Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Una umri gani wewe?Naomba niwe wazi tu kwako Mshana nakuamini Sana na nakupenda Sana uko makini Sana wewe,the boss na kikulachochako wote nyie ndo nawafuatilia Sana
Ila kwenye Hili la uchawi au ushirikina asee sitakaa niamini Kama Kuna kiumbe ambacho kinaweza kupotea au kupaa na ungo hizo zote kwangu Ni Kama uwongo tu labda useme mtu kulogwa maana unaweza ukawekewa hata kitu flani kwenye chakula ukipata matatizo ya kiafya tutasema umelogwa ila Hilo sijui la kubadilisha sura hawana uwezo huo.
Nina mengi ya kusema itoshe tu kwa kusema yanayosemwa mengi Ni tofauti na ambayo unaweza ukayaona
1. Kumumunya kibonge kimoja na kukinenea ulinzi, vikwazo mafanikio, kinga nk
2.Kushika chumvi mkononi kuinenea na kuirusha mbele
3. Kuchukua kibonge cha chumvi kiweke kwenye soksi au kiatu mguu wa kulia na hakikisha ukitoka ndio utangulie
Pelekeni maombi , nafasi bado ipo .Hivi mikoba ilipata mrithi!?
Natambua umepotoka pakubwa lakini si kosa lako unahitaji kuelimishwa kwa upole na kwa hekima.. Kumbuka chini ya jua hakuna kidumucho milele..! Kila chenye mwanzo huwa na mwishoHakuna mchawi aliyewahi kustaafu, once a witch always a witch. Yale makufuru mnayofanya kujiunga na uchawi hayasameheki mbinguni wala duniani, ni moto wa milele tu
Tunapoumwa hatukai tu nyumbani na kufanya maombi bali huenda hospital na kumuomba Mungu ampe kibali daktari cha kulitambua tatizo na kutupa tiba sahihi.. Halafu alete uponyaji kupitia dawaSasa hapo mshana si ndo kuamini chumvi na kutomuamini mungu, Hiyo ni kimshirikisha mungu, Yani wewe una amini kazi ya mungu ifanywe na chumvi kweli, camon get serious, Uliposema tutangulize maombi nilikuelewa sana
Kwa sababu sipendi wanga, wachawi na warozi. Hawana cha maana chochote wanachokifanya zaidi ya kuwaweka juu roho binadamu wenzao hivyo waishi kwa hofu kubwa asilimia kubwa ya maisha yao na mara nyingi huwaharibia kabisa maisha yao na kuwa unproductive citizens. Choma moto hizo tunguli zako badala ya kumrithisha mtu na hapo ndiyo uanze zoezi la kumrudia Mungu wako.
Sikushauri kabisa kwenda kwenda kwenye ushirikinaDah yan mi nateseka sana mwanangu anapungua damu kila mara na sicklecelly Hana nahis ni urozi tu japo bado sijajaribu kwa waganga naona Kama mambo yatakua mengi sana MUNGU amsaidie bint angu kwa kweli MUNGU ni mwema sana
Dah yan mi nateseka sana mwanangu anapungua damu kila mara na sicklecelly Hana nahis ni urozi tu japo bado sijajaribu kwa waganga naona Kama mambo yatakua mengi sana MUNGU amsaidie bint angu kwa kweli MUNGU ni mwema sana
Maombi na hospitaliPole sana uliponaje? Mshike sana Mungu na zingatia sana maombi
Duh[emoji848][emoji848][emoji3064][emoji3064][emoji3064]Kwenye karai la maji wengine wabishi wanajionyesha kinyume (matako) haonyeshi uso mpaka ageuzwe na mganga wa ngazi ya juu. Na kama uko sawasawa kukugeza hawawezi wanaishia kukuita mchawi.
Nina mtu asiejulikana ananikalia kooni kuhusu kipato,nikiomba pesa Benki inachelewa kutoka naishia kupishana na fulsa,nikifanaya kazi na vibarua mashamba hela inakata ghafla naanza migogoro na vijana wa kazi,kazini jina limechafuka viongozi lazima walikate kwenye mambo ya pesa ,masangoma wanagonga mkwanja na kutotatua tatizo.Ni shida ya miaka kibao,naenda taratibu mno kimaendeleo mpaka nijishtukia.Hatua za kuwa mshirikina (combine ya uchawi, uganga, ulozi, kuwanga, kuroga na kuwanga)...! Haya yote ndio yanatengeneza neno USHIRIKINA!
Hatua ya chini kabisa ni kuweza kupaa na ungo na kuingia kwenye majumba ya watu na kuwachezea... Katika hatua hii pia kuna masomo mengine kama chuma ulete, kuchukua kitu cha mtu mbele yake bila mwenyewe kukuona, kupiga zongo nk
Hatua ya pili ni uwezo wa kujigeuza maumbile, kuvaa sura ya mtu mwingine au kujigeuza kuwa mnyama... Na hii mara nyingi hufanyika bila hata kiza kuingia
Hatua ya tatu ni uwezo wa kufika mbali kwa kitendo cha kufumba na kufumbua macho, kumvuta mtu umtakaye aje mbele yako na uwezo wa kuua ukiwa mbali
Kwahiyo kati ya wanga wanaowasumbueni usiku wengine ni wpagazi wa kutumwa vitu mbalimbali kama kucha, nywele, nguo, kuchanja chale, kwenda kuchukua wafu mahospitalini ama kukusanya damu na nyama maeneo ya ajali ambapo mara nyingi ndio wao wanakuwa wamezisababisha ama aliyewatuma
Wale washirikina makonki wa madaraja ya juu huwa hawajihangaishi kutoka kwenda kutafuta chochote hata kana wana huo uwezo bali huwatumia vijana wanaowafundisha kazi ama wasaidizi wao kwa hiari!
Je na hawa watumwa ni akina nani? Watumwa wa kishirikina namaanisha! Hawa ni watu walioko huko si kwa ridhaa yao bali kwa matendo ya binadamu wengine na wengi wao huwa kiasili ni misukule.. Hawa hutokana na Kukosana na 'wazee wa busara kisha wakakukomoa.
Ugomvi wa familia au ndugu
Kugombea mirathi ama mali
Vyeo na nafasi kazini
Umaarufu na utajiri pia
Kuna namna tatu ya kupata watumwa
1. Kumtia mtu wendawazimu/ kumfanya chizi
2. Kumpoteza asionekane tena
3. Kumchukua msukule/ kumuua kishikirina hasa hasa kupitia ajali
Ushirikina ni sayansi ya ajabu kabisa na iko deep sana...!
Unaenda kumfanyizia mtu kwa mganga kwa nia yoyote ile.. Ukifika unapewa karai lenye maji kisha anaitishwa pale nawe unamuona live kabisa sura yake.. Kisha unapewa kisu umchome! Ukishafanya hivyo tu maji yote kwenye karai yanageuka damu na huko aliko mhusika anapata ajali yoyote na kufa!
Kwanini kuchoma uso? Sio popote bali unatakiwa kuchoma sehemu ya koromeo...
Kwanini huchomi sehemu nyingine za mwili? Inawezekana kabisa ila kama hutaki afe bali apate tu ajali mbaya .. Hapo ataumia zaidi sehemu husika
Magonjwa je?
Washirikina mara nyingi hawatumii magonjwa kwakuwa unaweza kupata tiba na kupona...lakini akikukamia ili akutese muda mrefu anakupiga na maradhi ambayo utamaliza hospital zote bila tatizo kuonekana
Dawa na kinga kwa washirikina ni hizi mbili zisizo na madhara ya baadae
1. Maombi na dua.. Usiache kufanya maombi wala dua kwa kila ufanyacho iwe chakula, iwe kinywaji, iwe ukitoka ndani, iwe ukipanda chombo cha usafiri, iwe ukiingia ofisini, iwe ukiingia nyumbani nknk
2. Tumia chumvi ya mabonge kadiri uwezavyo..itangulize popote unapotaka kwenda au chochote unachotaka kufanya na ukiweza inenee au nuia..!!!
Ulimwengu usioonekana una mengi mabaya na washirikina ni sehemu yao!
Laleni salama! Na Mungu awalinde na kuwapigania...!!!
Witchdoctor mstaafu.