Baadhi ya miradi ya uwekezaji inayoweza kufanywa na wastaafu

Baadhi ya miradi ya uwekezaji inayoweza kufanywa na wastaafu

Mkuu maisha ya Watanzania wengi ni duni kiuhalisia

Hao wanaopokea mshahara Kwa Mwezi ndiyo walau wanaonekana Wana unafuu wa maisha, maana Wana Bima wakiugua pamoja na Kipato cha uhakika japo hakitoshelezi

Ndiyo maana nimeandika Uzi wa kuwakumbusha waliopo makazini,kukumbuka kujiwekeza

Otherwise, maisha yao ya Uzee yatakuwa ni shida mno
Hao maisha yao ya uzeeni yatakuwa na uhakika wakiishi within their means.., tena unajua ni vema mtu ukafanya kitu ulichozoea sasa mtu ulikuwa Muhasibu miaka yako yote umestaafu eti ukawe mkulima (different lifestyles ) unaweza jikuta unanunua stress na ugonjwa wa moyo au pesa yako kupotea bila habari..., By the way unasema hawa watakuwa na maisha ya shida vipi wazee wa kesho ambao ndio wachuuzi wa leo ambao they are not pensionable.... (Tena hao itakuwa sio tu shida kwao bali Kero kwa jamii ya kipindi hicho kuzungukwa na wazee ombaomba)

 
Kina fanya kazi taasis nyingne ila sio jwtz, waligoma na wanalipwa yote.
Kumbe Jeshini wanakula yote ya Mkupuo??

Nadhani watumishi wengine wangekuwa na Umoja, wangekataa huo upuuzi wa kupewa 33% badala ya kupewa yote kama ilivyo Wabunge na hao JWTZ kama ulivyosema
 
Umesema sahihi Mkuu

Kuwa na shughuli baada ya kustaafu kunasaidia kuimarisha afya

Kuna Semina moja niliwahi kukutana na Mstaafu anaitwa Mathias, ndiyo mwenye lile eneo maarufu pale Kibaha (Kibaha Kwa Mathias)

Yule Mzee bado anafanya kazi zake za Ushauri (Consultant) kupitia Kampuni aliyoifungua

Na ukimwona, unaona bado ana nguvu, nafikiri kutokana na kuendelea kujishughulisha

Nina Mzee wangu baada ya kustaafu kazi miaka ya Mwanzoniwa 90, aliamua kujiajiri kupitia kazi za Utaalamu wa fedha, ama Kampuni yake ya Auditing

Yupo hai hadi sasa akifanya kazi ya kufungia hesabu makampuni binafsi pamoja na kufanya Ukaguzi (Auditing)

Bila kujishughulisha, haufiki miaka 65 unakuta umeshaaga Dunia
Unaona sasa, halafu mtu aniambie nilale tu
Mawazo ya uzee na maradhi hayajui labda
Kwanza bora kufa ila maradhi ndio mtihani mara pressure, miguu kuwaka moto, maradhi ya kusahau maana akili haifanyi kazi zaidi ya kuangalia kuku za jirani 😄 🤣
Yaani uzee unaleta majanga
Ntafanya kazi hata siku nne kwa wiki tosha kabisa
 
Hao maisha yao ya uzeeni yatakuwa na uhakika wakiishi within their means.., tena unajua ni vema mtu ukafanya kitu ulichozoea sasa mtu ulikuwa Muhasibu miaka yako yote umestaafu eti ukawe mkulima (different lifestyles ) unaweza jikuta unanunua stress na ugonjwa wa moyo au pesa yako kupotea bila habari..., By the way unasema hawa watakuwa na maisha ya shida vipi wazee wa kesho ambao ndio wachuuzi wa leo ambao they are not pensionable.... (Tena hao itakuwa sio tu shida kwao bali Kero kwa jamii ya kipindi hicho kuzungukwa na wazee ombaomba)

Umesema sahihi, ndiyo maana inashauriwa uwekeze eneo ambalo una ABC nalo

Mfano Engineer wa Ujenzi kuwekeza kwenye Ukandarasi/Local Fundi ama hardware za Vifaa vya Ujenzi

Lakini unakuta ni Engineer halafu unaenda kufungua Maabara ya afya, hapo unaweza kupata stress kwenye usimamizi
 
Hongera sana Kwa huyo Mstaafu mwenzetu kuweza kuwekeza mapema

Mtu wa hivyo hakosi milioni 100 hadi 300 Benki

Kwa Vijana waliopo makazini

Kupanga ni Kuchagua
Kabisa.kijijini kuna fursa nyingi kuliko mjini.mwl ukipangwa kojijini nunua kreti la bia sherekea.mjini utaishia kufundisha vitwisheni uchwara na kua dalali au winga kariakoo.kijijini utalima utafungua ma hard ware shops utafuga utapiga hela.hauna walimu wana maisha mazuri kama wa vijijini
 
Unaona sasa, halafu mtu aniambie nilale tu
Mawazo ya uzee na maradhi hayajui labda
Kwanza bora kufa ila maradhi ndio mtihani mara pressure, miguu kuwaka moto, maradhi ya kusahau maana akili haifanyi kazi zaidi ya kuangalia kuku za jirani 😄 🤣
Yaani uzee unaleta majanga
Ntafanya kazi hata siku nne kwa wiki tosha kabisa
Muhimu sana kujishughulisha baada ya kustaafu.

Kwanza unakuwa na direct intact na wateja wako, kwahiyo unafanya socialization. Kwa muda unaachana na Upweke

Lakini pia unafanya seli za mwili kuendelea kufanya kazi Kwa ufasaha, maana unazishughulisha kufikiri n.k

Kwahiyo utachelewa kuzeeka

Lakini pia unakuwa na uhakika wa kusimamia vizuri miradi na Kipato chako moja Kwa moja

Hata kama itakuwa Siku 4 Kwa wiki

Mimi yule Mzee wangu, yupo hai hadi sasa, na kama Mungu akipenda huenda akafika hata 95 huko
 
Kabisa.kijijini kuna fursa nyingi kuliko mjini.mwl ukipangwa kojijini nunua kreti la bia sherekea.mjini utaishia kufundisha vitwisheni uchwara na kua dalali au winga kariakoo.kijijini utalima utafungua ma hard ware shops utafuga utapiga hela.hauna walimu wana maisha mazuri kama wa vijijini
Ni kweli huko Vijijini Kuna fursa nyingi Kwa Walimu ama Watu wa afya wanaofanya kazi huko

Changamoto yao ni kushindwa kuamka(wengi vichwa vyao vimelala)

Lakini wangekuwa serious unanunua ekari zako 100 ama 50 unalima zako fresh tu

Wakati huo huo unafuga zako Kuku/Nguruwe/Ng'ombe wa Maziwa/Mbuzi ili kuongeza kipato

Shida yetu Watumishi wengi vichwa vimelala
 
Salaam,

Kila mtumishi aliyeajiriwa, akumbuke itafikia wakati atalazimika kustaafu kazi. Kustaafu huku inaweza kuwa ni kwa hiari ama kulazimishwa kutokana na Umri (Miaka 60 ama 65 kwa Wakufunzi wa Vyuo Vikuu) ama sababu za Ulemavu ama Maradhi yasiyotibika.

Kwa kujua huku kwamba kuna siku tutalazimika kustaafu na kupisha damu changa kwenye utumishi wetu, ndiyo maana inashauriwa kuanza kujiwekeza tangu tarehe ya kwanza unapokea mshahara wako wa kwanza.

Kama mnavyofahamu, Mtumishi akisha staafu, hunufaika na kulipwa kiasi cha 1/3 ya Mshahara wake aliokuwa anapokea wakati anastaafu. Mathalani ikitokea unastaafu ukiwa unapokea mshahara wa shilingi za Kitanzania 1,500,000 kwa Mwezi (Gross Salary) basi ukisha staafu utaanza kulipwa kiasi cha shilingi 500,000 tu hadi siku unaaga Dunia (Kufariki).

Pamoja na hilo, mtumishi huyu atalipwa kiiunua mgongo chake ambacho kwa kikokotoo kipya atalipwa 33% ya fedha zake za Mkupuo.

Kwa taarifa ambazo sio rasmi, watumishi wengi sasa wanapokea fedha zao za Mkupuo unao-range kati ya shilingi 25,000,000 hadi 200,000,000 kulingana na kiwango chako cha mshahara.

Kwa kutambua hili, napenda kuwasisitiza wastaafu watarajiwa, kuhakikisha mnajenga nyumba zenu za kuishi ukiwa bado upo kazini. Ili utakapolipwa fedha zako za kiinua mgongo, basi uzitumie kwenye shughuli nyingine lakini isiwe kujenga.

Kupitia andiko hili, tunaweza kupeana dondoo za aina ya miradi inayoweza kufanywa na Wastaafu ili kujikidhi na maisha yao ya baada ya kustaafu.

  • Uwekezaji kupitia Kilimo Biashara; Ufugaji wa Nyuki,mazao ya chai, matunda, Ufugaji na Kuku wa Kisasa kwaajili ya Mayai na Nyama.
  • Uwekezaji kupitia biashara ya Majengo(Real Estates); Biashara ya GuestHouses, Biashara ya kununua na kuuza viwanja, Nyumba za Kupangisha n.k
  • Biashara mtandao ya kununua na kuuza iwe ni vifaa vya Umeme ama vya nyumbani
  • Biashara kupitia Teknolojia; Kuna baadhi ni wataalamu wa Tehama kama vile Website development, Apps n.k. bila kusahau biashara ya fedha mtandao mfano Mpesa,Airtel Money,CRDB Wakala n.k.
  • Unaweza kuwekeza kwenye Utalii, kwa kufungua kampuni ya Utalii (Safari Tours) n.k, hii ni kwa wale wanaofanya kazi sekta ya Utalii ama wengine wowote.
  • Uwekezaji kupitia Usafirishaji; Iwe Uber/Bolt ama biashara ya kusafirisha mizigo ama parcels
  • Uwekezaji kupitia Vituo vya Elimu, iwe ni daycare centers, Tuitions centers hii ni maalumu kwa Walimu n.k
  • Kuwekeza kupitia huduma za afya iwe ni Maabara binafsi, maduka ya madawa, ama utoaji wa huduma tembezi ya kuwafikia wagonjwa majumbani (Mobile Health clinics)
  • Uwekezaji kupitia Ujenzi; Unaweza kufanya uwekezaji kwa kujisajiri kama Local Fundi na kisha kuanza kuchukua tenda za Ujenzi wa Miradi ya Serikali ama Binafsi, wakati mwingine unaweza kufanya biashara ya kuuza vifaa vya Ujenzi (Hardwares), kiwanda cha kuzalisha tofali n.k
  • Uwekezaji kupitia huduma za Kisheria (Kuanzisha Ofisi za Uwakili) n.k
  • Kufungua kampuni za Ulinzi, kwa wale wenzetu walioajiriwa kwenye idara za Ulinzi na Usalama
Kumbukeni, Uzee bila hela ni changamoto, utaanza kula kwa shida ya kukosa chakula, kukosa matibabu,kukosa sehemu nzuri ya kulala, kukosa hata fedha ya kwenda mapumziko ya Mwisho wa Mwaka. Anza kuwekeza sasa ili uepuke kutokupokelewa kwa simu zako, ukiwapigia Watoto wako, Ndugu,Jamaa na marafiki, bila kusahau kuepuka kuitwa Mchawi (Hakuna mtu mwenye kipato cha wastani/juu akaitwa Mchawi).

Kila la Kheri Wazee na Wastaafu wenzangu watarajiwa
Asante Sana ndugu
IMG-20240721-WA0002.jpg
 
Mkuu Mimi naona Kwa watu wote hata wale wasio ajiriwa!

Unatakiwa itegeshe vitega uchumi vya kudumu biashara ya kudumu ama kilimo endelevu pamoja na ufugaji. Hii itakupa uhakika wa maisha hata kama utapata faida kidogo ni vyako. Ahsantee sana Kwa Uzi huu.

Mzee wangu tulimshauri awekeze kwenye nyuki,ufugaji samaki pamoja na ng'ombe wa maziwa kamwe hakutuelewa kabisa Tena tulionekana sisi tunazitaka Hela zake!

Sasahivi anakumbuka misitu upo binde lipo Hela hamna na sisi tuna mambo yetu ya kuwekeza vilevile anapata laki ama 50k nikiwa nayo au zaidi hata400k mara Moja moja
 
Najua kusema ni rahisi sana ila elewa kuwa pension imetengenezwa na serikali na sio matakwa ya mtu na mtu
Kustaafu sawa ila je utaweza kuranda randa kwa wajukuu kila leo?
Hata kama una hela lakini uzee na kukaa kula bata ni shida
Utapata maradhi ya kila aina bila kuwa na harakati yaani activities
Kama niwe na miaka 67 halafu nikae tu kwa kweli siwezi

Ntaacha kufanya kazi mpaka mwili ugome kwenda na likizo itakuwa sina ulazima maana nimeisha tembea sana dunia hii
Pension za huku nitalipwa kama 3m ya bongo kila mwezi
Lakini siwezi kulala tu kila siku lazima nifanye kitu hata kusimamia mijengo itakuwa idea nzuri ila kulala tu na kukaa chini ya mti hapana
Mawazo yatakusumbua sana ukiwa umekaa tu unahitaji kazi isiyo ngumu ila sio biashara za duka au kukimbizana na mifugo

Shida ya kutoelewa unachosoma. kustaafu ni kupumzika hutafanya kazi kama ulivyokuwa mwanzoni, hutaamka na kukimbizana kama mwanzo, hutashinda kazini kama mwanzo.
Utapita kukusanya maokoto ina maana utakwenda kwenye shughuli zako ila si kwa ubize kama zamani, ni kama kusimamia na kuangalia tu kazi zinavvyoenda.
utakaa chini ya mwembe ina maana kuna wakati utapumzika hii haina maana wewe utakaa tuuuu maisha yako yote, nooo kuna vipindi vya kuburudika na kupiga umbea kwa kuwa shughuli zako ulizozianzisha zinaendelea vizuri na kukulipa huna stressss . ukistaafu sio muda wa kusimamia mijengo.... ni muda wa kupokea kinachozalishwa kwenye mijengo uliyonayo. Kutembelea wajukuu maana yake utakuwa na mitoko yako midogo midogo nje ya mkoa wako kwa raha ukasalimie kwenu au kokote utakako. THINK BIG EEEEEE
 
Salaam,

Kila mtumishi aliyeajiriwa, akumbuke itafikia wakati atalazimika kustaafu kazi. Kustaafu huku inaweza kuwa ni kwa hiari ama kulazimishwa kutokana na Umri (Miaka 60 ama 65 kwa Wakufunzi wa Vyuo Vikuu) ama sababu za Ulemavu ama Maradhi yasiyotibika.

Kwa kujua huku kwamba kuna siku tutalazimika kustaafu na kupisha damu changa kwenye utumishi wetu, ndiyo maana inashauriwa kuanza kujiwekeza tangu tarehe ya kwanza unapokea mshahara wako wa kwanza.

Kama mnavyofahamu, Mtumishi akisha staafu, hunufaika na kulipwa kiasi cha 1/3 ya Mshahara wake aliokuwa anapokea wakati anastaafu. Mathalani ikitokea unastaafu ukiwa unapokea mshahara wa shilingi za Kitanzania 1,500,000 kwa Mwezi (Gross Salary) basi ukisha staafu utaanza kulipwa kiasi cha shilingi 500,000 tu hadi siku unaaga Dunia (Kufariki).

Pamoja na hilo, mtumishi huyu atalipwa kiiunua mgongo chake ambacho kwa kikokotoo kipya atalipwa 33% ya fedha zake za Mkupuo.

Kwa taarifa ambazo sio rasmi, watumishi wengi sasa wanapokea fedha zao za Mkupuo unao-range kati ya shilingi 25,000,000 hadi 200,000,000 kulingana na kiwango chako cha mshahara.

Kwa kutambua hili, napenda kuwasisitiza wastaafu watarajiwa, kuhakikisha mnajenga nyumba zenu za kuishi ukiwa bado upo kazini. Ili utakapolipwa fedha zako za kiinua mgongo, basi uzitumie kwenye shughuli nyingine lakini isiwe kujenga.

Kupitia andiko hili, tunaweza kupeana dondoo za aina ya miradi inayoweza kufanywa na Wastaafu ili kujikidhi na maisha yao ya baada ya kustaafu.

  • Uwekezaji kupitia Kilimo Biashara; Ufugaji wa Nyuki,mazao ya chai, matunda, Ufugaji na Kuku wa Kisasa kwaajili ya Mayai na Nyama.
  • Uwekezaji kupitia biashara ya Majengo(Real Estates); Biashara ya GuestHouses, Biashara ya kununua na kuuza viwanja, Nyumba za Kupangisha n.k
  • Biashara mtandao ya kununua na kuuza iwe ni vifaa vya Umeme ama vya nyumbani
  • Biashara kupitia Teknolojia; Kuna baadhi ni wataalamu wa Tehama kama vile Website development, Apps n.k. bila kusahau biashara ya fedha mtandao mfano Mpesa,Airtel Money,CRDB Wakala n.k.
  • Unaweza kuwekeza kwenye Utalii, kwa kufungua kampuni ya Utalii (Safari Tours) n.k, hii ni kwa wale wanaofanya kazi sekta ya Utalii ama wengine wowote.
  • Uwekezaji kupitia Usafirishaji; Iwe Uber/Bolt ama biashara ya kusafirisha mizigo ama parcels
  • Uwekezaji kupitia Vituo vya Elimu, iwe ni daycare centers, Tuitions centers hii ni maalumu kwa Walimu n.k
  • Kuwekeza kupitia huduma za afya iwe ni Maabara binafsi, maduka ya madawa, ama utoaji wa huduma tembezi ya kuwafikia wagonjwa majumbani (Mobile Health clinics)
  • Uwekezaji kupitia Ujenzi; Unaweza kufanya uwekezaji kwa kujisajiri kama Local Fundi na kisha kuanza kuchukua tenda za Ujenzi wa Miradi ya Serikali ama Binafsi, wakati mwingine unaweza kufanya biashara ya kuuza vifaa vya Ujenzi (Hardwares), kiwanda cha kuzalisha tofali n.k
  • Uwekezaji kupitia huduma za Kisheria (Kuanzisha Ofisi za Uwakili) n.k
  • Kufungua kampuni za Ulinzi, kwa wale wenzetu walioajiriwa kwenye idara za Ulinzi na Usalama
Kumbukeni, Uzee bila hela ni changamoto, utaanza kula kwa shida ya kukosa chakula, kukosa matibabu,kukosa sehemu nzuri ya kulala, kukosa hata fedha ya kwenda mapumziko ya Mwisho wa Mwaka. Anza kuwekeza sasa ili uepuke kutokupokelewa kwa simu zako, ukiwapigia Watoto wako, Ndugu,Jamaa na marafiki, bila kusahau kuepuka kuitwa Mchawi (Hakuna mtu mwenye kipato cha wastani/juu akaitwa Mchawi).

Kila la Kheri Wazee na Wastaafu wenzangu watarajiwa
Uwekezaji kwenye masoko ya Fedha pia.wastaafu wengi wako huko
 
Ni kweli huko Vijijini Kuna fursa nyingi Kwa Walimu ama Watu wa afya wanaofanya kazi huko

Changamoto yao ni kushindwa kuamka(wengi vichwa vyao vimelala)

Lakini wangekuwa serious unanunua ekari zako 100 ama 50 unalima zako fresh tu

Wakati huo huo unafuga zako Kuku/Nguruwe/Ng'ombe wa Maziwa/Mbuzi ili kuongeza kipato

Shida yetu Watumishi wengi vichwa vimelala
Wiki iliyopita nilikuwa morogoro mvomero asee nisiseme Sana ila Tz Kwa upande wa ardhi imebarikiwa sana nitaenda huko kufuga na kulima
 
Private Sina uhakika kama nao wanalipwa Kila Mwezi

Maana private workers wengi, hata Mikataba ya kazi unakuta hawana.

Wengine hata yale makato kwaajili ya mifuko ya hifadhi ya kijamii hawachangii

Kwahiyo wakistaafu ama kuachishwa kazi hupata changamoto kubwa sana za kuweza kusimama tena, maana hata backup ya akiba hawana 🙌
Kwa Sasa hata kama mkataba wa miezi 3 nssf inakatwa na lazima uwe Tin no.
 
Changamoto iliyopo ni watumishi kukosa msimamo na Umoja, wangekuwa wengine mbona saivi wangekuwa wamepelekewa asilimia ya Mkupuo hadi 100 ama 75/25
Hii nchi umoja haupo, juzi nimetoka sehemu "shamba" ukifika kituo cha mafuta "sheli" hawakupi mafuta wanaswma ulete chombo kinachotumia mafuta, sasa mtu unawaza uyoe pampu km 50 utembee nayo ili ujaze wese, utarudi mara ngapi na pampu, au trekta au mashine zingine za shamba ila watu wapo kimya washakubaliana na hali wanatumiq boda boda unaijaza mnaenda pembeni ndo mnatia kwenye dumu
 
Shida ya kutoelewa unachosoma. kustaafu ni kupumzika hutafanya kazi kama ulivyokuwa mwanzoni, hutaamka na kukimbizana kama mwanzo, hutashinda kazini kama mwanzo.
Utapita kukusanya maokoto ina maana utakwenda kwenye shughuli zako ila si kwa ubize kama zamani, ni kama kusimamia na kuangalia tu kazi zinavvyoenda.
utakaa chini ya mwembe ina maana kuna wakati utapumzika hii haina maana wewe utakaa tuuuu maisha yako yote, nooo kuna vipindi vya kuburudika na kupiga umbea kwa kuwa shughuli zako ulizozianzisha zinaendelea vizuri na kukulipa huna stressss . ukistaafu sio muda wa kusimamia mijengo.... ni muda wa kupokea kinachozalishwa kwenye mijengo uliyonayo. Kutembelea wajukuu maana yake utakuwa na mitoko yako midogo midogo nje ya mkoa wako kwa raha ukasalimie kwenu au kokote utakako. THINK BIG EEEEEE
Nimekuelewa vizuri sana tangu mwanzo
Kusimamia shughuli sio kazi ya kunitoa jasho bali ni akili tu isiwe mahali pamoja
Wengi wa wastaafu hapa nilipo wanafanya kazi bado ila ni siku chache kwa wiki
Unakatwa NI number tu ila kodi hulipi na ni wengi sana
Nitakuwa na uwezo wa kula bila kumtegemea mtu ila ntafanya shughuli ndogo ndogo sana za kuni keep occupied

Unapokaribia kustaafu unapata ushauri kutoka kila sehemu serikalini hata bank pia wanatoa nao
Tuombeani kheri maana hata wewe bila umauti nakuombea ustaafu unavyotaka wewe na unavyoona ipi ni sawa kwako
 
Hii nchi umoja haupo, juzi nimetoka sehemu "shamba" ukifika kituo cha mafuta "sheli" hawakupi mafuta wanaswma ulete chombo kinachotumia mafuta, sasa mtu unawaza uyoe pampu km 50 utembee nayo ili ujaze wese, utarudi mara ngapi na pampu, au trekta au mashine zingine za shamba ila watu wapo kimya washakubaliana na hali wanatumiq boda boda unaijaza mnaenda pembeni ndo mnatia kwenye dumu
Hiyo Kali Mkuu, kwahiyo pamoja na hela yako lakini hawakupi huduma??

Hii Nchi kama ulivyosema, hatuna Umoja kabisa kwenye mambo ya msingi zaidi ya kufarijiana kwenye misiba tu
 
huu ni ushauri BORA na mzuri kwa waajiriwa wa serikalini.
mie mgalatia acha niendelee kupambana na maisha ya mtaa kwa mtaa.
Lakini Mkuu sio waajiriwa pekee, hata wewe uliyejiajiri kupitia shughuli za Kilimo ama biashara bado unaweza kujifunza dhima ya andiko hili

Kwamba tujipange kwaajili ya Uzee wetu

Tujitahidi kuwekeza ili tusiteseke kwenye Uzee wetu
 
Nimekuelewa vizuri sana tangu mwanzo
Kusimamia shughuli sio kazi ya kunitoa jasho bali ni akili tu isiwe mahali pamoja
Wengi wa wastaafu hapa nilipo wanafanya kazi bado ila ni siku chache kwa wiki
Unakatwa NI number tu ila kodi hulipi na ni wengi sana
Nitakuwa na uwezo wa kula bila kumtegemea mtu ila ntafanya shughuli ndogo ndogo sana za kuni keep occupied

Unapokaribia kustaafu unapata ushauri kutoka kila sehemu serikalini hata bank pia wanatoa nao
Tuombeani kheri maana hata wewe bila umauti nakuombea ustaafu unavyotaka wewe na unavyoona ipi ni sawa kwako
Ushauri murua kabisa Mkuu 🙏
 
Kwa Sasa hata kama mkataba wa miezi 3 nssf inakatwa na lazima uwe Tin no.
Hiyo safi, nafikiri watatofautiana kwenye Posho ya Kila Mwezi

Huyu wa Serikalini atakuwa na uhakika wa kuchukua Kila Mwezi

Wakati huyo wa private sector aliyefanya kazi Kwa muda mchache hatokuwa akipata Posho ya Kila mwezi
 
Back
Top Bottom