Bado kuna wazazi wanaendelea kuzaa hata baada ya mtoto wao wa kwanza kuolewa? Mtoto wa mwisho analingana na mjukuu wa kwanza? Huku ni kukosa maadili

Haya mambo kama wewe huwezi, Basi nyamaza waachie wanaoona wanaweza....


Tusipangiane namna ya kuzaliana....
Tatizo wanawaletea shida wengine. Unazaa ukiwa na miaka 60 wakati huna uwekezaji wowote kuweza kuwasaidia hao watoto, unaishia kutengeneza migogoro kwenye familia na jamii kiujumla.
 
Sawa mzee baba. Sasa baada ya kuzaa na miaka hiyo 17 alikuwa anafanya nini hapa kati mpaka aje kuzaa mtoto wa pili na umri wa miaka 35?
changamoto tu za kimaisha; kuna magonjwa, kutengwa, uchumi n.k......

kwa sababu yoyote ile iliyokuwa, je azae huyu au asizae kisa mtoto wake nae anazaa?!!!
 
changamoto tu za kimaisha; kuna magonjwa, kutengwa, uchumi n.k......

kwa sababu yoyote ile iliyokuwa, je azae huyu au asizae kisa mtoto wake nae anazaa?!!!
Kama anajali maadili asizae tena kwa maana aliweza kukaa miaka 18 bila kuzaa mtoto wa pili sasa kwanini asivumilie miaka mingine 18 mbele? Kama anataka watoto alee yatima au watoto wa ndugu.
 
Kama anajali maadili asizae tena kwa maana aliweza kukaa miaka 18 bila kuzaa mtoto wa pili sasa kwanini asivumilie miaka mingine 18 mbele?
miaka 18 mingine mbele?!!!!! utakuwa unatania kiongozi.

yaani asizae kisa tu kuna wachache wenye mawazo yao hasi?!!!........isitoshe hizi desturi zinatofautinana kati ya sehemu moja na nyingine, kisicho sahihi kwako ni sahihi kwa mwingine.
 
Tuseme alizaa mtoto akiwa na miaka 18.

Sasa akiwa na miaka 40 binti ana miaka 22, sawa wote wanazaa sioni ubaya hapo.

Mmh hesabu yenyewe sijui nimepata.
Ni aibu kwa mama wa miaka arobain kuendelea kuzaa , Huu ni umri wa kula maisha , umri wa kuzaa ni miaka 15 mpaka 38, ndani ya iyo miaka unaweza kuwa na watoto Saba.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
miaka 18 mingine mbele?!!!!! utakuwa unatania kiongozi.

yaani asizae kisa tu kuna wachache wenye mawazo yao hasi?!!!........isitoshe hizi desturi zinatofautinana kati ya sehemu moja na nyingine, kisicho sahihi kwako ni sahihi kwa mwingine.
Kama anataka watoto alee wa ndugu au yatima atapata thawabu kwa Mungu
 
Aisee ebu nieleze yangu,
Mimi ninao watoto 5 nina 42yrs sasa.First borne ana 14yrs yupo form 2,lastborn ana 4yrs yupo middleclass.
Nilimwomba Mungu sana nipate watoto 6 sasa nina watano.
Nilijitahidi sana kwa uwezo wake mola kujijenga kimaisha kabla sijaoa,so familia yangu imenikuta tayari nina kibanda na angalau kiusafiri cha kwendea kazini,kanisani nk.Nimeongeza familia pia nikaongeza miradi ya kudumu kwa ajili ya familia km vinyumba nyumba vya kupanga na kumfungulia mke kiduka ili apate pesa ya mboga na mahitaji yake madogomadogo.
Kilichobaki nimemwaahidi Mungu kuwajali watoto wangu na mke kwa namna yoyote ile wasome shule nzuri,chakula,malazi,mavazi na mahitaji yote ya msingi.
So mimi naamini watoto ni majaariwa na hakuna haja ya kuwabeza walio na watoto wengi km wamebarikiwa nao.
Mimi nina furaha na wanangu na nina wajibika nao 100%.Nipo kwenye utumishi mpk sasa na ninayafurahia Maisha haya na wanangu.
Note:Mungu umbariki kila mtu na uhitaji wake km una mtoto mmoja utepewa kwa kadri yako,km unao wengi Mungu anakujazia kwa kadri yako pia.

Sent from my SM-G531H using JamiiForums mobile app
 
Imani za kizamani eti kuzaa watoto ni baraka
Halafu unaposema uwezo ni kitu relative mwingine uwezo kwake ni kuwapeleka watoto international school ndio anajiona ana uwezo, mwingine akiweza kuwalisha ugali maharage usiku naye anajiona Ana uwezo
Whatever the case 3 children should be a maximum for everybody
 
Kwan mkiwa wachache ama wengi wote si watakufa tu mnaweza mkawa wengi mkafariki wote kwa moto mara moja
 
Jichunguze utagundua kuwa wewe ndio huna akili.
Umekariri life ya kizungu bila kuchuja hata moja.
Km uchumi wangu upo stable acha nipate hata watoto 50.
Kupanga uzazi kwangu ni big NO!
Kwani wazungu ndio wanazaa watoto wachache peke yao? Nenda Korea, nenda Japan, nenda Qatar huko kote sio wazungu na wana familia ndogo, stable na zenye mafanikio, na future za watoto wao zipo guaranteed
Wewe umeweza tu kuwalisha ugali maharage unajiona una uweeeezoooo, eti uchumi wangu upo stable...
 
Kaka mkubwa, sidhani kama umeisoma vema mada hii na ukaielewa...
 
Kama anataka watoto alee wa ndugu au yatima atapata thawabu kwa Mungu
akizaa wake na kuwalea kwa kuwa nafasi bado ipo, basi si thawabu tu atakazopata bali na furaha isiyo na kifani pamoja na uhakika wa usaidizi wa siku za mwisho za maisha yake
 
Nosense., Haya mambo si ya kujadili na yaonekana wazi ata dini huna, na unafkiri kila kitu ulimwenguni kinaendeshwa ni mawazo binafsi ya mwanadamu, na ndio mana sasa ukijisikia unakuja hapa jf na kuandika tu chochote.
 

Mwenzangu kama wewe huna uwezo wa kulea watoto zaidi ya watatu usiwaseme wenzio walio na uwezo hawana akili, eboo!!
 
Haya mambo si ya kujadili na yaonekana wazi ata dini huna, na unafkiri kila kitu ulimwenguni kinaendeshwa ni mawazo binafsi ya mwanadamu, na ndio mana sasa ukijisikia unakuja hapa jf na kuandika tu chochote.
Kuna uwezekano mkubwa sana hii mada ikakuhusu na inaonekana imekuchoma kweli kweli
 
Infantry,nimekuelewa mwenye mada vizuri ila nilikuwa najaribu kufanya quote ya jamaa mwingine anaeponda mzazi mwenye watoto zaidi ya 3 so mimi nimesahau kuunganisha ujumbe wake na wangu.Ujumbe wangu umekuja km wa mpinga mada.
Sawa mkuu, nimekuelewa ulikuwa unam-quote mtu ila kwa bahati mbaya ukakosea...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…