Bado CCM hakujatulia. Naziona teuzi na tenguzi nyingine muda si mrefu

Bado CCM hakujatulia. Naziona teuzi na tenguzi nyingine muda si mrefu

G4N

JF-Expert Member
Joined
Apr 6, 2014
Posts
4,283
Reaction score
9,925
Nadhani CCM hawakai kama Kamati katika kupendekeza, kuchambua na kupitisha nani awe nani ndani ya chama. Yawezekana maamuzi mengi hutegemea mahaba na mapendekezo ya mtu au kikundi cha watu wachache. Sina hakika na hili ndiyo maana nimetumia maneno nadhani na yawezekana.

Ukiangalia kwa nje, wanaccm wengi walifurahia sana uteuzi wa Makonda kuwa mwenezi na wamepigwa na butwaa baada ya kutenguliwa. Sasa unajiuliza ikiwa demokrasia ilifanya kazi ya kumteua iweje isitumike kumtengua, mpk inaacha malalamiko?

Hii ni ishara kuwa kuna kikundi cha watu wachache ama mtu mmoja (mwenyekiti) ndiye huamua nani awe ni nani ndani ya chama.

Pili, Jokate Mwegelo aliyeteuliwa Oktoba mosi 2023 kuwa Katibu wa UWT taifa, leo ametenguliwa na kuteuliwa kuwa katibu mkuu UVCCM. Je, Jokate amepwaya ktk nafasi hii kwa muda mchache kiasi hiki? Hamkumchunguza kabla ya kumteua?

Pamoja na uteuzi na utenguzi wa leo, bado nafasi ya katibu mkuu UWT taifa haijajazwa. Hivyo muda si mrefu utasikia mtu anateunguliwa halafu anateuliwa kujaza nafasi ya UWT taifa.

CCM bado kunafukuta, tutaendelea kushuhudia teuzi na tenguzi ndani chama hiki kikongwe.
 
Ni katika kuwatumikia wananchi, kujiimarisha na kujizatiiti mamlakani, CCM bila mbambamba yoyote haitasita kuteu lakini pia kutengua yeyote kadiri inavyoonekana inafaa....

Ina hazina ya kutosha ya waandamizi waadilifu na hodari wa kazi...
 
Teuzi na Tenguzi za CCM pamoja na serikali kwa ujumla, imekuwa ni miongoni mwa kero za nchi kama zilivo kero Nyingine, mfano kukatika kwa umeme, maisha magumu kwa wananchi na n. K
 
Teuzi na Tenguzi za ccm pamoja na serikali kwa ujumla, imekuwa ni miongoni mwa kero za nchi kama zilivo kero Nyingine, mfano kukatika kwa umeme, maisha magumu kwa wananchi na n. K
Kabisa. Unaangalia mtu A aliyetenguliwa miezi kadhaa tu anateuliwa tena. Sijui watanzania wengine hawawaoni??
 
Ingelikuwa na hazina kiasi hiki isingekuwa inahangaika. Hata jiwe alilazimika kukopa mawaziri toka nje ya ccm. Yaelekea ccm ukame wa watu weledi na waadilifu
Si kweli na hakuna kitu kama icho....

Anae hangaika ni wewe, ccm ni tulivu, imara na haibabaiki kwa lolote....
 
Nadhani ccm hawakai kama Kamati katika kupendekeza kuchambua na kupitisha nani awe nani ndani ya chama. Yawezekana maamuzi mengi hutegemea mahaba na mapendekezo ya mtu au kikundi cha watu wachache. Sina hakika na hili ndiyo maana nimetumia maneno nadhani na yawezekana...
MFAMAJI LAZIMA ATAPETAPE
 
Nadhani ccm hawakai kama Kamati katika kupendekeza kuchambua na kupitisha nani awe nani ndani ya chama. Yawezekana maamuzi...
State inamchosha mtangaza Nia mapema kabla ya wakati Ili waingize chaguo lao!!

Yes angejikalia kimya tu Ili wakati ukifika atushangaze!lakini wahuni wanamchosha tu !!!
 
Nadhani ccm hawakai kama Kamati katika kupendekeza kuchambua na kupitisha nani awe nani ndani ya chama. Yawezekana maamuzi mengi hutegemea mahaba na mapendekezo...
Sasa kukifukuta si ndiyo vizuri! Au mtoa mada unapata mfadhaiko!!
 
ni katika kuwatumikia wanainchi, kujiimarisha na kujizatiiti mamlakani, CCM bila mbambamba yoyote haitasita kuteu lakini pia kutengua yeyote kadiri inavyoonekana inafaa....

ina hazina ya kutosha ya waandamizi waadilifu na hodari wa kazi...
Hapo kwenye uadilifu hapo! Hapo hapoo!!

...kwa urefu wa kamba yako. Chukua Chako Mapema.
 
Teuzi kila baada ya miezi mitano au sita, ni mda gani sasa huyo kiongozi atakuwa amefanya mambo ya maana 🤔🤔??. Saa100 na genge lake ni tatizo sana ☹️☹️.
Remote ya kuleee,,, ndiyo inamsumbua.
 
Hapa Tundu LISu kajikalia kimya wao wako tabu

Sukuma gang na msoga Bado vuta nikivute ipo
 
Remote ya kuleee,,, ndiyo inamsumbua.
• Kinacho shangaza zaidi, mbona kipindi anamiliki Tv, alikuwa hafanyi hivyo kama anavyofanya sasa 🤔🤔🤔?. Ni uzee unamsumbua au nini?

• Alafu naskia mwenezi mpya ni miongoni mwa mtoto pendwa sana ndani ya list yake!!
 
Back
Top Bottom