati tusipojenga uchumi wetu unaendelea kusuasua!!..Tuache Umimi nchi hii ni ya watanzania wote!!.. Bandari itarahisisha Usafirishaji sana!!
Hiyo inakuwa Bandari ya Uchina. Nil sawa tumemuuzia Mchina ardhi ya kujenga bandari wakati sisi tuna Bandari zetu.
Halafu tumieni akili na kuona kisichoonekana kwa macho ya kawaida.
 
Back
Top Bottom