Baada ya Vyama vya Ukombozi kuziharibu nchi zao kwa kuingiza siasa kwenye Vyombo vya Ulinzi na Usalama, Kagame avifundisha nini maana ya Uongozi!

Baada ya Vyama vya Ukombozi kuziharibu nchi zao kwa kuingiza siasa kwenye Vyombo vya Ulinzi na Usalama, Kagame avifundisha nini maana ya Uongozi!

Lord denning

JF-Expert Member
Joined
Jun 3, 2015
Posts
15,819
Reaction score
33,255
Kwa wataalam wa masuala ya Ulinzi na Usalama aibu waliyoipata SADC baada ya Mission yao kufeli nchini Congo DRC, sio jambo lililotokea kwa bahati mbaya.

Baada ya kuingia siasa za ushindani kusini mwa Bara la Afrika, Vyama vinavyofahamika kama vyama vya ukombozi ambavyo vingi vinatawala nchi za Kusini mwa Bara hili, kwa uchu tu wa madaraka, viliamua kuingiza siasa kwenye majeshi yao na vyombo vya dola ili viendelee kubaki madarakani.

Vyama hivyo, CCM( hapo awali TANU) ANC, ZANU PF, FRELIMO, SWAPO na BDP kutokana na hofu ya kuwa vyama pinzani badala ya kuwekeza katika kuzijenga nchi zao kimaarifa na hatimaye kuwa imara katika Dunia hii inayozidi kuwa na ushindani kila siku viliamua tu kwa makusudi kuingiza siasa kwenye mifumo yake ya ulinzi na usalama kwa ajili ya kuvilinda na hatimaye kuvifanya vyombo vyao vya Ulinzi na Usalama kuwa vya kisiasa badala ya kutimiza majukumu yake ya Ulinzi na Usalama.

Ushahidi wa siasa kuingia kwenye vyombo vya Ulinzi na Usalama vya mataifa haya ni namna vyombo vya ulinzi na usalama katika mataifa hayo vilivyokuwa vinatumika katika kulinda rushwa na tawala mbovu katika nchi hizo ( Mfano Tanzania, Zimbabwe na Msumbiji)

Kuingia kwa siasa kwenye majeshi na taasisi za intelejensia za nchi hizo sio tu kumefanya kukua kwa rushwa katika nchi hizo bali pia kuanguka kwa mifumo thabiti ya ulinzi na usalama iliyokuwepo hapo awali katika block hii ya SADC

Pia kuingia kwa siasa katika nchi taasisi za majeshi na intelejensia za vyombo hivi kumesababisha ombwe kubwa la uongozi hasa kutokana na nchi hizi kushindwa kujilinda dhidi ya maadui wa ndani na nje.

Mfano wa kwanza wa kufeli kwa vyombo vya ulinzi na usalama vya nchi hizi ni matukio ya kigaidi yaliyoikumba nchi ya Msumbiji. SADC kama block kongwe katika Afrika ilishindwa kabisa kuisadia msumbiji kijeshi kupambana na Magaidi hadi pale Rwanda alipojitokeza kupeleka vikosi vyake Kaskazini mwa Msumbiji ambavyo vimesifika kwa kufanikiwa kurudisha hali ya utulivu.

Mfano wa pili kwa kufeli kwa nchi hizi kutokana na kuingiza siasa katika majeshi yao na taasisi zao za intelejensia ni namna Walivyoshindwa kusoma vizuri hali ya usalama ya Mashariki mwa Congo hadi vikosi vyao vilivyoenda kwa mbwembwe kufeli mission yao ya kuondoa vikosi vya uvamizi mashariki mwa Congo.

Kwa bahati nzuri sana, anayewafundisha nchi hizi namna ya kutumia Taasisi za Majeshi na Intelejensia kwa weredi na sio kisiasa ni Paul Kagame ambaye anazijua vizuri sana hizi nchi za SADC kihistoria na mwenendo wake wa sasa kwa sababu kwa miaka mingi alizitumia kufundisha majeshi yake.

Kagame akiwa Rais wa nchi ndogo sana iliyo na very limited resources amevifundisha vyama vya ukombozi vya nchi za SADC kuwa majeshi yanatakiwa kujikita kwenye masuala yake ya kijeshi na sio siasa kwa faida ya nchi kiuchumi. Na anafanya hivi kwa kutumia jeshi lake kuipaisha Rwanda kiuchumi.

Kagame anavifundisha vyama vya ukombozi kuwa intelejensia inatakiwa kutumika kwa maslahi mapana ya kijeshi na kiuchumi kwa faida ya nchi na sio kukandamiza tu upinzani na kuiba chaguzi tu.

Hongera Kagame. Sasa Waafrika watajifunza kwako.
 
Akili zetu sasa zimeishiq kuliambia Jeahi lifanye mazoezi au wazoe taka kuwatisha wapinzani wasiandamane.

Au kuwatumia TISS kuiba hadi chaguzi za vijiji.
Bandiko nzuri na ni Hali halisi kabisa, ila sisi hatuna la kujifunza kwa Kagame kwa sababu uroho wa madaraka umetupofusha macho, so hatuna mahali tunakwenda.
 
Hapa hutomuona Lucas Mwashambwa, Pascal Mayalla, Malaria 2 , Tlaatlaah , MamaSamia2025 , ChawaWaMama, chawa wa mama, ChoiceVariable wala mbuzi yeyote wa kijani kutoka chama Cha Mambuzi
vyombo vya ulinzi na usalama Tz, Africa na duniani kote, haviwezi kumtazama na kumkenulia tu muhalifu yeyote yule anaejaribu kuvuruga na kuhatarisha amani, umoja na mshikamano wa wananchi popote ulimwengu eti kwa kisingizio cha haki na uhuru wa kidemokrasia.

kila tasisi ikiwa ni pamoja na vyama vya siasa, ni muhimu kufanya na kutekeleza majukumu yao kwa kuwajibika kuzingatia sheria zilizopo mahali husika bila mbambamba yoyote,

vinginevyo watawajibishwa ipasavyo na vyombo vya kulinda amani kwa nguvu na gharama yoyote ile, hata kama watapiga mayowe makubwa kiasi gani.

Ni vizuri tasisi zote za umma, za kiraia na kidini kufanya kazi kwa uhuru kwa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu za nchi husika kama zilivyoainishwa kikatiba.

Kama Taifa,
hakuna la kujifunza kwingineko ispokua, kuendelea kutoa mafunzo na uzoefu kwa mataifa mengine jirani namna ya kuongoza nchi kidemokrasia na kwa amani 🐒
 
Mbona kagame mwenyewe amekuwa madarakani kwa kipindi kirefu zaidi? Amekuwa akishutumiwa kuwapoteza wapinzani wake hata wenye jinsia ya ke , analaumiwa kwa kukandamiza demokrasia kama ilivyo kwa Yoweli Kaguta Museveni, Robert Mugabe na waliofanyiwa mapinduzi ya kijeshi Somalia, Mali, Ghana na Niger
 
Huyo Mti mkavu wamemkauishia tu kwa sababu ya sheria za kiusalama ktk ulimwengu wa smartphone,ila angezabuliwa chini kwa chini kama 2014 na kuanza kulia lia.Maneno yalikua hayahaya 2014 kabla ya kuzibuliwa kidogo na kusambaratika
 
Taifa lolote likisha fanya rushwa kuwa sehemu ya taifa hilo ni wazi kwamba taifa hilo ni mfu.
Pk anamatatizo yake lakini linapo kuja suala la kuongoza nchi na maslahi ya nchi hacheki na mtu.
 
Inasikitisha tiss imekuja kuwa hovyoo kipindi cha nyerere na mkapa. Hawa tiss kipindi cha kikwete kuendelea YA UNAJUA MIMI NI NANI. tiss ndo ilianza kupoteza weledi wake.
 
Kwa wataalam wa masuala ya Ulinzi na Usalama aibu waliyoipata SADC baada ya Mission yao kufeli nchini Congo DRC, sio jambo lililotokea kwa bahati mbaya.

Baada ya kuingia siasa za ushindani kusini mwa Bara la Afrika, Vyama vinavyofahamika kama vyama vya ukombozi ambavyo vingi vinatawala nchi za Kusini mwa Bara hili, kwa uchu tu wa madaraka, viliamua kuingiza siasa kwenye majeshi yao na vyombo vya dola ili viendelee kubaki madarakani.

Vyama hivyo, CCM( hapo awali TANU) ANC, ZANU PF, FRELIMO, SWAPO na BDP kutokana na hofu ya kuwa vyama pinzani badala ya kuwekeza katika kuzijenga nchi zao kimaarifa na hatimaye kuwa imara katika Dunia hii inayozidi kuwa na ushindani kila siku viliamua tu kwa makusudi kuingiza siasa kwenye mifumo yake ya ulinzi na usalama kwa ajili ya kuvilinda na hatimaye kuvifanya vyombo vyao vya Ulinzi na Usalama kuwa vya kisiasa badala ya kutimiza majukumu yake ya Ulinzi na Usalama.

Ushahidi wa siasa kuingia kwenye vyombo vya Ulinzi na Usalama vya mataifa haya ni namna vyombo vya ulinzi na usalama katika mataifa hayo vilivyokuwa vinatumika katika kulinda rushwa na tawala mbovu katika nchi hizo ( Mfano Tanzania, Zimbabwe na Msumbiji)

Kuingia kwa siasa kwenye majeshi na taasisi za intelejensia za nchi hizo sio tu kumefanya kukua kwa rushwa katika nchi hizo bali pia kuanguka kwa mifumo thabiti ya ulinzi na usalama iliyokuwepo hapo awali katika block hii ya SADC

Pia kuingia kwa siasa katika nchi taasisi za majeshi na intelejensia za vyombo hivi kumesababisha ombwe kubwa la uongozi hasa kutokana na nchi hizi kushindwa kujilinda dhidi ya maadui wa ndani na nje.

Mfano wa kwanza wa kufeli kwa vyombo vya ulinzi na usalama vya nchi hizi ni matukio ya kigaidi yaliyoikumba nchi ya Msumbiji. SADC kama block kongwe katika Afrika ilishindwa kabisa kuisadia msumbiji kijeshi kupambana na Magaidi hadi pale Rwanda alipojitokeza kupeleka vikosi vyake Kaskazini mwa Msumbiji ambavyo vimesifika kwa kufanikiwa kurudisha hali ya utulivu.

Mfano wa pili kwa kufeli kwa nchi hizi kutokana na kuingiza siasa katika majeshi yao na taasisi zao za intelejensia ni namna Walivyoshindwa kusoma vizuri hali ya usalama ya Mashariki mwa Congo hadi vikosi vyao vilivyoenda kwa mbwembwe kufeli mission yao ya kuondoa vikosi vya uvamizi mashariki mwa Congo.

Kwa bahati nzuri sana, anayewafundisha nchi hizi namna ya kutumia Taasisi za Majeshi na Intelejensia kwa weredi na sio kisiasa ni Paul Kagame ambaye anazijua vizuri sana hizi nchi za SADC kihistoria na mwenendo wake wa sasa kwa sababu kwa miaka mingi alizitumia kufundisha majeshi yake.

Kagame akiwa Rais wa nchi ndogo sana iliyo na very limited resources amevifundisha vyama vya ukombozi vya nchi za SADC kuwa majeshi yanatakiwa kujikita kwenye masuala yake ya kijeshi na sio siasa kwa faida ya nchi kiuchumi. Na anafanya hivi kwa kutumia jeshi lake kuipaisha Rwanda kiuchumi.

Kagame anavifundisha vyama vya ukombozi kuwa intelejensia inatakiwa kutumika kwa maslahi mapana ya kijeshi na kiuchumi kwa faida ya nchi na sio kukandamiza tu upinzani na kuiba chaguzi.

Hongera Kagame. Sasa Waafrika watajifunza kwako.
Sahihi kabisa kagame ameshinda, baada ya kufaulu kujitanua Kongo anaweza kuigeukia nchi yetu jeshi letu lijipange kisawasawa
 
Kwa wataalam wa masuala ya Ulinzi na Usalama aibu waliyoipata SADC baada ya Mission yao kufeli nchini Congo DRC, sio jambo lililotokea kwa bahati mbaya.

Baada ya kuingia siasa za ushindani kusini mwa Bara la Afrika, Vyama vinavyofahamika kama vyama vya ukombozi ambavyo vingi vinatawala nchi za Kusini mwa Bara hili, kwa uchu tu wa madaraka, viliamua kuingiza siasa kwenye majeshi yao na vyombo vya dola ili viendelee kubaki madarakani.

Vyama hivyo, CCM( hapo awali TANU) ANC, ZANU PF, FRELIMO, SWAPO na BDP kutokana na hofu ya kuwa vyama pinzani badala ya kuwekeza katika kuzijenga nchi zao kimaarifa na hatimaye kuwa imara katika Dunia hii inayozidi kuwa na ushindani kila siku viliamua tu kwa makusudi kuingiza siasa kwenye mifumo yake ya ulinzi na usalama kwa ajili ya kuvilinda na hatimaye kuvifanya vyombo vyao vya Ulinzi na Usalama kuwa vya kisiasa badala ya kutimiza majukumu yake ya Ulinzi na Usalama.

Ushahidi wa siasa kuingia kwenye vyombo vya Ulinzi na Usalama vya mataifa haya ni namna vyombo vya ulinzi na usalama katika mataifa hayo vilivyokuwa vinatumika katika kulinda rushwa na tawala mbovu katika nchi hizo ( Mfano Tanzania, Zimbabwe na Msumbiji)

Kuingia kwa siasa kwenye majeshi na taasisi za intelejensia za nchi hizo sio tu kumefanya kukua kwa rushwa katika nchi hizo bali pia kuanguka kwa mifumo thabiti ya ulinzi na usalama iliyokuwepo hapo awali katika block hii ya SADC

Pia kuingia kwa siasa katika nchi taasisi za majeshi na intelejensia za vyombo hivi kumesababisha ombwe kubwa la uongozi hasa kutokana na nchi hizi kushindwa kujilinda dhidi ya maadui wa ndani na nje.

Mfano wa kwanza wa kufeli kwa vyombo vya ulinzi na usalama vya nchi hizi ni matukio ya kigaidi yaliyoikumba nchi ya Msumbiji. SADC kama block kongwe katika Afrika ilishindwa kabisa kuisadia msumbiji kijeshi kupambana na Magaidi hadi pale Rwanda alipojitokeza kupeleka vikosi vyake Kaskazini mwa Msumbiji ambavyo vimesifika kwa kufanikiwa kurudisha hali ya utulivu.

Mfano wa pili kwa kufeli kwa nchi hizi kutokana na kuingiza siasa katika majeshi yao na taasisi zao za intelejensia ni namna Walivyoshindwa kusoma vizuri hali ya usalama ya Mashariki mwa Congo hadi vikosi vyao vilivyoenda kwa mbwembwe kufeli mission yao ya kuondoa vikosi vya uvamizi mashariki mwa Congo.

Kwa bahati nzuri sana, anayewafundisha nchi hizi namna ya kutumia Taasisi za Majeshi na Intelejensia kwa weredi na sio kisiasa ni Paul Kagame ambaye anazijua vizuri sana hizi nchi za SADC kihistoria na mwenendo wake wa sasa kwa sababu kwa miaka mingi alizitumia kufundisha majeshi yake.

Kagame akiwa Rais wa nchi ndogo sana iliyo na very limited resources amevifundisha vyama vya ukombozi vya nchi za SADC kuwa majeshi yanatakiwa kujikita kwenye masuala yake ya kijeshi na sio siasa kwa faida ya nchi kiuchumi. Na anafanya hivi kwa kutumia jeshi lake kuipaisha Rwanda kiuchumi.

Kagame anavifundisha vyama vya ukombozi kuwa intelejensia inatakiwa kutumika kwa maslahi mapana ya kijeshi na kiuchumi kwa faida ya nchi na sio kukandamiza tu upinzani na kuiba chaguzi.

Hongera Kagame. Sasa Waafrika watajifunza kwako.
Mkuu naona unasifia kichaka.
Kagame mtoto wetu, tumemfundisha hapa, na hawezi kuwa zaidi ya anachotujua.
Jinsi ulivyo mtoto, hujui kwamba Afrika yote Kusini mwa Afrika ilikombolewa wakati wa chama kimoja.
Na nduli Iddi Amin alitandikwa wakati wa chama kimoja.
Mbinu za kijeshi na mapambano huzijui kwa sababu za utoto wako.
Kagame kaua askari wetu wawili Kongo, katika mission ya kweka amani nchi ya kiafrika.
Hatusahau hilo.
Payback time must come, watch this space.
 
Inasikitisha tiss imekuja kuwa hovyoo kipindi cha nyerere na mkapa. Hawa tiss kipindi cha kikwete kuendelea YA UNAJUA MIMI NI NANI. tiss ndo ilianza kupoteza weledi wake.
Wale ni maiti sasaivi. Kila kitu wanafanya kwa maelekezo ya CCM.
 
Back
Top Bottom