Bado sijaona mbadala wa Scandinavian katika usafiri wa Mabasi. Nauli ilitofautiana kwa aina ya SCANIA

Bado sijaona mbadala wa Scandinavian katika usafiri wa Mabasi. Nauli ilitofautiana kwa aina ya SCANIA

Sababu ya kifo cha Scandinavian ni baada ya mmiliki kujiingiza kwenye siasa za kijinga huku akijua analo deni beki ya ADB, ADB walikuwa wanamdai yeye akachukua mabasi kuwapeleka bure wanaccm Rufiji kuzindua daraja la Mkapa, mabasi yaliporudi ADB ikakamata mabasi yote ya Scandinavian na kuyafungia kwenye yadi ya serikali Temeke kusubiri mnada, huo ndio ulikuwa mwisho wake.
Kilichomponza ni kudhani kuwa CCM itaiambia benki mwacheni huyu ni mwenzetu, lakini ADB haiko Tanzania hivyo haiwezi kujua kama ni mwenzao.
Tajiri alibadili biashara ndiye wakala wa yutong
 
Ngojeni niwape mfano huu,nilipokuwa shule ya msingi kiwanja cha shuleni kwetu nilikuwa nakiona kikubwa sana na pia kanisa la kwetu Parokia ya Mango Moshi nilikuwa naliona kubwa sana
Pia nilipokuwa mdogo shule ya Msingi nilipokuwa nilitoka Moshi kwenda Dar na Ngorika au Masama safari au zafanana au Bembea au Tawaqal au dar express nilikuona naona miti inakimbia kwa kurudi nyuma sana
Likini leo nashangaa mbona kiwanja au kanisa ni vidogo kwasasa?
Hivyo hivyo na Scandinavia utaendelea kuiona ni Bora kuliko wengine ukibaki na mawazo ya kitoto kama mifano hiyo hapo Juu
Kwa sasa Huduma makampuni mengi sana yanajitaidi na wanamagari mazuri sana kuliko miaka hiyo

Pia swala la huduma vizazi vinabadilika ,wale mnaosifia kuwa Scandinavia ni bora mpaka sasa mkumbuke enzi hizo ukienda guest nikweli unaenda kulala sio kufanya ngono tofauti na nyakati hizi.acheni kuchukua vipindi hivi na vile
 
Ngojeni niwape mfano huu,nilipokuwa shule ya msingi kiwanja cha shuleni kwetu nilikuwa nakiona kikubwa sana na pia kanisa la kwetu Parokia ya Mango Moshi nilikuwa naliona kubwa sana
Pia nilipokuwa mdogo shule ya Msingi nilipokuwa nilitoka Moshi kwenda Dar na Ngorika au Masama safari au zafanana au Bembea au Tawaqal au dar express nilikuona naona miti inakimbia kwa kurudi nyuma sana
Likini leo nashangaa mbona kiwanja au kanisa ni vidogo kwasasa?
Hivyo hivyo na Scandinavia utaendelea kuiona ni Bora kuliko wengine ukibaki na mawazo ya kitoto kama mifano hiyo hapo Juu
Kwa sasa Huduma makampuni mengi sana yanajitaidi na wanamagari mazuri sana kuliko miaka hiyo

Pia swala la huduma vizazi vinabadilika ,wale mnaosifia kuwa Scandinavia ni bora mpaka sasa mkumbuke enzi hizo ukienda guest nikweli unaenda kulala sio kufanya ngono tofauti na nyakati hizi.acheni kuchukua vipindi hivi na vile
Umemaliza mkuu mi nimewambia ndugu zangu Kwa unyenyekevu kabisa kuwa wamemiss Scandinavia but haimaanishi kuwa yeye ndio GOT.
 
Royal?
Hakuna kampuni bora tena.
Ukaribu wa kuiga.
Huduma za kuunga unga tu.
Ubabaishaji mwingi sana
Punguzeni chuki Kwa watoa huduma za usafirishaji wamewakosea Nini? Huduma za kuunga unga kama zipi?
 
Alikuwa na huduma ya "loyal customers" au twaweza ita "frequent traveller service".
Yaani ukisafiri na bus zake mara kadhaa kwa kipindi cha muda fulani, unapata tiketi ya bure.
Hiyo huduma ilikuwepo karibia mabus yote usipotoshe umma
 
Sijawahi ona wauza dawa za miswaki ndani ya scandinavia lakini leo sauli mkifika moro mara mdada anapanda na shangazi kaja lake anaanza matangazo ya vitu kwa bei ya promosheni
Wauza miswaki hata Mimi sikuwahi kuwaona kwenye Sumry, Ottawa, na Superfeo Enzi hizo. Sasa population na ugumu wa ajira ndio umefanya watu hao uwaone ndani ya bus. Ukweli ni kuwa mmemic kampuni ya Scandinavia nothing else
 
Huwezi mlinganisha ratco na scandinavia kwakuwa ratco ana route chache sidhani kama zinazidi mbili, ninayoifahamu ni Dar-TA tu
Ishu ni service iliyokuwa inatolewa au kuwa na route nyingi?
 
Wazungu hata tuwapige vita vipi wako vizuri

Scandinavia ilikuwa kipindi kile meneja alikuwa mzungu ndio maana kila kitu kilikuwa kizuri kuanzia stendi yake, mabasi, mfuumo wa ukataji tickets sehemu za kupumzika abiria kama airport kabisa wahudumu wasafi.
Punguza uongo basi khaa
 
Route nyingi nayo ni mojawapo ya service mkuu
Sawa alikuwa na route nyingi kutokana na bus alizokuwa nazo. Je service iliyokuwa inatolewa kipindi Cha safari ndani ya bus hakuna kampuni yoyote inaitoa Sasa.?
 
Natumia sana usafiri wa mabasi, bado sijaona mbadala wa Scandinavian kwa kweli. Hawa akina Sauli, Shabiby, sijui ABC bado sana aisee.

Scandinavian ilikuwa bora kuanzia kwenye vyuma vyenyewe yaani Scania tupu hakuna Layland hadi kwenye huduma. Ligi ya sasa ni vyuma vya mchina aka kambi popote

Mungu wa mbinguni mbariki mzee Abdullah na Bob Said pale Iringa
Bei ya scania unaijua?
 
Hakuna mbadala wa Scandinavia kama ni kweli mbona watu wanaendelea kusafiri Tena zile sehemu ambazo hapo awali zilikuwa hazifikiki zinafikika Kwa Sasa. Sasa hiyo si ni zaidi ya mbadala

Route zimeongezeka Kuna options nyingi wakati wa kusafiri yaani kweli unaona improvement kwenye sekta ya usafirishaji.

Sasa watu ambao Kwao change ni ngumu Bado wanafikra za miaka ya tisini ambapo kuchimba dawa walikuwa wanachimba mbele ya watoto, wazazi na wakwe zao.
 
Back
Top Bottom