Baada ya ukweli wa Erick Kabendera kubainika, wote walionituhumu kuhusika nimewasamehe kwani Mungu amewasamehe. Msirudie tena!

Baada ya ukweli wa Erick Kabendera kubainika, wote walionituhumu kuhusika nimewasamehe kwani Mungu amewasamehe. Msirudie tena!

Kwani angekaakimya nani angemjibu. Alafu kwanini kuandika Uzi mreeeeefu, na ma reference lukuki yanini.

Vitabu vya dini vinasema majibuyenu yawe ndio, ndio, na sio,sio.
Hakuna haja ya kuandika maelezo meeeeengi,hayata saidia.
Nibora kukaa kimya alafu ukweli nauongo vitajickekecha vyenyewe kadiri muda unavyo kwenda.
Watanzania mna vichwa vibovu Sana , Una ushahidi gan anahusika....?? Ifikie hatua kila mmoja apambane na Hali yake na sio kujibanza kwa mtu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Pasco katika utetezi wako huu ndio umeharibu. Mmoja wa watu walio sema kwa nguvu kuwa makala zako hazikuwa za kumharibia Kabendera ni mie, lakini wote tulijua kuwa kesi alizofunguliwa ni za kutunga hazina uhusiano na yeye maana watesi wake wamesimamia msimamo kuwa Kabendera amekuwa akiichafua nchi nje.

Kwa makala yako nikama unataka tuamini kuwa kilichomtesa sio kazi yake bali ni utakatishaji fedha ndio maana amelipa 100M na atalipa mamilioni mengine for six month.

Pasco, Kabendera kalipa 100M? Au ni mchezo unachezwa kuipa serikali advantage kuwa mashtaka yetu yalikuwa sahihi?

Wewe ni Investigative Journalist, hebu ingia chimbo utuambie hela hizo zilizolipwa kwa DPP zilikuwa zimehifadhiwa bank gani? Na zimepokelewa na kuingizwa account gani ya serikali? Fuatilia kwa wakili wake akupe risiti ( ERV) ya mapokezi ya fedha hizo. TUANZIE HAPO.

Hili shinikizo la wafadhili lingekwepeshwaje kama sio kutumia hadaa? Na Kabendera bado alikuwa anauhitaji Uhuru wake hivyo sio ajabu kukubali maelekezo ya mchezo ili akakae na mkewe!

Anyway, naweza kuwa wrong kiasi Fulani. Lakini kuachiwa kwake sio sababu ya kufuta tuhuma zako dhidi yake bali tuhuma zako juu ya yaliyompata Kabendera zilisha futika siku nyingi kwa ukweli uliouweka hadharani kwa kauli zako. Achana na vibaka waliokuwa wanaendelea kukushikia bango kwa ushabiki.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Watanzania ndiyo tulivyo hua tunatuhumu tu kwa hearsay nakufanya ndo ukweli halisia. Ukishawafahamu watanzania hupati shida hata ya kuwaza kusamehe.
 
Kwa nini unamuita kaka, kwani mnauhusiano?
Tazama kichwamaji hiki kinachoamini kumuita mtu kaka au dada ni hadi uwe na uhusiano naye. Kwa taarifa yako, Pascal Mayalla namfahamu tangu nilipokuwa Sekondari na kiongozi wa TYCS akiwa anatoa mada pale Don Bosco. Ni kaka yangu kwakuwa simpati kiumri na nalifahamu hilo. Jitahidi kula samaki na dagaa kuchangamsha akili zako.
 
Mimi ni mmoja wa watu ambao nilikunyoshea kidole na kuandika makala zaidi ya moja. Paskali karma inakutesa tu...kumbuka kua usifanye mambo ya kujua mbele ya wengi wasiojua. Andika vyovyote vile bado deni utalipa tu....Kesho kutwa tunaenda kuhani matanga ( okwabya olufu) pale Katoma - Gera ila kaa ukijua nawe ni mzazi na binadamu tu
 
Pascal Mayalla, dah! okey poa nashukuru kwa msamaha wako kwani nami ni mmojawapo niliyekutwanga bonge la lawama kuhusiana na kabendera, ila naona kama ni mapema mno kwa wewe kujitoa hasa pale ulipojinasibu ulikuwa unamfahamu jamaa vizuri na ni rafiki yako, wengine bongo zetu zinachanganyaga mambo P.
 
Pascal ,,,kabendera kukiri makosa haina maana kuwa amekosa...amefanya hivyo ili asizidi kuumia maana serikali iliyopo ilikua inamkomoa na ndo maana kulikua na makubaliano.Nakuhakikishia ipo siku huu ukweli utajulikana na mtakua uchi.Huwezi kukaa mbali na uchafu huu.

Naisikitikia nchi yangu kwa sasa watu wananunua haki zao kwa mamilioni ya shilingi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kaka Pascal Mayalla wakati mwingine kukaa kimya huepusha na kuponya. Ingekuwa vyema kama ungebaki kimya. Sasa kwenye suala lile kuna ukweli gani uliothibitika? Wewe umetajwa wapi katika kusafishwa? Pole na chukua mkondo wa kubaki kimya.
Huaga napenda tu kumuona Pascal kama my real brother na usingeandika hapa nadhani nami ningeandika kitu kinacho fafana na ulicho kiandika na kwa kua wewe uliyeandika hapa ni mwana sharia kama Pascal, hope atayachukulia maandishi/ushauri wako kwa uzito unao stahiri, Mungu amfungue macho kaka Pascal
 
Wanabodi,

Kwa vile sisi binadamu tuna uwezo tofauti, na sio watu wengi wanajitambua uwezo wao katika kitu kinachitwa "self realization", ikitokea unajitambua, na unapokasirika kwa kutotendewa haki, kwa kutwishwa misalaba ambayo sio yako, na ukiumia na kulaani watesi wako, na unajua nini kitawatokea pale Mungu anapoamua kukutua msalaba huo, then sauti ya Mungu inakuingia, na hapo hapo unakumbuka na kuwasamehe watesi wako, kabla karma haijaanza kuwafanyia kazi.

Baada ya mwandishi wa habari za uchunguzi, Erick Kabendera kukamatwa na polisi na kushikiliwa mahabusu kwa miezi 7, msalaba wa kukamatwa nilibebeshwa mimi. Eti ni mimi Pascal Mayalla ndiye niliyesababisha kukamatwa kwa Erick Kabendera, kwasababu ya zile makala zangu za uzalendo humu JF.
Hizi ni Baadhi ya Makala Zangu Kuhusu Uzalendo, wale wenye muda, pitieni halafu mnieleze wapi nimemponza mtu yoyote?


Japo nilijifanya mgumu na sijali, kwasababu kiukweli kabisa, makala zile wakati zinaandikwa hazikuwa na lengo la kumchomea mtu yoyote, popote, na wala sikuwahi kuwafahamu waandishi wa makala hizo. Na mpaka sasa ninapoandika leo, bado siwafahamu waandishi wowote wa makala hizo, lakini kwa upande mwingine, kwa vile kuna mwandishi wa habari, Erick Kabendera, amekamatwa katika mazingira ya kutatatisha. Baada ya askari waliotumwa kumkamata kukataa kujitambulisha, hivyo kudhaniwa ni wasiojulikana na Erick akawagomea kuwafungulia, ndipo wakamfanyia utekaji kwanza; kwa kutekwa na kufichwa kusikojulikana kwa muda siku mbili za mwanzo, huku serikali wakitupiana mpira, mara ni polisi, mara ni immigration, na kosa lake mara ni uraia ila full kujiuma uma!.

Ila baada ya kufikishwa mahakamani ndipo kukaibuka uhujumu, utakatishaji fedha na magenge ya uhalifu. No one was sure axactly what is it, hivyo any reasonable man lazima ujiulize, "what if ni kweli mwandishi ni yeye?", "what if ni kweli zile makala zangu ndizo zimeiamsha serikali na kuichochea kumtafuta anayeandika?", "what if ni kweli mwanzo alitumiwa wasiojulikana ili wampoteze kama Azory Gwanda na Ben Saanane lakini baada ya Erick kuunguza picha, ndipo ikashindikana, na kuamua kumtafutia mashitaka yoyote ya kumbambikia just to silence him? Then japo nilikuwa najikaza kisabuni, lakini automatically nilianza kujihisi, na kila siku Erick alipokuwa akifikishwa mahakamani naumia, "what if sababu ni mimi?".

Kila uzi wowote kumhusu Erick Kabendera ukipandishwa humu JF lazima humo ndani ya uzi, lazima nilikuwa natajwa as a "snitch". Kila mateso aliyokuwa anakutana nayo Erick Kabendera, na mimi yalikuwa yananiumiza psychologically. Kwanza nikawa sichangii uzi wowote kuhusu jambo lolote kwa Erick Kabendera.

Mimi ni story teller, kwa wapenda nyuzi fupi, ishieni hapa, na kwenda kule kwenye hitimisho, wapenda mastory ya JF, tuendelee hapa

Sisi Wakristu wa kweli, tunaofuata mafundisho ya Mungu wa Kweli, na kufuata mafunzo ya Bwana wetu Yesu Kristo wa Kweli, tumefundishwa kusameme hata saba mara sabini, hivyo mimi kwa upande wangu, niliisha kusamehe toka siku ile ya kwanza ulipopandisha bandiko hili kwa kulipuuza, kwasababu ulikuwa hujui utendalo. Pia nimewasamehe wale wote walionituhumu ni mimi kwa kuamini kuwa kweli ni mimi.

Hitimisho:
Hivyo kwa uzi huu, baada ya ukweli wa mashitaka ya Erick Kabendera kubainika, mimi nimewasamehe "Wale Wote walionituhumu mimi kuhusika na kukamatwa kwa Erick Kabendera, na kufuatia msamaha huo, pia "Mungu nae, amewasamehe" Hakuna tena adhabu ya karma kwenye kunisingizia mimi issue ya Kabendera, ila tafadhalini sana, msirudie tena kumtuhumu mtu mwingine yoyote kwa tuhuma ambazo hamna hakina nazo! Kauli huwa zinaumba, sisi wengine tunajijua kauli zetu na madhara yake, hivyo mkituudhi tusiposamehe.


Hivyo kwa upande wangu, uwe na amani kabisa, na wote mlionituhumu humu na kungine kote, muwe na amani, nimekusamahe na kuwasamehe wengine wote kwa roho safi na roho nyeupe, lakini ili karma isikushughulikie na wewe kwa upande wako, baada ya kuujua ukweli huu, do the right thing, hata kimoyo moyo tu, inatosha Mungu anasikia kila kitu hata usipozungumza, ile kuwaza tuu, is enough!

Ubarikiwe sana.

Paskali.
Zaidi ya kuendelea kumhujumu Kabendera ndani ya uzi wako huu hakuna jipya , ni upi ukweli uliodhihirika ? mbona Kabendera hajalipa chochote na kaachiwa kwa msaada wa Wazungu !
 
Mayala tuliambiwa umezaliwa wakati wa njaa pengine hiyo ndo inakufanya uwe mnafiki.. Unarukaruka kama mahindi ya binsi kikaangoni embu tuambie huo ukweli uliodhihirika ni upi Alafu ngoja tukukumbushe kitu uzalendo sio kutetea serikali uzalendo ni kuitetea nchi kwa maslahi ya Mustakabali wa nchi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
EK kakiri makosa ya kubambikiwa na kesi ilikuwa ni fake hata wewe unajua. Waliokutuhumu kumchomea EK utambi hawajathibitishwa kuwa waongo bali EK alikiri makosa kununua uhuru wake.

Wale ambao hatukuamini kuwa una mkono kwenye hili saga sasa, kwa bandiko hili tunaanza kufikiri vinginevyo. Mara nyingine Pasco, kimya kinatunza heshima na ‘kuficha’ makosa!


Sent from my iPhone using JamiiForums
Halafu huo mkataba wa kukiri umekaa kikandamizaji sana:
  1. Ukishakiri kosa unapoteza haki ya kukata rufaa, isipokuwa tu kama rufaa hiyo ni dhidi ya adhabu
  2. Mkurugenzi wa Mashitaka bado ana haki ya kukata rufaa
  3. Kwa kukiri makosa unafutiwa pia mashitaka mengine yaliyoshitakiwa pamoja na hayo uliyokiri, lakini ukikiuka makubaliano makosa hayo yote yatafufuliwa (yaani hii iko kimafia kabisa, mfano kama Eric alivyokiri kosa la kutakatisha fedha amefutiwa pia shitaka la kuratibu kundi la kihalifu, lakini akikiuka makubaliano shitaka hili litafufuliwa, maana yake msoto wa jela na kauli za 'upelelezi haujakamilika' zitaendelea indefinitely)
Hii ni sheria ya ajabu sana.
 
Pascal Mayalla Kabendera amekiri makosa ya ML & tax evation. Wanaojaribu ku -spin hii story eti amelazimika kununua uhuru wake wanamchafulia jina kwa kumfanya mpiga dili za kukiuka mujibu wa sheria. Hamumsaidii kwa Hoja hizo za kitoto, bora mumuwache ajenge reputation yake afresh.Maana sasa huyu sio mshukiwa ni convict wa Kuhujumu Uchumi
 
Back
Top Bottom