Baba Diamond: Usisubiri nife mwanangu, nipeleke Hospitali

Baba Diamond: Usisubiri nife mwanangu, nipeleke Hospitali

Mimi nauliza swali nataka jawabu.
Mwanamke anakuwa na mume usiku wanafanya mambo ya baba na mama.
Baada ya wiki mbili mama anamwambia baba nina mimba..baba anatika nduki huku mapovu yakimtoka oooh hio sio yangu.
Haonekani tena.
Anampoteza kabisa mwamamke.
Mwana mke analea mimba
Anazaa
Analea mtoto
Ana msomesha kwa tabu
Baba hana habari wala mtoto hamjui
Mtoto anafanya yake
Anafanukiwa anatengeneza fedha
Ati Ndio li baba linakuja ooh mie baba ako...bulshit....
Suala kuwa baba ni kutia kumwaga sperm tu ndio una qualify kuitwa baba ?
Jee huyo ni baba au mtia mimba tu ?
Baba asie kuwa na wajibu sio baba na hastahili kuitwa baba.

Kutia mimba sada hivi unaweza kuwekwa kwenye maabara unawekwa sperm na unapata mimba...sasa yule mwenye sperm zake atakuja baadae aseme mie ni baba ako nisaidie ?
Mababa mna wajibu wa kulea watoto wenu.
Unapo fanya kama hivi wewe sio baba ni dada umekimbia wajibu wako kuwa baba
 
Diamond ni kijana mzuri, na mwelewa kama tulivyoona hata alimhurumia mzee ngurumo akampa gari, inabidi jamii itumie fursa hii kumuasa diamond na hasa mama yake diamond, anapaswa alione hili kwani naye bado anaishi huenda mwenyezi mungu anawapima imani, binafsi mimi kama mzazi nawaomba wampe adhabu ya kumpenda na kumsaidia bila masharti na Mungu atawabariki.
Be blsddddddd
 
Mimi nauliza swali nataka jawabu.
Mwanamke anakuwa na mume usiku wanafanya mambo ya baba na mama.
Baada ya wiki mbili mama anamwambia baba nina mimba..baba anatika nduki huku mapovu yakimtoka oooh hio sio yangu.
Haonekani tena.
Anampoteza kabisa mwamamke.
Mwana mke analea mimba
Anazaa
Analea mtoto
Ana msomesha kwa tabu
Baba hana habari wala mtoto hamjui
Mtoto anafanya yake
Anafanukiwa anatengeneza fedha
Ati Ndio li baba linakuja ooh mie baba ako...bulshit....
Suala kuwa baba ni kutia kumwaga sperm tu ndio una qualify kuitwa baba ?
Jee huyo ni baba au mtia mimba tu ?
Baba asie kuwa na wajibu sio baba na hastahili kuitwa baba.

Kutia mimba sada hivi unaweza kuwekwa kwenye maabara unawekwa sperm na unapata mimba...sasa yule mwenye sperm zake atakuja baadae aseme mie ni baba ako nisaidie ?
Mababa mna wajibu wa kulea watoto wenu.
Unapo fanya kama hivi wewe sio baba ni dada umekimbia wajibu wako kuwa baba

Nilitakakuingia DEEP nkashutka e jukwaasilake
 
Siku ya msiba ndiyo atajua umuhimu wa mzazi,Diamond hajui thamani ya sha.hawa
 
Hivi dayamondi ana baba? Mi nilijua babake bi mzee ngurumo
 
kwa hiyo analipiza kisasi?du jamani binadamu hatari kwa nini asimsamehe ili nae aje asamehewe hapo mbele ya safari,wengi tuliachwa na baba zetu kwa sababu moja au nyingine na siyo lazima kujua kwa nini baba yako alipotea,tunasubiri akianza kupukutika na kurudi mitaani kama kawaida ya wasanii wa bongo ndiyo tutaongea sana

Watu wana uchungu na maisha waliyopitia wakati wa makuzi yao hasa mahitaji ya lazima kwa mtoto na hata ukijana,then kirahisi tu baada ya mtu kufanikiwa mtu mwingine anaibuka kutaka kushare alivyotafuta wakati yeye alikimbia ku-share naye alivyotafuta yeye(baba) hapo kabla.

Then inategemea style alioachana na mama yake kama ilikuwa mabaya sana na ya udhalilishaji hata mimi pua yangu haiwezi kugusa kwake na hii itakuwa ndivyo ilivyo maana upendo alionao Diamond kwa mama yake inawezekana alipigania maisha uhai wake kipindi mama na baba wapo katika mtafaruku.

Huku ndo kujifunza bwana,ni wangapi wanaachana na wake zao kutokana na sababu mbalimbali na bado baba anatoa huduma home kwa mama na kwa watoto hata kama ameoa mwingine,je iwapao alifanya hivi Monds angemfanyia baba yake haya...asaidiwe na aliokuwa anawasaidia bwana!
 
Baba aliweza kupanda mbegu kisha akakausha huyo sio baba ni mvulana, mtu mwenye busara uhakikisha anatoa huduma au hata kumwona mwanae haijalishi kuna ugomvi kiasi gani baina yake na mwenzie. naomba diamond amache tu yeye aangalie maisha ya aliyemwangaikia.

SI ndio wanajisifu wavulana kuwa hata nikimtelekeza mtoto akikua atanitafuta sasa wajue dunia imebadilika watoto wa siku hizi wanajitambua, yeye afe tu.
wewe ni mwenyekiti wa wanawake wenye roho mbaya,
kama ndivyo ulivyo wazazi wako wamekula hasara.
 
Niwe open kabisa ningelikuwa Nasib Abdul hakyamungu baba huyu nisengeli msaidia hata kiduchi wacha mungu anihukumu

Usiseme hivyo, kama unaweza kumpa msaada usie mjua why not your Dad? Mpe na Usijali nini Anaongea wewe toa lile fungu lako ambalo hata Kwa mungu anaona Ukiwa kama mtoto wajibu wako umetimiza, Ya binadamu yawache ...
 
Wacheni upotofu......Mwenyezimungu ni mjuzi na ndiye atakayetoa hukumu ya haki.Kama baba anamakosa ataadhibiwa kwa makosa yake na mtoto pia ataadhibiwa kwa makosa yake.Kijana elewa kwamba kutokumtii baba yako ni makosa makubwa sana.Mfano mmoja nikupe...kama baba yako anafanya kazi ya udobi wewe kama mtoto huna haki kabisa ya kumpelekea nguo akufulie umlipe pesa.
 
Kuna tofauti kubwa kati ya mtia mimba(dungadunga) na baba.
 
So sad! Kuelekea Zari show. Baba yake Diamond ambae anaumwa sana miguu ameshindwa hata kutembea ameomba mwanae amsamehe kama baba na pia ameomba aje kumtembelea ampeleke hospitali asisubiri kufa.

Sisemi kwa ubaya, mi ni mmoja kati ya watu wanaojua maisha ya baba na mama waliotengena. Ukweli haijalishi uko level gani ugomvi wa mama yako na baba yako usiingilie hata siku moja tafadhalini...

Narudia tena, Diamond akifa leo baba yako hutopata Baba wa kukodi.

Kila la kheri..

==============

DIAMOND MWANANGU USISUBIRI NIFE!


Maskini! Wakati leo akiangusha pati ya nguvu na mpenzi wake, Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’ inayokwenda kwa jina la Zari All White Party kwenye Ukumbi wa Mlimani City, Dar, baba mzazi wa mwanamuziki Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, Abdul Jumaa yu hoi kitandani huku akimtaka mwanaye huyo kuonesha msamaha wa kweli aliotangaza kwenye vyombo vya habari na kwamba asisubiri hadi afe.


View attachment 248376
Baba mzazi wa ‘Diamond Platnumz’


TUJIUNGE NA CHANZO
Habari kutoka kwa chanzo makini kilicho karibu na baba Diamond kilidai kwamba kutokana na hali tete ya mzazi huyo ambapo kwa sasa anasumbuliwa na miguu kwa mara nyingine huku ikitoka magamba na kushindwa kutembea kwa muda mrefu, amekuwa akimlaumu mwanaye huyo kupita kiasi.


Chanzo hicho kilisema kuwa mzazi huyo amekuwa akisema kama alimkosea Diamond, alishamuomba msamaha na akasema amemsamehe lakini hakuonesha mabadiliko yoyote kwake wakati alikiri hadharani kupitia vyombo vya habari.

Kiliendelea kueleza kwamba kutokana na jambo hilo baba Diamond amekuwa akiumia kwani mwanaye huyo baada ya kutangaza amemsamehe hajaonesha mabadiliko yoyote ya kumjali.


MALALAMIKO
Chanzo hicho kilidai kwamba, baba Diamond amekuwa akilalamika kuwa ameugua kwa muda mrefu lakini Diamond hajawahi kwenda kumjulia hali hata siku moja.

“Ukweli baba Diamond anaumia sana. Sasa hivi anaumwa, ameshindwa hata kutoka nje, miguu imevimba na ina muonekano wa ajabu, amekuwa akisema hajui ni kwa nini mwanaye anashindwa kulegeza moyo wake na kumsamehe wakati alishakiri kwenye vyombo vya habari.“Anasema bora akaenda sasa hivi wakasameheane kuliko asubiri hadi siku akifa ndipo aende,” kiliongeza chanzo hicho.


BOFYA HAPA KUMSIKIA BABA DIAMOND
Baada ya kupata habari hizo, gazeti hili lilitinga nyumbani kwa baba Diamond au Dangote maeneo ya Magomeni-Kagera, Dar na kumkuta akiwa katika hali mbaya kwani miguu imevimba huku ikiwa imepoteza muonekano wa kawaida na kuwa na ngozi ya ajabu.

Baada ya salamu, wanahabari wetu walimuuliza kulikoni yupo katika hali hiyo na kama Diamond alikuwa amekwenda kumjulia hali ambapo alikuwa na haya ya kusema:“Ukweli nimeugua kwa muda mrefu lakini mwanangu Diamond hajawahi kuja kuniona.

AMTUMIA MESEJI
“Hali hiyo ilinifanya juzikati kumwandikia meseji ya kukata tamaa na kumwambia kwamba anaona ameshanizika kutokana na kunisahau kwake lakini Diamond hakunijibu.

“Namshukuru Mungu kwa sababu nina kibanda changu cha kulala, silipi kodi kuna watu walishanishauri eti niwatume watu wakaongee naye lakini nilikataa kwa sababu haoni thamani yangu.


ANASUBIRI NIFE?
“Kama ni tofauti na mama yake (Sanura Kassim), tulishamaliza na kabla hajaugua alikuwa anakuja kuniona, nikimuuliza kuhusu Diamond alikuwa akiniambia alishaongea naye lakini kila siku alikuwa akisema atakuja tu kuniona mpaka leo sijamuona labda anasubiri hadi nife ndiyo aje.

“Mara ya mwisho kumuona ilikuwa ni kipindi kile alivyomvisha pete ya uchumba Wema Sepetu ndiyo alimleta kwangu kumtambulisha, tangu hapo huwa namsikia tu kwenye vyombo vya habari. Inauma sana; “Yote kwa yote haya ni maisha tu.”

DIAMOND YUPO BIZE
Ijumaa lilimtafuta Diamond ili kumfikishia habari juu ya baba yake ambapo hakupatikana hewani lakini watu wake wakaribu (Wasafi Classic Baby) walidai kwamba bosi wao huyo alikuwa yupo bize na Zari kwa ajili ya pati yao leo.

Chanzo: GPL

Sikutaka kucoment ila nalazimika
Yy kama baba amemsaidia nn diamond mtt alipotaka msaada wa kusoma alimsomesha?
 
na hili liwe fundisho si huwa wanaume wanajigamba akikuwa atanitafuta tu sasa hayo, kwani mtt ni diamond peke yake? hao wanaonshauri muda huu aombe msaada walikuwa wapi kumshauri ajali mtt? diamond hakuna kama mama sugua gaga wangapi wamekufa ?
 
Wakati huyu mzee ana pesa ndefu ikawa Diamond akimfata magomeni kumsalimia tu alimfukuza akimwita chokoraa, akuwai kujua anakula nini wala anapona na nini akiugua. Leo unatafuta huruma kwenye media, malipo siku hizi ni hapa hapa duniani.
Watoto ulioona wa maana wako wapi? Diamond angeishia kwenye drugs kama wenzake wa Tandale ungemkumbuka? Mi naomba usife mapema ili uendeleee kukiona cha moto.
 
na hili liwe fundisho si huwa wanaume wanajigamba akikuwa atanitafuta tu sasa hayo, kwani mtt ni diamond peke yake? hao wanaonshauri muda huu aombe msaada walikuwa wapi kumshauri ajali mtt? diamond hakuna kama mama sugua gaga wangapi wamekufa ?
Unajuwa dada si kwamba hatutambui makosa ya babake diamond.la hasha lakini si lazima kumlipiza ubaya ndio utakuwa umemfundisha. ukimtendea mazuri utamfundisha zaidi kwani hatafanya ubaya kwa wengine tena.atajutia kosa lake maisha yake.
 
Back
Top Bottom