Bado tupo utumwani? kwanini tunasita kubadili jina la jiji kubwa zaidi Afrika mashariki

Fort Bragg ilibadilishwa jina na utawala wa Biden kwa sababu ya kumbukumbu mbaya ya uasi wa mwenye hilo jina.
 
Hapa hatuwezi kuelewana, you are very narrow minded you are thinking subjectively

Seems you would be ok if Sultan culstrated yo grandpa for the sake of slave trade profits
Hatuwezi kuelewana kwa sababu huwezi kufuatilia hoja.

Umefanya logical fallacy ya false dichotomy.

Nakuonesha hapa umefanya logical fallacy ya false dichotomy, badala ya kujifunza, unafanya logical fallacy nyingine ya strawman argument na logical fallacy ya kunitusi kwa ad hominem attack.

Hatuwezi kuelewana.

Posts zako zimejaa logical fallacies.
 
Mkuu ondoa chuki binafsi utafika mbali sana..
 
Fort Bragg ilibadilishwa jina na utawala wa Biden kwa sababu ya kumbukumbu mbaya ya uasi wa mwenye hilo jina.
Kubadili jina kila sehemu kuna sababu zake za kihistoria.

Trump kabadili mpaka Gulf of Mexico kaiita Gulf if America.

Na wewe utataka kumuiga uibadili bahati ya Hindi uiite bahari ya Tanganyika?
 
Sultani kauziwa ardhi mjini na Jumbe Tambaza ndiyo kajenga chuo cha Uislamu hiyo Ikulu ya Dar na maeneo ya mjini.

Kasome historia ujielimishe kabla ya kukurupuka.
Jumbe Tambaza itakuwa alirubuniwa tu, hakuwa anajua anachokifanya,
 
Kubadili jina kila sehemu kuna sababu zake za kihistoria.

Trump kabadili mpaka Gulf of Mexico kaiita Gulf if America.

Na wewe utataka kumuiga uibadili bahati ya Hindi uiite bahari ya Tanganyika?
Mleta uzi kaweka sababu zenye mashiko.
 
Wengi hatujui maana ni lugha aliyotumia Sultani aliyekwishafukuzwa

Yafaa zaidi jiji liitwe kwa maneno asili ya hapa hapa kwetu
Kwahiyo na Kiswahili tuache kukitumia? Maana asilimia zaidi 75 ya Kiswahili ni maneno ya Kiarabu na Kihindi.
 
Mleta uzi kaweka sababu zenye mashiko.
Sababu gani?

Ukibadili jina la mji Dar es salaam unatatua matatizo gani? Unatengeneza matatizo gani? Kwa gharama gani?

What is the cost benefit analysis of this exercise?
 
Tuanze na wewe kwanza, jina lako nani, Sudi au John? Hilo ndio jina laasili yako? Na baba, mama na ndugu zako je?

Anzia huko halafu ndio uje hapa
 
Twaelewa maana ya dar es salaam; ni bandari salama”. Je, maana ya mzizima ni nini mkuu.
 
Kwahiyo na Kiswahili tuache kukitumia? Maana asilimia zaidi 75 ya Kiswahili ni maneno ya Kiarabu na Kihindi.
Hawa watu wanachekesha sana.

Wana matatizo lukuki ya kweli, yanayohitaji ufumbuzi, yanayohitaji bajeti, hawajayatatua, mengine hata hawajaanza kuyatatua.

Halafu hapohapo, wanajitungia matatizo ambayo hayapo, wanataka kuyatatua hayo.

Ujinga mtupu.
 
Sababu gani?

Ukibadili jina la mji Dar es salaam unatatua matatizo gani? Unatengeneza matatizo gani? Kwa gharama gani?

What is the cost benefit analysis of this exercise?
Jina la mji ni nembo ya taifa. Mwenge nao unachukuliwa kama nembo ya taifa, unakimbizwa kwa mabilioni ya pesa lakini hautatui matatizo yoyote.
 
Mtanzania akienda ulaya anakuwa na ka ushamba flani ka kutumia kiingereza kingi kilichojaa jurgons, sijapotosha hoja yako kwa madhumuni ya kukushambulia (strowman fallacy), hizo ni facts huyo Sultan kabeba historia iliyoumiza waafrika, mtizamo wako ni mwembamba unafikiria kwa hisia zako probably kwa imani yako usianze kujitetea ad homen crap

Funny how historical pain is acknowledged selectively, I bet unaweza kuishi mji unaitwa abeed kisa ni jina la kiarabu ila huwezi kuishi mji ukiitwa carl peters
 
Jina la mji ni nembo ya taifa. Mwenge nao unachukuliwa kama nembo ya taifa, unakimbizwa kwa mabilioni ya pesa lakini hautatui matatizo yoyote.
Huo mwenge nao ni ujinga mtupu.

Kwanza uwe na taifa halafu ndiyo uwe na nembo ya taifa.

Sasa wewe huna taifa unataka nembo ya taifa?
 
Kwahiyo na Kiswahili tuache kukitumia? Maana asilimia zaidi 75 ya Kiswahili ni maneno ya Kiarabu na Kihindi.
Sio kweli kwamba zaidi ya 75% ya maneno ya Kiswahili ni maneno ya Kiarabu na Kihindi.
 
Hawa watu wanachekesha sana.

Wana matatizo lukuki ya kweli, yanayohitaji ufumbuzi, yanayohitaji bajeti, hawajayatatua, mengine hata hawajaanza kuyatatua.

Halafu hapohapo, wanajitungia matatizo ambayo hayapo, wanataka kuyatatua hayo.

Ujinga mtupu.
Mkuu akili ni nywele. Huenda uwezo wao wa kufikiri ndio huo, kwamba Dar ikiitwa Mzizima basi shida ya maji, imeme, barabara nk. itakuwa imeisha!
 
Mimi ni muumini wa historia na napenda sana majina ya sehemu yabaki kama yalivyokuwa ili tuweze kujua historia yetu. Hata mitaa ya Dar sidhani kama ilikuwa busara kubadilisha majina ya enzi zile. Nyumba pia walibomoa kwa makosa.
 
Mkuu akili ni nywele. Huenda uwezo wao wa kufikiri ndio huo, kwamba Dar ikiitwa Mzizima basi shida ya maji, imeme, barabara nk. itakuwa imeisha!
Hizi ni kasumba za Identity Politics tu.

This can be a big distraction from real issues.

Na afadhali hata uanze mambo ya Identity Politics wakati ushaendelea kiuchumi.

Wewe masikini bajeti ya afya haitoshi. Unataka ukate hiyo bajeti ya afya uipeleke kwenye project ya kubadili mji jina?

Ujinga mtupu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…