Babu wa Loliondo afungiwa kwa muda kutoa huduma...

Babu wa Loliondo afungiwa kwa muda kutoa huduma...

Hapo kwenye rangi ndo kuna kasoro: Kuna harufu ya UDINI. Nani alikulazimisha uende huko kutibiwa?? ulivutwa kwa mnyororo. Mchungaji amekuambia dawa yake inatibu kutegemea na imani ya mgonjwa-na hilo ulijua-je unajuaje shangazi yako alikuwa na imani ya dawa?? mbona mimi jirani yangu alikwenda akiwa anaumwa na yupo anajieeleza kuendelea vema!!! kwa sasa wakati uchunguzi wa kisayansi haujafanywa kuhusu ubora na uhahakika wa dawa, yeyote aendapo kutibiwa kwa dawa hiyo aende kwa imani yake na awe tayari kubeba dhamana ya mafanikio au madhara yeye mwenyewe (he/she has to take risk or responsibility him/herself).

Hapo penye rangi sijakuelewa!!! fafanua zaidi unamaana gani?
 
Mada haina ukweli wowote bali kuna harufu ya udini. Hivi unajisikiaje kumzushia ndugu yako kafa kisa tu kueneza udini?

Yawezekana kweli kafa maana tumesikia mama mmoja wa hapa moshi kapelekwa huko na jana tu kazikwa! Inawezekana ni kweli ila hakuna aliyeambiwa eende huko. Mtu anaenda kwa hiari yake. Ni upuuzi kusema kuwa watu wapuuze wachungaji na mapadre! Ni utoto na ujinga wa hali ya juu. Kuna gazeti nimesoma kuwa ustaadhi sijui nani vile anatibu kwa kutumia gongo, bangi na kila aina ya takataka! Kwa hiyo tuwapuuze maustaadhi wote?
 
Naiomba Serikali imkamate huyu Mganga wa Kienyeji kwa kusababisha vifo vingi vya Wagonjwa ktk wiki hii!! ni jana tu nimemzika Shangazi yangu aliyefariki huko Loliondo mara tu baada ya kunywa kikombe kimoja cha dawa ili kutibu gonjwa la kisukari!!! Marehemu Shangazi langu aliishi na ugonjwa huo zaidi ya miaka 20 lakini alipoambiwa kuna Mchungaji anatibu papohapo tulimpeleka Shangazi na kupewa hiyo dawa na tukiwa njiani kurudi nyumbani Shangazi aliaga dunia!!

Tunasikitika kumpoteza Shangazi wetu mpendwa na nimesikia kuna wagonjwa wengi waliofariki mara baada ya kunywa dawa za huyo Mchungaji na kunipa hofu na kukumbuka kisa cha Mchungaji mmoja huko Uganda miaka ya 90 alichoma Kanisa Moto na kuteketeza maelfu ya Waumini waliokuwa humo ndani kwa kudai alioteshwa na Mungu kuwa wakifia Kanisani kwa kujichoma moto basi wataenda mbinguni!!!

Naiomba Serikali imchukulie hatua kali huyu Mchungaji wa Loliondo kwani amesababisha madhara makubwa kwa Wananchi na hata kuharibu mazingira kwa kuwakusanya maelfu ya watu mahali finyu bila choo wala mahala pa kulala na pa kula!!

Familia yetu iko mbioni kushika wakili ili tumfungulie kesi kwa kusababisha kifo cha Shangazi wetu mpendwa!

Wananchi tuwe macho na hawa WACHUNGAJI NA MAPADRE wenye kudai kutibu maradhi baada ya kuoteshwa ndoto na Mungu wakiwa wamelala!!!!!!!!!


pole sana MS, familia ya mzee ngoda, jeykey. mimi sikujua kama ulikuwa loliondo
 
Wamekurupuka hao! Babu ni mjanja hii kitu ni 'Intellectual Property' yake kwa hiyo ni lazima wakubaliane kwanza. Hao wanataka kumuingiza mujini ili wai-patent kazi yake...

Bravo Babu wa Loliondo...:wink2:

Nafikiri ana haki ya kuamua kama wanaweza kuifanyia utafiti au la! Na waganga wengi wanaotoa tiba asili kama ile ya kutibu mifunjiko ya mifupa wamekuwa hawataki kushirikiana na watafiti kwa hofu ya kupoteza haki za kazi zao. Na wengine wanadai kwamba, ''...watakuambia dawa yako haifai lakini baadae watachukua na kujifanya wao ndio wamegundua''.
 
hao wametumwa wamwache huyu mtalaamu wa mitishamba aendelee kula kuku
na h uku akitoa huduma zake kwa wateja zake, ila nimekumbuka uchunguzi wa niuklia kule edeni
 
Yawezekana kweli kafa maana tumesikia mama mmoja wa hapa moshi kapelekwa huko na jana tu kazikwa! Inawezekana ni kweli ila hakuna aliyeambiwa eende huko. Mtu anaenda kwa hiari yake. Ni upuuzi kusema kuwa watu wapuuze wachungaji na mapadre! Ni utoto na ujinga wa hali ya juu. Kuna gazeti nimesoma kuwa ustaadhi sijui nani vile anatibu kwa kutumia gongo, bangi na kila aina ya takataka! Kwa hiyo tuwapuuze maustaadhi wote?

Tafadhali usinipachikie nisilosema mdomoni!!! mimi sijasema tuwapuuze Wachungaji na Mapdre wote, ila nimesema tuwapuuze tu wakija na kauli za kuoteshwa usiku na Mungu ili watibu wagonjwa! na hili linawahusu pia Mashehe wenye kutabiri mambo yanayokuja! ili kuondoa dhana yenu ya UDINI!!! imebidi nimseme na Shehe Yahya ambae kazi yake ni kutabiri bila kumsahau Askofu Kakobe na kazi yake ya kuombea wagonjwa ambao hakuna ushahidi wa kisayansi unaoonyesha wamepona!!!

Hawa Wachungaji na Mashehe hewa ndio wakuepukwa kama ukoma na nawashangaa watu wanaokuja hapa na kumtetea huyo Mchungaji wa LOLIONDO na hapa naanza kuaminini kuwa nchi yetu imeingia ktk giza tororo la imani za kichawi!!!!!!
 
Hii ni sawa, lakini kama serikali inabidi/ni muhimu ijiridhishe pia kwamba dawa hiyo licha ya kuponya kama inavyodaiwa haina madhara mengine makubwa kwa mtumiaji (sasa na baadae). serikali ina jukumu la kulinda afya na maisha ya watu wake.

Imeshindwa nini kulinda afya za wakaz wa bulyankhulu waliofoukiwa kupisha uchimbaji wa dhahabu? Huo muda si wautumie kuokoa maisha ya kina mama wajawazito wanaokosa hela za kujifungua? Hawa wamefata hiyo dawa au "pa diem"
 
Watanzania mkimfungia huyo babu, anaweza kuchukuliwa na nchi jirani, akasaidiwa mazingira mazuri, then hiyo huduma mtakuwa mnaifuata huko.

Hili ndo tatizo la kuamini vitu vinavyogunduliwa na wazungu na kudharau vya kwetu. Hebu jiulize kuna dawa ngapi za kienyeji za kichina zipo sokoni zinauzwa, tumewahi kuona mazingira wanayotengenezea?

Mi nakwambia babu kama huyu angekwepo China serikali ingemsadia kwa kumpa packaging material kama chupa ambazo ni disposable ili awe ana servia hiyo dawa badala ya kutumia kikombe kimoja, ingempa vyombo vya kuchemshia, jiko la kisasa nk, alafu huduma ingeendelea kadri anavyotaka yeye kwa imani yake.
 
Felister,

1. Wagonjwa wenye shida ambao hawana nauli watafikaje kwa babu kama yeye peke yake
ndie anayetoa hiyo dawa na si mwingine?

2. Southern countries ndio zilizoathirika sana kwa ugonjwa wa UKIMWI, are you telling me all
those people should come to TZ to get this treatment from him ONLY?

3. Kama kweli hii dawa Mungu ndiye aliyemfunulia, vipi kuhusu wagonjwa ambao wanafia
njiani wakielekea huko Loliondo? Hawakustahili kupata hii dawa ili wapone?

4. How come we only hearing story from people but we havent actually see someone who got
healed, utasikia tu mtoto wa rafiki yangu, mama yake rafiki yangu, mjomba wangu
anayekaa mbeya etc?

Ni vizuri kuwa na mashaka lakini ni bora kuelewa kuwa katika mambo haya imani ndiyo inatakiwa kutangulizwa. Kwani imeandikwa "heri aaminiye bila kuona."
 
Kitaalamu magonjwa yote anayoyatibu babu yanatokana na vyanzo tofauti; cha ajabu inaelekea anatumia dawa ile ile ya aina moja kutibu hayo magonjwa yenye vyanzo tofauti. Hao maafisa kutoka wizarani kama wangelikuwa watu makini, walitakiwa waanze kuchunguza kama ni kweli watu wenye magonjwa tofauti wanaponyeshwa na dawa ya aina moja. Baada ya kuridhibitisha hilo, hapakuwepo haja ya kuipima hiyo dawa, kwa maana ukweli huo ungelikuwa umethibitisha ya kuwa dawa ya Babu huyo inaanzia mahali ambapo sayansi inaishia.
 
watibishe basi ili tupate nafasi nzuri ya kuanzia mgomo mama lao. Wamehisi babu ni Cdm sasa wanaanza upupu wao. Tena nawaambieni , huyo aliyempa babu nguvu ana mamlaka kulioko Wakwere wote na majuha yao.
Unaweza kutupa angalau vidokezo vichache juu ya uhusiano wa Babu na Chadema?
 
Serikali ina jukumu la kutunza afya za watu wake. Hawa 6 ambao wameshakufa wakiwa njiani ni alarm ya kutosha kuwa lazima hatua zichukuliwa haraka. kwanza kuangalia mazingira halisi ya wagonjwa na huduma zilizopo kama maji, vyoo nk. Kwa kitalaamu, wale wagonjjwa waliopata dawa wanahitaji kujitoa wafanyiwe uchunguzi ili kukubali au kupinga haya anayodai huyu Mzee. Nina wasiwasi, kwa sababu kama kweli kuna watu waliopona wangekuwa wameshatoa ushuhuda

Ni kweli kabisa ndugu yangu kwani wagonjwa walioko hospitalini huwa hawafi ila wale wanaokwenda kwa Babu!
 
kuna siku hawa serikali watatahitaji kupima maji yanayotumika kubatiza watu ...au hata haya majivu niliyopakwa leo...

ki msimgi hapo hawapimi dawa ila wanatafuta kipima nguvu za Mungu.......mungu anaweza kuniotesha mimi hapa akaseam: mwanangu Edson huo mti wa mlonge unaouona hapo mbele ni dawa ya kutibu a, b, c, d, e, f, g, ect...chukua majan yake chemsha na kisha wape watu na watapona....kupitia wewe nasi mtu mwingine.....

jaman kuna miti mingi ya aina hii..lakini Mungu kauchagua mlonge huu na mimi pekee ndo nitoe dawa.....sasa hapa si mti wa mimi tunapaswa kupimwa...maana mimi ni chombo tu ila mungu kupitia mimi anatibu watu.....hawa serikali ni wapumbavu wakubwa......

maana hapa wanatak kumjaribu Mungu...kwa nini wasitumie wale waliopina kujiridhisha? kipindu pindu huwa kinachukua mda gan jamani...shemeji yangu schola amepona kisukari na mpka leo amepona sasa, alikunywa sawa ya babu sasa hawa wanaema nini

hapan ndipo pa kuandamana ndugu zangu......
Mkuu tusiilaumu sana serikali,inatimiza wajibu wake.leo ile dawa ikileta madhara tutaanza kutoa lawana tena.ni vizuri kujiridhisha kuwa dawa hizo si sumu wala haina madhara yoyote. .................
 
kwa wale wanaofikiria Nje ya BOX ...This is pure case of placebo effect. Huyu babu he is a priest "man of god" claim he saw this herb in his dream.. wht u except..? if u know about placebo effect u will have ur answer why people who are going to see him thy are getting better!!... P.L.A.C.E.B.O !! ... !

Huu ni ukweli kabisa kwani hata ile ndoto ya Ali Juuyawatu kuhusu Tanzanite kuwa pale Mererani ni uongo mtupu. Watu walipokwenda kuchimba Tanzanite pale Mererani walikuta kuwa yale ni mawe tu na huyo Ali Juuyawatu amebakia kuwa tapeli mkubwa kwani Tanzania sasa haipati Tanzanite kutoka pale Mererani. Kumbe ndoto zote ni uongo na watu wawakatae wote wanaodai kuoteshwa mambo ya kufanya katika ndoto.
 
mungu hapendi watu wake tuteseke ndio maana kwa huruma yake amemtuma mtumishi wake ili aponye magonjwa yote yanayo mtesa binadam kwa hiyo anayeamin ataenda atapewa dawa. na asiye amin aendelee kusubir hadi hapo uchunguzi utakapo kamilika .
 
mm ni mkazi wa loliondo na ujumbe huo ulikua haujawasili mida hiyo ya sa2 asubuhi mm nlipotoka kwa babu samunge kurudi loliondo mjini.na suala la kupmwa dawa ya babu, yupo confort na anasema that is spiritual matters,pia katoa onyo jwa wanaopandiha bei ya bdhaa kuwa hakika hawata nufaika,kwani hata amekataa suala la ushuru wa sh2000 eti utakaotozwa kila ajae kunya dawa,pia ukiingilia foleni ametoa onyo kua itakua hujanywa dawa bali ni maji.
Mengi ya kwa babu nmeshuhudia ila kuandika duh!
4more details nipigie kwa 075423809-
Simu yako inakosa namba moja ya mwisho.
 
watu wanywe dawa maadam ni miti ambayo ameumba mungu na hakuna maradhi yasio na dawa.kama kuna mgonjwa amepata reaction hapo lipo la kuchunguza.tena babu amekutajia mti anaotumia!
 
kumfungia babu ....halifai kwani yeye anatoa alternative medicine ......mbona kuna watabiri wanaotoa tabiri zinazotishia usalama wa nchi hawafungiwi......haya mambo ya kiasili waachiwe wananchi ..serikali isimamie usalama wao...kwa hili ingekuwa bora kwa serikali kuboresha miundombinu ili wananchi wasiteseke au wafikirie kumshauri apeleke huduma mjini kwenye huduma hasa malazi na chakula.....na kumsaidia usafiri wa kufuata dawa kijijini....angalizo ni kuwa babu sio mganga wa kienyeji!!..ni mtumishi wa mungu!!..na hatoi huduma kwa ubaguzi wa aiana yeyote!!
 
Back
Top Bottom