Baba adaiwa kumuuza mtoto, asafirishwa kwenda Canada, mama abaki analia akizunguka kuomba msaada

Baba adaiwa kumuuza mtoto, asafirishwa kwenda Canada, mama abaki analia akizunguka kuomba msaada

Umasikini haumalizwi kihivyo sema we ndo unamawazo ya kimaskini afu muoga wa maisha. Uza wanao kama kweli unao
Wangapi wamelala chumba kimoja na mbuzi, kuku na saivi wametusua maisha, kusikia canada ndo unaona kutoboa wangapi wameenda huko wamerudi mateja wengine mashoga, baki na ujinga wako usinishirikishe.
Mwanaume kamili anayejiamini mwenye mbegu zake na mwenye imani hawezi fanya huo uduanzi, labda bwabwa tu anaweza kuwa na mawazo mgando hivyo


Uko sahihi sana.
 
Watu mnamlaumu mama.Kama hao watu wahind na baba wangekuwa na nia njema kwa pamoja wangechukua muda kukaa na mama kumuelemisha faida zote za hiyo issue.Lakn pia hata huko kwenye taasisi za serikal mama angeitwa kuelimishwa.Lakn hiki walichofanya sio kitu kizur.
 
Inategemea mkuu, wataka kuniambia hilo jambo alilolitaka kulitelekeza ni tangia mtoto akiwa na mwaka mmoja akamkuza mpaka umri wa miaka 7 ndio atimize mission yake baada ya muda wote huo? Actually mhindi anamtaka mtoto kwasababu hana mtoto, hajawahi kuzaa maisha yake yote na wala hana mwanaume

IMG_6484.jpg


Inawezekana kabisa huyo mama muhindi ana dhamira njema na ya dhati kabisa kuhusu huyo mtoto.

Lakini Mama wa mtoto asikilizwe wasiwasi wake. Aulizwe mashaka yake ni yapi na vikwazo vinatoka wapi.

Taasisi za Serikali zinazohusika na mambo Kama haya, huyo muhindi na baba wa mtoto wazungumze nae kwa kina na ikiwezekana mtoto pia ashiriki hayo maazungumzo na maamuzi. (Nimeona picha ni mkubwa kiasi)

Lakini Kama dhamira ni ovu na mbaya kabisa, nani yupo tayari kubeba lawama za baadae?

Dunia kwa sasa imesimama pabaya sana kuhusiana na hizi kesi za usafirishaji, utumikishwaji na udhalilishwaji kingono na uasili wa watoto.

Kuna kimbunga kibaya sana huko huku wadhalilishaji watoto nao wakifukua “matundu “ ya kisheria yatakayowawezesha “kupewa” haki zao katika jamii Kama kundi lenye mahitaji maalum Kama walivyofanya wale wa Bendera ya marangi mengi mengi Kama upinde wa mvua.

Mwisho kabisa huyo mama mwenye mtoto, huyo ni mtoto wake wa kumzaa, damu na nyama yake. Anayo haki ya asilimia mia moja kukataa hayo makubaliano kati ya baba na huyo muhindi. Sheria na Katiba ya nchi ndio mlinzi wake.

KTY; wasiwasi ndio akili.
 
Kitendo cha muhindi kumchukua mtoto bila ruhusa ya mama yake. Yani hata hajataka mtoto kumuaga mama yake. Hiyo tu inaonyesha muhindi hakuwa na nia njema kwa huyo mtoto na wala hampendi na kafanya kitendo kikatili sana. Mungu amlinde mtoto maana yupo katika hatari kubwa sana maskini
 
Katika hali ambayo inaweza kuacha maswali mengi na mtazamo tofauti, mtoto Yusuph Issa Juma mwenye umri wa miaka 8, Mwanafunzi wa darasa la tatu katika Shule ya Msingi Istiqaama iliyopo Ilemela Jijini Mwanza amesafirishwa kwenda Nchini Canada bila ridhaa ya mama yake.

Mtoto huyo ameondoka katika mazingira tata akiongozana na Watanzania wawili wenye asili ya India, baada ya baba mzazi kutoa ruhusa huku mama mzazi akiwa hana taarifa.
View attachment 2701382

CHANZO CHA MKASA
Mama mzazi wa mtoto anayefahamika kwa jina la Khadija akiwa mfanyabishara maeneo ya Makoroboi, Mwanza, alianza kuzoeana na dada mwenye asili ya India anayefahamika kwa jina la Narina Haji Dawood.

Nariana alimpenda Yusuph kuanzia akiwa na umri wa mwaka mmoja, alipofikisha mwaka mmoja na nusu akawa anamuomba Khadija amchukue mtoto (Yusuph) akae kwake wakati yeye (mama mtu) akiendelea na biashara zake, Khadija hakupinga hilo.

Baadaye Narina akahamia Kiseke kutoka Makoroboi, akiwa huko akaomba akae na Yusuph na amsomeshe kwa makubaliano kuwa mama mtoto anaweza kwenda kumuona muda wowote na mtoto atakuwa anarudi kwa mama mzazi pindi anapopata nafasi.

MKASA UKAANZA
Baada ya kuishi na Yusuph kwa miaka kadhaa, Narina akaomba kwa mama mzazi ruhusa kuwa anataka kwenda likizo Canada aongozane na mtoto, Khadija akakataa ombi hilo.

Miezi kadhaa baadaye Narina akamjulisha Khadija kuwa ana mpango wa kuhamia Canada, akaomba aondoke na Yusuph, mama mzazi akashikilia msimamo wake wa kukataa ombi kwa mara nyingine.
View attachment 2701383

BABA MZAZI AKAANZA KUSHAWISHIWA
Baada ya kuona mama mzazi ameshikilia msimamo, ikabidi Narina aanze kumshawishi baba mzazi wa mtoto anayefahamika kwa jina la Issa Juma, wakaanza kumpoa zawadi mbalimbali ikiwemo fedha.

Baada ya muda wakamshawishi kuwa wana mpango wa kwenda na mtoto Canada, ikabidi baba mtu afungue kesi Mahakamani ya kutaka akae na mtoto.

Inadaiwa Mahakama ikaagiza Mtoto Akaishi na baba, ndipo baba mtu akatumia nafasi hiyo kuanza kufanya mipango kwa kushirikiano na familia ya kina Narina kwa ajili ya mtoto kusafiri.

JINA LA MTOTO LABADILISHWA
Ili kufanikisha mtoto kusafiri ikabidi majina ya mbele ya Yusuph yabadilishwe, kutoka Yusuph Issa Juma na kuwa Yusuph Haji Dawood zikatengenezwa nyaraka zinazoonesha Narina amemuasili (adapt) Yusuph na nyaraka nyingine kadhaa kisha Julai 20, 2023 wakasafiri kuelekeza Canada huku mama mtu akiwa ajui kinachoendelea.

BABA AELEZEA
Issa Juma alipoulizwa amesema “Kweli mtoto ameondoka kwenda Canada, familia iliyomchukua imesema itamsomesha, mimi sina kazi ya maana, nauza maziwa tu mtaani na sina uwezo wa kumsomesha, ni kweli pia uamuzi wa kuondoka kwa mtoto umefanywa kwa upande mmoja.

“Mzazi mwenzangu hakukubali uamuzi huo, tumeshazungumza na Ustawi wa Jamii na Uhamiaji kuhusu hili, msimamo wa mama mtoto ni kuwa anataka mtoto arudi.

“Familia iliyomchukua nimewasiliana nao, mtoto yuko salama na wameahidi kuwa watakuwa wanamrejesha kila baada ya miaka miwili kuja kusalimia.

“Ni kweli pia majina ya mbele yamebadilishwa ili kule anapokwenda ionekane kuna uhusiano kati yao.

“Huyo dada aliyemchukua mtoto hajaolewa wala hana mtoto wa kumzaa, anaishi yeye na kaka yake.”

BABA ASEMA YUPO TAYARI MTOTO ARUDISHWE
“Kwa hiki kinachoendelea, sikuzoea kuishi kwa wasiwasi, kama itawezekana basi wamrudishe tu mtoto, sina nia mbaya ndio maana nazungumza kwa uwazi.

“Maisha yangu ni magumu na sio kwamba nimemuuza mtoto kama inavyosemwa, zaidi nilipewa kompyuta tu, sio kweli kuwa nimepewa nyumba na gari, hiyo nyumba inayosemwa ameachiwa Mzee Felix ambaye ni mtu wa karibu na familia hiyo ya hao Wahindi.”

MAMA WA MTOTO AANGUA KILIO
Akizungumza huku analia, Khadija anasema “Ninachotaka mtoto wangu arudi, niliiachia hiyo familia imlee kwa kuwa waliomba na wakasema watamlipia ada lakini sikutaka waende naye nje ya nchi, nilimwambia msaada wowote anaotaka kwa mtoto autoe akiwa hapa Nchini.

“Nimeshaenda Ustawi wa Jamii, Polisi na Uhamiaji kote sijapata msaada, kwa sasa nipo ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza ili kutafuta msaada zaidi.”

MAELEZO YA AFISA ELIMU
Afisa Elimu Msingi wa Manispaa ya Ilemela, Marco Busungu anasema: Hayo masuala ya Wanandoa sisi tumesumbuka nayo sana, mimi siwezi kulisemea hilo kwa kuwa sijapata taarifa, pia hata kama lingefika tungeangalia ametoroshwa akishwa shuleni au nyumbani? Kwa kuwa baba mzazi yupo na anahusika basi aulizwe yeye kwa kuwa anajua kinachoendelea.

MAELEZO YA AFISA USTAWI WA JAMII
Afisa wa Ustawi wa Jamii, Edith Ngowi anasema: Hili suala halikuwa la kwetu, Khadija alikuja kupata ufafanuzi, huku ni Ustawi wa Jamii Nyamagana na suala lake lipo Ilemela, hivyo tulichofanya sisi ni kumshauri na kumsindikisha kwenda Polisi.

Tukiwa Polisi tukashauriwa kwenda Uhamiaji, tulipoenda Uhamiaji tulioneshwa taratibu zote zimefuatwa na baba mtu akakiri alidanganya ili upatikane uhalali wa mtoto kusafiri.

Lengo lake lilikuwa mtoto apate kuasiliwa na aende akasomeshwe, tumeshauri familia ikae pamoja na Wazazi wa pande zote kuangalia jinsi ya kulimaliza nak ama ni kumrejesha mtoto wafanye hivyo.

UHAMIAJI MWANZA WAULIZWA
Alipoulizwa Kamishna wa Uhamiaji Mkoa wa Mwanza, Peter Mbaku juu ya kudaiwa kuchezewa kwa nyaraka za mtoto na hadi kubadilishwa kwa jina kisha kuruhusiwa kwenda Canada, amesema: “Naomba muda nifuatilia hizo taarifa.”

SHULE YA ISTIQAAMA YAULIZWA
Alipotafutwa Kiongozi wa Shule ya Msingi Istiqaama, Rashid Seif Said kisha kuulizwa kuhusu taarifa za mwanafunzi huyo kwamba aliondokaje shuleni na kama alipewa ruhusa au kama wanajua kuhusu safari husika, aliomba jina na taarifa zingine za Mwanafunzi kabla ya kutoa majibu, alipotafutwa baadaye simu haikupokelewa.
Alafu utakuta huyo mama anasumbua watumishi makanisani kwa maombi kuwa MUNGU amfanyie miujiza mtoto wao apate elimu na maisha bora!
 
Wewe mleta mada inaonesha unawajuwa hawa watu.


Mwacheni huyo mtoto, kishapata maisha mema, mshaurini vizuri huyo mama. Awe na contacts zao tu, asiwe na wasiwasi, huyo ni mkubwa hatowasahau wazazi wake na alipotoka. Hiyo ni fursa ambayo wengi wanaitafuta.

“Kaishapata maisha mema “



Wallaih I never thought I would live to a day where I will read disgusting crap from you. Complete & all round brokenness. Utumwa na after effects zake vipo kwenye rojo za mifupa yako! It will be centuries before yote ikuishe through your generation, unless you work on it. Bado uko hai.

Wewe na wengine wengi sana humu wenye mitazamo ya utegemezi kwenye hii mada. Tena wengi ni wanaume?!? Yani uzalishe na uzae wewe utegemee kulelewa? How do you preserve your DNA and millions of years of culture & your peoples roots? Your histories?

Nawe mwanamke tena mama na bibi! Yaani kwamba bila huyo mtoto kwenda Canada maisha yake ndio yamehitimishwa?!?! Doh! Una mitazamo ya kitumwa sana. Sana!
 
Mama mzazi alishaonyesha dalili zakuzingua.

Upendo una nguvu sana, ndio maana Mhindi akaamua kuanza kudeal na BABA mtoto.

Kuhusu majina kubadilisha, hiyo ndio ilikuwa njia rahisi sana kwa huyo dogo kusepa.

Majina sio issue sana lakini, kwa wewe unaitwa macho?

“Upendo Una nguvu sana”

Hivi mnajisikia vizuri ndani ya vichwa vyenu as you type ama kuna mawimbi yanawazonga fikra zenu?

Upendo kati ya mama mtu mzima asiye na uwezo wa kuzaa watoto wake mwenyewe na mtoto mdogo chini ya miaka 10 asiye na uwezo wa kutambua jema na ovu kinagaubaga?

Upendo ndio umemtuma mpaka kughushi nyaraka za serikali ili kufanikisha jambo lake?

Ndugu yangu, nenda kafanye hivi huko kwao India ama huko Canada halafu lisanuke Kama hivi, child trafficking haikuachi. Mpaka waone huo “Upendo Una nguvu” Una mvi na cheo cha nyampara Gereza la Kisongo ya Canada!

Pesa inamfanya mwanaadam kuwa kiumbe wa ajabu sana. Hawa viumbe wa hii mada ni balaa!
 
Uchungu wa mwana aujuae mzazi...

huyo mama wa kihindi angetakiwa kupata consent ya wazazi wote wawili...

Kama ni maisha bora kwa mtoto angeweza kumtafutia mtoto international school,na kutuma allowance kwa wazazi wake kila mwezi....bado mtoto angekuwa comfortable tu...

Kumchukua mtoto kwa ridhaa ya mzazi mmoja tu inaonyesha alivyo na kiburi/manipulative...

Desperation yake ya kukosa mtoto inamfanya amekuwa selfish,kujali interests zake tu...

Kama ni watoto mbona wako mtaani wengi tu hawana wazazi..

Kumchukua mtoto in this aggressive way kutoka kwa mama yake...NO!,
 
Watanzania uchawi ni asili yetu, yani umaskini walionao Wazazi hawaridhiki mpaka mtoto naye arithi dhiki?

Kwa ninavyojuwa Mimi hapo kuna proper communication na huyo muhusika kwa Mimi binafsi sioni tatizo kabisa, kwa asiyeelewa vizuri mambo haya hawezi kuelewa na atamlaumu baba.

Lakini kwa maoni yangu baba amefanya uwamuzi wa busara kabisa kumpa kibali huyo muhindi na ameahidi mtoto atakuwa anarudi kwa Wazazi wake, na isitoshe huyo mtoto anakwenda kuwa RAIA wa Canada na amesoma Canada atakuja kuokowa ndugu zake mbele ya safari.
Unakuta hata uwezo wa kumpa mtoto milo miwili kwa siku hana.

Akirudishiwa mtoto anaanza kushindwa ustawi wa jamii kushinikiza baba wa mtoto ahudumie.
 
Katika hali ambayo inaweza kuacha maswali mengi na mtazamo tofauti, mtoto Yusuph Issa Juma mwenye umri wa miaka 8, Mwanafunzi wa darasa la tatu katika Shule ya Msingi Istiqaama iliyopo Ilemela Jijini Mwanza amesafirishwa kwenda Nchini Canada bila ridhaa ya mama yake.

Mtoto huyo ameondoka katika mazingira tata akiongozana na Watanzania wawili wenye asili ya India, baada ya baba mzazi kutoa ruhusa huku mama mzazi akiwa hana taarifa.
View attachment 2701382

CHANZO CHA MKASA
Mama mzazi wa mtoto anayefahamika kwa jina la Khadija akiwa mfanyabishara maeneo ya Makoroboi, Mwanza, alianza kuzoeana na dada mwenye asili ya India anayefahamika kwa jina la Narina Haji Dawood.

Nariana alimpenda Yusuph kuanzia akiwa na umri wa mwaka mmoja, alipofikisha mwaka mmoja na nusu akawa anamuomba Khadija amchukue mtoto (Yusuph) akae kwake wakati yeye (mama mtu) akiendelea na biashara zake, Khadija hakupinga hilo.

Baadaye Narina akahamia Kiseke kutoka Makoroboi, akiwa huko akaomba akae na Yusuph na amsomeshe kwa makubaliano kuwa mama mtoto anaweza kwenda kumuona muda wowote na mtoto atakuwa anarudi kwa mama mzazi pindi anapopata nafasi.

MKASA UKAANZA
Baada ya kuishi na Yusuph kwa miaka kadhaa, Narina akaomba kwa mama mzazi ruhusa kuwa anataka kwenda likizo Canada aongozane na mtoto, Khadija akakataa ombi hilo.

Miezi kadhaa baadaye Narina akamjulisha Khadija kuwa ana mpango wa kuhamia Canada, akaomba aondoke na Yusuph, mama mzazi akashikilia msimamo wake wa kukataa ombi kwa mara nyingine.
View attachment 2701383

BABA MZAZI AKAANZA KUSHAWISHIWA
Baada ya kuona mama mzazi ameshikilia msimamo, ikabidi Narina aanze kumshawishi baba mzazi wa mtoto anayefahamika kwa jina la Issa Juma, wakaanza kumpoa zawadi mbalimbali ikiwemo fedha.

Baada ya muda wakamshawishi kuwa wana mpango wa kwenda na mtoto Canada, ikabidi baba mtu afungue kesi Mahakamani ya kutaka akae na mtoto.

Inadaiwa Mahakama ikaagiza Mtoto Akaishi na baba, ndipo baba mtu akatumia nafasi hiyo kuanza kufanya mipango kwa kushirikiano na familia ya kina Narina kwa ajili ya mtoto kusafiri.

JINA LA MTOTO LABADILISHWA
Ili kufanikisha mtoto kusafiri ikabidi majina ya mbele ya Yusuph yabadilishwe, kutoka Yusuph Issa Juma na kuwa Yusuph Haji Dawood zikatengenezwa nyaraka zinazoonesha Narina amemuasili (adapt) Yusuph na nyaraka nyingine kadhaa kisha Julai 20, 2023 wakasafiri kuelekeza Canada huku mama mtu akiwa ajui kinachoendelea.

BABA AELEZEA
Issa Juma alipoulizwa amesema “Kweli mtoto ameondoka kwenda Canada, familia iliyomchukua imesema itamsomesha, mimi sina kazi ya maana, nauza maziwa tu mtaani na sina uwezo wa kumsomesha, ni kweli pia uamuzi wa kuondoka kwa mtoto umefanywa kwa upande mmoja.

“Mzazi mwenzangu hakukubali uamuzi huo, tumeshazungumza na Ustawi wa Jamii na Uhamiaji kuhusu hili, msimamo wa mama mtoto ni kuwa anataka mtoto arudi.

“Familia iliyomchukua nimewasiliana nao, mtoto yuko salama na wameahidi kuwa watakuwa wanamrejesha kila baada ya miaka miwili kuja kusalimia.

“Ni kweli pia majina ya mbele yamebadilishwa ili kule anapokwenda ionekane kuna uhusiano kati yao.

“Huyo dada aliyemchukua mtoto hajaolewa wala hana mtoto wa kumzaa, anaishi yeye na kaka yake.”

BABA ASEMA YUPO TAYARI MTOTO ARUDISHWE
“Kwa hiki kinachoendelea, sikuzoea kuishi kwa wasiwasi, kama itawezekana basi wamrudishe tu mtoto, sina nia mbaya ndio maana nazungumza kwa uwazi.

“Maisha yangu ni magumu na sio kwamba nimemuuza mtoto kama inavyosemwa, zaidi nilipewa kompyuta tu, sio kweli kuwa nimepewa nyumba na gari, hiyo nyumba inayosemwa ameachiwa Mzee Felix ambaye ni mtu wa karibu na familia hiyo ya hao Wahindi.”

MAMA WA MTOTO AANGUA KILIO
Akizungumza huku analia, Khadija anasema “Ninachotaka mtoto wangu arudi, niliiachia hiyo familia imlee kwa kuwa waliomba na wakasema watamlipia ada lakini sikutaka waende naye nje ya nchi, nilimwambia msaada wowote anaotaka kwa mtoto autoe akiwa hapa Nchini.

“Nimeshaenda Ustawi wa Jamii, Polisi na Uhamiaji kote sijapata msaada, kwa sasa nipo ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza ili kutafuta msaada zaidi.”

MAELEZO YA AFISA ELIMU
Afisa Elimu Msingi wa Manispaa ya Ilemela, Marco Busungu anasema: Hayo masuala ya Wanandoa sisi tumesumbuka nayo sana, mimi siwezi kulisemea hilo kwa kuwa sijapata taarifa, pia hata kama lingefika tungeangalia ametoroshwa akishwa shuleni au nyumbani? Kwa kuwa baba mzazi yupo na anahusika basi aulizwe yeye kwa kuwa anajua kinachoendelea.

MAELEZO YA AFISA USTAWI WA JAMII
Afisa wa Ustawi wa Jamii, Edith Ngowi anasema: Hili suala halikuwa la kwetu, Khadija alikuja kupata ufafanuzi, huku ni Ustawi wa Jamii Nyamagana na suala lake lipo Ilemela, hivyo tulichofanya sisi ni kumshauri na kumsindikisha kwenda Polisi.

Tukiwa Polisi tukashauriwa kwenda Uhamiaji, tulipoenda Uhamiaji tulioneshwa taratibu zote zimefuatwa na baba mtu akakiri alidanganya ili upatikane uhalali wa mtoto kusafiri.

Lengo lake lilikuwa mtoto apate kuasiliwa na aende akasomeshwe, tumeshauri familia ikae pamoja na Wazazi wa pande zote kuangalia jinsi ya kulimaliza nak ama ni kumrejesha mtoto wafanye hivyo.

UHAMIAJI MWANZA WAULIZWA
Alipoulizwa Kamishna wa Uhamiaji Mkoa wa Mwanza, Peter Mbaku juu ya kudaiwa kuchezewa kwa nyaraka za mtoto na hadi kubadilishwa kwa jina kisha kuruhusiwa kwenda Canada, amesema: “Naomba muda nifuatilia hizo taarifa.”

SHULE YA ISTIQAAMA YAULIZWA
Alipotafutwa Kiongozi wa Shule ya Msingi Istiqaama, Rashid Seif Said kisha kuulizwa kuhusu taarifa za mwanafunzi huyo kwamba aliondokaje shuleni na kama alipewa ruhusa au kama wanajua kuhusu safari husika, aliomba jina na taarifa zingine za Mwanafunzi kabla ya kutoa majibu, alipotafutwa baadaye simu haikupokelewa.


Kichwa cha habari kilinisisimua, mwacheni mtoto asome, kulaneni Mzae mwingine
 
Si rahisi kwa kweli, ameshindwa kumnyanyasa hapa, akafanya hivyo Canada?

By the way kwa wenzetu sheria zao ziko wazi balaa.
Huruhusiwi hata kumchapa mtoto akalia.

Watu wa makoroboi huko mwanza wanawaza manyanyaso 😀

IMG_6485.jpg



Kwamba hao Canadians ni watakatifu sana?

Katika hili jambo, mama wa mtoto asikilizwe kwanza wasiwasi wake ni upi na wampe majibu ya kuridhisha kwa kila inquiry yake na Kama bado akiona haiwezekani basi wamrudishe mtoto mpaka pale wazazi wawili wa huyo mtoto watakapokubaliana bila njama ovu wala ulaghai kati yao.

Tuache kuongozwa na hisia zetu na roho zetu za utegemezi na umarioo.

Utaratibu na sheria vifuatwe na haki itendeke na ionekane imetendeka.
 
Back
Top Bottom