Baby dady Drama: Ni ngumu sana kushindana na baba wa mtoto ukianzisha mahusiano na single maza, ngumu sana!

Baby dady Drama: Ni ngumu sana kushindana na baba wa mtoto ukianzisha mahusiano na single maza, ngumu sana!

Ukitaka kuoa singo mama hakikisha unaliona kabuli la Baba mtoto wake la si hivyo yajayo yanaburudisha....
 
Mimi naona hizo ni assumptions za watu wachache wanaotaka sisi tuliowapa mimba wadada na kuwaacha kwamba hatuachani. Mimi binafsi toka tulipoachana na mama wa mtoto wangu sijawahi kufikiria kumla tena baada ya yeye kuolewa yaani hata simu tu asipopiga yeye eiza niongee na mtoto au kuna tatizo lolote nahitajika kulikwamua siwezi kumupigia simu hata kidogo.
😂
 
Sitokuja niguse single mother mpaka naingia kaburini, kilichonikuta ni Siri yangu hao watu ukiwa nae kabla haujaanza Safari mchunguze vizuri kichwa chake ndio uchaguzi unasuka au unanyoa namaanisha kichwa chake sio chako
 
Sitokuja niguse single mother kamwe hao watu napita mbali nao kabisa, sitaki kabisa yaan sijui ni wote ndio wapo hivyo au baadhi Ila nahisi ni wote wapo hivyo aisee ogopa single mother hata akwambie nini kua nae makini hawakawii kugeuza kibao maana anaishi na reserve list sasa wewe jichanganye uambiwe kwani Mwanaume upo peke yako?
 
Unaweza ukajipa moyo kwamba waliachana kwa ugomvi na pengine baba wa mtoto hakutoa chochote tangu asikie mwanamke kapata mimba, waweza kudhani jamaa ndio basi tena kahsribu hawezi kuwa tatizo.

Kiufupi ni ngumu sana mwanamke kumuacha kirahisi mwanaume aliemtunga mimba hasa ya kwanza ile inayompa status ya kuitwa mama flani , hadi kaamua kuchukua maamuzi alee mimba miezi 9 si kitu kidogo.

Kuna kipindi itafika tu ataanza kuomba ruhusa ampeleke mtoto kwa baba yake, tena nae mtoto anaweza kuanza kukuita uncle ama kwa jina lako ila baba ni jina atalomtunzia huyo babake wa kibailojia, hii hasa kwa watoto wa kiume.

Mambo yanayoendelea huko pindi wakiwa wao bila uwepo wako ndio sumu inayoweza kuleta simanzi kwenye mahusiano yenu
Hayo ya singo mama yalimkuta mdogo wangu mpaka tukawa tunamshangaa.

Analishwa meza moja na baba wa mtoto, tena nyumbani kwake. Kisa nini? Eti baba kamtembelea binti yake na kaenda muda wa chakula.

Nikamwambia mdogo wangu, haifai hivyo, mwambie mkeo amtayarishe mtoto baba'ke aje kumchukuwa aebde kula nae apendako, tena aishie nje, kwako asiingie kabisa, wala mlangoni asisogee.

Hilo mdogo wangu lilimshinda, eti asionekane wa kizamani. Ikabidi niingilie kati nimweleze mkewe (wifi yangu), akanielewa. Ndiyo ikawa mwisho wa kuja.

Lakini vikaanza visa vingine.
 
Hayo ya singo mama yalimkuta mdogo wangu mpaka tukawa tunamshangaa.

Analishwa meza moja na baba wa mtoto, tena nyumbani kwake. Kisa nini? Eti baba kamtembelea binti yake na kaenda muda wa chakula.

Nikamwambia mdogo wangu, haifai hivyo, mwambie mkeo amtayarishe mtoto baba'ke aje kumchukuwa aebde kula nae apendako, tena aishie nje, kwako asiingie kabisa, wala mlangoni asisogee.

Hilo mdogo wangu lilimshinda, eti asionekane wa kizamani. Ikabidi niingilie kati nimweleze mkewe (wifi yangu), akanielewa. Ndiyo ikawa mwisho wa kuja.

Lakini vikaanza visa vingine.
Tatizo lipo kwa mdogo wako kujimilikisha shamba la watu, wachaa yamkute labda atatumia kichwa cha juu kufikiri badala ya kutumia kichwa cha chini kufanya maamuzi!!
 
Back
Top Bottom