Baba wa Mwimbaji wa Injili aliyeimba "Mnatuona Nyani tu" ahukumiwa miaka 3 jela kwa kuendesha Kanisa bila kibali

Hapo unaelekea kwenye Ukomunisti na jinsi Ukomunisti ulivyojaribu ku control dini, ukashindwa.

Uhuru wa kuabudu ni haki ya kikatiba, ni haki ya kibinadamu.

Ukishaanza kuusajikisajili serikakini uhuru huu, unatengeneza namna ya serikali kuuingikia uhuru huu.

Waacheni watu waabudu bika kuingikiwa na serikali.

Wakifanya uhalifu, washughulikiwe tu na sheria.

Ukianza kutaka nyumba za ibada zisajiliwe, mimi nikiwa nakutana na jirani zangu kwa faragha za kuabudu nyumbani kwangu napo utataka nisajiki nyumba yangu? Where do you draw the line?

Hii habari inatuonesha kabisa jinsi gani serikali inavyotumia hivi vibali kuwanyamazisha watu wenye maoni ya kukisia serikali.

Hivi vibali vinavunja katiba, vinavunja haki za binadamu.

Sent from my SM-S908U1 using JamiiForums mobile app
 
Hakimu kawakumbuka kondoo wakati akipiga mchungaji? Au amwaacha watawanyikie kwa shetani? Yesu mchungaji mkuu atalitama hili nalo.
 
Mtumishi wa mungu mwenye nyimbo nzuri za kuabudu za tenzi za rohoni mchungaji mbarikiwa mwakipesile leo amehukumiwa miaka 3 kwenda jela kwa kuanzisha kanisa bila kibali.

ikumbukwe kuwa awali mwanae alitunga nyimbo inayohusu mkataba mbovu wa bandari pamoja na kile kinachiendelea ngorongoro kuhusu matumizi ya nguvu yanayotumika kuhamisha wamasai aka kamatwa na jeshi la polisi na kupelekwa mahakamani kisha na kupata dhamana.

Nyimbo hiyo ilikuwa inaimbwa kuwa sisi tunaonekana nyani kuonesha kuwa sisi wananchi hakuna tunalolijuwa.leo mtumishi wa mungu na mwimbaji mashuhuri mchungaji mbarikiwa mwakipesile amehukumiwa kwenda jela miaka mitatu kwa kauli zake za kukosoa serikali kigezo cha kusema ameanzisha kanisa bila kibali hakina mashiko mbele ya jamii.[emoji116][emoji116][emoji116][emoji116][emoji116][emoji116][emoji116][emoji116]

Your browser is not able to play this audio.
 
Siku zite iko hivi, Ukiwa Mstaarabu
hata kama una mapungufu watu hukupuuza ila ukijikuta mjanja watu watataka wakuonyeshe kua hujui.
Ukiamua kukosoa wenzio hakikisha uko smart.
Sheria za wapi hizi? Kwamba ukiwa mpole hata kama huna vibali unaruhusiwa kufanya kazi, haiwezekani mtu aoperate miaka mitatu ndo wahusika wagundue Hana vibali, wanafanya kazi Gani sasa?

Au ndo Yale ya the cask kuonyesha bango la kupinga dp world... Kesho yake halmashauri na tra wakafurika bar kuwafungia kua hawana vibali?
 
Huyu mwamba, huwa namsikiliza tiktok na wale wakina mama wanaomzunguka asilimia kubwa huwa ni kupambana na serikali na kuikosoa kuliko kuikosoa serikali ya ufalme wa ibirisi na hila zake.

Kwa jinsi alivyomkakamavu, naona kama hiyo qdhabu haitafua dafu kwake. Akitoka ataendeleza harakati zake tu.
 
Serikali haingilii uhuru wa kuabudu....

Ila serikali ni lazima idhibiti vitu vyote kupitia SAJILI....

La kujiuliza.....yanapotokea makosa ya KIJINAI huko katika nyumba za ibada nayo serikali ikae pembeni ?!!! [emoji15][emoji15][emoji15]
Serikali inatumia vibali kufanya censorship.

Hapa tunaona kabisa habari ya vibali imekuja baada ya mtoto wa mchungaji kutoa wimbo ambao serikali haikuupenda.

Serikali haihitaji usajili ili kudhibiti jinai, mbona mitaani kuna nyumba kibao hazina usajili na serikali bado inaweza kudhibiti jinai?

Hawa wachungaji wakifanya jinai, wsshitakiwe, lakini tusilazimishe vibali, vinavunja haki za kikatiba na za kibinadamu.

Sent from my SM-S908U1 using JamiiForums mobile app
 
A
Jesus Christ he is crying, for his servant mwakipesile soon he will do something.
"Aonywaye mara nyingi na kushupaza shingo yake nae atavunjika ghafla Wala hatapata dawa" tumesema Sana na hao wakalia matawi ya juu yetu subira.
Ni hayo tu waheshimiwa.
 
Asiye na imani ya dini ndiye amekuwa mkweli na mpenda haki kuliko wenye dini zao wanaofunga wenye dini wenzao.
 
Wavunjaji wa sheria wakiwa misikitini na makanisani huchukuliwa kwa uzito MKUBWA....

Ulitaka DOLA liwaache wale masheikh wa UAMSHO wafanye watakavyo?!!! [emoji15][emoji15][emoji15]
 
Si ndiyoo, Si sahih ila ndo utarajia hayo ukiamua kushundana na Serikali.
 
Busara ingekuwa ni kulifunga kanisa na hio huduma kufungwa ,na sio mchungaji kufungwa
Ila kwa vile busara yao imeamua hivyo basi tuwape pongezi kwani wamejiandaa kwa matokeo yoyote dhidi ya hio hukumu.
 
Kanisa na misikiti si sehemu ya FARAGHA kulinganisha na jumuiya za ibada majumbani......

Kiranga unajitoa akili sana....
 
Hakuna mahali nyumba za ibada zitaanzishwa bila kuhakikisha uthibitisho wa kitakachukuwa kinafanyika kwenye nyumba hizo.

Kama wewe na jirani yako mtahitaji kutambulika kama waanzilishi wa Itikadi/falsafa fulani na kuhitaji kuungwa mkono na jamii yenu kwanini msimtambulike na kulindwa kisheria?
 
Mimi simo Mkuu, Ila mtazamo tu hajaonewa maana kweli hana vibari.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…