Bado natafuta mantiki ya kujenga hili Daraja la Kigongo - Busisi kwa Tshs. Bilioni 700

Bado natafuta mantiki ya kujenga hili Daraja la Kigongo - Busisi kwa Tshs. Bilioni 700

ILA UMESUBIRI MANTIKI YA KUONA MAMIA YA WATANZANIA WANAOISHI MWANZA NA GEITA WAMEZAMA NA KUTEGETEA NA VIVUKO VYA BUSISI NA KAMANGA NA KIGONGO.

HIVI CHADEMA KITU GANI KIMEWAVURUGA??

Ishu hapa ni kitendo mwenzenu kuchezea kodi zetu kwa kuwajengea miradi mikubwa isiyoendana na hadhi yenu.

Mara taa za kuongozea magari lakini mwisho wa siku inapita mikokoteni ya punda, mara uwanja mkubwa wa kimataifa halafubhakuna ndege yoyote ya kibiashara kutoka nje ya nchi inayotua, nk.

Na sasa mnajengewa daraja la bilioni 700! Hiyo pesa ingekua haina kazi si bora ingekopeshwa kwa wahitimu wa vyuo vikuu kwa riba ndogo ili waweze kujenga viwanda na kujiajiri? Kwani mngewekewa vivuko vya kisasa mngepungukiwa nini?
 
Uhuru wa mawazo ni mzuri lakini kwa watu wa upande wa mwanza hii ni faida na inaokoa muda sana...kuvuka pale ferry ukikuta dude limetembea unasubiri muda mrefu Sana na like Kuna watu wengi mno na magari, wanalata shida Sana tu sema ndio hivo tunaona shida ya mwenzio soup yako, yaani kwa umuhimu ni bora zaidi kuliko daraja la kigamboni
Kweli linaweza kuwa na muhimu, lakini je Bunge lilipitisha hiyo budget?
 
Una wazo zuri Sana subiri zamu yako

Kwani mwanzo nadhani wewe unaweza kuwa mmoja wapo au unakumbuka Ile pesa za Mikopo ya pale Chuo kikuu pale Dar, Ile Mikopo ya project ilivyokuwa inafanywa na vijana pale.

Ni mara kumi kujenga Faraja leo
 
Du, bora wangejenga Dar to Zanzibar [emoji24]
Yani Trilioni moja kasoro mia 3
Yani 90% ya mapato ya mwezi ya nchi.
Hi ni balaa
 
Ishu hapa ni kitendo cha mwenzenu kuchezea kodi zetu kwa kuwajengea miradi mikubwa isiyoendana na hadhi yenu.

Mara taa za kuongozea magari lakini mwisho wa siku inapita mikokoteni ya punda, mara uwanja mkubwa wa kimataifa halafubhakuna ndege yoyote ya kibiashara kutoka nje ya nchi inayotua, nk.

Na sasa mnajengewa daraja la bilioni 700! Hiyo pesa ingekua haina kazi si bora ingekopeshwa kwa wahitimu wa vyuo vikuu kwa riba ndogo ili waweze kujenga viwanda na kujiajiri? Kwani mngewekewa vivuko vya kisasa mngepungukiwa nini?
KWAHIYO HIYO FEDHA UMEILINGANISHA NA ROHO ZA WATANZANIA WANAOISHI MWANZA NA GEITA AMBAO WAKO HATARINI KUPOTEZA MAISHA. NA WENGINE WAMESHA POTEZA MAISHA, MAISHA YA WATU WANAOKUFA KWENU CAHADEMA SIO KITU. HURUMA IKO KWENYE FEDHA TUU.

CHADEMA FEDHA ZITAWAPELEKA MOTONI.

HOVYO KABISA.
 
UKANDA UKANDA UKANDA UKANDA

Kuna sehemu kule kusini ziwa nyasa barabara hazipitiki endapo mvua zikinyesha, sijui ikitokea vita na Malawi vifaa vya kijeshi vitaendaje kule.
 
Chadema wanahisi kuwampinzani ni kupinga kila jambo zuri la serikali.
Chadema mnapokea ruzuku ya chama kila mwaka,kwa nini mmeshindwa kujenga hata ofisi kuu ya chama chenu.mnakalia kukosoa tu?
 
KWAHIYO HIYO FEDHA UMEILINGANISHA NA ROHO ZA WATANZANIA WANAOISHI MWANZA NA GEITA AMBAO WAKO HATARINI KUPOTEZA MAISHA. NA WENGINE WAMESHA POTEZA MAISHA, MAISHA YA WATU WANAOKUFA KWENU CAHADEMA SIO KITU. HURUMA IKO KWENYE FEDHA TUU.

CHADEMA FEDHA ZITAWAPELEKA MOTONI.

HOVYO KABISA.

Tunachokataa Watanzania ni huu upendeleo wa kikanda unaojidhihirisha awamu hii. Unadhani Baba wa Taifa angeendekeza Ukabila na Ukanda, Mkoa wa Mara si ungekua ni zaidi ya Dar es Salaam kwa sasa?
 
Tunachokataa Watanzania ni huu upendeleo wa kikanda unaojidhirisha awamu hii. Unadhani Baba Taifa angeendekeza Ukabila na Ukanda, Mkoa wa Mara si ungekua ni zaidi ya Dar es Salaam?
KUMBE KINACHOKUWASHA USIKU KUCHA NI WIVUU??

Hakuna upendeleo atakidogoo. Ungekuwa ni mkazi wa Mwanza na Geita ukajionea halihalisi ya namna gani watu wanapoteza maisha mara kwa mara, hata we we ungewangea barabaraa, usafiri wa vivuko ni hatarishi kwa maisha ya binadamu.

Pia nenda ukawambie wahanga wa vivuko kwamba hakuna haja ya kujenga barabara hiyo, kama utarudi unapumua umushukuru Mungu wako.
 
Sasa ngoja hilo daraja likamilike uone watakaopita hapo kama watakuwa wengi kuzidi feri. Hivi unajua kurudisha bilioni 700 wewe! Hizo hela ni nyingi sana kwa kuelekeza kwenye mradi kama ule. Any way ila Jiulize kwanini hata yeye Magufuli anahisi alifanya kitu kisicho na tija hadi anahimiza waharakishe ili Rais mwingine asije akaufuta huo mradi.
Hilo daraja litakuwepo kea miaka 600, kila siku likiingiza 10m kwa miaka 600 si ni faida? Hizi ferry zinaendeshwa kea hasara safari mmoja unatumia mafuta ya 5m wakati nauli ni mianne kea kichwa huoni hiyo hasara?
 
Kwa ujenzi wadaraja Lile sipingi ata kidogo sisi watu tunaotumia ile njia Mara kwamara tunajua faida yake. Uktaka kujua umuhmu wadaraja Lile kivuko kikuzmikie upo majni afu katkati, ila kwaujenzi wa uwanja wandege Apo mjomba sipng amevulunda mbaya kabsa.daraja linagusa maisha yachn kabsa yamwananchi katka shughul zauchumi. Ule uwanja wandege na zle taa haina faida yoyote kwetu.
 
hivi wewe na akili zako hujui humuimu wa daraja linalounganisha mkoa mmoja na mkoa mwingine,kwanini lakini chadema mnakuwa hivyo ,kabla ya swali lako ungejiuliza umuhimu wa madaraja yafuatayo:nyerere la kigamboni,kikwete la malagarasi,mkapa la rufiji,wami la mto wami na maeneo hayo yote yalikuwa na vivuko kabla ya ujenzi wa madaraja hayo.
Humuimu ≠ Umuhimu
nyerere ≠ Nyerere
kikwete ≠ Kikwete
mkapa ≠ Mkapa
kigamboni ≠ Kigamboni
rufiji ≠ Rufiji
wami ≠ Wami
malagarasi ≠ Malagarasi
 
Kagombee urad
Ishu hapa ni kitendo cha mwenzenu kuchezea kodi zetu kwa kuwajengea miradi mikubwa isiyoendana na hadhi yenu.

Mara taa za kuongozea magari lakini mwisho wa siku inapita mikokoteni ya punda, mara uwanja mkubwa wa kimataifa halafubhakuna ndege yoyote ya kibiashara kutoka nje ya nchi inayotua, nk.

Na sasa mnajengewa daraja la bilioni 700! Hiyo pesa ingekua haina kazi si bora ingekopeshwa kwa wahitimu wa vyuo vikuu kwa riba ndogo ili waweze kujenga viwanda na kujiajiri? Kwani mngewekewa vivuko vya kisasa mngepungukiwa nini?
Una mawazo mazuri ulikuwa wapi kugombea Urais, anyway subiri 2025 uje na swagger zako
 
Lissu alipita hapo kigongo ferry akaubeza huo mradi lakini mhe Magufuli aliusifia na kueleza umuhimu wake. Ngoja tuone tar 28 wananchi watatuambia.

Mimi ninavyofahamu hilo eneo kwa siku linapitisha magari na watu wengi sana. Kuvuka kwa kivuko inakula kama dk 30 mpaka 45.
Hakwenda alipitia fela fumagila akaibukia kisesa akasepa tarime ukweni
 
Mantiki ni kuunganisha kwa huduma za usafiri ukanda huo ili kukuza utalii, sekta ya madini, uvuvi, afya, biashara na nchi jirani, kufungua uwekezaji wa hoteli za kisasa katika pwani yote ya ziwa victoria inayozu guka maeneo hayo na kuchochea fursa nyingi za kiuchumi zikiwemo usafiri wa haraka kwa wakaazi zaidi ya 5.6Millioni.

Ningelikuwa mimi ningeliuliza ufanisi wa daraja la kigamboni, fryovers na ujenzi wa viwanja vya ndege nchi nzima.
Daraja la kigongo-busisi umuhimu wake unafanana na daraja la Mkapa.
Kwa hili nami natia hoja hapa;

Ujenzi wa daraja la Busisi-Kigongo sio kweli kwamba hauna umuhimu kama wachangiaji wengi wasemavyo ila tujaribu kuangalia kwa mapana sana huku tukihusianisha gharama, mahitaji na alternatives ya mahali husika.

1. Kwa sasa mradi huu wa Tshs.700b kwa ujenzi wa daraja tena sehemu moja tu mimi naona ni matumizi yasiyokuwa na tija. Hii ni pesa nyingi sana kwa eneo hili ikiishia kwenye mradi mmoja tu huku ikiacha changamoto zingine lukuki za eneo hilo.

Maeneo ya kanda ya ziwa bado kuna changamoto kubwa ya upatikanaji wa maji safi majumbani hasa kwenye maeneo hayo hayo ya Misungwi, Sengerema, Geita, Nyamagana n.k kwanini pesa hii isitatue changamoto hii kwanza?

Maeneo mengi ya kanda ya ziwa bado barabara ni changamoto, ni mbovu na hazina lami ambapo kama inshu ni kuwahisha wagonjwa Bugando bado wengi wanacheleweshwa na barabara mbovu huko watokako kwanini pesa hii isitatue changamoto hii kwanza?

Ni kweli kusubiri vivuko pale ni kero kubwa sana lakini hili linatatulika kwa kuongeza idadi ya vivuko kuendana na mahitaji, hakika pale vikiongezwa vivuko vingine kama viwili au vitatu vyenye ukubwa na speed ya kutosha hakutakuwa tena changamoto ya foleni mahali pale ambapo ujenzi wa vivuko hivyo hauzidi bilioni 5 kwa kila kimoja pesa ambayo ingeweza kutumika haizidi bilioni 15 na kuacha hela zingine zikaingia kwenye hiyo miradi ya maji na ujenzi wa barabara za lami kanda ya ziwa.

Shida ninayoiona mimi ni maamuzi ya nchi hii kuwa ni ya mtu mmoja mwenye madaraka na mamlaka makubwa sana, akiamua tena majukwaani tu bila kutumia vyombo vya ushauri hili linatugharimu kama taifa. Watendaji wengine wamekuwa ni waoga kushauri kitaalamu maana hawawezi kumkosoa boss wao( kushauri maamuzi ya mkuu ni kumkosoa).

Turudi kwenye uongozi unazingatia kanuni za kiuongozi laiti kama ungewasikiliza wanakanda ya ziwa mahitaji yao nadhani daraja hilo si kapaumbele kikubwa kwa sasa japo kwa baadae ni sawa kabisa.
 
Miradi hii yote inatokana na Ilani ya uchaguzi. Isomeni vizuri.lakini kelele ni kwa vile ni kanda ya ziwa,Mbona Waziri mmoja alijenga sana Mwanga miaka 70 hamsemi,je mbona ilikuwa Bandari kubwa ijengwe Bagamoyo hamsemi, mbona Dodoma inajengwa kimataifa hamsemi,mbona Arusha kuna barabara njia nne na miradi mingi tu hamsemi,flyovers dar hamsemi lakini maendeleo yakifanika kanda ya ziwa kelele.

Ni kweli bado kuna barabara ambazo hazina lami Kanda hii lakni kumbuka maendeleo ni mchakato progressively akichaguliwa ataboresha maeneo yaliyobaki lakini msianze kupiga kelele tena miradi ikilindima hatutakubali.Tunaahidi kumpigia kura sote aendelee na utekelezaji wa Mipango yote ya maendeleo 2025 na ahadi za ilani ikiwemo ya kanda ya ziwa.

Tumepiga kelele jengo la abiria la uwanja wa ndege Mwanza wakahamishia ujenzi Mbeya miaka ya 90 na 2000 etc.Mwacheni Rais atekeleze mipango yake yote -kumbe alifanya vizuri kuwanyamazisha kimya wakati akitekeleza miradi miaka 5 iliyopita vinginevyo isingewezekana kwa mwenenendo na kelele hizi.

Ninakusihi Rais kamilisha miradi yote ndani ya miaka 10 na hususani ya kanda hii ili uache legacy vinginevyo kwa vile akija mwingine miradi mingi ya kanda ya ziwa kuna dalili itawekwa pembeni kwa upotoshaji na uchonganishi unaofanywa sasa. Lets us be vigilant on this issue.

MAENDELEO HAYANA CHAMA. HII NI NCHI YETU SOTE.
 
Mimi Chadema damu tena uanachama wa kidigital kabisa, Nataka Tundu Lissu ashinde urais lakin kikwazo changu ni kimoja tu, Ni hilo daraja la busisi. Nina hofu Lissu akishinda huenda akaachana na ujenzi wa hilo daraja, dah! Yaani napata wakati mgumu sasa, daraja nalitaka na Lissu namtaka. Lissu atuhakikishie ujenzi wa hilo daraja mioyo yetu itulie.
 
Kuna miradi ambayo imefanywa safari hii ambayo haikutakiwa iwe priority. Ununuzi wa ndege, Kuhamia Dodoma nafikiri hayo hayangekuwa kipaumbele.

Kwenye irani ya CCM wanadai awamu hii wataimarisha kilimo cha umwagiliaji kwa kulima ekali 1 million. Hii ilikuwa kwenye ilani yao ya 2015 lakini hawakuitekeleza. Sasa kilimo na Ndege kipi kilitakiwa kiwe kipaumbele? Maana kama ni ndege zilikuwepo na zilikuwa zinapeleka watu kila mahali tena kwa bei rahisi tu.

Binafsi nafikiri kama pesa za kutosha zingewekzwa kwenye kilimo, gas na Chuma huko Mchuchuma na kusimamiwa vizuri kama walivyofanya kwenye SGR na fly overs basi miaka hii mitano ingekuwa ya neema sana. Tungeweza kufanya miradi yote bila matatizo kwa kutumia pesa ya ziada ambayo tungeiteneza kutokana na kilimo, gas na chuma!

Kwa njia tuliyoitumia the catch is itabidi tuendelee kufanya miradi yote kwa jia ileile bila butegemea kipato cha ziada. Matokeo yake watu wasitegemee mabadiliko makubwa kwenye maisha yao kwani mishahara haitapanda.
 
Back
Top Bottom