Bado tupo utumwani? kwanini tunasita kubadili jina la jiji kubwa zaidi Afrika mashariki

Bado tupo utumwani? kwanini tunasita kubadili jina la jiji kubwa zaidi Afrika mashariki

round kick

JF-Expert Member
Joined
Feb 3, 2025
Posts
345
Reaction score
1,145
Tukiangalia majina karibia yote ya mikoa yana asili ya hapa kwetu iweje jiji kubwa nchini na Africa Mashariki tubaki kungangania jina la kikoloni lenye historia ya kitumwa ?

Jina la jiji kubwa zaidi Afrika Mashariki "Dar Es Salaam" lilipewa na Sultani Majid bin Said

Kabla ya hapo, eneo hilo lilikuwa kijiji kidogo cha wavuvi kilichoitwa Mzizima, neno lenye maana ya "mji wenye afya."

Sultani Majid alikuwa akifanya biashara ya kikatili ya utumwa iliyomtajirisha, Bandari aliyotumia aliisifia kwa kuiita Dar Es Salaam, kwa tafsiri ya kiswahili ni bandari salama, alisafirisha babu na bibi bila bugudha ndio maana akapaita Dar Es salaam,

Ni sehemu ambayo Sultan aliitumia kwa namna moja au nyingine kutumia bandari kujitajirisha na biashara yake ya kikatili iliyotumikisha babau zetu mashambani kwa mijeredi mashambani, babu zetu walioenda nchi walizotokea masultan hali ilikuwa mbaya walikatwa viungo vya uzazi ndio maana ni ngumu kukuta wajukuu zao ( utaowakuta ni waafrika waliohamia kuanzia miaka ya 70s)

Itapendeza zaidi paitwe MZIZIMA

1740580992894.png
 
Jina la jiji kubwa zaidi Afrika Mashariki "Dar Es Salaam" lilipewa na Sultani Majid bin Said, Jina hili linatokana na kiarabu lugha aliyotumia Sultan

Kabla ya hapo, eneo hilo lilikuwa kijiji kidogo cha wavuvi kilichoitwa Mzizima, neno lenye maana ya "mji wenye afya."

Itapendeza zaidi paitwe MZIZIMA
Jina la Dar es salaam tulishalikubali, tulikichukua na kulifanya letu, si la Sultani tena.

Ukishikilia kuwa ni la Sultani, wewe ndiye unampa Sultani umuhimu asiokuwa nao.

Pia, kihistoria Dar es salaam kama mji ni mji ulioanzishwa na Sultani. Hiyo ni historia ambayo haifutiki hata ukibadili jina.
 
Jina la Dar es salaam tulishalikubali, tulikichukua na kulifanya letu, si la Sultani tena.

Ukishikilia kuwa ni la Sultani, wewe ndiye unampa Sultani umuhimu asiokuwa nao.

Pia, kihistoria Dar es salaam kama mji ni mji ulioanzishwa na Sultani. Hiyo ni historia ambayo haifutiki hata ukibadili jina.
Sultani alichukua eneo kimabavu hana hadhi yoyote ya kusifiwa kuanzisha mji, kwao alikotoka ni uarabuni.

Hao masultan wamechukua babu zako kuwauza sehemu nyingi duniani, Hali ilikuwa mbaya zaidi kwa babu zetu waliopelekwa uarabuni walikatwa viungo vya uzazi ndio maana leo hii ni ngumu kukuta vizazi vya watumwa uarabuni
 
Wengi hatujui maana ni lugha aliyotumia Sultani aliyekwishafukuzwa

Yafaa zaidi jiji liitwe kwa maneno asili ya hapa hapa kwetu
Ukishasema "maana ni lugha" hapo tayari ushatumia maneno mawili yenye mzizi wa Kiarabu.

Maana limetokana na Kiarabu.

Lugha limetokana na Kiarabu.

Sasa hapo napo utasema tuondoe maneno yote yenye asili ya Kiarabu katika Kiswahili?
 
Sultani alichukua eneo kimabavu hana hadhi yoyote ya kusifiwa kuanzisha mji, kwao alikotoka ni uarabuni.

Hao masultan wamechukua babu zako kuwauza sehemu nyingi duniani, Hali ilikuwa mbaya zaidi kwa babu zetu waliopelekwa uarabuni walikatwa viungo vya uzazi ndio maana leo hii ni ngumu kukuta vizazi vya watumwa uarabuni
Sultani kauziwa ardhi mjini na Jumbe Tambaza ndiyo kajenga chuo cha Uislamu hiyo Ikulu ya Dar na maeneo ya mjini.

Kasome historia ujielimishe kabla ya kukurupuka.
 
Jina la jiji kubwa zaidi Afrika Mashariki "Dar Es Salaam" lilipewa na Sultani Majid bin Said, Jina hili linatokana na kiarabu lugha aliyotumia Sultan

Kabla ya hapo, eneo hilo lilikuwa kijiji kidogo cha wavuvi kilichoitwa Mzizima, neno lenye maana ya "mji wenye afya."

Itapendeza zaidi paitwe MZIZIMA
Lengo ni Nini hasa kubadili jina la mji?
Hii itasaidia nini?

Jiji la hovyo sana .mpangilio wa makazi ni hovyo.Tunazidiwa na jiji zuri la Kigali na Bunjumbula
Kweli kabisa.

Mji huo ni mchafu Sana.
Hauna Mipango-miji.
Miundombinu duni kabisa, nyumba nyingi sana (at least 70%) hazifikiki kwa barabara Wala kwa gari.
Kila kitu ni hovyo hovyo kabisa.
 
Jina la jiji kubwa zaidi Afrika Mashariki "Dar Es Salaam" lilipewa na Sultani Majid bin Said, Jina hili linatokana na kiarabu lugha aliyotumia Sultan

Kabla ya hapo, eneo hilo lilikuwa kijiji kidogo cha wavuvi kilichoitwa Mzizima, neno lenye maana ya "mji wenye afya."

Kuita jiji hili kubwa kwa jina la Sultan kunaambatana na kumbukumbu za historia yetu chungu ya utumwa wa masultan waliokuwa vinara wa biashara ya utumwa, wengine walienda Zanzibar kulimishwa karafuu, wengine walienda Marekani waliruhusiwa kuwa na watoto, walioenda uarabuni hali ilikuwa mbaya walikatwa viungo vya uzazi ndio maana ni ngumu kukuta wenzetu huko, utaowakuta ni waliohamia kuanzia miaka ya 70s

Itapendeza zaidi paitwe MZIZIMA
Tuanze padogo tuondoe Ilala iwe Mzzm
 
Dar es Salaam ni jina lenye asili ya Kiarabu linalomaanisha "Bandari ya Amani" au "Nyumba ya Amani". Jina hili linatokana na maneno mawili ya Kiarabu:

دار (Dar) – ikimaanisha "nyumba" au "bandari"

السلام (As-Salaam) – ikimaanisha "amani"


Mji huu ulianzishwa rasmi na Sultan Seyyid Majid wa Zanzibar mnamo karne ya 19. Awali, ulijulikana kwa majina tofauti kama Mzizima , Bandali ya sultan Majid nk kabla ya kupata jina la sasa. Leo, Dar es Salaam ni jiji kubwa zaidi nchini Tanzania na kitovu cha biashara, uchumi, na utamaduni.
 
Back
Top Bottom