Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Hopeless comment ever! Endelea kusubiri na utasubiri sana mpaka ufe!
Alitaka afanye matendo yapi?Mkuu;
Mtu smart hapimwi kwa kuongea bali kwa matendo yake!
Wapambe hao wakiongozwa na Mshana Jr na kundi lake. JF hatari sana.Kwenye mitandao ya kijamii kukaanzishwa alama ya reli (hashtag) inayosema ''Twende na Membe''! wapambe na mashabiki wakamjaza ''ujinga''!
Umetumia muda wako vibaya sana! hakuna mtanzania mwenye akili timamu asiyejua kuwa kuwa "kura ziliibwa"! hata kama Watzanzania wamekaa kimya, msifikiri kuwa hawajui kama mpo madarakani kwa wizi wa kura! kaeni kimya tu muda wenu uishe kama mtajisikia kuondoka madarakani hewala, kama mta apply u M7 hewala! Hizo ngonjera zingine hakuna anayewaelewa, na Lissu anajulikan kuwa aliwagalagaza mapema tu!Hawa wanasiasa wawili hawatawasahau Watanzania katika maisha yao yote!
Tundu Lissu alikuja nchini na ''mkwara mzito'' aliouanzia akiwa nje ya nchi alipokuwa anatoa hotuba mara kwa mara kwa Watanzania kama vile ameshakuwa Mkuu wa Nchi, Kiongozi wa Serikali na Amiri Jeshi Mkuu!
Wakati wa kampeni za Uchaguzi Mkuu, Tundu Lissu alikuwa anatoa vitisho vikali kwa kila mtu aliyejaribu kumpinga na kumkosoa! Watu wanaoifahamu vizuri nchi hii hasa watanzania wakawa wanamwangalia na kumhurumia huku wengine waliodhani kwa elimu yake anaijua vizuri Tanzania na wananchi wake wakihitimisha kwa kukubali methali isemayo ''akili nyingi huondoa maarifa''. Yaani Tundu Lissu ana akili nyingi lakini hana maarifa!
Watu wengine hawakujua kuwa kwa Watanzania ule ulikuwa ni ''mkwara mbuzi'' mpaka pale alipotangaza maandamano na baada ya kutangaza akakimbilia kwenye balozi za nchi za Ulaya kujificha!
Tukio la Tundu Lissu kukimbilia kwenye balozi za nchi za Ulaya lilihitimisha safari yake ya kuwa Rais wa Tanzania 2020 aliyekuwa amejaa ''mikwara mbuzi''.
Kwa dhana ile ile ya ''akili nyingi huondoa maarifa'', Tundu Lissu aliporudi Ubelgiji akaanza eti kuwalaumu watanzania kwa kutomuunga mkono huku akisema hawana uelewa mpana wa siasa!
Kuwalaumu watanzania ni kuonyesha jinsi ambavyo hawezi kuwasahau watanzania kwa yale walimfanyia! Hii ndio ikawa mwisho wa makelele mengi yenye mikwara mingi ambayo ilikuwa ni ''mikwara mbuzi''!
Bernard Membe naye ni mwanasiasa ambaye hatawasahau Watanzania baada ya kumpandisha juu na kumshusha haraka sana bila hata ya yeye kuelewa kinachoendelea!
Mitandao ya kijamii ilimuibua na kumpandisha juu bila ya yeye kujua kuwa wanaompandisha juu wanamfanya kama ni sehemu ya burudani ya kisiasa!
Membe alipewa majina yote ya ushujaa lakini majina ambayo alipenda kuitwa ni ''kachero mbobezi'' au ''nguli wa siasa za tanzania na kimataifa'' Kwenye mitandao ya kijamii kukaanzishwa alama ya reli (hashtag) inayosema ''Twende na Membe''! wapambe na mashabiki wakamjaza ''ujinga''!
Sifa alizokuwa anapewa kwenye mitandao ya kijamii zilimfanya akaanza kujiona ni ''invincible''!
Membe akaanza kudhani bila yeye wapinzani hawawezi ''kutoboa'' na kuingia Ikulu! Yaani yeye ndiye ''messiah'' wa wapinzani! Akaanza kutoa kejeli kwa Rais wa sasa wa Tanzania kuwa hana ''exposure'' huku akisema, ''"Ninataka kukabiliana na Rais aliyeko madarakani mimi peke yangu pamoja na kwamba wamenifukuza ndani ya chama''.
Akaanza kuwaambia wapinzani kama wanataka awasaidie kumtoa madarakani Rais Magufuli ni lazima kwanza waungane na kuunda kile alichokiita ''coalition'' na yeye kazi yake itakuwa kumtoa Ikulu aliyemuita ''yule mtu na kumpeleka nyumbani kwake Chato akapumzike''.
Kampeni zilipoanza, watu wenye uelewa wa mambo ya kisiasa wakajua huyu hawezi kufika mbali pale walipomuona anaingia kwenye uwanja wa kuhutubia akiwa ndani ya gari aina ya Range Rover Autobiography lakini akatumia matofali yaliyopangwa kama jukwaa kuhutubia!
Membe akiwa Mgombea Urais akatumia wiki mbili akizunguka katika kata ya Chiponda huko Lindi kama vile amekuwa mgombea Udiwani! Baada ya wiki mbili akapotea!
Akaibuka Airport akidai anaenda Dubai kwenye kikao muhimu! Baada ya kurudi kutoka Dubai ikawa ndio mwisho wa ''mbio za sakafuni'' za Urais wa Tanzania!
Viongozi wa ACT-Wazalendo hawakutaka tena kumsikia au kumuona na badala yake wakahamia kwa Tundu Lissu mwenye ''mikwara mizito'' kumbe naye pia ni ''mikwara mbuzi''!
Membe kwa sasa haonekani tena kwenye mitandao lakini kubwa zaidi, anaona aibu hata kuonekana mitaani!
Huu pia ndio ukawa mwisho wa Bernard Membe kama ''Kachero Mbobezi'' asiyejitambua ambaye nadhani hata kurudi CCM anaona aibu kwa jinsi ambavyo alikuwa anawabeza!
Wewe hujui kama viongozi wa upinzani walikamatwa kabla ya kuanza maandamano?Tatizo aliwaona Watanzania kama wajinga walipokuwa wanamshangilia akadhani ameshakuwa Rais wa Tanzania kwa kudhani akiwaambia lolote watafanya!
Uwezo wa mtu unapimwa kwenye matendo na matokeo!Huwezi kulinganisha Mbingu na Ardhi yaani Lissu na Membe Kiding
Niliposoma mchango wake ilibidi nicheke!Yani unataka alete mada ya kumsifia babaake na mamaake hapa jukwani?
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]Bange siyo nzuri
Unajifariji huku ukweli unaujua ile ni level nyingine, bila kupindua meza jiwe alishaaibika, kila mtu analijua hilo, Maandamano yalizuiwa na polisi
Unajifariji huku ukweli unaujua ile ni level nyingine, bila kupindua meza jiwe alishaaibika, kila mtu analijua hilo, Maandamano yalizuiwa na polisi
Lisu ana kiburi na dharau sana, hako ka elimu kake na ka kiingereza kake akawaona Watanzania mataahira tena mabogus kabisa na wao wakasema wewe ndio bogus tena mshenzi tu na tutakuonesha pumbavu zako [emoji23][emoji23].....na kweli bana tarehe 28 November wakamuonesha kama jinsi walivyosema waoKweli ile ni level nyingine kwa wasiyozijua siasa za Tanzania au wale wajinga!
Nadhani ulichokisema wanakijua lakini wanajaribu kujifariji ili ionekane hawakushindwa kuhamasisha maandamano!Usijidanganye ndugu yangu polisi hawana uwezo wa kuwazuia mamia ya raia walio choka na kuamua kuandamana kwa dhati ya mioyo yao, hawawezi kaka.
Watu waliwadharau na hawakuona sababu wala muda wakupoteza kufanya maandamano yasiyo na maana.
Alimhadaa Maalim kuwa watazuia majeshi toka Tanganyika yasiende Zanzibar hivyo Maalim atashinda safari hii.
Tatizo aliwaona Watanzania kama wajinga walipokuwa wanamshangilia akadhani ameshakuwa Rais wa Tanzania kwa kudhani akiwaambia lolote watafanya!
Kushinda kura kwa kutumia majeshi na gov't machinery sio jambo la kujisifia na kutamba hata kidogo.
Ni suala la muda tuu kama tulivyo kwisha ona madikteta wengi walivyo kuja ondoka madarakani eitha kwa aibu, kwenda jela au kuuwawa.
Yuko wapi Mugabe, Doe, Gaddafi, Mubarak, Bokassa, Nguema au Saddam?
Walikuwa wanatamba hadi watoto wao na jamaa zao lakini waliishia kufa kifo kama cha mbwa. Shinda uchaguzi kama wa Ghana hakuna mwenye kukulalamikia.
Na tambua ya kuwa Lissu ameanza kupata world recognition ambayo itamtesa sana dikteta uchwara wenu.
Kama uchaguzi ungekuwa huru na haki kwa 100%.... Nakuambia TL angekuwa president of this national.....