Waziri Ole Nasha ndiye aliyekuwa waziri ambaye kapewa majukumu ya ufuatiliaji wa mkataba wa ujenzi wa bandari ya Bagamoyo wenye makadirio ya thamani $10B. Watanzania wengi ni lazima tujiulize huyu waziri kijana kuondoka katika mazingira haya akiwa katikati ya mkataba mkubwa hivi.
Kwa kutoa Watanzania wasiwasi na kuzingatia tajari tulisha ambiwa kuna madudu mengi sana kwenye huu mkataba. Lakini China nayo imekuwa ikisema kusuhu kuwa na base za kijeshi kwenye bandari zao ni lazima mkataba uwe wazi ili Watanzania wote tujue tunaingia kwenye mkataba wa namna gani. Wakina Samia na Kikwete hawatakuwepo pale China ikipewa bandari kwa miaka 99 na bandari kuwa kama balozi hivyo China kufanya wanalotaka.
Pamoja na mambo ambayo hatuyajui ni
1. Kuna umuhimu gani wa kuwa na bandari tatu karibu ya Tanga, Dar na hii ya Bagamoyo
2. Bandari ya Bagamoyo watarudisha vipi uwekezaji wa $10B bila kuchukuwa mizigo ya bandari ya Dar!. Je itawezekana vipi hizi bandari mbili kuongeza mizogo kwa zote!?. Na bandari ya Dar kuna mtu anafikiri watapata tena mizigo ya kutoka China?.
3 Tujue China ni kama inatawala shaba kule Zambia ndiyo mjenzi wa Tazara Je mizigo ya Zambia itaendelea kupitia bandari ya Dar au Bagamoyo?
Ukiangalia vizuri hii bandari ya bagamoyo ni mradi wa watu wachache. Hivyo viwanda wanavyosema watajenga sio viwanda ni magodauni ya kuweka mizigo huo ndiyo ukweli. Hakuna kiwanda eti kinasubiri bandari kwasababu Tanzania tuna bandari na maeneo ya ujenzi sasa hivi. Lakini kuna pesa ya mafuta na bomba linaenda Tanga ni kwanini tusikuzi pale ambapo tayari tuna uhakika wa soko kubwa na pesa? Tanga kuna umbali gani???! na hii ingefanya bandari zote bado ziwe chini ya TPA. Hii bandari ya Bagamoyo haitakuwa ya TPA tujue hilo.
Msishangae mtoto wa Kikwete kualikwa China eti kwenye mafunzo na kuacha wabunge wengine wenye uzoefu. Hii yote ni mradi wa bandari na hawa Kikwetes tuwe nao makini sana. Vilevile tusiwaamini wapinzani kwenye hili China wanauwezo wa kuhonga mpaka upinzani. Kitu kimoja tu tunaomba ni uwazi mkataba wekeni hapa na sio kutudanganya kwa mambo ya kazi. Vilevile Ole Nasha kufariki ni kitu cha kujiuliza sana maana tunasikia alianza kupinga mambo mengine.
LOoooh, hata sijui kama wewe ndiye hasa mwasisi na mwandishi wa mada hii; na kama ni kweli, basi huenda Tanzania tumekwishaingiliwa hadi mvunguni.
Hii itakuwa ni hatari kubwa sana kwa taifa hili.
Kuna kitu ambacho waTanzania wengi inapasa wakijue na wasikichanganye kabisa katika kujadili habari za uwepo wa Bandari ya Bagamoyo au nyingine yoyote mpya.
Mkanganyiko uliopo ni huu wa kuihusisha Bagamoyo na waChina, tukiondoa mkanganyiko huo nadhani wengi watakubali kwamba Bandari ya Bagamoyo au Mwambani zilizobora kabisa ni muhimu kwa taifa letu. Tunahitaji uwepo wa bandari kubwa yenye uwezo zaidi ya ule unaopatikana kwa bandari zilizopo sasa. Hili ndio takwa.
Tatizo ni mpango upi unaotakiwa tuutumie ili kupata hiyo badari. Huu wa wachina, au watu wengine wowote wenye kuhusisha kutukamua ni tatizo, bila kujali ni nani anahusika.
Tunaweza kujenga bandari mpya na kubwa taratibu kwa uwezo wetu wa ndani; mfano ni hiyo Lamu, mbona bandari imejengwa na inaendelea kujengwa kwa hatua. Maswala ya kukabidhi miradi kama hii kwa watu/makampuni/nchi zingine yana umuhimu gani kwa ufanisi wa nchi yetu?
Kwa nini ushiriki wetu kama nchi kwenye miradi ya aina hii iwe ni nongwa, mbona bomba la mafuta tunashiriki kama nchi!
Kwa hiyo, niseme tu kwa ufupi. Kuna mambo ninakubaliana nawe kuhusu huu mradi wa bandari ya Bagamoyo.
1. Ninakubaliana nawe kwamba kuna kundi la watu wanaousukuma mradi huu kwa manufaa yao binafsi zaidi kuliko manufaa ya nchi yetu, na kundi hili linaonekana wazi kuwa hatari sana kwa nchi yetu. Lisipodhibitiwa haraka tutakuwa matatani.
2. Ninakubaliana nawe kwamba hatuhitaji bandari na viwanda kushusha na kupakia bidhaa toka nje, huku tukifaidika kidogo na uwekezaji wa namna hiyo.
Nisiyokubaliana nawe ni
1. Uhitaji wa bandari kubwa yenye uwezo mkubwa kuliko unaopatikana kutokana na zilizopo sasa hivi. Ni muhimu sana tuwe na bandari ya kisasa kabisa na kubwa kuhimiri ongezeko kubwa la biashara katika ukanda huu miaka michache iinayofuata.
2. Wachina, kwani wana kizuizi gani cha kupeleka miradi yao Lamu, ambako najua wakitaka ni haraka sana wanakabidhiwa kila kitu.
Hizi 'Consipiracy theories' hizi zinazoibuka kila mahali wakati huu, ni mwanzo tu wa makubwa yatakayofuata baada ya hapa.