Baadhi ya marafiki wakifanikiwa kipesa tu kidogo, wanaanza maneno ya kejeli

Baadhi ya marafiki wakifanikiwa kipesa tu kidogo, wanaanza maneno ya kejeli

Balqior

JF-Expert Member
Joined
Jun 8, 2021
Posts
2,406
Reaction score
8,039
Kuna siku moja nilikuwa kwenye kijiwe cha draft hapa Dar, mzee mmoja alisema msaki (mmiliki wa kibo complex) anatuona Sie wote hapa hatuna akili, nilidhani wanaongea hivyo sababu wanamwonea wivu Ila baadaye nilikuja gundua maneno yao yana ukweli kwa kiasi flani, wala si wivu.

Yani utakuta rafiki yako kabahatika kupata tenda yenye mshahara mnono anaanza kukwambia maneno kama haya Katika nyakati tofauti mkiwa mnapiga story:

1) Huna hata baiskeli
2) Fulani hana pesa anaishi maisha magumu Kama wewe
3) Una akili za kimaskini na za kifukara kabisa.

Wakati hapo mwanzoni kabla mambo hayajamnyookea, hakuwa na kauli hizo. Ni kauli za kuumiza roho ila kwavile ni mshkaji unazipotezea.

Yani mtu anakwambia hivyo wakati yeye alivyokuwa kwenye kipindi kigumu kiuchumi, na wewe uko kwenye neema hukuwahi kumtamkia kauli hizo.

Waliowahi kukutana na hali kama hizi nje hapa mtoe shuhuda zenu.
 
Tabia ya kupenda kuumizwa na maneno hayo nayo pia ni UGONJWA mkubwa wa nafsi, nayo pia inatokana na moyo wenye pupa ya mashindano makali na watu wengine.

Tunaishi duniani mara moja.

Maisha ni mafupi mno KUSIKILIZA maneno ya watu wengine especially IDIOTS, haina maana kuwa na KINGI/VYEO/ELIMU huwa ni lazima watu hao wasiwe "IDIOTS"

Mke/Mume/Ndugu/Rafiki/Jirani/Mpenzi muda wowote anaweza kumuumiza mwingine kwa MANENO NA VITENDO VYA KUKATA MOYO NA HISIA.

Kujipenda mwenyewe ni pamoja na kuupenda "ULIMWENGU" vyema na KUWAVUMILIA WENGINE hususani wale walio na upumbavu mwingi.

Mwenyezi Mungu akupe afya, nguvu ,fursa na uchumi mkubwa aamin aaamin aaaamin aaamin ili nawe uje KUNIKEBEHI, KUNIDHARAU NA KUNISIMANGA halafu nikuonyeshe jinsi gani NITAKAVYOKUVUMILIA NA KUKUPA HESHIMA yako ya kiubinadamu 🤣🤣🤣

#Yetzer Hatov

#Siempre JMT🙏
 
Hakuna cha kijiwe wala wazee wewe ndio huyo mzee, hili dongo ni kutoka kwako kwenda kwa huyo Msaki maana uliona mpaka uandike anachomiliki ili ajijue.

Sasa kama huna hata baiskeli kweli ulitaka akwambiaje? Ukute ulikuwa unamjua kabla hajatusua, kahangaika anavyojua mwenyewe kapata alichopata halafu ghafla unaona uhalali wa kugaiwa na wewe. Kama hiyo tenda ilikuwa rahisi kupata mbona hukupata wewe.

Ukiendelea na fikra hizi kuwa kila unaemjua akipata anapaswa kukupa na wewe basi utakufa fukara ndugu. Ondoka kijiweni nenda ukafanye kazi.
 
Tabia ya kupenda kuumizwa na maneno hayo nayo pia ni UGONJWA mkubwa wa nafsi....nayo pia inatokana na moyo wenye pupa ya mashindano makali na watu wengine.

Tunaishi duniani mara moja.

Maisha ni mafupi mno KUSIKILIZA maneno ya watu wengine, especially IDIOTS, haina maana kuwa na KINGI/VYEO/ELIMU huwa ni lazima watu hao wasiwe "IDIOTS"

Mke/Mume/Ndugu/Rafiki/Jirani/Mpenzi muda wowote anaweza kumuumiza mwingine kwa MANENO NA VITENDO VYA KUKATA MOYO NA HISIA.

Kujipenda mwenyewe ni pamoja na kuupenda "ULIMWENGU" vyema na KUWAVUMILIA WENGINE hususani wale walio na upumbavu mwingi.

Mwenyezi Mungu akupe afya, nguvu ,fursa na uchumi mkubwa aamin aaamin aaaamin aaamin ili nawe uje KUNIKEBEHI ,KUNIDHARAU NA KUNISIMANGA halafu nikuonyeshe jinsi gani NITAKAVYOKUVUMILIA NA KUKUPA HESHIMA yako ya kiubinadamu 🤣🤣🤣

#Yetzer Hatov

#Siempre JMT🙏
Mr Jumbe Brown kwenye jamii zetu mtu mwenye hela anaonekana ni Bright na Genius sana. Anaonekana wa maana. Na ndio maana wanaweza kuongea neno lolote wanalojisikia bila kujua wanawaumiza wenzao.

Napenda sana Wazungu wanavyoishi yaani ongea yake anajilinda sana asitamke neno la kumkera mwenzake maana maisha ni mafupi dunia tuifanye iwe ya furaha kwa kila mtu.
 
Hahaha hata hivyo maskini hapendi ukweli.

Umaskini uko kama kile ukimwambi ukweli wewe kilema anakwambia unamnyanyapaa.

Hao wazee mafaller tu, huyo Msaki ndio namjua alikuwa dalali wa mchanga lkn ni mpambanaji mwanzo mwisho.
 
Ni kweli kabisa tazama tu hata wanaopata madaraka.

Pesa na madaraka ni pombe inalevya sana.

Mtu anafika mahali hadi kaka zake anawaona hawana akili wakati mafanikio tu kayapata kwa ngekewa na zali.
Haha jana nliingia Insta story ya sirjeff dennis, Humu jf anatumia ID ya Ontario, alisema hawezi pokea ushauri kutoka kwa mtu ambaye hajui kesho atakula nini, yeye anatafuta pesa za kula za wajukuu wake Pythagoras Me too chizcom Toxic Concotion
 
Hahaha hata hivyo maskini hapendi ukweli.
Umaskini uko kama kile ukimwambi ukweli wewe kilema anakwambia unamnyanyapaa.

Hao wazee mafaller tu...huyo Msaki ndio namjua alikuwa dalali wa mchanga lkn ni mpambanaji mwanzo mwisho.

Haha shida sio kuitwa maskini, shida ni jinsi unavyoitwa.

Yani mtu anakwambia wewe ni maskini nia yake ni ili akuumize roho, na kukuonesha dharau Glenn
 
😅😅😅😅 kufanikiwa sio ishu ndogo bwashee

Learn to celebrate people when they r winning🤍
Hapana hajasema kuwa anachukia. Anasema tabia zao baada ya kufanikiwa.

Mwelewe vizuri ndugu.
 
  • Thanks
Reactions: THT
Mr Jumbe Brown kwenye jamii zetu mtu mwenye hela anaonekana ni Bright na Genius sana. Anaonekana wa maana. Na ndio maana wanaweza kuongea neno lolote wanalojisikia bila kujua wanawaumiza wenzao.

Napenda sana Wazungu wanavyoishi yaani ongea yake anajilinda sana asitamke neno la kumkera mwenzake maana maisha ni mafupi dunia tuifanye iwe ya furaha kwa kila mtu.
Hakika mkuu wangu,

Haswaaa

Jamii yetu HAIJIPENDI kiukweli, kwani mwenye kujipenda kidhati atajiamini vyema kwa hali yeyote uliyokuwa nayo.

Huku mitaani kunachekesha sana, sana yaani.

Ukiwa na maisha ya afadhali kipato na ukaishi hulka za "DOWN TO EARTH" wandewa wanashangaa sana, watakuita majina tofautitofauti mara mshamba, mara mchawi na mshirikina wa ngende. 🤣🤣

#Hatujawa duniani tuyaishi maisha ya wengine

#Siempre JMT🙏
 
Back
Top Bottom